Organization Logo

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707

spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Enyi watu wa Sudan, mna uwezo wa kufeli mpango wa kulichuna Darfur, basi simameni kumtii Mwenyezi Mungu!
Press Release

Enyi watu wa Sudan, mna uwezo wa kufeli mpango wa kulichuna Darfur, basi simameni kumtii Mwenyezi Mungu!

September 02, 2025
Location

Taarifa kwa vyombo vya habari

Enyi watu wa Sudan, mna uwezo wa kufeli mpango wa kulichuna Darfur, basi simameni kumtii Mwenyezi Mungu!

Katika hatua iliyotarajiwa, kiongozi wa vikosi vya msaada wa haraka, Muhammad Hamdan Daglo, ameapa kiapo cha katiba kama rais wa baraza la urais la kile kinachoitwa serikali sambamba, huko Nyala, mji mkuu wa kusini mwa Darfur, Jumamosi, 2025/8/30, na pia ameapa makamu wa rais, wajumbe wa baraza la urais, na waziri mkuu.

Hatua hii ilitarajiwa kama sehemu ya mpango wa uhalifu wa Marekani, unaolenga kuitenga Darfur, kwa njia ya vibaraka wake kutoka kwa viongozi wa jeshi, viongozi wa vikosi vya msaada wa haraka, na mamluki wa siasa.

Hatua hii imekuja kwa kasi, kufuatia mkutano wa Burhan na mshauri wa rais wa Marekani, Massad Boulos huko Zurich, Uswizi, ambayo imeharakisha hatua hiyo kabla ya kuanguka kwa Fashir.

Kutokana na uhalifu huu hatari, mitazamo ya watu wa Sudan imekuwa tofauti katika makundi yao mbalimbali, kama ifuatavyo:

- Wanaoharakisha utekelezaji wa mpango, na wanaoutekeleza, wakitamani kile kilicho kwa Marekani, na hawa lazima wazuiliwe, na wazuiwe kutekeleza uhalifu huu mkuu.

- Wavunjika moyo ambao wanawataka watu kukubaliana na hali halisi, kana kwamba kujitenga kwa Darfur ni hatima isiyoepukika ambayo lazima ikubaliwe! Na hawa ni pamoja na wanasiasa, wanahabari, na wengineo, na hatari yao inadhihirika wanapoamilika na kueneza kukata tamaa kwa wengine, na hawa lazima wazuiliwe na kuelekezwa kwa vipengele vya nguvu ambavyo vinawawezesha kushindwa mpango huo.

- Kundi ambalo halijali kinachoendelea kana kwamba kinachotokea kiko katika sayari nyingine! Kwa sababu hawajui kinachoendelea karibu nao, na hawa lazima waelimishwe na nguvu zao zihamasishwe kushindwa mpango huo.

- Jamii ambayo imefunuliwa na mpango huo, na inatarajia matukio na kuona kile kilicho nyuma ya ukuta, na hii inafaa kuunganisha usiku na mchana, na kuhamasisha nguvu za makundi yote, sio tu kushindwa mpango wa kuigawanya Sudan na kulichuna Darfur, lakini kwa ajili ya kuunda upya maisha, kupindua meza, na kuhamisha umma wetu kutoka kuwa lengo la njama za Magharibi kafiri na miradi yake ya uhalifu, hadi kuwa mbeba miali ya uongofu na nuru kwa Magharibi hii kafiri, na katika pande zote za ulimwengu.

Sisi katika Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Sudan, tulikuwa, na bado tunaendelea kuwa mwonya wazi, ambaye anafichua njama, na anazidisha juhudi za kushindwa mipango ya uhalifu.

Enyi watu wa Sudan: Mna uwezo wa kufeli mpango huu unaolenga kuipasua nchi yenu katika toleo lake la pili, ambalo linalenga kuitenga Darfur, ikiwa mngemtegemea Mwenyezi Mungu kwa utegemezi wa kweli, na kumwomba Yeye Mtukufu msaada, na kufanya yafuatayo:

* Kujitenga na kila kibaraka msaliti, ambaye amejitwika jukumu la kutekeleza mpango huu, kwa kuunda serikali sambamba, au kwa ulegevu na kuikabidhi Fashir ili vikosi vya msaada wa haraka vikamilishe udhibiti wake wa mkoa wote wa Darfur.

* Kuhamasisha nguvu za watu waaminifu kutoka kwa watu wa nguvu na ulinzi, ili kushindwa mpango huo na kuwazuia mawakala na wasaliti.

* Kuhamasisha nguvu zote za vyombo vya habari, majukwaa ya misikiti, na mengineyo ili kufichua mpango huo, na zana za utekelezaji wake ndani, na kuhamasisha watu kusimama kidete kuukabili.

* Kuhamasisha nguvu za watu waaminifu, wasiohusika na wasaliti, kutoka kwa viongozi wa makabila, viongozi wa koo, wasomi, wenye maoni, viongozi, wanasiasa, wanasheria, na watu wote mashuhuri, kuunda ukuta imara ambao unalinda umoja wa kile kilichosalia cha nchi yetu.

Je, haya yote kwa pamoja si nguvu kubwa, inayoweza kushindwa mpango wa Marekani, ambao ni hila ya shetani, ﴿Hakika hila za shetani ni dhaifu﴾, ﴿Wanapanga mipango, na Mwenyezi Mungu anapanga mipango, na Mwenyezi Mungu ni mbora wa wapangaji﴾, na Mtume ﷺ anasema: «Hakika yeyote atakayeishi miongoni mwenu baada yangu ataona tofauti nyingi, basi shikamaneni na sunna zangu na sunna za makhalifa waongofu waongozaji, shikamaneni nayo na ishikilieni kwa meno ya magego». Imesimuliwa na Al-Irbadh bin Sariyah Radhi za Allah ziwe juu yake, na ameitoa Abu Daud, Tirmidhi, Ahmad na Ibn Hibban.

Ibrahim Othman (Abu Khalil)

Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir

Katika Wilaya ya Sudan

Official Statement

السودان - مكتب - ناطق

ولاية السودان

السودان - مكتب - ناطق

Media Contact

السودان - مكتب - ناطق

Phone: 0912240143- 0912377707

Email: spokman_sd@dbzmail.com

السودان - مكتب - ناطق

الخرطوم شرق- عمارة الوقف الطابق الأرضي -شارع 21 اكتوبر- غرب شارع المك نمر

Tel: 0912240143- 0912377707 | spokman_sd@dbzmail.com

www.hizb-ut-tahrir.info

Reference: PR-01990a6f-2440-7a4e-87ac-7a67b76b525f