Organization Logo

الباكستان مكتب

ولاية باكستان

Twitter: http://twitter.com/HTmediaPAK

Tel:

HTmediaPAK@gmail.com

http://www.hizb-pakistan.com/

Iwe ni Kuhusu Mafuriko au Kashmir, au Uchumi au Ukaliaji wa India wa Mito Yetu, Tutaendelea Kungoja Hadi Lini Kinachoitwa Mfumo wa Kimataifa Utatue Matatizo Yetu?!
Press Release

Iwe ni Kuhusu Mafuriko au Kashmir, au Uchumi au Ukaliaji wa India wa Mito Yetu, Tutaendelea Kungoja Hadi Lini Kinachoitwa Mfumo wa Kimataifa Utatue Matatizo Yetu?!

September 09, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Iwe ni Kuhusu Mafuriko au Kashmir, au Uchumi au Ukaliaji wa India wa Mito Yetu

Tutaendelea Kungoja Hadi Lini Kinachoitwa Mfumo wa Kimataifa Utatue Matatizo Yetu?!

Baada ya mafuriko makubwa katika maeneo ya kaskazini ya Mkoa wa Khyber Pakhtunkhwa, haswa huko Boner na maeneo ya jirani, ambapo mamia ya watu walipoteza maisha yao na nyumba, mifugo, mali na magari yalisombwa, mawimbi mapya ya mafuriko sasa yanapita kupitia Mkoa wa Punjab, kuelekea Mkoa wa Sindh. Hapo awali, mvua kubwa pia ilikumba Karachi. Tunamuomba Mwenyezi Mungu, Subhaanahu wa Ta’ala, atupe salama na afya, kwani utabiri wa mvua zaidi bado upo, huku watawala wetu hawajachukua hatua yoyote isipokuwa kuinua mikono yao na kuachia jambo hilo lote kwa mfumo wa kimataifa! Wanatoa suala zima kana kwamba ni mabadiliko ya hali ya hewa tu ambayo yako nje kabisa ya matakwa yao, na kwamba ikiwa mfumo wa kimataifa hautaingilia kati, wataachwa bila msaada, kana kwamba kulinda maisha na mali za watu sio jukumu lao bali ni jukumu la mfumo wa kimataifa!

Ama kwa watawala hawa, mateso ya mamilioni ya watu ni fursa mpya tu ya kukusanya sadaka na misaada kutoka sehemu mbalimbali za dunia chini ya kivuli cha "msaada"; pesa ambazo huishia katika hazina zao. Katika muongo uliopita, Pakistan imepokea kati ya dola bilioni 1.4 na 2 kila mwaka kama "ufadhili wa hali ya hewa". Hasa baada ya mafuriko ya 2020, ambapo Pakistan ilipokea dola bilioni 4 mwaka 2021. Tayari imewasilisha madai kwa mfumo wa kimataifa kwa ufadhili wa hali ya hewa ambao ni mara nane zaidi ya kile inachopokea sasa, ikiwa ni pamoja na dola bilioni 1 chini ya jina la "Kituo cha Ustahimilivu na Uendelevu" cha Shirika la Fedha la Kimataifa kilichotengwa kwa ajili ya kukabiliana na hali ya hewa na usimamizi wa hatari za maafa. Mnamo Januari 9, 2023, Mkutano wa Kimataifa wa Pakistan ya Kukabiliana na Hali ya Hewa ulifanyika Geneva, ambapo ahadi zilikatwa zinazozidi ombi la Pakistan la dola bilioni 8, lakini hadi leo ni chini ya 20% tu ndio imetimia. Kwa hivyo, badala ya kuchukua jukumu la kushughulikia mzozo huo, watawala wamehamisha mzigo kwa mfumo wa kimataifa, na wakajitosheleza kwa kuhamisha sehemu ya pesa zinazoingia kwenye hazina zao za kibinafsi.

Suala hili halizuiliwi tu kwa mafuriko, lakini linaonyesha maono ya kudumu ya watawala hawa, walioshawishika kwamba suluhisho la matatizo yetu liko mikononi mwa mfumo wa kimataifa, na kwamba bila wao hatuna nguvu wala uwezo wa kutatua matatizo yetu. Watawala wetu na watunga sera wanaangalia kwa mshangao mifumo ya kufanya maamuzi ya Magharibi na wanaona kushikamana nayo kama kigezo cha maendeleo, ustaarabu na taaluma, na wengi wao wamefundishwa moja kwa moja mikononi mwao. "Maono" haya haswa ndiyo yanayopa mataifa makuu njia ya kuingilia masuala yetu na kulazimisha ajenda zao kulingana na sera zao. Iwe kwa kuachia suala la Kashmir kwa Umoja wa Mataifa, au kumkabidhi Benki ya Dunia kutekeleza Mkataba wa Maji wa Indus, hii ni matokeo ya maono haya. Iwe ni nakisi ya akaunti ya sasa, au nakisi ya mapato ya serikali, au mzozo wa nishati, watawala wetu - kulingana na maono haya - wameweka ajenda na maagizo ya Shirika la Fedha la Kimataifa. Na kwa sababu ya maono haya haya, haki za makundi mbalimbali ya jamii zinaundwa kulingana na ajenda za Ulaya na Amerika, ambayo inazusha maandamano ya mara kwa mara kutoka kwa watu wa Pakistan. Hata katika taasisi muhimu zaidi za serikali, uingiliaji unafanyika chini ya jina la "mageuzi ya taasisi", kwa maagizo kutoka Benki ya Dunia au Benki ya Maendeleo ya Asia. Ama sera za kijeshi na ulinzi za Pakistan, mizozo ya mpaka, au mkakati kuelekea Afghanistan, zinasimamiwa moja kwa moja na Pentagon, Kamandi Kuu ya Marekani na Wizara ya Mambo ya Nje, huku watawala wetu wakisalia kuwa waaminifu kwao daima. Kama matokeo ya maono haya, uhuru wetu umekuwa tegemezi kwa mfumo wa kimataifa. Na cha kushangaza ni kwamba watawala hawa, kutokana na maono haya ya utumwa, wanajaribu kuficha kushindwa kwao kutatua masuala ya kitaifa kwa kusema "hili ni kadari ya Mungu"! Laiti wangekuwa na ujasiri wa kimaadili wa kukiri kushindwa kwao!

Ama katika Uislamu, Khalifa anawajibika kulinda mambo yote ya watu, na hairuhusiwi yeye kukabidhi jambo lolote katika mambo ya Waislamu kwa mamlaka ya ukafiri. Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, amesema katika Kitabu chake Kitukufu: ﴿WALA HATAWAJAALIA ALLAH MAKAFIRI KUWA NA NJIA YA KUWASHINDA WAUMINI﴾, na aya hii inawataka Waislamu waziwazi kutowezesha makafiri kuwa na mamlaka yoyote juu ya mambo yao, na inaharamisha hilo kabisa. Hakika Khalifa atakataa maono haya ya utumwa na atachukua jukumu la moja kwa moja kwa mambo yote ya Waislamu. Kwa mujibu wa nyaraka za sasa za bajeti, Pakistan inalipa Rupia trilioni 8.2 kama malipo ya riba. Khalifa atasimamisha matumizi ya nafasi hii ya kifedha katika benki kama hizo zilizoharamishwa na zisizo halali, na badala yake atazielekeza kwenye miradi ya muda mrefu ya kulinda maisha na mali za Waislamu kutokana na mafuriko na migogoro mingine. Bila kuondoa watawala hawa, na kung'oa maono ya saratani ya utegemezi ambayo wanawakilisha, hakuna njia ya ukombozi kwa Waislamu wa Pakistan.

Ofisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Katika Wilaya ya Pakistan

Official Statement

الباكستان مكتب

ولاية باكستان

الباكستان مكتب

Media Contact

الباكستان مكتب

Phone:

Email: HTmediaPAK@gmail.com

الباكستان مكتب

Twitter: http://twitter.com/HTmediaPAK

Tel: | HTmediaPAK@gmail.com

http://www.hizb-pakistan.com/

Reference: PR-01990a69-a600-7753-8c70-8602959b4935