Organization Logo

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707

spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Jimbo la Sudan Wakutana na Mkurugenzi wa Idara ya Khalawi na Misikiti katika mji wa Port Sudan
Press Release

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Jimbo la Sudan Wakutana na Mkurugenzi wa Idara ya Khalawi na Misikiti katika mji wa Port Sudan

September 10, 2025
Location

Habari kwa Vyombo vya Habari

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Jimbo la Sudan

Wakutana na Mkurugenzi wa Idara ya Khalawi na Misikiti katika mji wa Port Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Jimbo la Sudan, chini ya uongozi wa Ustadhi Nasser Reda, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Sudan, akiambatana na Ustadhi Abdullah Ismail, mwanachama wa Kamati ya Mawasiliano, walimtembelea Sheikh Onour Muhammad Ahmed, Mkurugenzi wa Idara ya Khalawi na Misikiti katika mji wa Port Sudan ofisini kwake, kama sehemu ya kampeni inayoandaliwa na chama, ili kukwamisha mpango wa kuigawa Sudan kwa kutenganisha Darfur.

Ustadhi Nasser alizungumzia yanayoendelea sasa Sudan mikononi mwa Magharibi makafiri, hasa Amerika; ambayo ilitenganisha kusini mwa Sudan, na sasa inajitahidi kutenganisha Darfur, kisha hatua inayofuata ni mashariki mwa Sudan. Jambo hili ni miongoni mwa mambo muhimu, na masuala ya hatima, hakuna uzembe ndani yake, na linahitaji kutoka kwa maimamu wa misikiti, na wanasiasa, na wasomi, na viongozi wa jeshi, na watu kwa ujumla, kufanya kazi kwa bidii ili kukwamisha mpango huu. Nasser alitoa ushahidi kadhaa unaothibitisha aliyoyasema.

Sheikh Onour alikubaliana na mazungumzo ya Nasser na akasema, jukumu letu ni lipi? Ustadhi Nasser alimueleza kinachotakiwa kutoka kwa maimamu na walinganiaji, hivyo Sheikh alimtaka amtumie programu ya chama ya kukwamisha mpango mzima.

Mkutano huo ulihudhuriwa na Naibu Mkurugenzi wa ofisi, na Sheikh Labab, mwanachama wa Baraza la Maulamaa wa Jimbo, na Sheikh Al-Tayeb Al-Shambali, Mkurugenzi wa Masuala ya Wahifadhi katika jimbo la Bahari Nyekundu.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)

Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir

Katika Jimbo la Sudan

Official Statement

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

السودان - مكتب - ناطق

Media Contact

السودان - مكتب - ناطق

Phone: 0912240143- 0912377707

Email: spokman_sd@dbzmail.com

السودان - مكتب - ناطق

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707 | spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Reference: PR-01992e16-d3c0-733b-a756-e69a6e918b41