Organization Logo

فلسطين المنطقة

الأرض المباركة فلسطين

Tel:

Ee, kwa ajili ya ujasiri wa Kiislamu katika umma wa Muhammad ﷺ! Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «SIYO MWENYE KUAMINI YULE ANALALA ASHIKI NA JIRANI YAKE ANA Njaa PEMBENI YAKE» Imesimuliwa na Al-Hakim Miti na mawe yamenena kutokana na ukubwa wa yaliyotufika; vifua vyetu vinatoa damu na uchungu, watoto wetu wanajikunyata kwa njaa na kiu, wanawake wetu wanaomba msaada.
Press Release

Ee, kwa ajili ya ujasiri wa Kiislamu katika umma wa Muhammad ﷺ! Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «SIYO MWENYE KUAMINI YULE ANALALA ASHIKI NA JIRANI YAKE ANA Njaa PEMBENI YAKE» Imesimuliwa na Al-Hakim Miti na mawe yamenena kutokana na ukubwa wa yaliyotufika; vifua vyetu vinatoa damu na uchungu, watoto wetu wanajikunyata kwa njaa na kiu, wanawake wetu wanaomba msaada.

July 23, 2025
Location

Ee, kwa ajili ya ujasiri wa Kiislamu katika umma wa Muhammad ﷺ!

Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «SIYO MWENYE KUAMINI YULE ANALALA ASHIKI NA JIRANI YAKE ANA Njaa PEMBENI YAKE» Imesimuliwa na Al-Hakim

Miti na mawe yamenena kutokana na ukubwa wa yaliyotufika; vifua vyetu vinatoa damu na uchungu, watoto wetu wanajikunyata kwa njaa na kiu, wanawake wetu wanaomba msaada wa waja wenye imani. Yule asiyekufa kwa makombora atakufa kwa njaa na kiu. Ama uchungu wa kukataliwa ni mbaya zaidi kwetu kuliko makombora, njaa na kiu. Ndugu zenu huko Gaza wanazurura bila makazi, na sauti zao zimekatika kwa udhaifu wa njaa na kiu, baada ya kukata tamaa ya kuokolewa na mtu yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu, wanaita: Uko wapi umma wa Kiislamu? Uko wapi ujasiri wa dini? Uko wapi msaada wa waumini?

Na kinacho umiza moyo ni "mitego ya mauti", vituo vile ambavyo vimeitwa kwa uongo "vituo vya kibinadamu", watu wa Gaza wanaenda huko huku wakijua kwamba wanaenda kwenye mauti, lakini njaa ya watoto wao na familia zao inawasukuma kuelekea kwenye mauti wakitumaini kupata unga kidogo hata kama rangi yake itabadilika kuwa nyekundu kwa damu yao!

Enyi Waislamu:

Je, watoto wa Gaza wanawadhalilisha wanapokufa kifo cha polepole mbele ya macho ya baba zao na mama zao huku hawawezi kufanya lolote isipokuwa kumwaga machozi na kumeza majuto?!

Je, nafsi zenu zimefurahishwa na matukio ya mauaji na ukatili?! Au umeridhika na usaliti wa watawala wako ambao wamefanya hatima yako na hatima ya umma wako mikononi mwa Amerika na Wayahudi?! Au unakubali kuuliwa, kufukuzwa na kuondolewa kutoka katika nchi yetu na Amerika na Wayahudi?!

Je, kuna usaliti mkuu zaidi kuliko kufanya hatima ya watu wa Gaza itegemee uamuzi wa Trump au Netanyahu?!

Je, kuna kukataliwa kukubwa zaidi kuliko kuwaacha watu wako na ndugu zako wachinjwe, wafe kwa njaa na kiu huku mna uwezo wa kuwasaidia?!

Je, kuna uhalifu mkubwa zaidi kuliko kubaki kwa majeshi katika kambi zao na ndege na maroketi katika sehemu zao, na maadui wa Mungu "waliokasirikiwa" wanalichafua Msikiti wa Al-Aqsa na kuruhusu damu yetu na heshima yetu?!

Huo ni udanganyifu wa kutokuwa na uwezo ambao watawala vibaraka wameupanda katika umma, mpaka majeshi ya umma, wanazuoni na watu wa kawaida wameukubali. Je, kweli jeshi la Misri linashindwa kupeleka maji kwa watu wake na jamaa zake?! Je, kweli mashujaa wa jeshi la Jordan wanashindwa kufungua mipaka na kusonga mbele kuukomboa Msikiti wa Al-Aqsa?! Je, kweli jeshi la Pakistani la Mujahidina linashindwa kuushambulia utawala wa waliokasirikiwa kwa makombora ambayo yanawafanya kama majani yaliyoliwa?!

Na vipi kuhusu majeshi ya Uturuki, Iraq, Hijaz, Algeria... nk? Je, wanashindwa kuvunja mipaka na kuokoa Palestina na mahali alipoenda Mtume wa Mungu ?!

Ole kwa umma wa Kiislamu, ikiwa wangenyanyuka na kwenda Gaza na ardhi iliyobarikiwa kama vile makabila yalivyokwenda Suwayda ya Sham kulinda watoto wao na heshima yao, "waliokasirikiwa" wangegeuka na kukimbia kwa hofu kwamba kisasi cha umma wa Kiislamu kitawapata.

Enyi umma wa Kiislamu, enyi umma bora uliotolewa kwa watu:

Mseme kweli kwa Mwenyezi Mungu katika imani yenu, semeni kweli kwa Mwenyezi Mungu katika msaada wenu, semeni kweli kwa Mwenyezi Mungu katika misimamo yenu, kwa maana mnajua kuwa hakuna njia ya kusimamisha dini yenu, kuwasaidia ndugu zenu, na kuukomboa Al-Aqsa wenu, isipokuwa kwa kuangusha viti vya enzi vya watawala wenu waoga vibaraka, kuvunja mipaka na kusonga mbele kuelekea Msikiti wa Al-Aqsa.

Na kwa hivyo, hakuna kilichobaki kwa umma wa Kiislamu isipokuwa kuazimia na kuhamasisha jeshi lake, na kuangusha viti vya enzi ambavyo vimeweka Gaza katika njaa pamoja na Wayahudi na Wamarekani, hakuna kilichobaki kwa umma wa Kiislamu isipokuwa kuitikia wito wa Mwenyezi Mungu: ﴿ENYI MLIO AMINI! MNA NINI, MKIAMBIWA: NENDENI KATIKA NJIA YA MWENYEZI MUNGU, MNAZIDI KUELEKEA ARDHINI? JE! MERIDHIKA NA UHAI WA DUNIA BADALA YA AKHERA? BASI VITU VYA KUJIFURAHISHA KATIKA UHAI WA DUNIA SI KITU, VILINGANISHWA NA AKHERA, ILA NI KIDOGO. MSIPOENDA VITANI ATAWAADHIBU ADHABU IUMIZAYO, NA ATAWALETA WATU WENGINE BADALA YENU, WALA HAMTAMDHURU CHOCHOTE. NA MWENYEZI MUNGU NI MWENYE UWEZO WA KILA KITU﴾.

Ewe Mwenyezi Mungu, tunakulalamikia udhaifu wa nguvu zetu, uchache wa hila zetu, na udhaifu wetu kwa watu, Ewe Mwenye kurehemu kuliko wote wenye kurehemu, Wewe ndiye Mola wa wanyonge, na Wewe ndiye Mola wetu, unatuachia nani? Kwa mtu wa mbali anayetukunjia uso au kwa adui ambaye umemmilikisha jambo letu? Ikiwa hasira yako haiko juu yetu, hatujali, lakini afya yako ni pana zaidi kwetu, tunajikinga kwa nuru ya uso wako ambayo giza limeangazwa, na jambo la ulimwengu huu na Akhera limetengenezwa juu yake, ili ghadhabu yako isitushukie, au hasira yako itufikie, kwako wewe ni kuridhika mpaka uridhike, na hakuna uwezo wala nguvu isipokuwa kwako.

Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu.

Official Statement

فلسطين المنطقة

الأرض المباركة فلسطين

فلسطين المنطقة

Media Contact

فلسطين المنطقة

Phone:

Email:

فلسطين المنطقة

Tel: |

Reference: PR-01982527-c4a0-7443-96c7-141a0c48ccf7