Ukandamizaji wa Kisiasa wa Upinzani unaounga mkono Wapalestina nchini Uingereza
(Imetafsiriwa)
Habari:
Mnamo Julai 5, 2025, serikali ya Uingereza ilitangaza kupiga marufuku shirika la Palestine Action, ambalo ni shirika la kampeni ya amani linalolenga msaada wa kijeshi unaotolewa na Uingereza kwa taasisi ya Kiyahudi inayofanya mauaji ya kimbari huko Gaza, ilitangaza marufuku yake chini ya Sheria ya Kupambana na Ugaidi, na kufanya usemi wa msaada kwa shirika hilo kuwa haramu na kuadhibiwa na kifungo cha hadi miaka 14 jela. Waziri wa Mambo ya Ndani, Evette Cooper, alilipiga marufuku shirika hilo baada ya wanachama wake kupaka rangi nyekundu kwenye ndege za Jeshi la Anga la Kifalme la Uingereza, lakini wakosoaji walisema kuwa kitendo hicho kilikuwa uharibifu wa mali, sio vurugu.
Katika wiki zilizofuata, polisi waliwakamata zaidi ya watu 100 kote nchini chini ya sheria za kupambana na ugaidi, akiwemo kasisi mwenye umri wa miaka 83 na wastaafu kutoka dhehebu la Quaker. Hata maafisa wenye silaha walitishia kuwakamata wale waliobeba mabango yaliyoandikwa "Waacheni huru Gaza" au "Mauaji ya Kimbari".
Maoni:
Lengo la kwanza lilikuwa upinzani wa Kiislamu kwa Uzayuni, lakini sasa zamu ya siasa za mrengo wa kushoto imefika nchini Uingereza. Ukandamizaji huu wa kikatili wa maandamano ya amani dhidi ya mauaji ya kimbari chini ya kivuli cha kukabiliana na ugaidi ni sehemu ya kampeni iliyo na mizizi ya kupotosha ukosoaji wowote mkubwa wa taasisi ya Kiyahudi kama chuki dhidi ya Wayahudi, ambayo ni mama wa uhalifu. Kuheshimu Wayahudi kama kisingizio cha kuunga mkono mradi wa Kizayuni wa Magharibi katika Mashariki ya Kati kumefikia vipimo vya kubuniwa wiki hii na kusimamishwa uanachama wa Mbunge wa Chama cha Labour Diane Abbott - mwanamke mweusi mzee zaidi katika Baraza la Commons - baada ya kutetea matamshi yake ya awali kuhusu ubaguzi wa rangi.
Abbott aliandika mwaka 2023 kwamba "Wayahudi, Waayalandi, na wahamiaji wanakabiliwa na ubaguzi sawa na ubaguzi wa rangi, lakini si katika maisha yao yote kwa njia ile ile ambayo watu wa rangi wanakabiliwa nayo." Ubaguzi wake ulizua mfululizo wa madai ya chuki dhidi ya Wayahudi, na aliomba msamaha wakati huo lakini bado amesimamishwa. Abbott baadaye aliiambia BBC kwamba anasimama na hoja ya msingi: "Ni wazi kuna tofauti kati ya ubaguzi wa rangi unaohusiana na rangi na aina zingine za ubaguzi wa rangi, kwa sababu unaweza kumwona mtu kutoka kwa wahamiaji au Wayahudi akitembea barabarani, na haujui. Hungejua isipokuwa usimame kuzungumza nao au uwe kwenye mkutano nao. Lakini ukimwona mtu mweusi akitembea barabarani, utatambua mara moja kwamba yeye ni mweusi. Ni aina mbili tofauti za ubaguzi wa rangi." Kwa sababu hii, Chama cha Labour kilimsimamisha mara moja.
Waziri wa zamani wa Fedha katika serikali kivuli, John McDonnell, alielezea kuadhibiwa kwa Abbott kwa mahojiano "ambayo alilaani waziwazi chuki dhidi ya Wayahudi na ubaguzi wa rangi wa kila aina" kama "ajabu sana," wakati watu wenye ushawishi mkubwa hawakukabiliwa na adhabu yoyote kwa kutumia lugha ya kibaguzi.
Kosa la Abbott lilikuwa kinyume na fundisho la Magharibi kwamba chuki dhidi ya Wayahudi ni uovu wa kipekee, na kusema kwamba kwa kuwa ni vigumu kuwatambua Wayahudi kwa ujumla nchini Uingereza, kwa kweli wanakabiliwa na ubaguzi wa rangi kidogo kuliko watu wenye rangi tofauti za ngozi. Mlinganyo bandia wa kupinga taasisi ya Kiyahudi kama chuki dhidi ya Wayahudi ulitumiwa kuhalalisha marufuku ya Uingereza dhidi ya Hizb ut-Tahrir mnamo Januari 2024. Waziri wa Mambo ya Ndani James Cleverly alidai kwamba Hizb ut-Tahrir "inakuza na kuhimiza ugaidi kikamilifu," kwa mfano, kwa kusherehekea mashambulizi ya Oktoba 7, 2023, licha ya ukweli kwamba inajulikana sana kuwa chama hicho kinafanya kazi katika ngazi ya kisiasa tu.
Wachambuzi wa kupambana na ugaidi wameonya kwa miaka mingi kwamba kupiga marufuku Hizb ut-Tahrir kwa hivyo ni ishara ya kisiasa na sio jibu kwa tishio lolote la kigaidi. Baada ya shambulio la mauaji ya kimbari la taasisi ya Kiyahudi dhidi ya Gaza kufuatia Operesheni Tufani ya Al-Aqsa, ukosoaji uliongezeka dhidi ya mauaji ya kila siku dhidi ya raia wa Palestina, kutoka kwa Waislamu na sehemu zingine nyingi za jamii ya Uingereza. Ilidaiwa kuwa chuki dhidi ya Wayahudi iliongezeka kwa kiasi kikubwa, lakini hii ilitokana na uwongo mbaya kwamba kukosoa taasisi ya Kiyahudi ni chuki dhidi ya Wayahudi.
Vyombo vya habari vikuu vilipunguza umuhimu wa mateso ya Wapalestina na kunyesha huruma isiyo sawa na masimulizi ya Kizayuni. Kwanza, Hizb ut-Tahrir ilipigwa marufuku, kisha harakati ya Palestina ya kilimwengu, na hivi karibuni, mbunge kutoka Chama cha Labour alipewa adhabu kwa mara ya pili. Hali ya hofu ilitawala, ambapo maneno batili yanaharamishwa. Hakuna aliye salama kutokana na tuhuma za chuki dhidi ya Wayahudi; Waislamu hakika hawako, wala mrengo wa kushoto, wala hata Wayahudi, hawako salama kutokana na tuhuma za chuki dhidi ya Wayahudi ikiwa watathubutu kupinga au hata kuhoji mafundisho matakatifu ambayo yamepotosha mjadala wa kijamii nchini Uingereza.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Dkt. Abdullah Rubin