Jarida la Al-Raya: Je, Mzozo Utawaka Moto Tena Nchini Libya?
November 11, 2025

Jarida la Al-Raya: Je, Mzozo Utawaka Moto Tena Nchini Libya?

Al Raya sahafa

2025-11-12

Jarida la Al-Raya: Je, Mzozo Utawaka Moto Tena Nchini Libya?

Katikati ya jangwa kubwa la Sahara, kuna mistari fiche inayo unganisha Darfur ya Sudan na kusini mwa Libya sio tu kupitia mchanga na njia za zamani bali kupitia makabila, maslahi, na mitandao ya ushawishi isiyotambua mipaka.

Tangu kuanguka kwa Gaddafi mwaka 2011, mzozo wa kimataifa ulianza kuhusu Libya kati ya Amerika na Uingereza, ambapo mzozo uliendelea hadi mamlaka mpya ya utendaji iliyochaguliwa ilipopata kura 132 kati ya 188 katika Baraza la Wawakilishi la Libya mnamo Machi 10, 2021, na hivyo kuipa serikali ya Abdul Hamid Dbeibeh uaminifu - mgombea kutoka kwa mjumbe wa Marekani Stephanie Williams - na baada ya hapo serikali ya Fayez al-Sarraj ilishindwa na kukabidhi mamlaka kwa urahisi.

Baada ya hapo, mzozo wa kisiasa ulianza na baadhi ya nchi zilitumia pesa chafu za kisiasa kama rushwa na kununua kura na dhamiri. Hili lilionyeshwa kwa Umoja wa Falme za Kiarabu na jaribio lake la kushawishi uteuzi wa wanachama wa Jukwaa la Mazungumzo la Libya (Al Jazeera Net, 2020/11/16), na baada ya hapo Amerika ilipunguza kumtegemea Haftar na kujiondoa kwa muda kutoka eneo la kisiasa, na eneo lote la kisiasa nchini Libya lilibadilika kwa faida ya Amerika, pamoja na majaribio yasiyokoma kutoka Uingereza na nchi za Ulaya kwa sababu ya uwepo wa mazingira ya kisiasa na maslahi ya nchi kama vile Ufaransa na Italia.

Katika kipindi hiki cha kutokuwepo kwa serikali, wanamgambo wa kikabila wa ndani walianzishwa kusini mwa Libya, wakidhibiti magendo na njia na wana uhusiano wa karibu na makundi kutoka Darfur, hasa kutoka harakati za Haki na Usawa na Ukombozi wa Sudan, ambapo kusini mwa Libya kilitumika kama mahali salama pa kupokea fedha, mafunzo, au biashara ya dhahabu na silaha. Hili lilitokea kati ya 2012 na 2015, na baada ya hapo Haftar alikuja na kupanua ushawishi wake kutoka mashariki mwa Libya kuelekea kusini, akifaidika na msaada wa Misri, na kwa nguvu ya silaha, udhibiti wa kiasi ulipatikana na Haftar. Katika kipindi hicho, kulikuwa na wapiganaji kutoka Darfur nchini Libya wakifanya kazi kama mamluki, na serikali ya Bashir ilikuwa ikifaidika na hilo, na baada ya kuanguka kwa Bashir mwaka 2019, mizizi ya uhusiano kati ya Sudan na Libya ilibadilika.

Baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano ya Libya chini ya uangalizi wa Umoja wa Mataifa mwaka 2020, wito ulitolewa kwa wapiganaji wa kigeni kuondoka Libya, pamoja na mamluki wa Sudan, lakini wengi wao walibaki huko Sabha, Murzuq, na Kufra, hadi 2022. Baada ya kuzuka kwa vita kati ya Jeshi la Sudan na Vikosi vya Msaada wa Haraka mwaka 2023, baadhi ya makundi yalikimbilia kusini mwa Libya, na kwa ushindi wa Hemedti sasa huko Darfur baada ya mauaji aliyofanya katika ngome ya mwisho ya Darfur katika mji wa Al-Fasher, ishara zinaweza kuanza kuonekana za harakati za makabila yanayomuunga mkono Hemedti kusini mwa Libya, hasa kutoka Tebu na Mahamid, na hii itawasha mzozo nchini Libya tena, hasa katika Fezzan katikati ya mvutano kati ya vikosi vya Haftar na uwepo wa Urusi, na tunaweza kushuhudia uingiliaji wa Kituruki dhidi ya harakati za Hemedti. Na hili linaweza kumsukuma Hemedti kwa amri za Marekani bila shaka kuingia kusini mwa Libya na kuunda mzozo wa kikabila kulingana na upanuzi wa kikabila unaomuunga mkono, ambayo itaunga mkono kujitenga kwa kusini mwa Libya kutoka Libya au kugawana na nguvu zinazokinzana na itakuwa njia ya kutoka kwa Hemedti.

Kusini mwa Libya ndio eneo dhaifu zaidi nchini Libya na mara nyingi liko nje ya udhibiti kamili wa upande wowote, na Hemedti ana tamaa huko. Hemedti anaweza asilenge kukalia kusini mwa Libya kikamilifu lakini anaweza kuitumia kama karata ya shinikizo kufikia malengo mengi, tunataja yafuatayo:

* Karata ya shinikizo kubwa kwa Haftar kupitia uwepo wa makabila yanayomuunga mkono ambayo anaweza kuitumia kulazimisha uwiano wa uwanja kuhusu masuala ya biashara ya dhahabu na mafuta, na hata hali ya Urusi huko Fezzan.

* Kusini inakutana na mipaka ya Chad, Niger, na Sudan, ambayo ni eneo muhimu kwa biashara ya dhahabu na uranium. Na kwa kudhibiti pembetatu hii, uwezo wa Hemedti wa kusimamia biashara ya madini kuvuka mipaka unaongezeka, na anaweza kusaini mikataba ya kimataifa na Amerika na pande zingine zikatoka.

* Anaweza kuifanya kuwa karata ya mazungumzo katika faili za uhamiaji, nishati, na usalama wa mpaka, na hivyo kujifanya kuwa upande ambao hauwezi kupuuzwa.

* Na kwa kuzingatia Darfur kama ugani wa asili wa kusini mwa Libya kwa upande wa kikabila na kijiografia, itampa Hemedti kina cha ulinzi dhidi ya tishio lolote kutoka kwa Jeshi la Sudan au nguvu yoyote adui kwake kutoka mashariki mwa Sudan na kuimarisha hali ya kujitenga na Sudan.

Kwa hiyo, uwezekano wa kuingilia kati kwa Hemedti katika uwanja wa Libya unaonekana kuwa wa kweli zaidi kwa sababu ya kile atakachopata kutoka kwake na ndani ya mabadiliko yanayoendelea nchini Sudan, ambapo ameimarisha ushawishi wake magharibi mwa Sudan na anataka kupanua wigo wa harakati zake kuelekea kusini mwa Libya, ambapo maslahi ya kikabila yanakutana na utengano wa kikabila unakuwa, na bila shaka hii inakubaliana na mtazamo wa Amerika kwa eneo hilo kuhamisha mipaka ya sasa kwa mipaka ya kikabila, na pia udhaifu wa hali ya serikali ya Libya unamruhusu kufikiria hatua kama hiyo, na bila shaka jambo kama hilo haliwi rahisi kama maneno lakini lina gharama ambayo watu wa Sudan na Libya watalipa na bahari ya damu ya Waislamu, na haya yote yanahusiana na uwezo wa Libya wa kulinda mipaka yake ya kusini na kiwango cha kukubalika kwa Amerika kwa mpango huu.

Jambo la kusikitisha na la kuumiza ni kuona nchi za Waislamu zikiwa viwanja vya mapigano kati ya watu wake kutekeleza mipango ya Magharibi ya kukata kile kilichobaki cha mkusanyiko wetu, na kupora utajiri wetu na kuzuia hata kufikiria wazo la umoja kwa sababu linatushughulisha daima na migogoro ya kikabila, kidini na kimadhehebu ... nk. Hata kuondoa hofu ya wazo tu la kurudi kwetu kama nchi moja.

Ukweli ni kwamba hatutatoka kwenye mzunguko huu isipokuwa tukichochea mwendo na Hizb ut-Tahrir kuanzisha tena maisha ya Kiislamu na kuanzisha dola ya Khilafah Rashidah ya pili kwa misingi ya unabii ahadi ya Mungu Mtukufu na bishara ya Mtume ﷺ.

Imeandikwa na: Mwalimu Nabil Abdul Karim

Chanzo: Jarida la Al-Raya

More from null

Gazeti la Ar-Raya: Mkataba wa Amani wa Kimarekani Wenye Mtego kati ya Morocco na Algeria, Kichocheo cha Trump cha Kuchochea Ukoloni wake!

Al Raya sahafa

2025-11-05

Gazeti la Ar-Raya:

Mkataba wa Amani wa Kimarekani Wenye Mtego kati ya Morocco na Algeria

Kichocheo cha Trump cha Kuchochea Ukoloni wake!

Steve Witkoff, mjumbe wa Rais wa Marekani Donald Trump katika Mashariki ya Kati, alitangaza kwamba timu yake inafanya kazi ya kukamilisha mkataba wa amani kati ya Algeria na Morocco katika kipindi kijacho. Hii ilikuja katika mahojiano ya televisheni yeye na Jared Kushner waliyoyafanya, Jumapili jioni, katika kipindi cha "Dakika 60" kwenye kituo cha CBS cha Marekani. Witkoff alisema: "Timu yetu inafanya kazi sasa kuhusu Morocco na Algeria, na ninatarajia kufikia mkataba wa amani ndani ya siku 60."

Suala la Sahara liliunda mojawapo ya masuala hatari zaidi ya mzozo wa kikoloni wa Marekani na Ulaya magharibi mwa nchi za Kiislamu tangu katikati ya miaka ya sabini ya karne iliyopita. Pamoja na utawala wa kwanza na wa pili wa Trump na maendeleo ya kimkakati ambayo yalitokea kwenye suala hilo baada ya Trump kutambua uhuru wa Morocco juu ya Sahara na kuunga mkono mpango wa uhuru kama suluhisho pekee linalowezekana, ambayo ni sehemu ya kile kinachoitwa mkakati wa kiuchumi na kibiashara wa Trump na maono yake ya ulimwengu kama soko la mikataba na kiwango cha faida atakayopata na wakati ni jambo muhimu katika kuharakisha matokeo, anaiona Sahara kama ardhi bikira tajiri ya madini ya kimkakati na lango la Afrika mbele ya ubepari wa Marekani na nguzo ya ushawishi wake wa kisiasa, kijeshi na kiuchumi katika nchi za Maghrib, ambayo lazima itwaliwe na kueneza ushawishi wake wa kikoloni juu yake.

Na Marekani pamoja na mfanyabiashara mkuu Trump wanaongeza kasi ya kukamilisha mpango wao wa kikoloni katika kushughulika kwao moja kwa moja na pande kuu mbili; Morocco na Algeria, na taarifa ya Witkoff kuhusu mkataba wa amani ndani ya siku sitini zijazo na kwamba timu yake inafanyia kazi hilo, ni ishara kwamba hatua za kivitendo na mawasiliano na pande husika zinafanyika na ni ukweli, na hili ndilo lililothibitishwa na Msaid Boles, shemeji wa Trump na mshauri wake wa masuala ya Afrika, alifichua katika mahojiano na kituo cha Al-Sharq cha Saudi Arabia, wiki iliyopita kwamba "Algeria inataka kupata suluhu la kimsingi na la mwisho kwa suala la Sahara Magharibi, na pia inaonyesha utayari wa kuboresha uhusiano na Morocco", akieleza matumaini yake kwamba tofauti hii inaweza kutatuliwa, na akaongeza "kwamba alikutana na Rais wa Algeria Abdelmadjid Tebboune (hivi karibuni) na alipata ukaribisho wa kujenga upya madaraja ya uaminifu na watu wa Morocco, na na mfalme, serikali na taifa la Morocco. Mwishowe, nchi hizo mbili ni watu ndugu na majirani, wana historia ya pamoja na idadi kubwa ya maadili na maslahi."

Ama kuhusu Morocco, Msaid Boles alisema "Hotuba ya mwisho ya Mfalme ilikuwa ya kihistoria, alithibitisha kupitia hiyo dhamira yake ya kufanya kazi ili kupata suluhisho la mwisho kwa suala la Sahara ambalo litawaridhisha washiriki wote, kwa sababu kinachotakiwa ni suluhisho la kudumu na kamili."

Hii ni ishara kwamba serikali za Morocco na Algeria zinashiriki katika mpango wa kikoloni wa Marekani, pamoja na utumiaji wa Trump wa serikali ya Al Saud kama dalali kati ya pande hizo mbili ili kuharakisha kukamilika kwa mpango huo, Tebboune na Mohammed VI wote walipokea, ujumbe kwa wakati mmoja kutoka kwa bin Salman, baadhi ya makadirio yameonyesha kuwa yana uhusiano na upatanishi wa kutatua tofauti kati ya Rabat na Algeria. Baadaye, Rais Tebboune alitoa hotuba mbele ya viongozi wa jeshi iliyorushwa hewani kikamilifu siku ya Ijumaa, Oktoba 10, 2025 "Kuna baadhi ya ndugu waaminifu, wanatuomba kufungua mipaka na Morocco, kutatua suala la Sahara, mipaka haikufungwa kwa sababu ya suala la Sahara, lakini ilifungwa kwa sababu zingine, miaka 63 ya uhuru, mipaka yetu imefungwa kwa zaidi ya miaka 45".

Hii ilifuatiwa na mabadiliko katika mtindo wa hotuba ya kisiasa nchini Algeria na mwelekeo wake kuelekea maridhiano, kwani Tebboune alithibitisha kupokea maombi kutoka kwa wale aliowaita "ndugu" kuhusu mzozo kati ya Algeria na Morocco, ambayo ilijumuisha ombi kutoka Morocco la kufungua mipaka kati ya nchi hizo mbili, ambayo itasaidia katika kutatua mzozo wa Sahara.

Jambo la kushangaza katika taarifa ya Witkoff ni kupuuza kwake kabisa kwa chama cha Polisario, na alizuia tatizo kati ya Morocco na Algeria, akionyesha uwezekano kwamba utawala wa Trump umeachana na karatasi ya Polisario na sasa unategemea mkakati wa mikataba ya kiuchumi na kibiashara ya mfanyabiashara Trump katika kuvunja milango na kung'oa kufuli ili kupenya serikali hizo mbili moja kwa moja bila zana ya Polisario.

Ama ushiriki wa Algeria na Morocco katika mpango wa Trump, unatokana na kuhakikisha kuendelea kwa serikali hizo mbili vibaraka hasa kwa Uingereza, na utayari wao wa kulipa bei ghali na bei kubwa kwa matumaini ya dhamana ya uongo kutoka kwa mamlaka ya kikoloni ya Marekani katika eneo hilo.

Utambuzi wa Trump wa Morocco juu ya Sahara na matokeo yake mabaya yaliyofuata uliharibu Morocco, na miongoni mwa matokeo yake ni:

- Kuiwezesha ubepari mbaya wa Marekani wa mali ya Sahara, hasa madini yake adimu ya kimkakati.

- Kupenya katika sekta ya kilimo ya nchi kupitia kilimo mseto, mbegu zilizobadilishwa vinasaba, malisho na mifugo na makampuni ya ubepari ya Marekani, na kunyakua matunda adimu nchini Morocco kama vile tini na mti wa Argan na kuyamiliki katika utengenezaji wa vipodozi, pamoja na mradi wa mashamba ya uvuvi na umiliki wa baadhi ya bidhaa za bahari, pamoja na majanga mengine.

- Na hatari zaidi ni Marekani kupanda uongozi wake wa kijeshi wa kikoloni kwa Afrika (Africom) katika moyo wa Morocco, na inakaribia kukamilisha uhamisho wake kwenda Morocco, tovuti ya Hespress (mdomo wa serikali) iliripoti kwamba Morocco "imependekeza miji kadhaa kuipokea kama vile Laayoune, Dakhla, Boujdour na Agadir, lakini Wamarekani wameonyesha nia ya kuchagua Kenitra au Ksar El Kebir, kwa sababu za kihistoria, kiufundi na kimantiki, ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa kambi ya zamani ya anga ya Marekani huko Kenitra, na hamu yao ya kupanua viwanja vyake ili kupokea ndege kubwa za kijeshi zinazohitaji vifaa maalum."

Uongozi wa kijeshi wa Marekani kwa Afrika utakuwa kama kambi kubwa zaidi ya mkoloni wa Marekani magharibi mwa nchi za Kiislamu na katika moyo wa Morocco, na pamoja nayo Marekani haitakubali ila uaminifu na utumishi kamili kwake, ambayo ina maana kwamba nchi hiyo iko juu ya mlipuko wa volkeno ya kikoloni ambayo haitachelewa kulipuka!

Na aibu zaidi ya hilo ni kuanzisha uhusiano na taasisi ya Kiyahudi inayonyakua ardhi na matokeo yake ya Sayuni ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni, ushirikiano na msaada kwa mauaji ya kimbari ya Gaza.

Ama serikali ya Algeria, kwa kufika kwa mkoloni wa Marekani kwenye mipaka ya mashariki na kusini ya Algeria, kupitia nchi za Sahel kusini ambazo Marekani ilinyakua kutoka kwa mkoloni Mfaransa, kisha kufika kwake Libya kupitia wakala wake Haftar, kulifanya serikali kuwa kati ya makucha ya ukoloni wa Marekani, ambayo ilifanya iwe rahisi kukamua na kujiunga na mpango wa kikoloni wa Trump.

Kwa hivyo Marekani ya Trump na amani yake yenye mtego kwa hila zake za kikoloni, baada ya kile kinachoonekana kuwa imemtupa chama cha Polisario kwenye kikapu cha zana zake zilizochakaa na kukiondoa kutoka kwa hesabu zake, inataka Sahara ichukuliwe na kampuni zake na kuwa kambi ya majeshi yake na lango la Afrika kwa ukoloni na kupenya nchi zote za Maghrib, na inakuja na serikali za usaliti na aibu nchini Morocco na Algeria kama mashahidi wa aibu kwa mpango wake mbaya!

Hili ndilo tatizo letu linaloendelea mradi tu serikali hizi zinaendelea kuwa vibaraka wa ukoloni, hazijawahi kuwa kwetu ila serikali za madhara na mawakala ambao watawala wao ni watunza sanamu na masanamu ya ukoloni.

Imeandikwa na: Mwalimu Munaji Muhammad

Chanzo: Gazeti la Ar-Raya