Kutotangazwa Rasmi na Umoja wa Mataifa kwa Njaa huko Gaza Hakubadilishi Ukweli!
Habari:
Idadi ya waathiriwa wa njaa huko Gaza inaongezeka chini ya mzingiro, wakati ambapo maonyo yanaendelea kuhusu upanuzi wa wigo wa njaa huko.
Licha ya picha, habari zinazoendelea na video zinazoonyesha ukubwa wa janga hilo, Umoja wa Mataifa bado haujatangaza rasmi njaa huko Gaza kwa madai ya ukosefu wa takwimu sahihi na umeishia kutoa maonyo!
Maoni:
Inashangaza hali ya ulimwengu wetu leo, kwani licha ya kuwa umejaa picha, data, taarifa za kila siku, video, mitandao ya kijamii na mengineyo yanayoakisi ukweli, lakini Umoja wa Mataifa umeshindwa kutangaza rasmi njaa huko Gaza kwa sababu ya ukosefu wa takwimu kwa mujibu wa madai yao na kutokuwa na uwezo wa kukusanya taarifa sahihi kwa sababu ya mzingiro!
Jua haliwezi kufunikwa kwa ungo na tangazo la Umoja wa Mataifa au kutotangaza kwake hakuna faida wala madhara, habari zinazoendelea ambazo tunazipokea kila siku kuhusu vifo vya watoto wachanga, watoto na watu wazima kwa njaa na kuhusu mistari mirefu ambayo watu wa Gaza wanasimama ili kupata makombo ya chakula na picha za watoto na miili yao dhaifu iliyo wazi, inatosha kuonyesha janga na njaa ambayo watu wa Gaza wanaishi, janga liko wazi kuliko kufichwa.
Je, mazingatio ya kiufundi yasiyobadilika yanapewa kipaumbele kuliko mazingatio ya kibinadamu ya dharura, hasa kwa uwepo wa ushahidi halisi ulio wazi?
Yeyote anayejua ukweli wa mashirika ya kimataifa na jukumu lake hawezi kupuuza uwepo wa mazingatio ya kisiasa ambayo yanazuia kutolewa kwa tangazo la aina hii. Umoja wa Mataifa haujawahi kuwa mbali na usawa wa kisiasa na shinikizo la kimataifa. Uzoefu uliopita umeonyesha kuwa maamuzi ya Baraza la Usalama, au rufaa za Mahakama ya Kimataifa ya Jinai, au hata baadhi ya ripoti za Umoja wa Mataifa yenyewe, mara zote zimekuwa wazi kwa mazungumzo au usumbufu chini ya shinikizo la mikataba ya kisiasa au shinikizo kutoka kwa mataifa yenye nguvu!
Je, Umoja wa Mataifa, mkono wa Marekani, unatarajiwa kufanya kinyume na maslahi yake na kuwa na msimamo na uadilifu na kuwasaidia watu wa Gaza, na mikono ya Marekani imejaa damu ya mashahidi na ndio mshiriki katika kile kinachotokea na ndio inayoilisha taasisi ya Kiyahudi na misingi ya kuishi kwake na uimara wake?!
Ucheleweshaji wa shirika hilo kutangaza njaa unaonyesha kushindwa kimaadili katika kukabiliana na janga lililorekodiwa kwa sauti na picha, na ukweli utabaki wazi licha ya madai yao, picha za watoto wakifa kwa njaa na picha za familia zikitafuta unga kwenye takataka, na picha za mistari ya misaada iliyoshambuliwa kwa makusudi, yote hayo yatabaki akilini na yatawekwa kumbukumbu kwenye skrini za ulimwengu, na hawataweza kamwe kupotosha ukweli.
Imeandikwa kwa Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Minna Allah Taher - Jimbo la Tunisia