Je, haijafika wakati kwetu kumtegemea Mwenyezi Mungu kisha umma bora uliotolewa kwa watu, wala si makafiri na vibaraka wao?
Habari:
Wakati awamu ya kwanza ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya Hamas na shirika la Kiyahudi ikiendelea, ambayo ilianza kutekelezwa mnamo Oktoba 10, licha ya vikwazo na ukiukwaji, mazungumzo kuhusu awamu ya pili yanaendelea pia.
Katika muktadha huu, ujumbe kutoka Hamas uliongozwa na Khalil al-Hayya, mwanachama wa ofisi ya kisiasa ya Hamas, na ujumbe kutoka Fatah uliongozwa na Makamu wa Rais wa Palestina Hussein al-Sheikh, na mkurugenzi wa ujasusi wa Palestina Majid Faraj, walikutana nchini Misri.
Kulingana na kituo cha "Cairo News" cha Misri, pande hizo mbili zilijadili awamu ya pili ya makubaliano ya kusitisha mapigano, na hali katika Gaza baada ya kusitishwa kwa mapigano.
Lakini shirika la Kiyahudi lilivunja usitishaji mapigano mara kwa mara, na makumi ya Wapalestina walipoteza maisha yao katika mashambulizi yaliyofanywa. Shirika la Kiyahudi liliruhusu tu malori 986 kuingia kati ya malori 6,600 ambayo yalipaswa kuingia Ukanda wa Gaza kati ya Oktoba 10, tarehe ya kuanza kutumika kwa kusitisha mapigano, na Oktoba 20.
Awamu ya pili ya makubaliano ya kusitisha mapigano inaangazia mambo kama vile kuondoa silaha kwa Hamas, kupelekwa kwa kikosi cha kimataifa cha kulinda amani huko Gaza, kuanzishwa kwa utawala wa mpito, na ujenzi mpya. (TRT Haber, 2025/10/23).
Maoni:
Zaidi ya miaka miwili imepita tangu mauaji, uharibifu, na mauaji ya kimbari yaliyofanywa na shirika la Kiyahudi katika vita vyake dhidi ya watu wa Gaza, na katika kipindi hiki ulimwengu wote ulishuhudia uhalifu huu mbaya na hatukuona hatua yoyote kutoka kwa watawala wasaliti wa Waislamu kuuzuia. Mbaya zaidi, Sisi, dikteta wa Misri, hakufyatua risasi moja dhidi ya shirika la Kiyahudi kuwasaidia watu wetu huko Gaza, lakini aliwanyima hata kipande cha mkate na tone la maji. Hili halifichiki kwa mtu yeyote. Kwa upande mwingine, ukatili, uchoyo, kiburi na chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu, kutofuata makubaliano yoyote, na kutenda ukatili usioweza kufikiria kwa upande wa shirika la Kiyahudi linalokalia ardhi, si siri. Si siri kwa mtu yeyote kwamba watawala wa Waislamu, hasa mjinga aliye madarakani Palestina, hawajafanya chochote isipokuwa matamko matupu kwa watu wetu huko Gaza wakati wa vita vilivyodumu kwa zaidi ya miaka miwili, na hawakujali madai ya Waislamu, na walipendelea neno la Trump kuliko neno la Mwenyezi Mungu, na walikimbilia kukutana naye kwa mwaliko wake, na bado wanaunga mkono shirika la Kiyahudi moja kwa moja au isiyo moja kwa moja.
Ndiyo, tunaumia sana na mateso ya watu wa Gaza na tunahisi hasira kali dhidi ya watawala wasaliti ambao hawawasaidii. Tunaona kwamba kutelekezwa kwa watu wa Gaza na watawala wasaliti na vibaraka wa Waislamu ni usaliti mkubwa zaidi kwa Mwenyezi Mungu, Mtume wake, na waumini. Je, usaliti wao unahalalisha kuzunguka kwenye korido za Amerika ya kikafiri na vibaraka wake, na kujisalimisha kwa masharti ya makubaliano yaliyopendekezwa na Amerika kichwa cha ukafiri, na kuketi kwenye meza moja na shirika la Kiyahudi, na kupuuza amri za Mungu, na kupuuza madai ya umma ambao Mungu ameuita umma bora?
Hata hivyo, je, msimamo wa Kiislamu si kumtumaini Mungu, kushikamana na amri za Mungu na madai ya Waislamu, kutokuwaamini au kuwatii makafiri na vibaraka wao, na kukataa masharti ya makubaliano yao ya kishetani? Waislamu wanapojikuta hawana uwezo na katika hali ngumu, je, kimbilio lao pekee si Mungu, na kimbilio lao pekee si umma wa Kiislamu na majeshi yake? Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: ﴿Wala usiwatii makafiri na wanafiki, na uache maudhi yao, na umtegemee Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mtegemewa wa kutosha﴾.
Ukweli ni kwamba ikiwa masharti ya awamu ya pili ya makubaliano yatakubaliwa, haswa kifungu kinachohusiana na kuweka chini silaha, basi shirika la Kiyahudi, kama kawaida, halitawahi kuzingatia makubaliano haya na halitaacha ukatili wake. Kama vile alivyoivunja awamu ya kwanza ya makubaliano na kuwachinja makumi ya Waislamu wasio na hatia, ataendelea kufanya hivyo. Kwa hiyo, makundi na ujumbe wote wa Kiislamu, pamoja na ujumbe wa Hamas, hawapaswi kupoteza ushujaa wa wapiganaji wa Gaza, uvumilivu wao, uthabiti wao, na imani yao kali kwa Mungu katika korido na meza za makafiri na vibaraka wao. Ikiwa kweli wanataka ubora na ushindi, wanapaswa kumgeukia Mungu, umma wa Kiislamu, na majeshi ya umma, na wawaamini peke yao, na wasiombe msaada isipokuwa kutoka kwao. Ndipo tu ushindi wa Mungu utakuja bila shaka, na itakuwa suala la muda kabla ya dola ya Khilafa Rashidah kuanzishwa kwa mbinu ya Utume, ambapo hukumu za Uislamu zitatekelezwa, dawa pekee ya ukombozi wa umma wa Kiislamu na ubinadamu wote, kwa sababu Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Mkimnusuru Mwenyezi Mungu, Yeye atakunusuruni na atafanya imara nyayo zenu﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya redio ya ofisi ya habari kuu ya Hizb ut-Tahrir
Ramadhan Abu Furqan