Uchaguzi wa Baraza la Wanafunzi la Chuo Kikuu cha Dhaka
Kushindwa kwa Siasa za Kidemokrasia Kutumia Nguvu za Vijana kwa Mabadiliko ya Kweli
(Imetafsiriwa)
Habari:
Wanafunzi wa vyuo vikuu vya Dhaka, Jahangirnagar, na Rajshahi walikuwa wanatarajia kwa nguvu mabadiliko chanya ya kisiasa na uhakikisho thabiti wa kulinda maslahi ya wanafunzi kufuatia uchaguzi ulioakhirishwa wa mabaraza yao makuu ya wanafunzi mnamo mwezi Septemba. Wengi wa wanafunzi hawa walieleza waziwazi hamu yao ya kukomesha mila ya unyonyaji katika siasa za vyuo vikuu, na waliwahimiza wawakilishi wanaokuja kufanya kazi ili kulinda haki za wanafunzi. Walisisitiza kuwa viongozi wa wanafunzi waliochaguliwa wanapaswa kuwa sauti ya wanafunzi wote, kuhakikisha mazingira rafiki kwa wanafunzi ndani ya chuo, haswa kufuatia mabadiliko ya kisiasa mnamo Julai 2024 yaliyopatikana kupitia uasi wa wanafunzi ambao uliangusha utawala wa Jumuiya ya Awami mnamo Agosti 5 ya mwaka huo (Imeripotiwa kutoka gazeti la New Age, Agosti 23, 2025)
Maoni:
Chuo Kikuu cha Dhaka daima kimekuwa mstari wa mbele katika harakati nchini Bangladesh, kuanzia harakati ya lugha mwaka 1952 hadi uasi wa hivi karibuni dhidi ya utawala wa Sheikh Hasina. Chuo kikuu kimeacha urithi wa kihistoria katika kuunda mazingira ya kisiasa nchini, kiasi kwamba hatima ya Baraza Kuu la Wanafunzi la Chuo Kikuu cha Dhaka, ni kubwa kuliko uchaguzi wa wanafunzi tu, bali ni suala la uzito wa kisiasa katika ngazi ya kitaifa. Baraza hilo, kama chombo kikuu cha wanafunzi katika chuo kikuu cha serikali cha juu kabisa nchini, daima limekuwa kitovu cha harakati kubwa za kitaifa, na uwanja wa kuwaandaa viongozi wa baadaye. Vile vile, wanafunzi wa vyuo vikuu vingine vya serikali daima wamekuwa mstari wa mbele katika mabadiliko makubwa ya kimaendeleo katika siasa za Kibengali. Hata tulishuhudia katika uasi wa Julai 2024 ushiriki hai na wa ufahamu kutoka kwa wanafunzi wa vyuo vikuu binafsi, ambao walicheza jukumu la kichocheo madhubuti katika mabadiliko ya utawala.
Hata hivyo, licha ya matumaini yote katika uwezo wa vijana, historia inaonyesha kwamba harakati za wanafunzi nchini Bangladesh hazijaweza kamwe kuleta mabadiliko ya kweli. Dhabihu za wanafunzi zimetumiwa mara kwa mara na vyama vya siasa vilivyoingia katika mfumo wa kidemokrasia ulioharibika. Mfumo wa kidemokrasia, kinadharia, unapaswa kuonyesha matakwa ya watu, lakini kivitendo umedumisha ubepari ambao unawahudumia wasomi wa kisiasa, wachache wa kibepari, na wakoloni wa Magharibi.
Hata kuondolewa kwa Sheikh Hasina, ambayo ni hatua muhimu katika historia ya siasa za wanafunzi, inafichua ukweli huu. Kwani matarajio na dhabihu za vijana zimepotezwa tena mikononi mwa wabebaji wa mfumo huu wa kidemokrasia ulioharibika. Licha ya kuanguka kwa utawala, miundombinu ya kimsingi - ubepari wa kilimwengu - bado ipo, inalindwa na watawala wanaoungwa mkono na Magharibi na idadi ya mabepari wachoyo. Wanafunzi - haswa katika Chuo Kikuu cha Dhaka - haijalishi shauku yao, wanalazimika kufanya kazi nje ya vituo vya nguvu halisi, ambavyo vinabaki chini ya utawala wa walezi wa ukoloni mamboleo, haswa Merika.
Ukweli mchungu ni kwamba mfumo wa kisiasa uliopo nchini Bangladesh unawazuia vijana kufikiri na kufanya kazi nje ya mipaka nyembamba ya demokrasia. Kinachohitajika sio mzunguko mpya wa matumaini ya uongo, lakini mabadiliko makubwa katika mfumo; sera ambayo inatumia nguvu kubwa za vijana katika kazi ya kujenga kwa ajili ya mabadiliko ya kweli. Mabadiliko haya yanatokana na kubadilisha mfumo mkuu wa kimungu ambao Mwenyezi Mungu ameuteremsha, ambao ni Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume, na sura ya kidemokrasia iliyoharibika ambayo inauzwa chini ya kauli mbiu za uhuru, ubinadamu, na uhuru wa mawazo, na ni pale tu vijana wa Bangladesh wanapoelekeza wenyewe kuelekea maono haya, dhabihu zao zitazaa mabadiliko ya kweli, ambayo yanahakikisha ujenzi wa kesho iliyoangaza na yenye ustawi zaidi kwa watu wao.
Imeandikwa kwa Idhaa ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Irtida Chowdhury - Jimbo la Bangladesh