Hakuna wokovu kwenu watu wetu nchini Sudan
Wala amani wala usalama ila katika kivuli cha mfumo wa Kiislamu
Katika historia yote, wingi wa makabila nchini Sudan haujawahi kuwa sababu ya mzozo na mapigano, bali sababu ya hayo ni mzozo mkali wa kisiasa na kijeshi kati ya nchi za kikoloni na vibaraka wao, ambao uliharibu mazao na vizazi, haswa baada ya kuzigawanya nchi na kupanda mbegu za fitina na mapigano ya kikabila na ya kijamii kama inavyotokea leo, sawa kabisa na ilivyokuwa ikitokea siku za ujinga wa kwanza, tangu kupotea kwa Uislamu na kubomolewa kwa dola yake, watu walirudi kwenye hukumu za kijahiliya wakipigana kwa misingi ya ukabila ambao Mtume ﷺ alikataza na kusisitiza juu ya hilo, ambapo alisema: «Yeyote anayepigana chini ya bendera ya upofu akilingania ushabiki au anaghadhibika kwa ushabiki, basi mauaji yake ni ya kijahiliya».
Kwa hivyo, ni lazima watu wa Sudan watambue kuwa mazingira ya kisiasa yaliyopo, ambayo hayana wazo la kisiasa lenye ufahamu na yanahusiana na Magharibi kafiri, ndiyo sababu ya migogoro na matatizo, kutokana na mgawanyiko wa kisiasa unaotegemea misingi ya kikabila mbaya, ambapo serikali zilizofuata zilitumia makabila kama kuni kwa ajili ya migogoro yao, hivyo ziliendeshwa kwa mwelekeo wa vyama katika mgawanyiko wa kikabila, na kile kilichotokea Darfur na kinachoendelea ndiyo mfano dhahiri wa hilo, pale ambapo baadhi ya makabila yaliunga mkono harakati za waasi wenye silaha, jambo ambalo liliifanya serikali kwa upande mwingine kuyapa silaha makabila yanayoiunga mkono na kuyatumia katika kupigana na waasi, na pima kwa mtindo huu jinsi serikali zilizofuata zilivyoshughulika katika mikoa yote nchini Sudan, jambo ambalo liliunda hali ya wasiwasi na hofu katika maeneo yote, mpaka nchi yote ikawa pipa la baruti linaloweza kuwaka wakati wowote, huku mshindi pekee katika mzozo huu na mapigano ya kikabila ya kishenzi ni watu wa nchi, bado wanalipa gharama kubwa kwa damu na roho zao, kwa bahati mbaya hawawi ila vyombo vya bei rahisi vinavyotumiwa kuuana!
Uislamu umeheshimu sana utakatifu wa damu ya Muislamu, kwani Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: ﴿Na anayemwua Muumini kwa kukusudia, basi malipo yake ni Jahannamu atadumu humo, na Mwenyezi Mungu amemkasirikia na amemlaani, na amemuandalia adhabu kubwa﴾ Na Mtume ﷺ amesema: «Kuangamia kwa dunia ni jepesi zaidi kwa Mwenyezi Mungu kuliko kumuua Muumini bila ya haki» Na pia alisema: «Waislamu wawili wanapokutana na panga zao, basi muuaji na muuwaji wote wawili wako motoni» Kwa hivyo tuko wapi katika kumfuata Mtume ﷺ? Na tuko wapi katika kufuata Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu anayesema: ﴿Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane. Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule aliye mchamungu zaidi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye khabari.﴾ Kwa hivyo, ilikuwa ni lazima kwetu kufanya bidii kukomesha umwagaji damu unaoendelea na kukomesha mpango wa Magharibi kafiri kwa kufuata amri za Mwenyezi Mungu na Mtume wake, yaani kwa kuhukumu Uislamu, mapigano ya kikabila hayatakoma, hali haitatulia, na uchezaji na roho za wasio na hatia hautakoma ila kwa kurudi kwenye Uislamu na kubatilisha kila kinachokhalifu.
Lakini Uislamu hautakuwa ila kwa mamlaka, yaani dola inayoutekeleza na kuupeleka ulimwenguni kwa njia ya da'wa na jihad, nayo ni dola ya Khilafa Rashidah ya pili kwa njia ya Utume, ambapo utawala ndani yake utakuwa ni jukumu na sio faida, hivyo itatekeleza wajibu wa kuwahudumia watu kwa afya, elimu, usalama na kuwawezesha watu kulima, kutengeneza bidhaa na kufungua njia za malisho ili kusiwe na mwingiliano kati ya wakulima na wachungaji, hivyo itakata mikono ya waharibifu bila huruma, na itakomesha kila aina ya mauaji, moto na uporaji, kwa kutumia adhabu kwa wanaokiuka sheria.
Hakika dola ya Khilafa ndiyo pekee inayoweza kuwachanganya watu kama umma mmoja kwa misingi ya Uislamu mkuu, si kwa misingi ya ubaguzi wa rangi, ukabila, au utaifa, kwani inaendeshwa kwa hukumu za Uislamu na mamlaka yake, mamlaka hii ambayo iliwakusanya Waislamu na kuwafanya ndugu wanaopendana kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, hivyo ikamkusanya Abu Bakr Mwarabu, Bilal Habeshi, Salman Farisi, Suhayb Rumi, Hamza Quraishi, na Muadh Ansari...
Hakika Uislamu mkuu ndiyo pekee katika historia ya wanadamu ambao uliwachanganya watu, rangi na makabila mbalimbali katika umma mmoja, haikuwa imefungiwa Madina, bali ilienea katika kisiwa chote na kufanyika ufunguzi wa Kiislamu kwa ajili ya kueneza Uislamu, hivyo Waislamu walifungua Iraq, na ilikuwa ikikaliwa na Wakristo, Mazdaki na Zaradashti kutoka kwa Waarabu na Waajemi, na walifungua Farsi na ilikuwa ikikaliwa na Waajemi, Wayahudi na Warumi, na walifungua Sham na ilikuwa ni mkoa wa Kirumi uliokaliwa na Wasuri, Waarmenia, Warumi na Waarabu, na walifungua Afrika Kaskazini ambapo walikuwa Berber, na walifungua Sindh, Khwarazm, Samarkand na Andalusia, na wakawachanganya watu hao wote katika umma mmoja, hakuna ubaguzi kati yao, hivyo nuru ya Uislamu ilienea katika pembe za dunia katika kipindi kifupi; kwa sababu amri za Uislamu zinataka kuwatazama raia kwa mtazamo wa kibinadamu, si mtazamo wa kibaguzi, au wa kidini, au wa kimadhehebu, kwani hukumu za Uislamu zilitumika kwa wote, hivyo watu wote wakawa raia wa dola ya Kiislamu bila tofauti kati ya Muislamu na asiye Muislamu, wala hakuna anayemdhulumu mwenzake, na ikiwa itatokea, Uislamu utamkemea na kumzuia, Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Wala kuchukiana na watu kusikupelekeeni kuto fanya uadilifu. Fanyeni uadilifu, huko ndiko kunako mpeleka karibu zaidi na uchamungu.﴾ Na watu wote wako sawa katika hukumu mbele ya mahakama, na mfumo wa utawala unatoa wito wa umoja kati ya sehemu za dola, kama vile unatoa wito wa kuhakikisha mahitaji ya kila jimbo bila kujali mapato yake kwa hazina, jambo ambalo linafanya muungano kuwa wa lazima kati ya watoto wa majimbo yote ya dola.
Kwa hivyo, ilikuwa ni wajibu kwa kila Muislamu na Muislamu kufanya kazi ya kusimamisha faradhi hii kuu iliyopotea, ngome ya Khilafa Rashidah kwa njia ya Utume. ﴿Hakika huu umma wenu ni umma mmoja, na Mimi ndiye Mola wenu Mlezi, basi niabuduni.﴾.
#Mgogoro_wa_Sudan #SudanCrisis
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Rana Mustafa