Organization Logo

مصر - المكتب

ولاية مصر

Tel:

info@hizb.net

www.hizb.net

Enyi Wanajeshi wa Kinana: Vituo vya Gaza havitaji malori bali vinahitaji majeshi na magari ya kivita
Press Release

Enyi Wanajeshi wa Kinana: Vituo vya Gaza havitaji malori bali vinahitaji majeshi na magari ya kivita

September 28, 2025
Location

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Enyi Wanajeshi wa Kinana: Vituo vya Gaza havitaji malori bali vinahitaji majeshi na magari ya kivita

Hali ya kibinadamu huko Gaza imefikia kiwango cha janga lisilo la kawaida; ambapo idadi ya mashahidi imezidi mashahidi elfu 65, na kuna ripoti za kimataifa zinazosema kwamba idadi hiyo ni zaidi ya hiyo kwa 40%, ambayo ni zaidi ya mashahidi 100,000, na takriban wakimbizi wa ndani milioni 1.9, ambayo ni sawa na 90% ya wakazi wa Ukanda huo, wanaishi katika hali zisizo za kibinadamu, wakiwa wamenyimwa mahitaji ya msingi ya maisha, kwani Gaza ina njaa halisi, haswa kaskazini mwa Ukanda huo. Ama hospitali zinafanya kazi chini ya 30% ya uwezo wake, na uhaba wa dawa na mafuta unawafanya makumi elfu ya wagonjwa kuwa katika hatari ya kifo cha polepole. Takwimu hizi zinafunua ukubwa wa janga na zinathibitisha kwamba kinachotokea ni vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Waislamu huko Gaza.

Sisi anasema kwamba kufungua vivuko kwa nguvu kunamaanisha kuingia katika mzozo na mataifa makubwa, akakataa kualikwa na mtu yeyote kuingia katika mzozo kwa ajili ya watu wa Gaza, akidai kwamba hataki kuingiza Misri na watu wake katika vita vipya! Wakati kwa hakika anazingira Gaza na watu wake, na kama angeweza, angewazuia hata hewa wanayopumua, na yeye ndiye yule yule aliyepoteza gesi ya Misri na maji ya Mto wake wa Naili na kuifunga kwa mikopo, mikataba na makubaliano ambayo inaiweka chini ya utegemezi kwa miongo ijayo, na hakuna dalili bora zaidi ya hii kuliko ishara ya mfumo wake kwa lengo la kupunguza deni hadi 55% mwaka 2050, katika dharau dhahiri kwa Misri na watu wake.

Tatizo la msingi sio ukubwa wa misaada na mifumo ya kuiingiza, lakini ni kutokuwepo kwa taasisi ya kisiasa ya kimsingi ambayo inaongoza Umma kwa msingi wa Uislamu, inaunganisha nguvu zake, na inaweka uwezo wake katika kukabiliana na adui yake. Umma umeishi karne kumi na tatu chini ya Khilafah, na hakuna adui aliyekalia hata shubiri moja ya ardhi yake isipokuwa alisimama kuirejesha. Na leo, baada ya kutokuwepo kwake, Palestina imekuwa mateka wa kugawanyika na tawala tegemezi, na watu wake wanaomba msaada lakini hakuna anayewajibu!

Wanazuoni wa Umma wamekubaliana kuwa kuwasaidia Waislamu waliodhoofishwa ni wajibu, Imam Shafi'i alisema: "Ikiwa adui atatua katika uwanja wa Waislamu, ni wajibu kwa kila mtu anayeweza kutoka kupigana naye." Na Ibn Qudamah alisema katika al-Mughni: "Ikiwa adui atashambulia nchi, ni wajibu kwa watu wake kumlinda, na jihad inakuwa wajibu wa kibinafsi wakati huo." Hiyo ni kusema, kuwatetea watu wa Gaza ni wajibu mkubwa kwa Umma wote, na ni jambo la muhimu zaidi kwa nchi zinazozunguka na hasa Misri.

Kauli ya Sisi kwamba kuingiza misaada kwa watu wa Gaza hakufanyiki ila kwa uratibu na Mayahudi ni utetezi usio na thamani. Je, mshambulizi anafanywaje kuwa mpinzani na hakimu kwa wakati mmoja?! Sheria haikubali kwamba adui wa Umma aombwe ruhusa ya kupitisha dawa au chakula kwa watoto wa Waislamu. Bali wajibu ni kuondoa vivuko na kile kilicho kati ya Misri na Gaza cha mipaka, kuta na waya, na kwamba uwezo wa Umma uelekezwe kuwasaidia watu wa Gaza, sio kuwapa uhalali Mayahudi ambao wanadhibiti kipande chao cha mkate na tone la dawa!

Enyi watiifu katika majeshi ya Umma kwa ujumla na jeshi la Misri haswa: Damu ya watoto wa Gaza, heshima ya wanawake wake na vipande vya miili ya wanaume wake ni amana katika shingo zenu. Na Mungu atawauliza Siku ya Kiyama: Mlifanya nini kuwasaidia ndugu zenu? Hamna udhuru wa kumiliki nguvu na vifaa kisha mkaacha vimeganda ilhali ndugu zenu wanaomba msaada na kuomba msaada wenu. Wajibu wenu ni kuutetea dini ya Mwenyezi Mungu na kuunga mkono Umma wenu, ili muangushe minyororo ambayo wakoloni wamewafunga nayo, na muweke silaha zenu pale panapostahili: katika kukabiliana na adui wa Mwenyezi Mungu na adui yenu. Na mjue kwamba Umma uko pamoja nanyi, na Mungu atawasaidia ikiwa mtakuwa wakweli kwake, ﴿Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, Yeye atakunusuruni na atawathibitisha nyayo zenu.

Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Katika Wilaya ya Misri

Official Statement

مصر - المكتب

ولاية مصر

مصر - المكتب

Media Contact

مصر - المكتب

Phone:

Email: info@hizb.net

مصر - المكتب

Tel: | info@hizb.net

www.hizb.net

Reference: PR-0199900d-de20-7792-ab96-60ae35573348