Ukhalifa ni ahadi ya Mwenyezi Mungu ambayo haizimwi na kutokuwepo wala haikatizwi na uonevu
Katika zama ambazo majanga yanaongezeka na umma unagawanyika kati ya mifumo na katiba za kibinadamu, swali muhimu linajitokeza: Je, kuna njia ya kweli ya kutoka katika hali hii? Jibu liko wazi kwa kila anayetazama kwa uaminifu: Kwamba Ukhalifa ndio suluhisho pekee.
Ukhalifa kwa njia ya Utume si tu kauli mbiu au wazo la kufikirika; bali ni mradi kamili wa kisiasa wa kisheria ambao unategemea kwamba utawala ni wa Mwenyezi Mungu pekee, na kwamba sheria inatokana na ufunuo si matamanio ya wanadamu au maslahi ya kimataifa. Ni ule unaorejesha umoja wa kisiasa na kisheria kwa umma, na kuubadilisha kutoka mkusanyiko wa nchi zilizogawanyika zinazokabiliwa na utawala hadi kuwa chombo chenye uamuzi, ambacho kinaendesha nguvu zake za kiuchumi, kisiasa na kijeshi chini ya hati moja ya kisheria ambayo inasimamia sheria ya Mwenyezi Mungu katika nyanja zote. Katika muktadha huu, masuala ya kisasa yanatazamwa kutoka utegemezi wa kimataifa hadi upotovu wa kijamii na kiuchumi kama matokeo ya asili ya kutokuwepo kwa mamlaka kamili ya kisheria. Kwa hivyo, ni mfumo wa utawala wa kweli, wa kimungu, unaojumuisha vipengele vyote vya maisha. Vipi?
Kwanza: Kwa kutumia sheria kikamilifu
Ukhalifa unalazimisha dola kutumia sheria ya Mwenyezi Mungu katika nyanja zote: siasa, uchumi, mahakama, familia, elimu, na vyombo vya habari. Hakuna nafasi ya mgongano kati ya dini na maisha, bali dola imejengwa juu ya haki ya kimungu si juu ya matamanio ya wanadamu, hivyo basi haki na utulivu unapatikana kupitia mfumo kamili wa kimungu.
Pili: Kuunganisha Umma wa Kiislamu
Ukhalifa unaondoa mipaka bandia ambayo imewagawa Waislamu, na kuwarejesha kuwa mwili mmoja chini ya bendera moja. Hapo ndipo hali ya udhaifu na mgawanyiko inaisha, na umma unageuka kuwa nguvu ya kisiasa, kijeshi na kiuchumi inayoheshimika, ambayo haivunjwi na wala haiamrishwi.
Tatu: Kwa kujitegemea kutoka kwa Utawala wa Magharibi
Ukhalifa unakataa kujisalimisha kwa taasisi za kimataifa kama Umoja wa Mataifa na Shirika la Fedha la Kimataifa, na kuunda upya mahusiano ya kimataifa kwa msingi wa uhuru na heshima ya Kiislamu. Hakuna utegemezi wala amri, bali ni shughuli ya usawa inayotegemea kanuni: "UISLAMU UMETUKUKA, NA HAUJAJUULIWA".
Nne: Kwa haki halisi ya kiuchumi
Chini ya Ukhalifa, riba inaharamishwa, ukiritimba unazuiliwa, na mali inasambazwa kwa haki, hivyo basi haki za msingi za watu zinahakikishwa: makazi, elimu, afya, chakula, na usalama. Ni mfumo ambao unahifadhi heshima ya binadamu na kufikia usawa, si kama tunavyoona leo mapengo makali ya kitabaka na mfumo wa kibepari ambao hauwahurumii wanyonge.
Tano: Kwa kuwasaidia wanaodhulumiwa na kubeba wito kwa ulimwengu
Ukhalifa haujifungi wenyewe, bali unahamia kuwasaidia Waislamu kila mahali, na kubeba ujumbe wa Uislamu kwa ulimwengu kama wito, haki na huruma. Ni mfano wa kipekee wa kistaarabu, ambao hautafuti utawala, bali kuwatoa wanadamu kutoka katika utumwa wa wanadamu kwenda katika utumwa wa Mola wa wanadamu.
Sita: Kwa kuimarisha maadili ya Kiislamu
Kupitia elimu na vyombo vya habari, Ukhalifa huzaa vizazi vya waumini wenye ufahamu, wanaojua utambulisho wao na kujivunia dini yao, wasiyeyuke katika mikondo ya Magharibi wala kuvutiwa na uongo wa ustaarabu wa kimwili. Kwa hivyo, familia na jamii inahifadhiwa kutokana na anguko la maadili, na utambulisho wa Kiislamu unabaki imara na wenye nguvu.
Ukhalifa si ukasisi bali ni mfumo wa utawala wa kimungu, ni mfumo wa kisiasa wa kivitendo unaotegemea ufunuo, na unalenga kufikia haki, heshima na umoja, na kumfanya mtawala awajibike mbele ya Mwenyezi Mungu na umma. Chini yake, mkubwa na mdogo wanawajibishwa, na hakuna mtu aliye na kinga, kwa sababu mamlaka ndani yake ni ya sheria si ya watu binafsi.
Kinyume chake: tunaishi leo chini ya demokrasia ya Magharibi na ubepari, ambapo sheria zinatungwa na wanadamu, hubadilika kulingana na maslahi na shinikizo la kisiasa. Hakuna umma mmoja bali nchi za kitaifa zinazoimarisha mgawanyiko na uaminifu (kwa taifa) badala ya uaminifu kwa dini. Mabunge na vyama vinaendeshwa na maslahi, vinatawaliwa na mtaji au jeshi. Uchumi unategemea soko huria na riba, na maskini wanaachwa kwa hatima yao. Ama sera ya kigeni imefungamana na Magharibi, inatambua chombo cha Kiyahudi na inaratibu usalama nao. Na mfumo wa kijamii umefikia hatua ya kuhalalisha upotovu: ndoa ya kiraia, usawa katika urithi, kuzuia wake wengi... hadi familia zilipovunjika na uongozi ukapotea. Wakati Ukhalifa unarejesha maana yake halali kwa uongozi kupitia sheria ambayo inahifadhi familia na kuweka kila mwenye haki katika haki yake ndani ya mfumo wa haki ambao hauna matamanio wala ukandamizaji. Na kwa kuanzisha mfumo huu, sababu za utengano zinaanguka: kutokuwepo kwa sheria, kupoteza utambulisho, na shinikizo la kiuchumi, hivyo familia inarudi kuwa ngome imara na msingi wa kuinuka kwa umma.
Kuanzisha upya maisha ya Kiislamu kwa kuanzisha Ukhalifa kwa njia ya Utume kutasimamisha haki kati ya watu na kujitahidi kumridhisha Mwenyezi Mungu, wakati mifumo iliyopo inaendeshwa na maslahi, ushawishi na utawala, na imeleta umaskini, vita na ufisadi. Kwa hivyo tunangoja nini?
Hakika, Ukhalifa si ndoto kutoka zamani, bali ni faradhi ya kimungu na wajibu wa kisheria kwa umma kufanya kazi kwa ajili yake kama unavyofanya kwa sala na funga zake. Ni ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kuwatawaza, na kwa hayo pekee umma utarejesha heshima na utukufu wake, na utainuka kuongoza ulimwengu baada ya kupotea kwa muda mrefu na kupotea.
Ubinadamu umepotea kati ya mifumo bandia iliyoharibika ambayo imewapeleka watu katika umaskini, vita na uharibifu, na hakuna kitakachowainua isipokuwa mfumo kutoka kwa Mwenyezi Mungu, ambao unamkomboa mwanadamu kutoka katika utumwa wa wanadamu.
Na umma umefika wakati wa kutambua kwamba tatizo lake si katika watu binafsi wala katika serikali zinazofuata, bali katika mfumo wenyewe ambao unaondoa sheria ya Mwenyezi Mungu kutoka kwa utawala, na kusimamia matamanio na maslahi badala ya ufunuo. Kwa hivyo kuanzisha Ukhalifa si anasa ya kiakili, bali ni suala la hatima kwa umma mzima, na wajibu ambao unawaamsha watu huru kurejesha mamlaka ya Uislamu duniani.
Enyi umma wa Muhammad ﷺ, usisubiri muujiza, bali uutengeneze kwa kumtii Mwenyezi Mungu na kufanya kazi ya kuanzisha Ukhalifa kwa njia ya Utume, kwa sababu ni ahadi ya Mola wako, na kwa hayo pekee mamlaka itarudi kwa sheria na heshima kwa Waislamu. Hakuna wokovu kwa umma isipokuwa kwa kuvunja minyororo na kuangusha mifumo ya usaliti, na kuanzisha upya maisha ya Kiislamu kwa kuanzisha Ukhalifa kwa njia ya Utume. Utukufu wote ni katika kutumia sheria ya Mwenyezi Mungu, na yeyote anayeutafuta kwa mwingine, Mwenyezi Mungu atamfedhehesha. Umefika wakati kwa umma kutambua kwamba tatizo lake si katika watu binafsi bali katika mfumo wenyewe, na kwamba njia ya kuinuka inaanza na khalifa ambaye hamwogopi isipokuwa Mwenyezi Mungu.
Na mwisho, tunafurahia ahadi ya kweli ya Mwenyezi Mungu ambayo haitendi kinyume na miadi: ﴿Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walio amini miongoni mwenu na wakatenda mema, ya kwamba atawafanya makhalifa katika ardhi kama alivyo wafanya makhalifa wale walio kuwa kabla yao, na kwa yakini atawawezesha Dini yao aliyo wapendelea, na atawabadilishia amani baada ya khofu yao﴾.
Imeandikwa kwa Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Manal Ummu Ubaida