Msururu wa Majibu ya Mwanachuoni Mkuu Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, Amir wa Hizb ut-Tahrir
Kwa Maswali ya Wafuasi wa Ukurasa Wake wa Facebook "Fikri"
Jibu la Swali
Taasisi katika Nchi za Kiislamu
Kwa Jumah Alsaad
Swali:
Ndugu mpendwa,
As-salamu alaykum wa rahmatullahi wa barakatuh,
Swali: Katika ukurasa wa 80 wa kitabu cha Dhana za Hizb ut-Tahrir - mstari wa kumi kutoka juu, kumeandikwa yafuatayo: (Bali inafanya kazi kung'oa hali zilizowekwa na kafiri mkoloni kutoka kwenye mizizi yake, kwa kukomboa nchi, taasisi na mawazo, kutoka kwa uvamizi,). Mwisho wa nukuu.
Nini maana ya neno (na taasisi)?
Mwenyezi Mungu akuongoze kwa kile anachokipenda na kukiridhia
Ndugu yako/ Radhi
Jibu:
Wa alaikum as-salam wa rahmatullahi wa barakatuh,
Hakika mahali unapo ulizia pamekuja mwishoni mwa kitabu cha Dhana za Hizb ut-Tahrir ukurasa wa 83 faili ya word, na hii ndio maandishi yake:
[Na kwa ajili ya hili, Hizb ut-Tahrir inafanya kazi ya kukomboa maeneo ya Kiislamu kutoka kwa ukoloni wote. Kwa hivyo, inapinga ukoloni kwa vita visivyo na huruma, lakini haitafuti tu kuondoka kwa majeshi, wala haitafuti uhuru bandia, bali inafanya kazi ili kung'oa hali zilizowekwa na kafiri mkoloni kutoka kwenye mizizi yake, kwa kukomboa nchi, taasisi na mawazo, kutoka kwa uvamizi, iwe uvamizi huu ni wa kijeshi, au wa kiitikadi, au wa kitamaduni, au wa kiuchumi, au vinginevyo. Na inapigana na kila mtu anayetetea upande wowote wa ukoloni mpaka maisha ya Kiislamu yatakapoanzishwa tena kwa kuanzishwa dola ya Kiislamu ambayo inabeba ujumbe wa Uislamu kwa ulimwengu wote, na tunamuomba Mwenyezi Mungu, na kwake tunaomba kwa unyenyekevu, atusaidie kwa msaada kutoka kwake, ili kutekeleza majukumu haya mazito, hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujibu.] Mwisho wa nukuu.
Na maana ya neno "taasisi" katika muktadha huu ni taasisi za elimu, iwe ni shule, vyuo au vyuo vikuu ... nk, kwa hivyo taasisi zote za elimu zinajumuishwa na neno "taasisi" katika muktadha huu, kwa sababu kafiri mkoloni aliweka sera za elimu katika nchi za Waislamu kulingana na mawazo yake na mtazamo wake wa maisha, na kwa hivyo alitia sumu mawazo ya wanafunzi na kuwaondoa kutoka kwa mawazo ya Uislamu na mtazamo wake wa maisha, kwa hivyo ilikuwa lazima katika mchakato wa ukombozi kujumuisha taasisi zilizopo katika nchi za Waislamu ili sera za elimu ndani yake ziwe kulingana na Uislamu... Na tumetaja katika kitabu cha Daula maneno ambayo yanaelezea maana hii ukurasa wa 224-226 faili ya word, na tulisema ndani yake:
[Na mara tu kafiri mkoloni alipoikalia nchi, alitekeleza sheria zote za Magharibi moja kwa moja kama sheria za kiraia ambazo hazihusiani na Uislamu, na hukumu za kisheria ziliachwa, kwa hivyo hukumu ya ukafiri ilithibitishwa na hukumu ya Uislamu iliondolewa, na alisaidiwa na hilo kwamba alithibitisha nguzo zake na akaanzisha mambo yake yote kwa msingi wa sera ya elimu aliyoichora, na mitaala ya elimu aliyo iweka, ambayo inaendelea kutumika hadi leo katika nchi zote za Kiislamu, na imetoa kile ilichotoa kutoka kwa majeshi haya makubwa ya walimu ambao wengi wao wanasimamia kulinda programu hizi, na ambao wengi wao wanachukua uongozi wa mambo, na wanaenda kulingana na kile anachotaka kafiri mkoloni. Sera ya elimu imeanzishwa na mitaala yake imewekwa kwa misingi miwili: moja yao ni kutenganisha dini na maisha, na matokeo yake ya asili ni kutenganisha dini na dola, na hilo linafanya iwe lazima kwa watoto wa Waislamu kupigana na kuanzishwa kwa dola ya Kiislamu, kwa sababu inapingana na msingi ambao wamejifunza juu ya sera yake, ama msingi wa pili ni kumfanya mtu wa kafiri mkoloni kuwa chanzo kikuu cha kile ambacho akili zinazokua zinajazwa na maarifa na habari. Na hilo linafanya iwe lazima kumheshimu kafiri huyu mkoloni na kumtukuza, na kujaribu kumwiga na kumfuata, hata kama ni kafiri mkoloni, na inafanya iwe lazima kumdharau Muislamu na kumwepuka na kumchukia na kukataa kuchukua kutoka kwake. Na hii inahitaji kupigana na kuanzishwa kwa dola ya Kiislamu na kuizingatia kuwa ni ya kizamani. Na ukoloni haukutosheka na mitaala ya shule ambazo unasimamia au serikali ambazo umesimamisha badala yake zinasimamia. Bali uliweka kando yake shule za kimisionari ambazo zinasimama kwa msingi safi wa kikoloni, na taasisi za kitamaduni ambazo zinachukua jukumu la uongozi mbaya wa kisiasa, na uongozi mbaya wa kitamaduni. Na kwa hivyo hali ya kiakili katika shule tofauti na taasisi za kitamaduni tofauti zote zilianza kuielimisha umma kwa utamaduni ambao unawaondoa kufikiria juu ya dola ya Kiislamu, na unazuia kati yao na kufanya kazi kwa ajili yake.
Na mitaala ya kisiasa katika nchi zote za Kiislamu ilisimama kwa msingi wa kutenganisha dini na maisha, na ikawa ni kawaida kwa wasomi kutenganisha dini na dola, na kwa watu wa kawaida kutenganisha dini na siasa, na matokeo yake yalikuwa ni kupatikana kwa makundi ya wasomi wanaodai kuwa sababu ya ucheleweshaji wa Waislamu ni kushikamana kwao na dini, na kwamba njia pekee ya maendeleo ni utaifa na kufanya kazi kwa ajili yake...] Mwisho wa nukuu.
Kwa hivyo, ni lazima kukomboa nchi za Kiislamu na taasisi katika nchi za Waislamu na mawazo ya Waislamu kutoka kwa dosari yoyote ya dosari za wakoloni, ili mizizi yake ikatwe na umma uwe safi katika mawazo yake.
Ndugu yenu Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah
21 Muharram 1447 Hijria
Sawa na 2025/07/16 Miladia
Kiungo cha jibu kutoka ukurasa wa Amir (Mungu amhifadhi) kwenye:Facebook