Ulaikishaji na Uislamu ni Vitu Viwili Visivyopatana
Habari:
Haraka | Viongozi wa Dini: Ushiriki mpana katika mchakato wa uchaguzi unawakilisha ujumbe wa ufahamu na uwajibikaji!! (Shirika la Habari la Iraqi (INA), Jumanne Oktoba 7, 2025)
Maoni:
Ulaikishaji unaotawala nchi unatenganisha dini na dola, hilo linamaanisha nini?
Hakika kutenganisha dini na maisha ni kutoishirikisha dini katika kusimamia masuala ya ndani na nje ya nchi, na hii ndiyo asili ya fikra za kisekula na hakuna ubishi katika uhalisia wake, hawaoni haya kusema hilo waziwazi.
Mizizi ya ulaikishaji inarejea kwenye falsafa ya Kiyunani ya kale, kwa wanafalsafa wa Kiyunani kama vile Epicurus (311 KK - 270 KK), lakini ilitoka na dhana yake ya kisasa wakati wa Zama za Mwangaza za Ulaya kuanzia 1685 BK; kutokana na Vita vya Miaka Thelathini (1618 BK - 1648 BK) kati ya Wakatoliki na Waprotestanti, ambayo ilisababisha vifo vya watu milioni 8, karibu robo au theluthi ya wakazi wa Ulaya wakati huo, jambo ambalo liliwafanya baadhi ya wasomi kutafuta njia ya kuondokana na migogoro na vita vya kidini na kimadhehebu kupitia msimamo wa upande wowote wa serikali kuelekea dini, na kutenganisha mamlaka ya kisiasa na taasisi za kidini, na ilianzishwa na idadi ya wataalamu wa Zama za Mwangaza kama vile John Locke, Denis Diderot, Voltaire, Baruch Spinoza, James Madison, Thomas Jefferson na Thomas Paine.
Cha ajabu ni kwamba baadhi ya wanaoitwa wanazuoni wa dini na ni wa taasisi ya kidini wanaona kuwa wajibu wa kidini na wa kitaifa unamlazimu mtu kushiriki katika kuwachagua watu wa kuwawakilisha katika taasisi ya kutunga sheria, ambayo ni bunge.
Inawezekanaje kwamba itikadi ambayo ulaikishaji umejengwa juu yake, ambayo ni kutenganisha dini na dola, inatumia dini kuwashawishi watu kushiriki katika kile kinachotenganisha dini yao na udhibiti au ushawishi juu ya sheria za bunge?!
Uislamu na ulaikishaji ni vitu viwili visivyopatana, basi ulaikishaji unatafutaje kwa kutumia wale unaowakataa na kukataa itikadi yao ikiwa haitoshi kuwashawishi Waislamu kuwa inawafaa?! Kwa hivyo ni kosa kubwa na ukiukaji wazi wa kisheria kutoka kwa baadhi ya wanaojinasibisha na Uislamu, na ni aibu na udanganyifu dhahiri kwa ulaikishaji na watu wake na taasisi zake kutumia hisia za Waislamu kuwahimiza kushiriki chini ya jina la ufahamu na maslahi!
Hakika Uislamu ni dini na ndio dola na ni mbinu kamili ya kutunza mambo ya watu, na hatima ya yule anayechukua sehemu yake na kuacha nyingine ni fedheha duniani na adhabu Akhera, Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Je, mnaamini baadhi ya Kitabu na mnakataa baadhi yake? Basi malipo ya afanyaye hivyo miongoni mwenu hayawi isipokuwa ni fedheha katika uhai wa dunia, na Siku ya Kiyama watapelekwa kwenye adhabu kali kabisa, na Mwenyezi Mungu si mwenye kughafilika na yale mnayoyatenda﴾.
Hakika kuchezea maelezo ya Uislamu wa Hanifa ni kosa kubwa linalobebwa na wale wanaotoa fatwa, Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Hakika wale wanao ficha yale aliyo teremsha Mwenyezi Mungu katika Kitabu, na wakanunua kwayo thamani ndogo, hao hawali matumboni mwao ila Moto, wala Mwenyezi Mungu hatawasemesha Siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watakuwa na adhabu chungu﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya ofisi kuu ya habari ya Hizb ut-Tahrir
Wael Al-Sultan - Wilaya ya Iraq