Historia Inaiita Jeshi la Pakistani: Ni Wakati wa Uongozi Halisi wa Kiislamu
(Imetafsiriwa)
Habari:
Shambulio lililotokea Pahalgam mwezi Aprili 2025, ambapo wanamgambo waliwaua raia 26 na kuwajeruhi wengine, liliirejesha Kashmir kwenye kiini cha hali ngumu ya kisiasa ya kimadhehebu. Huku mamlaka zikionyesha mara moja uwajibikaji wa makundi ya wanamgambo yanayoungwa mkono na Pakistani, tukio hilo lilitiwa siasa haraka na kuunganishwa katika masimulizi mapana ambayo yameunda utawala wa Narendra Modi kwa zaidi ya muongo mmoja: mgogoro kati ya taifa la Wahindu na maadui wake wanaodaiwa kuwa wa ndani na nje.
Maoni:
Makabiliano ya hivi majuzi ya kijeshi kati ya Pakistani na India kwenye mstari wa udhibiti huko Kashmir, yameangazia udhaifu unaoongezeka wa usawa wa kijiografia. Mashambulizi yaliyoshindwa ya India na mashambulizi ya kukabiliana nayo yaliyoendelezwa na Pakistani yamefichua udhaifu katika uwezo wa kijeshi wa India, na kuilazimu India kutafuta usitishaji mapigano. Hii haiiwakilishi ushindi wa kimbinu kwa Pakistani tu, bali pia inawakilisha fursa muhimu inayowezekana. Kwa miongo kadhaa, Pakistani imewekeza katika teknolojia ya kisasa ya kijeshi na imeendeleza uwezo wake kwa msaada wa pande kama vile China.
Kwa upande mwingine, India imetegemea teknolojia za zamani, ingawa hivi karibuni imepokea masasisho kutoka kwa washirika wa Magharibi kama vile Ufaransa, taasisi ya Kiyahudi na Amerika. Shambulio hilo liliendana kikamilifu na simulizi lililoanzishwa na chama tawala cha Bharatiya Janata katika miaka yake ya utawala. Kwa serikali ya Modi, wahalifu hawakuwa magaidi tu, bali alama za adui mkuu, yaani Uislamu na Waislamu. Bila kusubiri uchunguzi wa kina, ililaumu makundi yaliyoko Pakistani, ikiitaja Lashkar-e-Taiba na shirika lake la wapiganaji linalodaiwa, The Resistance Front. Licha ya The Resistance Front kukana kuhusika na ukosefu wa ushahidi wa kuaminika, simulizi lilikuwa limeimarika tayari. Chama cha Bharatiya Janata, ambacho kimekuwa na uzoefu kwa muda mrefu katika kugeuza migogoro ya kitaifa kuwa mali ya kisiasa, kiliunganisha mauaji ya Pahalgam katika maono yake ya kisiasa ya "Hindu Rashtra".
Ufunguzi wa hekalu la Ram huko Ayodhya ulikuwa kilele cha miongo kadhaa ya siasa za kimadhehebu. Pia ilikuwa ishara wazi: katika India inayoongozwa na Modi, serikali ya Kihindu inatambuliwa, huku dini zingine zikionekana kwa shaka. Tangu kufutwa kwa Kifungu cha 370 mnamo 2019, Kashmir imenyang'anywa uhuru wake na imekuwa chini ya udhibiti mkubwa wa kiutawala na kijeshi kutoka kwa serikali ya India.
Kile ambacho hapo awali kilikuwa eneo lililotawaliwa na haki na huruma ya Kiislamu sasa kimekuwa eneo la kijeshi, linalotawaliwa kutoka New Delhi na kuumbwa na matarajio ya kitaifa. Miradi ya miundombinu kama vile daraja jipya la reli linalounganisha Kashmir na bara la India inawasilishwa kama ishara za maendeleo. Lakini kwa kweli, maendeleo haya yanawakilisha uvamizi na sio ujumuishaji. Kukamatwa kiholela, kukatwa kwa mtandao, unyakuzi wa ardhi kwa nguvu, na ukandamizaji wa kisheria vimekuwa zana za kawaida za utawala katika eneo hilo. Usalama unatafutwa kwa gharama ya uaminifu, na kila tukio jipya linakuwa haki ya ukandamizaji zaidi na ushahidi wa kutofaa kwake. Hii inaakisi kwa usahihi mbinu zilizotumiwa na vikosi vya Kiyahudi dhidi ya Wapalestina kwa miongo kadhaa.
Matokeo ya shambulio hilo yanaenea zaidi ya Kashmir pia. Muda mfupi baadaye, serikali ya Modi ilichukua hatua ya kusitisha sehemu muhimu ya Mkataba wa Maji ya Mto Indus, ambao umekuwa msingi wa diplomasia ya India na Pakistani tangu 1960. Tishio la kuzuia mtiririko wa maji kwenda Pakistani ni la ishara na la kimkakati. Haionyeshi tu jibu la kulipiza kisasi, lakini pia nia ya kutumia rasilimali za pamoja kama silaha katika michezo ya kisiasa.
Wasomi wa Pakistani bado wanaiona Amerika kama mshirika muhimu, lakini ukweli unaonyesha kuwa Amerika inawekeza zaidi kwa India kama mshirika mkuu wa kimkakati barani Asia. Hii haitokani tu na masuala ya kiuchumi na kijeshi, bali pia na jukumu la India katika mkakati wa Amerika wa kuizuia China. Pakistani inaonekana kukwama kati ya maslahi ya mataifa yenye nguvu; ikitafuta msaada wa Amerika kwa upande mmoja, na ushirikiano unaoongezeka wa China kupitia Ukanda wa Kiuchumi wa China na Pakistani na uhusiano wa kijeshi kwa upande mwingine.
Pakistani inasimama katika njia panda ya kihistoria: ama kubaki chombo katika mikakati ya mataifa makubwa au kuchukua udhibiti wa hatima yake na kuinua hadhi ya umma wa Kiislamu. Ukombozi wa Kashmir na ukombozi kutoka kwa utegemezi kwa Amerika ndio ufunguo wa mabadiliko haya ya kimkakati na ya kimsingi. Machafuko ya sasa ya kimataifa sio tishio tu, bali ni fursa nzuri ya uongozi na mabadiliko ya Kiislamu. Pakistani haipaswi kutafuta hali ilivyo au kusitisha mapigano, lakini ichukue hatua ya kihistoria kwa kukomboa Kashmir nzima, kulinda udhibiti wa rasilimali zake muhimu, na hivyo kuchukua uongozi katika mfumo wa ulimwengu usio na utulivu. Hii inaweka njia kwa enzi mpya ambapo Pakistani inachukua jukumu muhimu katika kuanzisha Ukhalifa ulioongozwa vyema. Hili ni ono la kimsingi ambalo halihitaji nguvu za kijeshi na uongozi wa kisiasa tu, bali pia utashi wa kisiasa wa kupinga mfumo wa ulimwengu uliopo. Ni wakati wa Pakistani kukomesha ono la Modi la "taifa la Wahindu" kwa kuungana na nchi za Asia ya Kati, kukomboa Kashmir nzima, na kuanzisha Ukhalifa ulioongozwa vyema juu ya magofu ya hekalu la Ram na ono la taifa la Wahindu.
Imeandikwa kwa Idhaa ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Muhib Abdullah