Wanamgambo wenye silaha ni uovu ambao lazima uondolewe na sio kuondolewa tu kutoka mji mkuu!
Habari:
Rais wa Baraza la Utawala la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, alitoa, Ijumaa, uamuzi wa kuondoa mji mkuu wa Sudan, Khartoum, kutoka kwa miundo ya kijeshi ndani ya wiki mbili. (Sudan Tribune, 18/7/2025)
Maoni:
Wanamgambo na harakati za silaha zimekuwa kisu cha sumu mwilini mwa Sudan, zikikata sehemu zake na kuharibu muundo wake wa kijamii, badala yake adui kafiri mkoloni anazitumia kutekeleza mipango yake michafu.
Kusini ilitengwa kwa ushirikiano wa Vuguvugu la Watu na serikali ya al-Bashir chini ya uangalizi wa Marekani kwa kupanga mazungumzo katika kile kilichoitwa Mkataba mbaya wa Naivasha wa 2005, na watawala hao hao ndio walioanzisha Kikosi cha Msaada wa Haraka ili kutekeleza jukumu hilo hilo chafu kama inavyotokea sasa huko Darfur la kujiandaa kwa uvunjaji na kujitenga, pia chini ya uangalizi wa Marekani.
Kwa bahati mbaya, wanamgambo hawa wanaanzishwa ama chini ya udhamini na usimamizi wa watawala vibaraka au chini ya kusikia na kuona kwao. Hawa hapa wanamgambo wanaongezeka sana kaskazini, mashariki na magharibi mwa Sudan kwa uungaji mkono wa kamanda wa jeshi na serikali yake.
Lau si malalamiko mengi kutoka kwa watu wa maeneo mbalimbali ya Khartoum, kuhusu vitendo vya wizi na uporaji mkubwa uliofanywa na wanachama wa jeshi na vikundi vinavyoliunga mkono na watu wasio waaminifu, wakichukua fursa ya hali ya ombwe la usalama na udhaifu wa ufanisi wa vyombo vya polisi, rais wa Baraza la Utawala asingechukua uamuzi huu.
Asili ya wanamgambo hawa ni ama kujiunga na jeshi ili jeshi liwe kitu kimoja chini ya uongozi mmoja, au kuvunjwa na watu wao kufanya maisha yao ya kawaida kama watu wengine wa nchi. Uislamu unakataza taifa kugawanyika katika wanamgambo na mashirika yenye silaha, Mtume ﷺ anasema kuhusu Arfaja bin Asad: "Yeyote atakayekujieni na amri yenu yote iko kwa mtu mmoja, akitaka kuvunja fimbo yenu, au kutenganisha kundi lenu, basi muuweni." Muslim alisimulia.
Kuenea kwa wanamgambo hawa ni moja ya dhihirisho la kutokuwepo kwa dola ya Kiislamu ya Khilafah Rashidun juu ya njia ya unabii ambayo ikiwa itasimamishwa jeshi litakuwa lenye nguvu, la kutisha na la umoja.
Huu ndio wajibu wa umma leo; kurejesha faradhi hii kuu; Khilafah Rashidun juu ya njia ya unabii. Mtume ﷺ anasema: "Hakika yeyote kati yenu atakayeishi baada yangu ataona tofauti nyingi, basi shikamaneni na sunna yangu na sunna za Makhalifa Waongofu, shikamaneni nazo kwa magego." Abu Daud, al-Tirmidhi, Ibn Majah, na Ahmad wamesimulia.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Muhammad Jami (Abu Ayman)
Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan