Marekebisho ya 27 ya Katiba ni ya Kuimarisha Utawala wa Trump nchini Pakistan
na Utawala wa Sharia pekee ndio unaoweza kufunga mlango wa uingiliaji wa kigeni kabisa
Habari:
Marekebisho ya 27 yanayopendekezwa ya Katiba, ambayo yanalenga kurekebisha Kifungu cha 243 na kuunda upya safu ya uongozi wa kijeshi nchini Pakistan, ni juhudi kabambe zaidi za urekebishaji kwa miongo kadhaa, na labda yenye utata zaidi, kwani inakinzana na tamaduni za taasisi zilizoimarika na usawa dhaifu kati ya nguvu za kiraia na kijeshi... Kiini cha mradi huu kiko katika kanuni rahisi inayoonekana, ambayo ni kuboresha uratibu wa ulinzi kwa kuunda wadhifa wa mkuu wa majeshi na kuondoa wadhifa wa mkuu wa wafanyakazi wa pamoja. Lakini kivitendo, mageuzi haya yatamwinua kamanda wa jeshi hadi nafasi ya kikatiba yenye mamlaka ya juu, ikijumuisha uongozi wa kiutendaji na udhibiti wa jumla wa vyombo vyote vya kijeshi. (Gazeti la Dawn)
Maoni:
Nafasi ya mkuu wa majeshi inachukuliwa kana kwamba ni nafasi ya kisiasa ya mamlaka, kinyume na ukweli wake wa kijeshi ambao haupaswi kuwa huru kutoka kwa muundo wa serikali, iwe ni ya kimagharibi ya kiraia au ya kisheria chini ya serikali ya Kiislamu. Hii inaonyesha ukweli wa uongozi wa kijeshi unaoendesha utawala wa moja kwa moja katika taifa la Pakistani, ambayo pia ni ukiukaji wa utawala wa kiraia ambao mataifa ya kiraia yanadai kusimamia. Kwa hivyo, maelezo ya kweli ya hali halisi ya serikali ya Pakistani ni kwamba ni serikali ya polisi, sio serikali ya kisiasa au ya kiraia kama inavyodai.
Ama katika Uislamu, nafasi ya Amir wa Jihad, ambaye ni kamanda wa kijeshi anayeongoza majeshi ya dola ya Kiislamu, huteuliwa na Khalifa, na pia huondolewa wakati Khalifa anaona inafaa. Khalifa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ Abu Bakr Al-Siddiq alimteua Khalid bin Al-Walid kuwa kamanda wa jeshi, kisha Omar akamwondoa na kumweka Abu Ubaidah badala yake. Kamanda katika jeshi ni askari anayeteuliwa na kuondolewa kwa maoni ya Khalifa kwa njia ambayo inafanikisha ushindi dhidi ya maadui wa Uislamu na Waislamu na inafanikisha lengo la jihad katika njia ya Mwenyezi Mungu, sio kufanikisha maslahi ya makafiri katika eneo hilo au katika nchi za Kiislamu na kuzunguka kati ya Misri, Jordan, Saudi Arabia na Uturuki kutuma vikosi vya mamluki kukandamiza watu wa Palestina kwa niaba ya Wayahudi!
Ama kuhusu marekebisho ya katiba, kipengele kibaya zaidi katika marekebisho ya 27 hakihusiani na mtu fulani, au ubabe wa kijeshi, au udhibiti wa kimahakama, lakini kinahusiana na kufanya mamlaka ya kufanya maamuzi nchini Pakistan iwe chini ya ushawishi wa Marekani.
Asim Munir ndiye wakala mkuu wa Trump nchini Pakistan na "kamanda wake mkuu wa kijeshi anayependelea". Munir anaendana kikamilifu na maono ambayo Trump ameweka kwa Pakistan kuhusiana na taasisi ya Kiyahudi, silaha za nyuklia za Pakistani, Afghanistan, China, Asia ya Kati, na rasilimali kubwa za nishati na madini nchini Pakistan.
Marekebisho ya 27 yanaweka msingi wa kupanua wigo wa mamlaka ya Asim Munir, sawa na mamlaka iliyopewa majenerali wa zamani kama vile Musharraf nchini Pakistan, au kama mamlaka ya Jenerali Sisi nchini Misri kwa sasa.
Harakati ya maandamano dhidi ya marekebisho ya katiba inapaswa kuzingatia mabadiliko kamili, sio mabadiliko ya sehemu, kwa sababu kila mabadiliko ya sehemu yatafungua mlango wa kuibuka kwa watu zaidi kama Munir, Musharraf na Sisi. Ili kufunga mlango wa ujanja mwingine wowote wa hatima ya Pakistan kutoka kwa majenerali, wanasiasa wafisadi na Marekani, Waislamu lazima wadai utawala wa sheria za Kiislamu.
Sharia inahitaji mamlaka ya kufanya maamuzi iendane na ufunuo wa Kiungu. Hakuna sheria yoyote inayopaswa kutungwa isiyoegemea ushahidi kutoka kwenye Qur'ani Tukufu na Sunnah za Mtume, na kile walichoongoza kwacho cha makubaliano ya Masahaba, na kipimo cha kisheria.
Khalifa, Amir wa Jihad, au Hakimu Mkuu katika Ukhalifa hawana haki ya kutenda nje ya hukumu za Sharia, bali Khalifa mwenyewe anaweza kuondolewa kutoka madarakani ikiwa anasisitiza kukiuka hukumu za Sharia zenye uhakika hadharani.
Enyi Waislamu nchini Pakistan: Elekezeni upinzani wenu wa kisiasa kukomesha utawala wa maagizo, matamanio na tamaa za Kimarekani juu ya mambo yenu. Msiache kupinga mpaka msimamishe utawala wa sheria za Mwenyezi Mungu Mtukufu nchini Pakistan, nchi safi.
﴿Na wahukumu baina yao kwa yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, wala usifuate matamanio yao. Na tahadhari nao wasije kukufitini ukaacha baadhi ya aliyo kuteremshia Mwenyezi Mungu.﴾
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Musab Umair - Wilaya ya Pakistan