Majasusi Wadogo Wanauawa, Huku Majasusi Wakubwa Wakitawala Nchi za Kiislamu kwa Msaada wa Wafuasi Wao Wanafiki
(Imetafsiriwa)
Habari:
Kufuatia mashambulizi ya chombo cha Kiyahudi dhidi ya Iran ambayo yalijumuisha operesheni za uharibifu kwa ndege zisizo na rubani na magari yaliyojazwa mabomu, kichwa cha habari cha Shirika la Habari la CNN mnamo Juni 17 kilisema kwamba (wazimu wa Iran dhidi ya Mossad unaongezeka, huku kukiwa na hofu ya majasusi wa Israeli wamevaa "barakoa, kofia na miwani ya jua").
Maoni:
Hofu ya ujasusi wa nguvu za kigeni kwenye nchi ni jambo la halali katika nchi yoyote. Chombo cha Kiyahudi kinapeleleza Iran, na Iran ina majasusi wake katika chombo cha Kiyahudi, lakini kinachofanya nchi za Waislamu ziwe hatarini kwa majasusi na wasaliti sio wale waliofichika, bali wale wanaofanya usaliti mkubwa kwa kukabidhi ardhi yote ya Waislamu kwa Magharibi. Hao ndio watawala wanaojizungusha na wanafiki ambao wanashindana kuwasifu na kuwavuruga watu kutoka kwa uhalifu wao kwa uzalendo bandia. Miongoni mwa haya ni kuwafuatia na kuwaadhibu majasusi wanaofichua siri za nchi, huku watawala wenyewe wakitangaza kila kitu kwa mameneja wao katika Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA).
Usaliti wa watawala hawa unadhihirika katika kuandaa kwao kambi za kijeshi za Kimarekani makafiri ambazo zilitumiwa kuleta mauti na uharibifu kwa Waislamu, na nyingi kati ya hizo zinatumika, au zinaandaliwa kutumika, sasa dhidi ya watu wa Iran. Nchini Uturuki, chini ya uongozi wa Erdogan, Amerika inaendesha Kambi ya Anga ya Incirlik, kituo kikuu cha Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) ambacho kina silaha za nyuklia za kimbinu. Qatar, inayoongozwa na Amir Tamim bin Hamad Al Thani, inaandaa Kambi ya Anga ya Al Udeid, kituo kikubwa zaidi cha kijeshi cha Marekani katika Mashariki ya Kati, na inafanya kazi kama kituo cha kamandi na vifaa vya kikanda. Nchini Kuwait, inayoongozwa na Meshal Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah, kambi kama vile Camp Arifjan, Kambi ya Anga ya Ali Al Salem na Camp Buehring zinaunga mkono vifaa na utayarishaji wa vikosi. Falme za Kiarabu, inayoongozwa na Mohammed bin Zayed Al Nahyan, inaandaa Kambi ya Anga ya Al Dhafra, inayotumiwa katika operesheni za ndege zisizo na rubani, upelelezi na matangi ya mafuta. Nchini Bahrain, inayoongozwa na Mfalme Hamad bin Isa Al Khalifa, Shughuli ya Msaada wa Wanamaji huko Bahrain na Kambi ya Anga ya Isa inaunga mkono Fleet ya 5 ya Amerika na operesheni za wanamaji za kikanda. Oman, inayoongozwa na Sultan Haitham bin Tariq, inaruhusu ufikiaji wa Kambi ya Anga ya Thumrait na Kisiwa cha Masirah kwa ajili ya kuongeza mafuta na vifaa. Nchini Saudi Arabia, inayoongozwa na Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud, Kambi ya Anga ya Prince Sultan inaunga mkono operesheni za anga za Marekani. Iraq, inayoongozwa na Waziri Mkuu Mohammed Shia al-Sudani, inaandaa vikosi vya Marekani katika kambi za Al Asad, Ain al-Asad na Kambi ya Anga ya Erbil kwa ajili ya mafunzo na misheni za operesheni za siri. Ama Jordan, inayoongozwa na Mfalme Abdullah II, inaruhusu ufikiaji wa Kambi ya Anga ya Muwaffaq Salti, Kambi ya Anga ya King Faisal na Kituo cha Operesheni Maalum (KASOTC), ikisaidia operesheni za ndege zisizo na rubani na mafunzo ya vikosi maalum. Ama nchini Syria, inayoongozwa na Bashar al-Assad, vikosi vya Marekani vimeendelea kuwepo katika kambi ya Al-Tanf kwa kisingizio cha kupambana na Al-Qaeda, na inaonekana mrithi wa Bashar ana hamu zaidi ya kuhudumia maslahi ya Magharibi. Hatimaye, Djibouti, inayoongozwa na Rais Ismail Omar Guelleh, inaandaa Camp Lemonnier, kambi ya pekee ya kudumu ya Marekani barani Afrika, ambayo inafanya kazi kama kituo cha ndege zisizo na rubani na operesheni maalum katika Pembe ya Afrika na Rasi ya Arabia.
Licha ya usaliti wote uliowekwa wazi kwenye meza ya nchi za Waislamu ambapo maadui zetu wanashindana kuandaliwa karamu juu yetu, watawala na wanafiki wao hawaoni aibu kuunda hadithi zisizoisha na migogoro ya uongo katika majaribio yao ya kukengeusha umma. Mtume ﷺ alisema: «Karibu mataifa yatakualika kama vile wanaokula wanavyoalikana kwenye sahani yao» Msemaji mmoja akasema: Je, tutakuwa wachache siku hiyo? Akasema: «Bali mtakuwa wengi siku hiyo lakini mtakuwa povu kama povu la maji, na Mwenyezi Mungu ataondoa kutoka katika vifua vya adui zenu hofu yenu, na Mwenyezi Mungu atatupa udhaifu katika mioyo yenu». Msemaji mmoja akasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, udhaifu ni nini? Akasema: «Kupenda dunia na kuchukia mauti». Vijana mashujaa wa umma huu wamethibitisha katika medani za mapambano kwamba kupenda dunia hakujajaza mioyo yao, lakini majeshi ya wanafiki wanaowazunguka watawala wafisadi ni mengi, na kazi yao katika kueneza ufisadi na fitna imeenea. Tunamuomba Mwenyezi Mungu atunusuru dhidi ya upotofu wao na ufisadi wao.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir
Dkt. Abdullah Rubin