Jimbo la Sudan: Msimamo wa Port Sudan wa Kufelisha Mpango wa Kutenganisha Darfur!
Mwitikio kwa takbira, shangwe, uungaji mkono na harakati za vyombo vya habari na kisiasa uliambatana na msimamo uliowekwa na Hizb ut-Tahrir / Jimbo la Sudan kufelisha mpango wa kutenganisha Darfur mbele ya Msikiti Mkuu katika mji wa Port Sudan. Waumini walikusanyika baada ya Sala ya Ijumaa, 20 Rabi' al-Awwal 1447 Hijria, 2025/09/12 Miladia katika Msikiti Mkuu katika mji wa Port Sudan katika msimamo uliowekwa na Hizb ut-Tahrir Jimbo la Sudan mbele ya Msikiti Mkuu kama sehemu ya kampeni inayoongozwa na chama kufelisha mpango wa kutenganisha Darfur.
Ambapo bendera za Mtume ﷺ ziliinuliwa katika msimamo huo, zikipepea angani na mabango yakitoa wito wa kufelisha mpango wa Darfur ... na kufanya kazi kwa ajili ya umoja wa umma na kusimamisha hukumu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kutekeleza sheria Zake kwa kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume.
Msemaji rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Jimbo la Sudan, Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil) alitoa hotuba mbele ya waliohudhuria, ambao waliingiliana nayo kwa takbira na shangwe, wakikataa mpango huu wa uhalifu, wakisisitiza kwamba wao ni pamoja na umoja wa umma wa Kiislamu na kusimamisha dini yake na kutekeleza sheria ya Mola wao Mtukufu. Alisema katika hotuba yake:
[Enyi watu wa Sudan: Simameni ili kufelisha mpango huu, na kuondoa mizizi ya vibaraka na wanafiki, na kurekebisha mwelekeo wa maisha yenu, kwani muumini haumwi mara mbili kutoka shimo moja, na tumeumwa kutoka shimo la Amerika kwa kuitenganisha Sudan Kusini, kwa hivyo tutairuhusu kuitenganisha Darfur?! Bukhari na Muslim wameripoti kutoka kwa Abu Huraira, Mwenyezi Mungu awe radhi naye, kutoka kwa Mtume ﷺ, kwamba alisema: "Muumini haumwi mara mbili kutoka shimo moja"].
Idadi ya tovuti za habari zimeripoti ripoti kuhusu msimamo huo, zikiambatana na picha ... Pia imeunda mwingiliano wa hali ya juu wa kisiasa na vyombo vya habari katika vikundi vya kisiasa na vya habari, ambayo iliunda harakati za kisiasa na vyombo vya habari ambavyo vilifanya suala la Darfur kuwa mbele ya macho ya watu wa nchi, labda hiyo itawahamasisha watu waaminifu kutoka kwa watu wa umma, kutoka kwa wasomi, wanasiasa, wanahabari na maafisa wa jeshi, kufelisha mpango huu wa uhalifu.
Tunamwomba Mwenyezi Mungu Mtukufu aunganishe safu za umma wa Kiislamu na kuunganisha neno lao ili kusimamisha dini yao katika dola ya Kiislamu, Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume, kwani ni yeye pekee anayeondoa mipango ya makafiri wavamizi.
Mjumbe wa Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Katika Jimbo la Sudan
Jumamosi, 20 Rabi' al-Awwal 1447 Hijria, Sawia na 12 Septemba 2025 Miladia


{gallery}2025_09_12_SDN_ACTV_PICs.{/gallery}

Kwa maelezo zaidi, tafadhali tembelea tovuti za Hizb ut-Tahrir / Jimbo la Sudan:
Tovuti Rasmi ya Hizb ut-Tahrir / Jimbo la Sudan
Kituo cha Daily Motion cha Hizb ut-Tahrir / Jimbo la Sudan
