Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Ziara za Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Lebanon kwa Wabunge
Delegeshani kutoka Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Lebanon, iliyoandaliwa na Dkt. Muhammad Jabir na Mhandisi Saleh Salam, kama sehemu ya kampeni yake ya kuwatembelea wabunge, ilimtembelea Mbunge Dkt. Emad Al-Hout huko Beirut kwa takriban saa moja. Delegeshani ilisisitiza mambo yafuatayo, ambayo yanahitaji msimamo na hatua kutoka kwa wabunge katika Bunge la Lebanon:
1- Umuhimu wa kukabiliana na mradi wa utambuzi rasmi wa chombo cha Kiyahudi, ambacho utangulizi wake unaharakishwa miongoni mwa wanasiasa na vyombo vya habari kwa kisingizio cha shinikizo la Kimarekani, ambalo linataka kuanzishwa kwa uhusiano wa kawaida.
2- Kwamba majeshi yatekeleze wajibu wao wa kisheria wa kutumia silaha dhidi ya adui wa Ummah, Mayahudi, na viongozi katika majeshi haya wanapaswa kujua kwamba ikiwa hawatofanya hivyo, silaha zao zitachukuliwa kutoka kwao au zitaharibiwa, kwa ushirikiano wa tawala zao tawala zinazohusiana na Magharibi na kulinda chombo hicho.
3- Kila mtu lazima akae mbali na fitina za kimadhehebu na kile kinachoziunga mkono au kuzichochea kati ya Waislamu; kwa sababu hii inamtumikia adui tu, na inawagawa Waislamu ambao wanapaswa kuunganishwa na dola moja, ambayo ni dola ya Khilafah, licha ya tofauti za kimadhehebu na ijtihadi za kisiasa kati yao.
4- Umuhimu wa kupaza sauti kuhusu mradi wa dola ya Kiislamu jumuishi ambao tunauchukua, ambao ni mradi wa dola ya Khilafah, na watu wote, bungeni, katika kila mkutano wa kisiasa na katika matukio yote, na Waislamu na wasio Waislamu miongoni mwao, kama Hizb ut-Tahrir inavyofanya bila aibu yoyote, lakini kinyume chake kwa furaha na shangwe zote kwa uhakika wake kwamba ndiyo ukombozi pekee kwetu na kwa wengine kutokana na hali hii ngumu.
Mwisho wa ziara, tulikubaliana juu ya mawasiliano endelevu kwa faida ya Ummah.
Delegeshani hiyo hiyo pia ilimtembelea Mbunge Nabil Badr huko Beirut wiki iliyopita ili kujadili mambo yaleyale, na kuweka wawakilishi wa watu wa Lebanon mbele ya majukumu yao, haswa katika kuwasilisha suluhisho la msingi, na katika kuwawajibisha watawala.
Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut-Tahrir / Wilaya ya Lebanon itaendeleza mawasiliano yake na wabunge ili kuwasilisha mradi wake wa suluhisho katika siku zijazo, Mwenyezi Mungu akipenda.
Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Katika Wilaya ya Lebanon