
13/6/2025
Wakala wa Habari: Hizb ut-Tahrir: Hakitaacha kuenea kwa wanamgambo na majeshi sambamba isipokuwa Ukhalifa Rashidah kwa njia ya Utume
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Hakitaacha kuenea kwa wanamgambo na majeshi sambamba isipokuwa Ukhalifa Rashidah kwa njia ya Utume
Kongamano la Tementai limetangaza muungano wa kijeshi unaoitwa Kikosi cha Pamoja cha harakati za mashariki mwa Sudan, ambacho kinajumuisha vikosi vya Kongamano la Beja, Uongozi Mkuu, unaoongozwa na Muhammad Tahir, vikosi vya Orta ya Mashariki, vinavyoongozwa na Kamanda Al-Amin Daoud, na Upinzani wa Watu, na Wanahamasishaji, wakiongozwa na Al-Nadhir Turk. Tangazo hili linakuja katika mazingira ya vita ambavyo visingekuwepo bila kuwepo kwa jeshi sambamba na jeshi la serikali; Vikosi vya Msaada wa Haraka, vita hivi ambavyo vimeharibu kila kitu, vimeharibu miundombinu, vimefukuza watu, vimekiuka heshima, na kuua maelfu ya raia wasio na hatia kwa damu baridi, baada ya yote yaliyotokea, na bado yanaendelea kutokea, serikali bado inafumbia macho kuibuka kwa majeshi mapya, badala yake inatumia baadhi yao, ambayo inahimiza kila mtu kuanzisha wanamgambo na jeshi sambamba na jeshi la serikali, na mbaya zaidi ni kwamba majeshi haya yanayozozana yote yameanzishwa chini ya bendera za upofu, ama za kikanda, au za kikabila, na ingawa kuwepo kwake kuna maana ya uharibifu wa nchi, na kupoteza nguvu zake, na kuitayarisha kwa mgawanyiko na utengano unaotakikana na Magharibi kafiri mkoloni ambaye alianza kwa kutenganisha kusini mwa Sudan, na sasa anajitahidi kwa hatua za haraka kutenganisha Darfur.
Mazungumzo kuhusu vikosi vya pamoja katika mashariki mwa Sudan, ambavyo ni vikosi vya kikanda, inamaanisha kuiweka mashariki mwa Sudan kwenye mashine ya kutengana.
Ama kwa upande wa kisheria, haijuzu kwa dola kuwa na majeshi mawili, achilia mbali kuwepo majeshi yanayotegemea ushabiki wa kikabila, au kikanda, Mtume ﷺ anasema: «Na yeyote anayepigana chini ya bendera ya upofu, anakasirika kwa ajili ya ushabiki, au anatoa wito wa ushabiki, au anashinda ushabiki, kisha akauawa, basi kifo chake ni cha kijahiliya».
Na Hizb ut-Tahrir imeeleza katika rasimu ya katiba ya dola ya Khilafah umoja wa jeshi, ambapo imekuja katika kifungu cha 66 cha rasimu ya katiba ya dola ya Khilafah: (Jeshi lote linafanywa kuwa jeshi moja ambalo linawekwa katika kambi maalum, isipokuwa kwamba baadhi ya kambi hizi lazima ziwekwe katika majimbo mbalimbali na baadhi yao katika maeneo ya kimkakati, na baadhi yao yanafanywa kuwa kambi za kusafiri zinazosafiri daima ambazo ni vikosi vya kupiga, na kambi hizi zimepangwa katika makundi mbalimbali, kila kundi linaitwa jeshi, na huwekwa nambari na kuitwa Jeshi la Kwanza, Jeshi la Tatu, kwa mfano, au linaitwa kwa jina la jimbo mojawapo au wilaya mojawapo).
Sisi katika Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, tunasisitiza kwamba kuanzisha harakati za silaha na wanamgambo wa kikabila au kikanda hakihudumii chochote isipokuwa mpango wa kafiri mkoloni anayetaka kuivunja Sudan na kuitenganisha.
Kwa hiyo, tunawaomba wenye akili timamu kutoka Sudan kufanya kazi ya kukata njia kwa mipango ya kafiri mkoloni na vibaraka wake ndani, kwa kufanya kazi kwa bidii na Hizb ut-Tahrir; kiongozi ambaye hasemi uongo kwa watu wake, ili kusimamisha Ukhalifa Rashidah kwa njia ya Utume, ambayo inaunganisha nchi na kuondoa machafuko haya yote, bali inajitahidi kuunganisha na nchi nyingine za Waislamu.
﴿Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuombeni kwa lile linalo kuhuishieni﴾
Alhamisi 16 Dhul-Hijjah 1446 AH
2025/6/12 BK
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan
Chanzo: Wakala wa Habari

