Kuhamasisha Watu Wenye Nia ya Kufanya Wajibu Wao
Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿NA TUMEKUTEREMSHIA KITABU KIELEZO CHA KILA KITU﴾, basi ubainifu huu wa Kiungu unasisitiza kuwa Uislamu si mawaidha tu ya kiroho, bali ni mfumo kamili wa maisha, umekuja na itikadi thabiti inayoshawishi akili na kujaza moyo utulivu, na kwa hukumu zinazoongoza maisha ya mwanadamu katika mambo yake yote: katika utawala, uchumi, jamii, siasa, elimu na uhusiano wa kimataifa... Hakika hii ni dini ya haki, kwa sababu inatoka kwa Mwenyezi Mungu, na imejengwa juu ya msingi imara, nayo ni itikadi ya Kiislamu ambayo mfumo hutokana nayo, hivyo basi uhusiano wa mwanadamu nayo unakuwa ni wa kiakili kwa ushawishi, siyo kwa kufuata wala hisia, basi inakubaliana na fitra njema na inazungumza na akili, na kwa hivyo anayemwamini kwa imani timamu hawezi ila kuubeba na kuulingania na kupigania kuudhihirisha na kuutekeleza, basi kuubeba Uislamu ni wajibu wa kisheria, na faradhi tukufu, Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿NA HII NDIO NJIA YANGU ILIYONYOOKA, BASI IFUATENI﴾, je tumefuata aliyo tuamrisha Mwenyezi Mungu, hasa kwa vile tumejitolea nafsi zetu kubeba amana kubwa na kubadilisha hali hii dhalimu kwa kusimamisha Khilafah Rashidah?
Enyi ndugu: Hakika sisi tunabeba amana kubwa, nayo ni amana ya da’wa, amana ya kuubeba Uislamu ili kusimamisha dini katika uhalisia wa maisha, nayo ni amana ya Mitume, na urithi wa Nabii wetu na mpendwa wetu Muhammad ﷺ, na hakika Mwenyezi Mungu atatuuliza kuhusu tuliyochunga, basi tufanye kazi kwa ajili ya siku ambayo mali wala watoto havitafaa, ila yule aliyemjia Mwenyezi Mungu na moyo safi. Naam enyi ndugu, leo ni amali wala hakuna hesabu, na kesho ni hesabu wala hakuna amali; leo tunaulizwa: Je tumefikisha ujumbe wa Mola wetu? Je tumeifuata njia ya kisheria ya mabadiliko kama alivyotuamrisha Mwenyezi Mungu? Je tumethibiti juu ya msimamo bila ya unafiki au kurudi nyuma? Basi kila kitu kitatoweka, na ufalme wote utaondoka, na mamlaka itaelekea kuondoka. ﴿NA ITA BAKIA USO WA MOLA WAKO MWENYE UTUKUFU NA HESHIMA﴾.
Enyi Watu wenye heshima: Mna dhana gani kuhusu msimamo siku ya Kiyama?! Msimamo huo wa kutisha, siku ambayo kila mnyonyeshaji atasahau alichonyonyesha, na kila mwenye mimba ataiweka mimba yake, na nafsi zitazimia na machozi yatalia, hakika huo ni msimamo wa dhiki na udhalili na hofu kubwa, haumwokozi mtu humo ila amali safi inayokubaliana na amri ya Mwenyezi Mungu. Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ: «MTU MWENYE AKILI NI YULE ANAYEDHIBITI NAFSI YAKE NA AKAFANYA KAZI KWA AJILI YA BAADA YA MAUTI, NA MJINGA NI YULE ANAYEFUATA NAFSI YAKE MATAMANIO YAKE NA AKATAMANI MENGI KWA MWENYEZI MUNGU».
Enyi wabebaji wa da’wa, enyi ambao Mwenyezi Mungu amewaridhia muwe askari wake katika ardhi: Fanyeni amali njema sahihi, kama alivyoiomba Mwenyezi Mungu siyo kama zinavyoona matamanio au zinavyolazimisha maslahi. Thibitini juu ya njia, takaseni nia, na shikamaneni na fikra na njia, na subiri kama walivyosubiri Mitume wenye azma.
Tuwe enyi ndugu miongoni mwa wale wanaoacha athari isiyofutika, miongoni mwa wale wanaoandika kwa damu zao na maneno yao njia ya Khilafah na ushindi, basi njia hii, hata ikirefuka, ni njia ya izza na milele, basi tushikamane na azma, na tuwe tayari kwa ajili ya siku ya kuonyeshwa kubwa, basi da’wa inaita, na ushindi unakaribia, na umma unatusubiri sisi mambo mengi.
Enyi ndugu, enyi wabebaji wa da’wa: Sikilizeni yaliyomo katika athari kutoka kwa Abu Dharr: "Fanyeni upya jahazi kwa sababu bahari ni kubwa, na zidisheni zadi kwa sababu safari ni ndefu, na takaseni amali kwa sababu mkosoaji anaona, na punguzeni mzigo kwa sababu mteremko ni mgumu", naam, basi bahari ni kubwa, na fitna zinazunguka, na watu wanahangaika, lakini nyinyi mko juu ya nuru kutoka kwa Mola wenu, basi lifanyeni jahazi lenu liwe imara lililoshikiliwa kwa kamba za imani, wala msibebe isipokuwa amali safi, basi mizani ni sahihi, na mkosoaji anaona.
Tuwe miongoni mwa watu wenye hima ya juu, tusiridhike na uduni, wala tusifanye suluhu juu ya haki, wala tusiegemee kwenye raha, basi mwenye hima ni yule aliyeiuza nafsi yake kwa Mwenyezi Mungu ili aisimamishe dini yake, anaona katika Khilafah ahadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu haina shaka ndani yake, na anajua kuwa ushindi uko pamoja na subira, na mwisho mwema ni kwa wachamungu.
Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿MKI MUNUSURU MWENYEZI MUNGU ATA KUNUSURUNI NA ATAZITHIBITISHA NYAYO ZENU﴾ basi yule ambaye amenusuriwa na Mwenyezi Mungu basi hakuna mshindi wake, na yule ambaye ameachwa na Mwenyezi Mungu basi wapi atapata ushindi?! Hakika mbele yetu kuna umma unaotamani mabadiliko, mbele yetu kuna damu huko Gaza zinaita, na mayowe kutoka msikiti wa Al-Aqsa yanaomba msaada, na uhaini unaizunguka nchi kutoka kila upande, je tumesimama kwa ajili ya haki, tukapaza sauti zetu mbele ya batili, na tukahamia kwa ajili ya kunusuru dini ya Mwenyezi Mungu?! Basi tukumbuke kauli ya Hassan Al-Basri: "Dunia ni siku tatu: Ama jana imekwenda pamoja na yaliyomo ndani yake, na ama kesho huenda hutaifikia, na ama leo ni yako basi fanya kazi ndani yake". Naam leo ni siku yetu, basi tufanye kazi ndani yake, na tutumie vizuri yaliyobakia ya umri wetu, basi tufanye kazi kwa sababu sisi tuko juu ya njia ya Nabii wetu, na hakika Mwenyezi Mungu haupotezi ujira wa yule anayetenda vyema.
Enyi ndugu enyi wabebaji wa da’wa: Naam, da’wa yetu ni nyeupe safi kama alfajiri, haichafui giza, wala haipatikani na uchafu, da’wa yetu haisimami juu ya ushabiki, wala haifungwi na mahusiano ya nasaba au maslahi au jiografia au maslahi ya kidunia, bali uhusiano wetu ni itikadi, na msingi wetu ni Uislamu, na chanzo chetu ni radhi ya Mwenyezi Mungu pekee asiye na mshirika. «KUWENI WJA WA MWENYEZI MUNGU NDUGU» hili ni wasia wa Mtume wetu ﷺ, na tunatarajia kuwa miongoni mwa wale ambao maana hii imetimia ndani yao, basi Uislamu uliunganisha undugu baina ya Ansar na Muhajirina, na walikuwa miongoni mwa mifano mikuu ya kujitolea na kuwapa wengine.
Enyi ndugu: Hakika kuibeba da’wa siyo kazi au anasa ya kiakili, bali ni amali ya Manabii na Mitume, na kurithi njia yao, na kutembea juu ya nyayo zao, basi ni heshima kubwa na jukumu zito. Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ: «LA YULE AMBAYE MWENYEZI MUNGU AMEMUONGOZA MTU KWA AJILI YAKO NI BORA KWA AJILI YAKO KULIKO UWE NA NGAMIA WENYE THAMANI», basi wangapi miongoni mwa watu leo wanahitaji uongofu? Na wangapi miongoni mwa waliodhulumiwa wanasubiri faraja kupitia mikono yetu?! Je tunaridhika kuishi bila ya lengo? Tuwe namba ya ziada katika maisha?! Umri wetu utapita na tunaulizwa: Tumefanya nini kwa ajili ya dini yetu na umma wetu?!
Hapana Wallahi, basi tuwe miongoni mwa wanaotangulia, miongoni mwa wenye kuwahi, miongoni mwa wale wanaoacha athari siyo maumivu, na wanajenga hawangojei.
Amesema Mwenyezi Mungu: ﴿SEMA HII NDIO NJIA YANGU NINAYO LINGANIA KWA MWENYEZI MUNGU JUU YA UFAHAMU﴾, basi ni njia iliyo wazi, juu ya ufahamu, hakuna utata ndani yake wala shaka, da’wa ya kusimamisha dini, na kutimiza ahadi ya Mwenyezi Mungu Subhanahu kwa Khilafah juu ya manhaj ya Utume.
Enyi ndugu: Sisi si miongoni mwa wale wanaoishi ili wale na wanywe tu, bali sisi ni umma wa ujumbe, umma wa uongozi, umma wa uongofu. Basi tuchague tuwe kama Omar na Saad na Swalahu Din na Khalid... Watu walibadilisha mkondo wa historia, waliacha alama zao nuru, na sira yao manukato, na athari yao shahidi.
Ewe unayesikia maneno haya, hima kuelekea msamaha kutoka kwa Mola wako wala usiwajali wanaokukatisha tamaa, wala usishughulike na wanaolia, bali uwe mwenge wa matumaini, na nuru ya uongofu, na tofali katika jengo kubwa la Uislamu. Basi amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ: «IKIFA MTOTO WA ADAMU AMALI YAKE HUKATIKA ILA KWA VITU VITATU: SADAKA INAYOENDELEA, AU ELIMU INAYONUFAISHA, AU MTOTO MWEMA ANAYEMUOMBEA» (Ameipokea Muslim). Na hadithi hii inatukumbusha kuwa kinachombakia mwanadamu baada ya mauti yake ni alichokitoa katika maisha yake katika athari yenye manufaa na amali njema, basi dunia ni shamba la akhera, na tunachokipanda leo tutavuna matunda yake kesho. Basi tujitahidi tuwe miongoni mwa wale wanaoacha elimu yenye manufaa katika umma, na da’wa iliyobarikiwa wanainufaika nayo vizazi, na kizazi chema kinaendeleza njia ya haki, basi hii ndiyo uwekezaji wa kweli ambao haupotezi kabisa.
Ewe Mwenyezi Mungu tufanye miongoni mwa wale wanaosikiliza kauli na wanafuata bora yake, Ewe Mwenyezi Mungu tufanye miongoni mwa wale wanaoitikia da’wa yako, na wanafanya kazi ili kusimamisha dini yako, na wanathibiti mpaka waone ushindi kwa macho yao au wakukutane na wewe nawe umeridhika nao. Ameen.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut Tahrir
Abdul Mahmoud Al-Amiri - Wilaya ya Yemen