Hadithi Tukufu
Kunong'ona Kati ya Watu
Tunawasalimu nyote wapenzi popote mlipo, katika kipindi kipya cha kipindi chenu "Pamoja na Hadithi Tukufu" na tunaanza na salamu bora, Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Malik amenisimulia kutoka kwa Nafi', kutoka kwa Abdullah bin Omar, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu, swallallahu alayhi wasallam, alisema: "Wakiwa watatu, basi wasinong'one wawili wakamwacha mmoja". (Muwatta Malik 1816)
Hakika bora ya maneno ni maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, na bora ya uongofu ni uongofu wa Nabii wake, rehema na amani zimshukie, Muhammad bin Abdullah, ama baada ya hayo:
Hakika hadithi hii tukufu inakataza tabia iliyoenea miongoni mwa watu na imeenea katika jamii zetu, ambayo ni kumtenga mtu mmoja kutoka kwa mazungumzo kwa sababu moja au nyingine, nayo ni kunong'ona, ambayo hupelekea katika dhambi, na hupelekea katika matatizo ambayo hayana mwisho mwema.
Ikiwa mmoja wetu atanong'ona na mwingine au wengine huku akimtenga mtu mmoja, hapa shetani anaweza kuingia kati yetu na kunong'oneza katika vifua na kuchochea chuki na dhana mbaya, kwa hivyo Uislamu ulikuja na kukataza hilo. Tunapaswa kukata njia ya shetani kuelekea nafsi zetu, na kujenga uaminifu katika nafsi zetu kwa kila mmoja.
Hukumu hii inakata njia kwa shetani na inahifadhi nafsi, hakika Uislamu ni kuzifunza nafsi, na kukata chuki na njia za shetani, kwa hivyo inahifadhi mahusiano kati ya watu.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu atusaidie kutumia Uislamu katika kila jambo dogo na kubwa katika maisha yetu, na tuwe miongoni mwa wenye kushikamana na sheria zake, wenye kufuata njia ya Nabii wetu mteule na wenye kuifuata kwa uadilifu, Allahumma Aamin.
Ndugu zetu waheshimiwa, na hadi tutakapokutana nanyi na hadithi nyingine ya kinabii, tunawaacha katika uangalizi wa Mwenyezi Mungu, na Assalamu Alaikum Warahmatullahi Wabarakatuh.
Imeandikwa kwa ajili ya redio na: Dk. Maher Saleh