Mapinduzi na chimbuko lake linatoa uovu wake
Habari:
Baada ya kuingia katika mkoa wa Suwayda, makabila ya Syria yanaomba serikali isiingilie. (Kituo cha Al-Mawsiliya, 2025/7/18).
Maoni:
Jambo hili, kwa kiasi fulani linafurahisha kwa kuonyesha kuendelea kwa mapinduzi kuonyesha kutoridhika kwake na mwenendo wa kundi tawala katika kusimamia masuala ya nchi, lakini ni la kutisha kwa sababu linapelekea mapigano ya ndani kwa kukosekana kwa mamlaka, ambayo yanapelekea machafuko na kutoa kisingizio cha uingiliaji wa kimataifa na kikanda, na hivyo kinatokea ambacho matokeo yake hayapendezi, isipokuwa makabila na watu wote waasi wafuate njia sahihi katika kuwapa viongozi wao watu waaminifu, ili kuanzisha mfumo unaoonyesha matakwa ya umma na kulinda maslahi yao kwa sheria ya Kiislamu, na kukata uingiliaji wa nje.
Enyi waasi huko Sham, kitovu cha Uislamu na nguzo yake: Shikamaneni na umoja wenu na mteue uongozi wenu mwaminifu, wenye ufahamu, unaofanya kazi kwa Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna za Mtume wake, na mutangaze Ukhalifa wenu, kwani nguvu ni yenu sasa na amri ni yenu na nyinyi mnawajibika mbele ya Mwenyezi Mungu, kwani Yeye ndiye aliyewawezesha, na tahadharini na fitna na bendera za batili na upotoshaji, kwani chombo cha Kiyahudi na wafuasi wake kutoka Waarabu wa zama za ujinga bado wanapanga njama za kupotosha mapinduzi kutoka kwenye njia yake, iwe kwa mawakala na wanafiki au kwa tishio la moja kwa moja la kijeshi ambalo walifanya na ushindi wa mapinduzi kama vile kukalia Jabal al-Sheikh, na kuharibu silaha na vifaa vya jeshi la Syria kwa hofu ya kuangukia mikononi mwa waaminifu, na kujenga kambi za kijeshi ndani ya Syria, na kumuua baadhi ya makamanda wa ngazi za chini, na kutoa maagizo kwa serikali ya Al-Julani huko Idlib kabla ya ushindi wa mapinduzi na baada yake kuwakamata watu waaminifu kutoka miongoni mwa watoto wa mapinduzi, na kusaidia masalia ya utawala uliopita kuasi katika pwani na Jabal al-Duruz, na mwisho ni kulenga makao makuu ya jeshi ili kuangusha mapinduzi na kuyapotosha kutoka kwenye mwelekeo wake wa msingi kupitia wasaliti ambao waliwafikisha kwenye kiti cha utawala na uhaini wao wa kuipiga umma, na huyu hapa Al-Julani anaweka vizuizi mbele ya makabila na kukata usambazaji kwa waasi!
Enyi Waislamu huko Sham na ulimwenguni: Endelezeni safari, kwani mapinduzi ya Sham ni mapinduzi ya umma na Mwenyezi Mungu amewadhamini ushindi kwa kusema Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ «KITOVU CHA NYUMBA YA UISLAMU NI SHAM».
﴿NA MWENYEZI MUNGU NI MWENYE KUSHINDA KATIKA JAMBO LAKE, LAKINI WATU WENGI HAWAJUI﴾
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Muhammad Al-Hamdani - Jimbo la Iraq