Taarifa ya msiba wa mbeba da'wa Saleh bin Muhammad Al-Shafra
﴿Miongoni mwa Waumini wapo watu walio sadikisha waliyo ahidiana na Mwenyezi Mungu. Basi wapo walio kwisha timiza nadhiri yao,
na wapo wanangojea, wala hawakubadilisha (ahadi yao) hata kidogo﴾
Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Tunisia inamtangazia msiba mmoja wa vijana wake, ndugu Saleh bin Muhammad Al-Shafra, ambaye amefariki dunia siku ya Jumamosi tarehe Ishirini na Moja Rabi'ul Awwal 1447 Hijria, inayolingana na 2025/09/13 Miladia, ambaye ni miongoni mwa vijana wa Hizb ut-Tahrir wa eneo la Qairouan, alifanya kazi katika safu zake katika nyakati ngumu zaidi za ukandamizaji na uonevu, na alikuwa akishikamana na da'wa yake na kujitolea katika kuibeba, akiitolea wito Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume, akiamini ahadi ya Mola wake Mwenyezi na Mtukufu, na bishara ya Mtume wake Mtukufu ﷺ, mpaka umauti ulipomfika, hivyo ndivyo tunavyomuhesabu na hatumtakasi yeyote mbele ya Mwenyezi Mungu.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu Mtukufu amkubali katika watu wema, na ainue daraja yake katika daraja za juu, na awape familia yake, jamaa zake na wapenzi wake, subira, uthabiti na hesabu.
﴿Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye tutarejea﴾
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Katika Jimbo la Tunisia