Chaguzi za Kidemokrasia Sio Chochote Ila Ni Vishawishi Vya Shetani
(Kimetafsiriwa)
Habari:
Mnamo Septemba 13, 2025, kampeni ya uchaguzi wa rais ilizinduliwa rasmi Zanzibar, ambapo chama tawala, Chama Cha Mapinduzi, na chama cha upinzani, Alliance for Change and Transparency, walizindua kampeni zao. Chama Cha Mapinduzi kilisisitiza "utulivu", "amani" na "umoja", huku chama cha Alliance for Change and Transparency kiliweka kipaumbele uwajibikaji, usawa na fursa za kiuchumi.
Maoni:
Kipindi cha kampeni za uchaguzi nchini Tanzania kinaisha tarehe 28 Oktoba 2025, ambapo tarehe 27 Oktoba 2025 itakuwa siku ya kupiga kura kwa uchaguzi wa Zanzibar, huku siku ya Jumatano tarehe 29 Oktoba 2025 itakuwa siku ya kupiga kura kwa uchaguzi wa Tanzania, kulingana na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi nchini Tanzania. Hii ni uchaguzi wa tano wa vyama vingi tangu Tanzania ilipoamua kukumbatia demokrasia ya vyama vingi mwaka 1992. Uchaguzi wa mwaka huu ulionekana kufanana na chaguzi zilizopita, huku kukiwa na hali ya kutojali, kukabiliana na kususia, na kuwepo hisia za wasiwasi ambazo zilionekana kuwa uchaguzi haukuwa huru na wa haki, kutokana na kutofanyika mageuzi ya uchaguzi.
Suala la demokrasia na kila kinachohusiana nayo, kama vile ushiriki na kuunga mkono kampeni za kidemokrasia na chaguzi zake, ni jambo lililo wazi katika Uislamu. Ambapo Uislamu unaharamisha kupiga kura kwa mfumo usio wa Kiislamu, na hairuhusiwi kuutekeleza au kuutoa wito. Kwa mtazamo mpana zaidi, haifai kutekeleza, kushiriki, kukumbatia au kutoa wito kwa mfumo wowote unaokhalifu Uislamu.
Sheria na hukumu katika Uislamu haziwezi kutolewa kutoka kwa mfumo wa kimanadamu, kama vile demokrasia, ambao ni mfumo wa kisiasa wa kibepari, bali lazima utoke kwa Mwenyezi Mungu pekee. Kwa hivyo, mfumo wowote wa kisiasa, kijamii au kiuchumi ambao haujajengwa juu ya sheria ya Kiislamu hauna nafasi katika Uislamu, na lazima ukataliwe. Kwa hakika, watu wa kawaida wanatambua, iwe Zanzibar, Tanzania, Afrika au ulimwenguni kote, kwamba demokrasia imewaangusha. Zaidi ya hayo, hakuna tofauti kati ya chama tawala na upinzani, vyama vyote vya siasa za kidemokrasia vinategemea misingi ileile ambayo itikadi ya kibepari ya kimagharibi ya kikoloni inategemea, ambayo inatokana na maslahi binafsi, unyonyaji na kutenganisha dini na maisha ya watu.
Nchi nyingi za Afrika zinaongozwa, isipokuwa nchi chache kama vile Tanzania, na kile ambacho hapo awali kiliitwa vyama vya upinzani, lakini hakuna kitu kilichopatikana ndani yake. Pamoja na hayo yote, Afrika inachukuliwa kuwa bara maskini zaidi licha ya kuwa na rasilimali nyingi za asili, ambazo zinachukuliwa bure na wakoloni wa Magharibi, kupitia ukoloni mamboleo, kupitia wanasiasa tunaowachagua mara kwa mara chini ya demokrasia!
Afrika na ulimwengu hauhitaji uchaguzi wa kilimwengu wa udanganyifu ambao hufanya kazi tu kwa ajenda ya kikoloni ya unyonyaji bila kuleta uamsho wowote wa kweli kwa watu.
Kanuni na mfumo mbadala wa kisiasa lazima utoke katika Uislamu. Chini ya Uislamu, ambao ni ufunuo kutoka kwa Mwenyezi Mungu, uongozi wa kisiasa wa Kiislamu utaanzishwa barani Afrika, chini ya Khilafah ya kimataifa. Ndipo Afrika na ulimwengu utakapokombolewa kutoka kwa minyororo ya uovu na mfumo wa kisiasa wa kidemokrasia wa unyonyaji, na utashuhudia uongozi wa kweli na maendeleo ya haraka, kinyume na uharibifu, ucheleweshaji, umaskini uliokithiri na unyonyaji ambao uvamizi wa kikoloni ulileta mwishoni mwa karne ya kumi na tisa BK na hadi sasa.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut Tahrir
Saeed Bitumwa
Mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir nchini Tanzania