Marekani Yavunja Sheria za Kimataifa Tena
Marekani Yavunja Sheria za Kimataifa Tena

Habari:

0:00 0:00
Speed:
June 27, 2025

Marekani Yavunja Sheria za Kimataifa Tena

Marekani Yavunja Sheria za Kimataifa Tena

(Imetafsiriwa)

Habari:

Jioni ya Jumapili, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza shambulio lililofaulu la Jeshi la Anga la Marekani kwenye maeneo matatu makuu katika mpango wa nyuklia wa Iran. (BBC)

Maoni:

Shambulio hili la Marekani dhidi ya ardhi ya Iran, bila kujali kisingizio kilichotumiwa, ni mfano wazi kwamba kile kinachoitwa "sheria ya kimataifa" ni udanganyifu tu, ambao lengo lake ni kuhalalisha ukoloni wa mataifa yenye nguvu kwa mataifa dhaifu.

Wakati kuna makubaliano kati ya wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu suluhisho la tatizo fulani la kimataifa, wanatoa azimio linalofaa na kulazimisha mapenzi yao kwa nguvu chini ya kivuli cha uhalali wa kisheria. Katika hali kama hizo, kila mtu anazungumza kuhusu utawala wa sheria za kimataifa.

Hili lilitokea kwa mfano katika azimio nambari 1973, ambalo kimsingi liliruhusu kuondolewa kwa dikteta wa Libya Muammar Gaddafi.

Lakini ikiwa mataifa makubwa hayakubaliani kati yao na hayawezi kufikia msimamo mmoja au uratibu wa kijeshi wa pamoja, basi "sheria ya kimataifa" mara moja inageuka kuwa kauli mbiu tupu ambayo inaweza kupuuzwa kwa urahisi.

Kitu kama hicho kilitokea mwaka wa 2003, wakati Marekani ilishindwa kupata azimio kutoka Baraza la Usalama, na ikaamua kuivamia Iraq ki unilateral. Na kabla ya hapo, mwaka wa 1999, mataifa ya NATO yalivamia Yugoslavia, kisha Urusi ilivamia Georgia mwaka wa 2008, na Ukraine mwaka wa 2014 na 2022.

Kila mara kitu kama hiki kinapotokea, taifa linaloshambulia hujaribu kuwasilisha uhalifu wake katika bahasha nzuri ya "kulinda raia", au "kurejesha haki iliyovunjwa", au kauli mbiu nyingine zinazovutia.

Kwa mfano, mzozo wa Ukraine unawakilisha mzozo mkali na wa ushindani kati ya mataifa makubwa ndani ya kile kinachojulikana kama "tatizo la Ulaya." Urusi, baada ya kuona kwamba kufuata sheria ya kimataifa kunatishia uhai wake, iliamua kuivamia Ukraine, ikipuuza mikataba yake yote ya kimataifa na ahadi zake.

Kuhusu shambulio dhidi ya Iran, Marekani imekanyaga sheria za kimataifa tena. Kwa hakika, nguvu ya nyuklia ya Marekani, pamoja na entiti ya Kiyahudi - ambayo inadhaniwa kuwa na silaha za nyuklia - inalazimisha mapenzi yake unilaterally kwa taifa lingine huru. Ni muhimu kutambua kwamba ninaondoa katika maoni haya ukweli kwamba uchokozi huu wa Marekani dhidi ya Iran unatokea ingawa nchi hiyo imekuwa mmoja wa watekelezaji mashuhuri wa sera za Marekani katika Mashariki ya Kati kwa miongo kadhaa.

Kwa upande mmoja, Marekani inatumia kura ya turufu dhidi ya azimio lolote linalotolewa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linalolaani entiti ya Kiyahudi, licha ya ukweli kwamba mtoto huyu mpendwa wa Marekani anafanya kila uhalifu wa kivita unaoweza kuwaziwa dhidi ya watu wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.

Na kwa upande mwingine, ikitambua kwamba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kwa sababu ya kura ya turufu - wakati huu kutoka Urusi - halitatoa azimio linaloruhusu matumizi ya nguvu za kijeshi dhidi ya Iran, Marekani inaelekeza shambulio la unilateral dhidi ya vituo vyake vya nyuklia.

Kiini ni kwamba dhana ya "sheria ya kimataifa" haiwezi kuwepo kweli, kwa sababu dhana za "sheria" na "kimataifa" hazipatani kiasili. Kuna sababu tatu za hii:

1- Sheria ni kitendo cha kisheria cha kimfumo kinachotolewa na chombo cha uwakilishi (cha kutunga sheria), yaani, na mamlaka tawala. Ukweli ni kwamba mamlaka tawala ya kimataifa haiwezi kuwepo kwa ufafanuzi.


2- Sheria lazima itekelezwe, yaani, lazima kuwe na utaratibu wa kuitekeleza. Ndani ya nchi, utaratibu kama huo upo katika vyombo vya kutekeleza sheria. Lakini katika ngazi ya kimataifa, hilo haliwezekani, kwa sababu "vikosi vya kulinda amani" vya sasa ni tu makundi ya majeshi kutoka nchi binafsi. Majeshi haya kwa upande wake hayatalinda sheria ya kimataifa au, kwa mfano, uhuru na maslahi ya nchi nyingine ikiwa ulinzi huo unaleta hatari kwa nchi zao au unapingana na maslahi yao, kama ilivyo katika mzozo wa Ukraine na katika ukiukaji wa Mkataba wa Budapest na nchi iliyoshambulia - Shirikisho la Urusi - na pia na wasaini wengine wa makubaliano haya.


3- Sheria inasimamia mahusiano, na udhibiti huu unafaa tu ndani ya mfumo wa jamii moja, na hauwezi kutumika wakati wahusika ni mataifa huru, kwa sababu kila nchi ina haki huru ya kuanzisha au kuepuka mahusiano na nchi nyingine kulingana na maslahi yake.

Tangu kuibuka kwa wazo la sheria ya kimataifa, kumekuwa na mgogoro kati ya wasomi wa sheria wa Magharibi kuhusu kiini cha kanuni zake. Wengi wametilia shaka nguvu yake ya kulazimisha. Kwa mfano, wasomi na wanafalsafa wa Magharibi kama vile Immanuel Kant, Thomas Hobbes, John Austin, na Georg Hegel walikanusha kuwepo kwa sheria ya kimataifa ya umma.

Lakini baadaye, chini ya shinikizo kutoka kwa mataifa makubwa ambayo yalikuwa yanakuza wazo hili, kile kinachoitwa "sheria ya kimataifa" kikawa ukweli uliopitishwa katika mahusiano ya kimataifa.

Matokeo yake, sheria ya kimataifa na taasisi zake zote zimekuwa chombo tu cha migogoro na mashindano kati ya nchi kama vile Marekani, Urusi, Uingereza, Ufaransa, na China. Wakati mataifa mengine yote, watu wake, rasilimali zao, na ardhi zao zimekuwa wahanga wa matumizi ya uhalifu ya "sheria" hii na nguvu hizo kubwa.

Hii hasa ndiyo sababu kuu ya hali ya ukosefu wa utulivu ambayo inaenea katika maeneo mengi ya ulimwengu leo, ambapo mateso ya watu wa Palestina, Iran, au Ukraine ni msururu mdogo tu ndani ya mlolongo usio na mwisho wa uhalifu unaofanywa na mataifa makubwa.

Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Fadl Amzaev

Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir nchini Ukraine

More from Habari na Maoni

Uturuki na Serikali za Kiarabu Zilitaka Hamas Iache Silaha

Uturuki na Serikali za Kiarabu Zilitaka Hamas Iache Silaha

(Imetafsiriwa)

Habari:

Mkutano wa ngazi ya juu wa kimataifa wa Umoja wa Mataifa ulifanyika New York mnamo Julai 29 na 30, wenye kichwa "Kupata Suluhu ya Amani kwa Suala la Palestina na Utekelezaji wa Suluhu la Mataifa Mawili," ukiongozwa na Ufaransa na Saudi Arabia. Kufuatia mkutano huo, ambao ulikusudia kuitambua Palestina kama nchi na kumaliza vita huko Gaza, tamko la pamoja lilitiwa saini. Pamoja na Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu, Uturuki pia ilitia saini tamko hilo pamoja na nchi zingine 17. Tamko hilo, lililokuwa na vifungu 42 na kiambatisho, lililaani operesheni ya Al-Aqsa iliyofanywa na Hamas. Nchi zilizoshiriki ziliitaka Hamas iache silaha na kuwataka wakabidhi utawala wao kwa serikali ya Mahmoud Abbas. (Mashirika ya habari, Julai 31, 2025).

Maoni:

Kwa kuzingatia nchi zinazoendesha mkutano, ni wazi kuwepo kwa Amerika, na licha ya kutokuwa na mamlaka au ushawishi wa kufanya maamuzi, kuandamana kwa utawala wa Saudi, mtumishi wake, kwa Ufaransa ni ushahidi dhahiri wa hilo.

Katika suala hili, Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron alisema mnamo Julai 24 kwamba Ufaransa itatambua rasmi taifa la Palestina mnamo Septemba, na itakuwa nchi ya kwanza kutoka kwa kundi la nchi saba kufanya hivyo. Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Faisal bin Farhan Al Saud na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Noël Barot walifanya mkutano na waandishi wa habari katika mkutano huo, wakitangaza malengo ya tamko la New York. Kwa kweli, katika taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo, mauaji ya kimbari ya chombo cha Kiyahudi yalilaaniwa bila kuchukua uamuzi wowote wa adhabu dhidi yake, na Hamas iliombwa kuacha silaha zake na kukabidhi utawala wa Gaza kwa Mahmoud Abbas.

Katika mkakati mpya wa Amerika wa Mashariki ya Kati ambao inataka kutekeleza kwa kuzingatia makubaliano ya Abraham, utawala wa Salman unawakilisha kichwa cha mkuki. Utawala wa kawaida na chombo cha Kiyahudi utaanza baada ya vita, na Saudi Arabia; kisha nchi zingine zitafuata, na wimbi hili litageuka kuwa muungano wa kimkakati unaoenea kutoka Afrika Kaskazini hadi Pakistani. Pia, chombo cha Kiyahudi kitapata dhamana ya kiusalama kama sehemu muhimu ya muungano huu; kisha Amerika itatumia muungano huu kama mafuta katika mapambano yake dhidi ya China na Urusi, na kujumuisha Ulaya yote chini ya mabawa yake, na kwa kweli, dhidi ya uwezekano wa kuanzishwa kwa Ukhalifa.

Kizuizi kwa mpango huu kwa sasa ni vita vya Gaza na kisha hasira ya umma, ambayo inaongezeka, na inakaribia kulipuka. Kwa hivyo, Marekani ilipendelea Umoja wa Ulaya, tawala za Kiarabu na Uturuki kuchukua hatamu katika tamko la New York. Ikidhani kwamba kukubalika kwa maamuzi yaliyomo kwenye tangazo itakuwa rahisi.

Ama serikali za Kiarabu na Uturuki, kazi yao ni kumridhisha Marekani, na kulinda chombo cha Kiyahudi, na badala ya utiifu huu, kujilinda na hasira ya watu wao, na kuishi maisha ya unyonge na makombo ya mamlaka duni hadi watupwe au kuadhibiwa kwa mateso ya akhera. Hifadhi ya Uturuki juu ya tangazo, mradi tu utekelezaji wa kile kinachoitwa mpango wa suluhisho la mataifa mawili, ni jaribio tu la kufunika lengo halisi la tangazo na kupotosha Waislamu, na haina thamani yoyote ya kweli.

Kwa kumalizia, njia ya ukombozi wa Gaza na Palestina yote sio kupitia taifa la uwongo ambalo Wayahudi wanaishi. Suluhisho la Kiislamu kwa Palestina ni utawala wa Uislamu katika ardhi iliyoporwa, na ni kupigana na mporaji, na kuhamasisha majeshi ya Waislamu kuwang'oa Wayahudi kutoka ardhi iliyobarikiwa. Na suluhisho la kudumu na la msingi ni kuanzisha Ukhalifa Uongofu na kulinda ardhi ya Israa na Mi'raj iliyobarikiwa na ngao ya Ukhalifa. Mungu akipenda, siku hizo haziko mbali.

Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ alisema: «Saa haitasimama mpaka Waislamu wapigane na Wayahudi, na Waislamu watawaua, mpaka Myahudi atajificha nyuma ya jiwe na mti, kisha jiwe au mti utasema: Ewe Muislamu, Ewe mja wa Mwenyezi Mungu, huyu Myahudi yuko nyuma yangu, njoo umuue» (Imesimuliwa na Muslim)

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Muhammad Amin Yildirim

Kile ambacho Amerika inataka ni kutambuliwa rasmi kwa taifa la Kiyahudi, hata kama silaha itabaki

Kile ambacho Amerika inataka ni kutambuliwa rasmi kwa taifa la Kiyahudi, hata kama silaha itabaki

Habari:

Habari nyingi za kisiasa na kiusalama nchini Lebanon zinahusu suala la silaha inayolenga taifa la Kiyahudi, bila silaha nyingine yoyote na kulizingatia na wachambuzi wengi wa kisiasa na wanahabari.

Maoni:

Amerika inaomba kukabidhiwa silaha iliyopigana na Wayahudi kwa jeshi la Lebanoni, na haijalishi silaha yoyote itakayobaki mikononi mwa watu wote ambayo inaweza kutumika ndani ya nchi itakapoona faida yake au kati ya Waislamu katika nchi jirani.

Amerika, adui yetu mkuu sisi Waislamu, ilisema waziwazi, bali kwa ukosefu wa adabu, wakati mjumbe wake Barrack alipotamka kutoka Lebanon kwamba silaha ambayo lazima ikabidhiwe kwa serikali ya Lebanoni ni silaha ambayo inaweza kutumika dhidi ya taifa la Kiyahudi linalonyakua Palestina iliyobarikiwa, na sio silaha nyingine yoyote ya mtu binafsi au ya kati kwa sababu hii haidhuru taifa la Kiyahudi, bali inawahudumia na inahudumia Amerika na nchi zote za Magharibi katika kuhamasisha mapigano kati ya Waislamu kwa kisingizio cha watu wenye msimamo mkali au wenye itikadi kali au watu wa kale au walio nyuma, au maelezo mengine ambayo wao huyaeneza kati ya Waislamu kwa kisingizio cha madhehebu au utaifa au ukabila, au hata kati ya Waislamu na wengine ambao wameishi nasi kwa mamia ya miaka na hawakupata kutoka kwetu ila kuhifadhi heshima, mali na roho, na kwamba tulikuwa tunatumia sheria juu yao kama tunavyozitumia juu yetu wenyewe, wanayo yao na wanayo juu yao. Hukumu ya kisheria ndiyo msingi wa hukumu kwa Waislamu, iwe kati yao, au kati yao na raia wengine wa dola.

Na maadamu adui yetu mkuu Amerika anataka kuharibu au kutoa upande silaha ambayo inaumiza taifa la Kiyahudi, kwa nini wanasiasa na wanahabari wanaangazia hilo?!

Na kwa nini mada muhimu zaidi zinaibuliwa kwenye vyombo vya habari na katika baraza la mawaziri, kwa ombi la adui wa Kimarekani, bila kuzichunguza kwa kina na kufafanua ukubwa wa hatari yake kwa umma, na hatari zaidi kati yao ni kuchora mipaka ya nchi kavu na taifa la Kiyahudi, ambayo ni kutambua taifa hili la wanyang'anyi rasmi, na kwa namna ambayo hakuna mtu atakayeweza kubeba silaha baada ya hapo, silaha yoyote kwa ajili ya Palestina, ambayo ni mali ya Waislamu wote na sio watu wa Palestina pekee, kama wanavyojaribu kutushawishi kana kwamba inawahusu watu wa Palestina pekee?!

Hatari ni katika kuibua suala hili mara moja chini ya kichwa cha amani, na mara nyingine chini ya kichwa cha upatanisho, na nyingine chini ya kichwa cha usalama katika eneo hilo, au chini ya kichwa cha ustawi wa kiuchumi, utalii na kisiasa, na ustawi ambao wanaahidi Waislamu ikiwa watatambua chombo hiki kilichopotoka!

Amerika inajua vizuri kwamba Waislamu hawawezi kukubali kutambua taifa la Kiyahudi kamwe, na ndiyo maana unaiona inawapenyeza kupitia mambo mengine ili kuwatoa akili zao kutoka kwa jambo muhimu zaidi la hatima. Ndiyo, Amerika inataka tuangazie suala la silaha, lakini inajua kwamba silaha, haijalishi ni yenye nguvu kiasi gani, haitafaa na haiwezi kutumika dhidi ya taifa la Kiyahudi ikiwa Lebanon rasmi itatambua kwa kuchora mipaka nayo, na kwa kufanya hivyo itakuwa imetambua na kustahili kwake ardhi ya Palestina iliyobarikiwa, ikisingizia watawala wa Kiislamu, na mamlaka ya Palestina.

Utambuzi huu wa taifa la Kiyahudi ni usaliti kwa Mungu na Mtume wake na kwa waumini, na kwa damu yote ya mashahidi ambayo ilimwagwa na bado inamwagwa kwa ajili ya ukombozi wa Palestina, na licha ya yote hayo bado tunatumai mema katika taifa letu ambalo baadhi yao wanapigana huko Gaza Hashem na Palestina, na wanatuambia kwa damu yao: Hatutatambua taifa la Kiyahudi kamwe, hata kama itatugharimu haya yote na zaidi... Je, tunakubali nchini Lebanon kutambua taifa la Kiyahudi haijalishi hali ni ngumu kiasi gani?! Na je, tunakubali kuchora mipaka nalo, yaani, kulikubali, hata kama silaha itaachwa nasi?! Hili ni swali ambalo lazima tulijibu kabla halijachelewa.

Imeandikwa kwa ajili ya idhaa ya ofisi ya habari kuu ya Hizb ut-Tahrir

Dkt. Muhammad Jaber

Mkuu wa kamati ya mawasiliano kuu ya Hizb ut-Tahrir katika jimbo la Lebanon