Ulaikishaji na Uislamu ni Vitu Viwili Visivyopatana
Ulaikishaji na Uislamu ni Vitu Viwili Visivyopatana

Habari:

0:00 0:00
Speed:
October 13, 2025

Ulaikishaji na Uislamu ni Vitu Viwili Visivyopatana

Ulaikishaji na Uislamu ni Vitu Viwili Visivyopatana

Habari:

Haraka | Viongozi wa Dini: Ushiriki mpana katika mchakato wa uchaguzi unawakilisha ujumbe wa ufahamu na uwajibikaji!! (Shirika la Habari la Iraqi (INA), Jumanne Oktoba 7, 2025)

Maoni:

Ulaikishaji unaotawala nchi unatenganisha dini na dola, hilo linamaanisha nini?

Hakika kutenganisha dini na maisha ni kutoishirikisha dini katika kusimamia masuala ya ndani na nje ya nchi, na hii ndiyo asili ya fikra za kisekula na hakuna ubishi katika uhalisia wake, hawaoni haya kusema hilo waziwazi.

Mizizi ya ulaikishaji inarejea kwenye falsafa ya Kiyunani ya kale, kwa wanafalsafa wa Kiyunani kama vile Epicurus (311 KK - 270 KK), lakini ilitoka na dhana yake ya kisasa wakati wa Zama za Mwangaza za Ulaya kuanzia 1685 BK; kutokana na Vita vya Miaka Thelathini (1618 BK - 1648 BK) kati ya Wakatoliki na Waprotestanti, ambayo ilisababisha vifo vya watu milioni 8, karibu robo au theluthi ya wakazi wa Ulaya wakati huo, jambo ambalo liliwafanya baadhi ya wasomi kutafuta njia ya kuondokana na migogoro na vita vya kidini na kimadhehebu kupitia msimamo wa upande wowote wa serikali kuelekea dini, na kutenganisha mamlaka ya kisiasa na taasisi za kidini, na ilianzishwa na idadi ya wataalamu wa Zama za Mwangaza kama vile John Locke, Denis Diderot, Voltaire, Baruch Spinoza, James Madison, Thomas Jefferson na Thomas Paine.

Cha ajabu ni kwamba baadhi ya wanaoitwa wanazuoni wa dini na ni wa taasisi ya kidini wanaona kuwa wajibu wa kidini na wa kitaifa unamlazimu mtu kushiriki katika kuwachagua watu wa kuwawakilisha katika taasisi ya kutunga sheria, ambayo ni bunge.

Inawezekanaje kwamba itikadi ambayo ulaikishaji umejengwa juu yake, ambayo ni kutenganisha dini na dola, inatumia dini kuwashawishi watu kushiriki katika kile kinachotenganisha dini yao na udhibiti au ushawishi juu ya sheria za bunge?!

Uislamu na ulaikishaji ni vitu viwili visivyopatana, basi ulaikishaji unatafutaje kwa kutumia wale unaowakataa na kukataa itikadi yao ikiwa haitoshi kuwashawishi Waislamu kuwa inawafaa?! Kwa hivyo ni kosa kubwa na ukiukaji wazi wa kisheria kutoka kwa baadhi ya wanaojinasibisha na Uislamu, na ni aibu na udanganyifu dhahiri kwa ulaikishaji na watu wake na taasisi zake kutumia hisia za Waislamu kuwahimiza kushiriki chini ya jina la ufahamu na maslahi!

Hakika Uislamu ni dini na ndio dola na ni mbinu kamili ya kutunza mambo ya watu, na hatima ya yule anayechukua sehemu yake na kuacha nyingine ni fedheha duniani na adhabu Akhera, Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Je, mnaamini baadhi ya Kitabu na mnakataa baadhi yake? Basi malipo ya afanyaye hivyo miongoni mwenu hayawi isipokuwa ni fedheha katika uhai wa dunia, na Siku ya Kiyama watapelekwa kwenye adhabu kali kabisa, na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na yale mnayoyatenda﴾.

Hakika kuchezea maelezo ya Uislamu wa Hanifa ni kosa kubwa linalobebwa na wale wanaotoa fatwa, Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Hakika wale wanao ficha yale aliyo teremsha Mwenyezi Mungu katika Kitabu, na wakanunua kwayo thamani ndogo, hao hawali matumboni mwao ila Moto, wala Mwenyezi Mungu hatawasemesha Siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watakuwa na adhabu chungu﴾.

Imeandikwa kwa ajili ya redio ya ofisi kuu ya habari ya Hizb ut-Tahrir

Wael Al-Sultan - Wilaya ya Iraq

More from null

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Habari:

Uchunguzi wa Al Jazeera, unaotegemea uchambuzi wa picha za satelaiti, umefichua mifumo ya uharibifu wa kimfumo iliyofanywa na uvamizi huko Gaza kati ya Oktoba 10 na 30 iliyopita.

Shirika la "Sanad" la uhakiki wa habari la mtandao wa Al Jazeera limegundua operesheni za ulipuaji, ubomoaji wa kihandisi na mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na uvamizi ndani ya Ukanda huo tangu kuanza kutekelezwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. (Al Jazeera Net)

Maoni:

Baada ya kutangazwa kwa usitishaji wa vita vilivyojaa mabomu dhidi ya Ukanda wa Gaza chini ya usimamizi wa Trump na kwa makubaliano na baadhi ya nchi za Kiarabu, ilikuwa wazi kuwa ilifikiwa kwa faida ya taasisi ya Kiyahudi. Hili limebainika kulingana na uchambuzi wa picha za satelaiti na ripoti za hivi karibuni za habari, kwamba jeshi la Kiyahudi lililipua maelfu ya majengo huko Gaza, haswa huko Shuja'iyya na Khan Yunis katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao, na vile vile Rafah, na maeneo yaliyo mashariki mwake ambayo yalishuhudia operesheni kubwa za uharibifu.

Uharibifu mkubwa huko Gaza sio wa bahati mbaya, lakini una malengo ya kimkakati ya muda mrefu, kama vile kuharibu mazingira yanayounga mkono upinzani. Kuondoa Gaza ya miundombinu yake, shule zake na makazi yake, inafanya kuwa ngumu kwa upinzani kujipanga upya au kujenga upya uwezo wake. Hii ni kizuizi cha muda mrefu kwa kuharibu uwezekano na kulazimisha ukweli mpya ambao unaifanya Gaza kuwa dhaifu na kuiacha ikiwa imepooza kiuchumi na haifai kwa makazi, ambayo huandaa njia ya kukubali suluhisho zozote za kisiasa au kiusalama, au hata kukubali wazo la uhamishaji, kwa sababu kuacha Gaza kama kifusi, inafanya kuwa ngumu kwa ujenzi kuwa mikononi mwa watu wake pekee. Badala yake, nchi na mashirika yataingilia kati kwa masharti ya kisiasa, na uvamizi unatambua kuwa yeyote anayejenga upya ndiye anayemiliki uamuzi. Hivyo basi uharibifu wa leo ni sawa na udhibiti wa kisiasa kesho!

Kwa kweli, kuelezea makubaliano ya kusitisha vita dhidi ya Gaza kama "yenye mabomu" haikuwa bure, kwa sababu ilikuwa ya sehemu, na malengo ya madai ya kijeshi hayakujumuishwa, ambayo inaruhusu Wayahudi kuendelea na uvamizi na uharibifu kwa kisingizio cha kiusalama. Vivyo hivyo, ilifikiwa na nchi kubwa zaidi inayounga mkono taasisi bila dhamana thabiti za kimataifa, ambayo inafanya kuwa dhaifu na inakabiliwa na ukiukwaji, haswa kwa kukosekana kwa uwajibikaji wa kimataifa, ambayo inafanya taasisi ya Kiyahudi kuwa juu ya uwajibikaji.

Tutaendelea kuwa taifa lenye unyenyekevu na linalokubali, tukitazama watu waliodhoofika, waliochoka, waliopotea na wenye njaa mpaka lini?! Na juu ya yote hayo, wanaruhusiwa wakati wowote?! Hebu sote tuwe Saladin al-Ayyubi, kwa sababu Gaza leo inakumbusha taifa kwamba Saladin hakuwa tu mtu shujaa, lakini alikuwa kiongozi katika dola iliyokuwa na mradi na jeshi na taifa moja nyuma yake. Kwa hivyo, wito wa kuwa Saladin haimaanishi ushujaa wa mtu binafsi, lakini kufanya kazi ya kuanzisha dola ambayo inafanya watoto wote wa taifa kuwa askari katika safu moja chini ya bendera moja.

Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Mna nini hamkupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya wanyonge miongoni mwa wanaume na wanawake na watoto﴾.

Imeandikwa kwa Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Manal Um Ubaidah

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Habari:

Kituo cha Yemen Sana'a kilirusha hewani Jumatano jioni, 2025/11/12, kipindi cha kibinadamu "Nchi Yangu", na katika sehemu ya "Tuko nanyi", kipindi kilionyesha kesi ya mwanamke ambaye alikuwa ameambukizwa ugonjwa adimu na alihitaji kusafiri kwenda India kwa gharama ya dola elfu 80, ambapo kiasi cha dola elfu 70 kilikusanywa kutoka kwa mashirika na wahisani, lakini mtangazaji wa kipindi alizungumzia sana sifa za mchangiaji wa mwisho wa dola elfu kumi, na ikawa wazi kuwa alikuwa Abdul Malik al-Houthi, na alisifu jukumu lake la mara kwa mara katika kusaidia kesi za kibinadamu ambazo zinaonekana kwenye kipindi.

Maoni:

Hakika, mtawala katika Uislamu ana jukumu kubwa, ambalo ni kutunza maslahi ya watu kwa kutumia kile kinachowanufaisha na kutoa kila kitu kinachowafariji. Kimsingi yeye ni mtumishi wao, na hawezi kufurahia maisha hadi atakapohakikisha hali zao. Jukumu hili sio ihsani au upendeleo, bali ni wajibu wa kisheria ambao Uislamu umemlazimisha, na anahesabiwa kuwa amepungukiwa ikiwa atalipuuza. Uislamu umewajibisha umma kumuwajibisha anapopungukiwa. Amani na baraka zimshukie: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, ni upuuzi kufurahia usikivu wa watawala au serikali kwa mahitaji fulani na kuita hiyo kazi ya kibinadamu, wakati kimsingi ni kazi ya kichungaji ya lazima.

Moja ya dhana hatari zaidi ambayo imekita mizizi na ubepari na utawala wake duniani ni kukataa kwa serikali kutunza watu na kuacha utunzaji wa watu kwa mashirika na vyama vya hisani vinavyoendeshwa na watu binafsi au vikundi, na watu huenda kwao mara nyingi kuwasaidia na kutimiza mahitaji yao. Wazo la vyama lilionekana kwanza huko Uropa wakati wa Vita vya Ulimwengu, ambapo familia nyingi zilipoteza wazazi wao na zikawa zinahitaji mlinzi, na serikali, kulingana na mfumo wa kidemokrasia wa kibepari, haitunzi masuala, bali ni mlinzi wa uhuru tu. Matajiri waliogopa mapinduzi ya maskini dhidi yao, kwa hivyo walianzisha vyama hivi.

Uislamu umefanya kuwepo kwa sultani kuwa wajibu wa kutunza masuala ya umma ili kuhifadhi haki zao za kisheria na kukidhi mahitaji yao sita ya msingi ambayo lazima yakidhiwe kwa watu binafsi na vikundi; chakula, mavazi na makazi lazima yatolewe na serikali kwa kila mtu mmoja mmoja, Waislamu na wasio Waislamu, na usalama, matibabu na elimu hutolewa na serikali bure kwa wote. Mtu mmoja alikuja kwa Khalifa wa Waislamu, Omar bin al-Khattab, Mungu amuwiye radhi, akiwa na mke wake na binti zake sita, akasema: (Ewe Omar, hawa ni binti zangu sita na mama yao, walishe, wavishe na uwe ngao kwao kutoka kwa wakati) Omar akasema: (Na vipi ikiwa sitafanya hivyo?!) Bedui akasema: (Nitakwenda) Omar akasema: (Na vipi ikiwa utakwenda?) Akasema: (Utaulizwa kuhusu hali yao Siku ya Kiyama, ukisimama mbele ya Mungu ama kuelekea Motoni au Paradiso), Omar akasema: (Umma huu hautapotea maadamu kuna watu kama hawa).

Enyi Waislamu: Hii sio ndoto, bali ni Uislamu ambao umefanya utunzaji kuwa wajibu kwa Khalifa wa Waislamu kwa kila mtu mmoja mmoja, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehma na amani zimshukie, alisema: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, lazima turudishe hukumu hizi na kuzifanya ziwe za utekelezaji, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: ﴿Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyomo kwa watu mpaka wabadili yaliyomo katika nafsi zao﴾. Hivyo, kitakachobadilisha hali yetu kuwa haki na ustawi ni Uislamu.

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Sadiq al-Sarari