Risala ya rambirambi kwa mbeba da'wa
Mzee Bashir Qasila
﴿Miongoni mwa Waumini wapo watu waliosadiki ahadi waliyo ahidiana na Mwenyezi Mungu. Basi wapo kati yao walio kwisha timiza nadhiri yao,
na wengine wanangojea, wala hawakubadilisha (ahadi) hata kidogo﴾
Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Tunisia inamtangazia msiba wa mmoja wa wanaume wake kutoka kwa wabebaji da'wa, ami na ndugu simba wa da'wa Bashir Qasila, ambaye amefariki, siku ya Jumapili tarehe ishirini na sita ya Dhul-Hijjah 1446 Hijria, sawia na 2025/06/22 Miladia, baada ya kuugua, ugonjwa uliomlemaa mwili wake lakini haukuzima mwenge wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi katika safu za wafanyakazi wa kurejesha maisha ya Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume, na alikutana na giza la magereza na kubanwa katika riziki kwa sababu hiyo.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu amkubali miongoni mwa wema, na atukuke daraja yake katika waliyo juu, na awape ahli zake, jamaa zake na wapenzi wake subira, uthabiti na thawabu.
﴿Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye ndio marejeo yetu﴾
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Katika Jimbo la Tunisia