2025-11-12
Jarida la Al-Raya: Je, Mzozo Utawaka Moto Tena Nchini Libya?
Katikati ya jangwa kubwa la Sahara, kuna mistari fiche inayo unganisha Darfur ya Sudan na kusini mwa Libya sio tu kupitia mchanga na njia za zamani bali kupitia makabila, maslahi, na mitandao ya ushawishi isiyotambua mipaka.
Tangu kuanguka kwa Gaddafi mwaka 2011, mzozo wa kimataifa ulianza kuhusu Libya kati ya Amerika na Uingereza, ambapo mzozo uliendelea hadi mamlaka mpya ya utendaji iliyochaguliwa ilipopata kura 132 kati ya 188 katika Baraza la Wawakilishi la Libya mnamo Machi 10, 2021, na hivyo kuipa serikali ya Abdul Hamid Dbeibeh uaminifu - mgombea kutoka kwa mjumbe wa Marekani Stephanie Williams - na baada ya hapo serikali ya Fayez al-Sarraj ilishindwa na kukabidhi mamlaka kwa urahisi.
Baada ya hapo, mzozo wa kisiasa ulianza na baadhi ya nchi zilitumia pesa chafu za kisiasa kama rushwa na kununua kura na dhamiri. Hili lilionyeshwa kwa Umoja wa Falme za Kiarabu na jaribio lake la kushawishi uteuzi wa wanachama wa Jukwaa la Mazungumzo la Libya (Al Jazeera Net, 2020/11/16), na baada ya hapo Amerika ilipunguza kumtegemea Haftar na kujiondoa kwa muda kutoka eneo la kisiasa, na eneo lote la kisiasa nchini Libya lilibadilika kwa faida ya Amerika, pamoja na majaribio yasiyokoma kutoka Uingereza na nchi za Ulaya kwa sababu ya uwepo wa mazingira ya kisiasa na maslahi ya nchi kama vile Ufaransa na Italia.
Katika kipindi hiki cha kutokuwepo kwa serikali, wanamgambo wa kikabila wa ndani walianzishwa kusini mwa Libya, wakidhibiti magendo na njia na wana uhusiano wa karibu na makundi kutoka Darfur, hasa kutoka harakati za Haki na Usawa na Ukombozi wa Sudan, ambapo kusini mwa Libya kilitumika kama mahali salama pa kupokea fedha, mafunzo, au biashara ya dhahabu na silaha. Hili lilitokea kati ya 2012 na 2015, na baada ya hapo Haftar alikuja na kupanua ushawishi wake kutoka mashariki mwa Libya kuelekea kusini, akifaidika na msaada wa Misri, na kwa nguvu ya silaha, udhibiti wa kiasi ulipatikana na Haftar. Katika kipindi hicho, kulikuwa na wapiganaji kutoka Darfur nchini Libya wakifanya kazi kama mamluki, na serikali ya Bashir ilikuwa ikifaidika na hilo, na baada ya kuanguka kwa Bashir mwaka 2019, mizizi ya uhusiano kati ya Sudan na Libya ilibadilika.
Baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano ya Libya chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa mwaka 2020, wito ulitolewa kwa wapiganaji wa kigeni kuondoka Libya, pamoja na mamluki wa Sudan, lakini wengi wao walibaki huko Sabha, Murzuq, na Kufra, hadi 2022. Baada ya kuzuka kwa vita kati ya Jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka mwaka 2023, baadhi ya makundi yalikimbilia kusini mwa Libya, na kwa ushindi wa Hemedti sasa huko Darfur baada ya mauaji aliyofanya katika ngome ya mwisho ya Darfur katika mji wa Al-Fasher, ishara zinaweza kuanza kuonekana za harakati za makabila yanayomuunga mkono Hemedti kusini mwa Libya, hasa kutoka Tebu na Mahamid, na hii itawasha mzozo nchini Libya tena, hasa katika Fezzan katikati ya mvutano kati ya vikosi vya Haftar na uwepo wa Urusi, na tunaweza kushuhudia uingiliaji wa Kituruki dhidi ya harakati za Hemedti. Na hili linaweza kumsukuma Hemedti kwa amri za Marekani bila shaka kuingia kusini mwa Libya na kuunda mzozo wa kikabila kulingana na upanuzi wa kikabila unaomuunga mkono, ambayo itaunga mkono kujitenga kwa kusini mwa Libya kutoka Libya au kugawana na nguvu zinazokinzana na itakuwa njia ya kutoka kwa Hemedti.
Kusini mwa Libya ndio eneo dhaifu zaidi nchini Libya na mara nyingi liko nje ya udhibiti kamili wa upande wowote, na Hemedti ana tamaa huko. Hemedti anaweza asilenge kukalia kusini mwa Libya kikamilifu lakini anaweza kuitumia kama karata ya shinikizo kufikia malengo mengi, tunataja yafuatayo:
* Karata ya shinikizo kubwa kwa Haftar kupitia uwepo wa makabila yanayomuunga mkono ambayo anaweza kuitumia kulazimisha uwiano wa uwanja kuhusu masuala ya biashara ya dhahabu na mafuta, na hata hali ya Urusi huko Fezzan.
* Kusini inakutana na mipaka ya Chad, Niger, na Sudan, ambayo ni eneo muhimu kwa biashara ya dhahabu na uranium. Na kwa kudhibiti pembetatu hii, uwezo wa Hemedti wa kusimamia biashara ya madini kuvuka mipaka unaongezeka, na anaweza kusaini mikataba ya kimataifa na Amerika na pande zingine zikatoka.
* Anaweza kuifanya kuwa karata ya mazungumzo katika faili za uhamiaji, nishati, na usalama wa mpaka, na hivyo kujifanya kuwa upande ambao hauwezi kupuuzwa.
* Na kwa kuzingatia Darfur kama ugani wa asili wa kusini mwa Libya kwa upande wa kikabila na kijiografia, itampa Hemedti kina cha ulinzi dhidi ya tishio lolote kutoka kwa Jeshi la Sudan au nguvu yoyote adui kwake kutoka mashariki mwa Sudan na kuimarisha hali ya kujitenga na Sudan.
Kwa hiyo, uwezekano wa kuingilia kati kwa Hemedti katika uwanja wa Libya unaonekana kuwa wa kweli zaidi kwa sababu ya kile atakachopata kutoka kwake na ndani ya mabadiliko yanayoendelea nchini Sudan, ambapo ameimarisha ushawishi wake magharibi mwa Sudan na anataka kupanua wigo wa harakati zake kuelekea kusini mwa Libya, ambapo maslahi ya kikabila yanakutana na utengano wa kikabila unakuwa, na bila shaka hii inakubaliana na mtazamo wa Amerika kwa eneo hilo kuhamisha mipaka ya sasa kwa mipaka ya kikabila, na pia udhaifu wa hali ya serikali ya Libya unamruhusu kufikiria hatua kama hiyo, na bila shaka jambo kama hilo haliwi rahisi kama maneno lakini lina gharama ambayo watu wa Sudan na Libya watalipa na bahari ya damu ya Waislamu, na haya yote yanahusiana na uwezo wa Libya wa kulinda mipaka yake ya kusini na kiwango cha kukubalika kwa Amerika kwa mpango huu.
Jambo la kusikitisha na la kuumiza ni kuona nchi za Waislamu zikiwa viwanja vya mapigano kati ya watu wake kutekeleza mipango ya Magharibi ya kukata kile kilichobaki cha mkusanyiko wetu, na kupora utajiri wetu na kuzuia hata kufikiria wazo la umoja kwa sababu linatushughulisha daima na migogoro ya kikabila, kidini na kimadhehebu ... nk. Hata kuondoa hofu ya wazo tu la kurudi kwetu kama nchi moja.
Ukweli ni kwamba hatutatoka kwenye mzunguko huu isipokuwa tukichochea mwendo na Hizb ut-Tahrir kuanzisha tena maisha ya Kiislamu na kuanzisha dola ya Khilafah Rashidah ya pili kwa misingi ya unabii ahadi ya Mungu Mtukufu na bishara ya Mtume ﷺ.
Imeandikwa na: Mwalimu Nabil Abdul Karim
Chanzo: Jarida la Al-Raya