Marekani Yataka Kurekebisha Ramani ya Njia ya Mgogoro wa Yemen kwa Kuwavua Silaha Wahouthi
Marekani Yataka Kurekebisha Ramani ya Njia ya Mgogoro wa Yemen kwa Kuwavua Silaha Wahouthi

Habari:

0:00 0:00
Speed:
November 06, 2025

Marekani Yataka Kurekebisha Ramani ya Njia ya Mgogoro wa Yemen kwa Kuwavua Silaha Wahouthi

Marekani Yataka Kurekebisha Ramani ya Njia ya Mgogoro wa Yemen kwa Kuwavua Silaha Wahouthi

Habari:

Shinikizo kutoka Marekani na Saudi Arabia kwa Wahouthi kurekebisha ramani ya njia inajumuisha kuwavua silaha Wahouthi. (Gazeti la Al-Akhbar la Lebanon, 4 Novemba 2025).

Maoni:

Saudi Arabia ilikuwa imefichua ramani ya njia kati yake na Wahouthi kwa baraka za Amerika inayohusiana na kusitisha mapigano, kufungua barabara na viwanja vya ndege, na kulipa mishahara, kisha kuanza mazungumzo ya kisiasa yanayoongoza kwa kuunda serikali kwa usawa na serikali ya Rashad al-Alimi, lakini serikali ya Al-Alimi ilikataa kwa kuwa inawapa Wahouthi karibu theluthi mbili ya mapato ya mafuta na marupurupu mengine.

Na tena mazungumzo yamerudi kuhusu kufufua mchakato wa amani nchini Yemen, na Wahouthi walisema wako tayari kutekeleza ramani hiyo ya njia, na vile vile waziri wa mambo ya nje wa Saudi Arabia, Faisal bin Farhan, alirudia kwamba ramani ya njia iko tayari kutekelezwa. Wakati viongozi wa Baraza la Urais la Yemen na waziri wake wa mambo ya nje wanasema haifai tena na wanadai suluhisho la kisiasa kulingana na marejeleo yao matatu, ambayo ni: Mpango wa Magharibi unaoitwa Mpango wa Ghuba, ambao chini yake marehemu Ali Abdullah Saleh aliondolewa madarakani, na matokeo ya Mkutano wa Kitaifa wa Mazungumzo, uliofanyika chini ya uangalizi wa Magharibi na kusababisha mfumo wa utawala wa shirikisho katika mfumo wa jamhuri ya kidemokrasia iliyoanzishwa kwa uhuru, uwezeshaji wa wanawake, na kupambana na ugaidi, na rejeleo la tatu ni azimio la Umoja wa Mataifa 2216 ambalo linawaona Wahouthi kama wanamgambo walioteka nyara serikali! Lakini Saudi Arabia na Wahouthi wanashikilia ramani ya njia ya Amerika ambayo haikutaja marejeleo hayo.

Katika muktadha huo huo, Baraza la Ushirikiano la Ghuba lilisititiza kwamba suluhisho nchini Yemen linapaswa kuzingatia marejeleo matatu bila kuathiri umoja wa Yemen, ikiashiria kukataa kwao mradi wa kugawanya Yemen, ambao unaungwa mkono na Baraza la Mpito, lililoanzishwa na UAE mnamo 2017.

Na tukirudi kwenye mazungumzo juu ya kurejea kwa mchakato wa kisiasa, gazeti la Al-Akhbar la Lebanon lilifichua kuwa kuna marekebisho ambayo yatafanywa na Amerika na Saudi Arabia ambayo yanajumuisha kuwavua silaha Wahouthi, na inaonekana kuwa marekebisho haya yatakuwa ili serikali ya Al-Alimi, inayoungwa mkono na Uingereza, ikubali. Huku ushindani wa kimataifa ukiendelea kwa ushawishi nchini Yemen, watu huko wanabaki chini ya mamlaka ya mgawanyiko wa kijeshi na kisiasa kati ya Saudi Arabia na UAE, ambao unawakilisha ushindani kati ya Amerika na Uingereza kwa ushawishi na utajiri nchini Yemen. Tawakkol Karman alionyesha ushindani huo akitoa maoni yake kuhusu ufunguzi wa uwanja wa ndege wa Mokha, unaoendeshwa na mwanachama wa Baraza la Urais, Tariq Saleh, na unaoendeshwa chini ya ushawishi wa UAE, akisema kwamba yeye ni wakala wa wakala (akimaanisha Tariq Saleh na UAE kama wakala wa Uingereza), na akasema kwamba Uingereza ilijenga uwanja wa ndege wa Aden, nyumba na hospitali huko kwa ajili ya kutumikia askari wake na kuacha makazi mengine yakivurugika, yaani, bila kujaliwa lolote, ikimaanisha kile wanachokifanya leo huko Mokha, ambako walijenga uwanja wa ndege huko kwa ajili ya kutumikia maslahi yao ya kijeshi, wakati miji yenye watu wengi haipati uangalizi wowote!

Na kilichopo ni kwamba viongozi hawa wa ndani wanaiachia nchi, masuala yake, na mali zake kwa mawakala wanaoidhibiti kwa niaba ya kafiri wa Magharibi, na wanawadanganya watu kwa itikadi za kimadhehebu, kikanda, na hata za kidini ili kuficha uhalifu wao dhidi ya nchi na watu.

Uislamu umeamrisha kutokuruhusu makafiri kudhibiti na kutawala nchi zetu. Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Na Mwenyezi Mungu hatowapa makafiri njia ya kuwashinda Waumini﴾, na Mtume ﷺ alisema: «Hakika sisi hatuombi nuru kwa moto wa washirikina», yaani hatuwatumii kutatua masuala yetu, na Uislamu umefanya mamlaka kuwa ya Mwenyezi Mungu pekee bila mshirika yeyote kutoka kwa wanadamu katika kupanga maisha, kuunda mfumo wa utawala ndani yake, na sheria zote zinazolinda damu ya Waislamu, mali zao, na kusimamia masuala ya maisha yao kulingana na hukumu za Uislamu katika utawala, uchumi, siasa za kigeni, fedha, elimu, na zinginezo, na si kama vile watawala wa Waislamu wanafanya leo kwamba wamewafanya makafiri wa Magharibi kuwa watawala wa nchi, utawala na mifumo ya maisha, wakiidhibiti mali na mamlaka, na kuwaweka watu, ambao ndio wamiliki wa nchi na mali zake, katika umaskini uliokithiri, uharibifu na vita vinavyoendeshwa kutoka mbali na askari wa ndani!

Enyi watu wa Yemen: Hakika mfumo wa Khilafa ndio mfumo ambao Mola wenu amewaridhia, na si mfumo wa jamhuri, shirikisho la kidemokrasia, wala mfumo wa kimadhehebu, wala mfumo wa kifalme. Kusimamishwa kwa Khilafa ni jambo linalowezekana na linalopatikana, bali wakati wake umefika baada ya utawala wa kidhalimu tunaoishi nao leo. Lakini hatua ya kwanza kuelekea Khilafa iko katika kutowachukua viongozi hawa wa ndani, kaskazini na kusini, kama watawala, bali wao ni wanyang'anyi wa utawala kwa uwezeshaji kutoka kwa kafiri wa Magharibi ili iwe rahisi kwake kupora mali, kutawala nchi, njia zake, na bandari zake za kimataifa katika mfumo wa ushindani wa kikoloni kati ya nchi zao.

Basi njooni tufanye kazi na Hizb ut Tahrir kusimamisha Khilafa Rashidah ya Pili kwa njia ya Utume ili Mola wenu Subhaanahu wa Taala akuridhieni na mpate utukufu wa dunia na Akhera. Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Hakika Sisi tutawanusuru Mitume wetu na wale walio amini katika uhai wa dunia na siku watakapo simama mashahidi﴾.

Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut Tahrir

Abdul Aziz Al-Hamid - Wilaya ya Yemen

More from null

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Habari:

Uchunguzi wa Al Jazeera, unaotegemea uchambuzi wa picha za satelaiti, umefichua mifumo ya uharibifu wa kimfumo iliyofanywa na uvamizi huko Gaza kati ya Oktoba 10 na 30 iliyopita.

Shirika la "Sanad" la uhakiki wa habari la mtandao wa Al Jazeera limegundua operesheni za ulipuaji, ubomoaji wa kihandisi na mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na uvamizi ndani ya Ukanda huo tangu kuanza kutekelezwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. (Al Jazeera Net)

Maoni:

Baada ya kutangazwa kwa usitishaji wa vita vilivyojaa mabomu dhidi ya Ukanda wa Gaza chini ya usimamizi wa Trump na kwa makubaliano na baadhi ya nchi za Kiarabu, ilikuwa wazi kuwa ilifikiwa kwa faida ya taasisi ya Kiyahudi. Hili limebainika kulingana na uchambuzi wa picha za satelaiti na ripoti za hivi karibuni za habari, kwamba jeshi la Kiyahudi lililipua maelfu ya majengo huko Gaza, haswa huko Shuja'iyya na Khan Yunis katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao, na vile vile Rafah, na maeneo yaliyo mashariki mwake ambayo yalishuhudia operesheni kubwa za uharibifu.

Uharibifu mkubwa huko Gaza sio wa bahati mbaya, lakini una malengo ya kimkakati ya muda mrefu, kama vile kuharibu mazingira yanayounga mkono upinzani. Kuondoa Gaza ya miundombinu yake, shule zake na makazi yake, inafanya kuwa ngumu kwa upinzani kujipanga upya au kujenga upya uwezo wake. Hii ni kizuizi cha muda mrefu kwa kuharibu uwezekano na kulazimisha ukweli mpya ambao unaifanya Gaza kuwa dhaifu na kuiacha ikiwa imepooza kiuchumi na haifai kwa makazi, ambayo huandaa njia ya kukubali suluhisho zozote za kisiasa au kiusalama, au hata kukubali wazo la uhamishaji, kwa sababu kuacha Gaza kama kifusi, inafanya kuwa ngumu kwa ujenzi kuwa mikononi mwa watu wake pekee. Badala yake, nchi na mashirika yataingilia kati kwa masharti ya kisiasa, na uvamizi unatambua kuwa yeyote anayejenga upya ndiye anayemiliki uamuzi. Hivyo basi uharibifu wa leo ni sawa na udhibiti wa kisiasa kesho!

Kwa kweli, kuelezea makubaliano ya kusitisha vita dhidi ya Gaza kama "yenye mabomu" haikuwa bure, kwa sababu ilikuwa ya sehemu, na malengo ya madai ya kijeshi hayakujumuishwa, ambayo inaruhusu Wayahudi kuendelea na uvamizi na uharibifu kwa kisingizio cha kiusalama. Vivyo hivyo, ilifikiwa na nchi kubwa zaidi inayounga mkono taasisi bila dhamana thabiti za kimataifa, ambayo inafanya kuwa dhaifu na inakabiliwa na ukiukwaji, haswa kwa kukosekana kwa uwajibikaji wa kimataifa, ambayo inafanya taasisi ya Kiyahudi kuwa juu ya uwajibikaji.

Tutaendelea kuwa taifa lenye unyenyekevu na linalokubali, tukitazama watu waliodhoofika, waliochoka, waliopotea na wenye njaa mpaka lini?! Na juu ya yote hayo, wanaruhusiwa wakati wowote?! Hebu sote tuwe Saladin al-Ayyubi, kwa sababu Gaza leo inakumbusha taifa kwamba Saladin hakuwa tu mtu shujaa, lakini alikuwa kiongozi katika dola iliyokuwa na mradi na jeshi na taifa moja nyuma yake. Kwa hivyo, wito wa kuwa Saladin haimaanishi ushujaa wa mtu binafsi, lakini kufanya kazi ya kuanzisha dola ambayo inafanya watoto wote wa taifa kuwa askari katika safu moja chini ya bendera moja.

Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Mna nini hamkupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya wanyonge miongoni mwa wanaume na wanawake na watoto﴾.

Imeandikwa kwa Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Manal Um Ubaidah

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Habari:

Kituo cha Yemen Sana'a kilirusha hewani Jumatano jioni, 2025/11/12, kipindi cha kibinadamu "Nchi Yangu", na katika sehemu ya "Tuko nanyi", kipindi kilionyesha kesi ya mwanamke ambaye alikuwa ameambukizwa ugonjwa adimu na alihitaji kusafiri kwenda India kwa gharama ya dola elfu 80, ambapo kiasi cha dola elfu 70 kilikusanywa kutoka kwa mashirika na wahisani, lakini mtangazaji wa kipindi alizungumzia sana sifa za mchangiaji wa mwisho wa dola elfu kumi, na ikawa wazi kuwa alikuwa Abdul Malik al-Houthi, na alisifu jukumu lake la mara kwa mara katika kusaidia kesi za kibinadamu ambazo zinaonekana kwenye kipindi.

Maoni:

Hakika, mtawala katika Uislamu ana jukumu kubwa, ambalo ni kutunza maslahi ya watu kwa kutumia kile kinachowanufaisha na kutoa kila kitu kinachowafariji. Kimsingi yeye ni mtumishi wao, na hawezi kufurahia maisha hadi atakapohakikisha hali zao. Jukumu hili sio ihsani au upendeleo, bali ni wajibu wa kisheria ambao Uislamu umemlazimisha, na anahesabiwa kuwa amepungukiwa ikiwa atalipuuza. Uislamu umewajibisha umma kumuwajibisha anapopungukiwa. Amani na baraka zimshukie: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, ni upuuzi kufurahia usikivu wa watawala au serikali kwa mahitaji fulani na kuita hiyo kazi ya kibinadamu, wakati kimsingi ni kazi ya kichungaji ya lazima.

Moja ya dhana hatari zaidi ambayo imekita mizizi na ubepari na utawala wake duniani ni kukataa kwa serikali kutunza watu na kuacha utunzaji wa watu kwa mashirika na vyama vya hisani vinavyoendeshwa na watu binafsi au vikundi, na watu huenda kwao mara nyingi kuwasaidia na kutimiza mahitaji yao. Wazo la vyama lilionekana kwanza huko Uropa wakati wa Vita vya Ulimwengu, ambapo familia nyingi zilipoteza wazazi wao na zikawa zinahitaji mlinzi, na serikali, kulingana na mfumo wa kidemokrasia wa kibepari, haitunzi masuala, bali ni mlinzi wa uhuru tu. Matajiri waliogopa mapinduzi ya maskini dhidi yao, kwa hivyo walianzisha vyama hivi.

Uislamu umefanya kuwepo kwa sultani kuwa wajibu wa kutunza masuala ya umma ili kuhifadhi haki zao za kisheria na kukidhi mahitaji yao sita ya msingi ambayo lazima yakidhiwe kwa watu binafsi na vikundi; chakula, mavazi na makazi lazima yatolewe na serikali kwa kila mtu mmoja mmoja, Waislamu na wasio Waislamu, na usalama, matibabu na elimu hutolewa na serikali bure kwa wote. Mtu mmoja alikuja kwa Khalifa wa Waislamu, Omar bin al-Khattab, Mungu amuwiye radhi, akiwa na mke wake na binti zake sita, akasema: (Ewe Omar, hawa ni binti zangu sita na mama yao, walishe, wavishe na uwe ngao kwao kutoka kwa wakati) Omar akasema: (Na vipi ikiwa sitafanya hivyo?!) Bedui akasema: (Nitakwenda) Omar akasema: (Na vipi ikiwa utakwenda?) Akasema: (Utaulizwa kuhusu hali yao Siku ya Kiyama, ukisimama mbele ya Mungu ama kuelekea Motoni au Paradiso), Omar akasema: (Umma huu hautapotea maadamu kuna watu kama hawa).

Enyi Waislamu: Hii sio ndoto, bali ni Uislamu ambao umefanya utunzaji kuwa wajibu kwa Khalifa wa Waislamu kwa kila mtu mmoja mmoja, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehma na amani zimshukie, alisema: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, lazima turudishe hukumu hizi na kuzifanya ziwe za utekelezaji, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: ﴿Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyomo kwa watu mpaka wabadili yaliyomo katika nafsi zao﴾. Hivyo, kitakachobadilisha hali yetu kuwa haki na ustawi ni Uislamu.

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Sadiq al-Sarari