Kuanguka kwa Al-Fashir Kunaharakisha Mpango wa Marekani wa Kuitenga Darfur
Vikosi vya Msaada wa Haraka vilitangaza asubuhi ya Jumapili, 26/10/2025, udhibiti wao wa Al-Fashir, baada ya kuzingirwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, ambayo inamaanisha kuenea kwa ushawishi wao juu ya majimbo yote matano ya Darfur, na kugawanyika kwa nchi kati ya mashariki inayodhibitiwa na Jeshi la Sudan, na magharibi chini ya udhibiti wa Msaada wa Haraka. Inafahamika kuwa udhibiti wa Vikosi vya Msaada wa Haraka juu ya Al-Fashir ni zaidi ya ushindi katika vita dhidi ya mji, lakini ni udhibiti wa mkoa mzima kwa njia ya kushangaza.
Maendeleo haya katika eneo la tukio, kufuatia kuanguka kwa Al-Fashir baada ya kujiondoa kwa jeshi la Sudan, yaliambatana na mazungumzo yanayoendeshwa na Marekani kati ya wajumbe wa pande zote mbili, serikali na Vikosi vya Msaada wa Haraka, huko Washington kwa lengo la kusitisha mapigano. Ni wazi kwamba Marekani ndiyo iliyoamuru viongozi wa pande hizo mbili kutekeleza kuingia kwa Vikosi vya Msaada wa Haraka huko Al-Fashir, na kujiondoa kwa jeshi kutoka huko, ili kuharakisha mpango wa Marekani wa kuitenga Darfur, kama sehemu ya mpango wa kuigawanya Sudan katika mataifa madogo!
Imeelezwa katika karatasi ya Kimarekani iliyojadiliwa katika mkutano wa Rais wa zamani wa Marekani George W. Bush, na washauri wake mwanzoni mwa muhula wake wa pili mwaka 2005 kujadili karatasi ya kazi kuhusu Mashariki ya Kati, karatasi hiyo inazungumzia Sudan, na matukio matatu ya baadaye, ambayo hayakatai uwezekano wa kuigawanya Sudan katika nchi tatu kama ifuatavyo:
* Misri ina uhusiano na moja yao kaskazini.
* Na Marekani ina uhusiano wa kimkakati na nyingine kusini.
* Na chombo cha Kiyahudi kina uhusiano na dola ambayo inaweza kuzaliwa magharibi mwa Sudan (Darfur)
Mkakati na diplomasia ya Marekani iliyopendekezwa katika eneo la Mashariki ya Kati ilikuwa kwamba mawazo yanatayarishwa na kutayarishwa, kisha marais na viongozi wa nchi za Mashariki ya Kati wanaitwa Ikulu ya White House, ili kuyakubali na si kuyachunguza au kuyaweka sawa, na kinachotakiwa ni makubaliano, na viongozi wa nchi katika eneo hilo, juu ya njia bora ambayo mawazo haya ya kisiasa, au mipango ya kidiplomasia inaweza kutekelezwa kupitia mashauriano ya awali katika mfumo wa nchi mbili kisha katika mfumo wa pamoja. Hii ndiyo sera ya Marekani kwa nchi za Waislamu kwa ujumla na Sudan haswa; kuweka mipango ya kuivunja, mipaka ya damu na kufanya kazi ya kuitekeleza kupitia watawala na mazingira ya kisiasa na kuitangaza kupitia vyombo vya habari.
Kwa hiyo, amri za Marekani zilikuwa wazi kutumia kila kitu kinachowezekana kudhibiti Vikosi vya Msaada wa Haraka juu ya Al-Fashir na kuuangusha, na kwa hiyo vikosi hivi viliangamiza watu wasio na hatia na kumwaga damu nyingi katika ardhi ya Al-Fashir na miji mingine ya Sudan, huku uongozi wa jeshi ukishindwa kutekeleza wajibu wao wa kulinda Al-Fashir na watu wake na kuiacha ivamiwe na Vikosi vya Msaada wa Haraka vya wahalifu kwa njia mbaya zaidi zinazoweza kusimuliwa, na chochote kinachotolewa kutoka kwa taarifa, mazungumzo na majuto juu ya mauaji ya Al-Fashir kutoka Marekani na zana za kikanda na za ndani ni kutupa mchanga machoni kuhusu ukweli na njama iliyokubaliwa.
Kinachotakiwa kutoka kwa watu wa Sudan kwa ujumla ni ufahamu wa ukweli na ukatili wa Marekani na zana zake za kikanda na za ndani ambazo zinaimba amani, wakati kwa kweli zinaleta uharibifu na mauaji kwa nchi za Waislamu katika utekelezaji wa mpango wa mipaka ya damu.
Ufahamu pia juu ya mradi wa ukombozi kutoka kwa mipango ya Kimarekani na ya Magharibi ya kikoloni ya kuzimu; mradi wa Khilafa ambao unategemea umoja wa dola na umoja wa umma, na kujiunga na kazi na Hizb ut-Tahrir, kiongozi ambaye watu wake hawadanganyi, ambaye anafanya kazi hii, akiunganisha usiku wake na mchana wake, na kupaza sauti yake ya juu kupitia majukwaa mbalimbali, lakini anafanya kampeni kubwa kwa zaidi ya miezi miwili akionya juu ya kuanguka kwa Al-Fashir na nia ya Kimarekani imetimia.
Hakika vijana wa chama na uongozi wake hawatochoka wala kuchoshwa katika kuendeleza kazi yao kwa ajili ya Mwenyezi Mungu hadi ahadi ya Mwenyezi Mungu itimie na bishara ya mpendwa wetu Muhammad ﷺ; ﴿ALLAH amewaahidi wale walio amini miongoni mwenu na wakatenda mema, ya kwamba atawafanya makhalifa katika ardhi kama alivyo wafanya makhalifa wale walio kuwa kabla yao, na kwa yakini atawathibitishia Dini yao aliyo wapendelea, na atawabadilishia amani baada ya khofu yao. Waniabudu Mimi, wala wasinishirikishe na chochote. Na watakao kufuru baada ya hayo, basi hao ndio wapotovu﴾, na Imam Ahmad amepokea katika Musnad kutoka kwa Hudhaifa, amesema: Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amesema: «Utume utakuwa miongoni mwenu muda ambao Mwenyezi Mungu atapenda uwe, kisha atauondoa atakapopenda kuuondoa, kisha utakuwa Ukhalifa juu ya njia ya Utume, utakuwa muda ambao Mwenyezi Mungu atapenda uwe, kisha atauondoa atakapopenda kuuondoa, kisha utakuwa ufalme wa kuuma, utakuwa muda ambao Mwenyezi Mungu atapenda uwe, kisha atauondoa atakapopenda kuuondoa, kisha utakuwa ufalme wa kidhalimu, utakuwa muda ambao Mwenyezi Mungu atapenda uwe, kisha atauondoa atakapopenda kuuondoa, kisha utakuwa Ukhalifa juu ya njia ya Utume».
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Abdullah Hussein (Abu Muhammad Al-Fatih)
Mratibu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Sudan