Ardhi Takatifu ya Palestina Inapotea na Watawala Wanashughulika Kulinda Viti Vyao vya Enzi!
Habari:
Mnamo Septemba 23, mazungumzo yalifanyika kati ya Rais wa Uzbekistan Shavkat Mirziyoyev na Rais wa Amerika Donald Trump. Mazungumzo hayo yalifanyika katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa kama sehemu ya kikao cha themanini cha Baraza Kuu la Shirika. (Tovuti ya Urais wa Uzbek, 2025/09/25).
Maoni:
Ziara ya Mirziyoyev nchini Marekani na mkutano wake na Trump zimezua mijadala mingi ndani na nje ya Uzbekistan ambayo bado inaendelea hadi leo. Ukweli ni kwamba ziara hii sio tu moja ya matukio muhimu katika nyakati za hivi karibuni, lakini pia inaweza kuwa hatua muhimu katika hali ya kisiasa katika Asia ya Kati. Kwa sababu wakati wa ziara hiyo, matukio kadhaa mashuhuri yalitokea. Kwa mfano, mikataba kati ya nchi hizo mbili yenye thamani ya rekodi ya dola bilioni 105 ilisainiwa. Miongoni mwao, inafaa kumbuka ununuzi wa ndege kutoka Boeing yenye thamani ya dola bilioni 8 na makubaliano juu ya rasilimali muhimu za madini ambazo maelezo yake hayakufunuliwa. Trump pia alipongeza hilo na kumuelezea Mirziyoyev kama "mtu wa maneno na kiongozi mkuu". Sergio Gore, mwakilishi maalum wa Rais wa Marekani katika Asia Kusini na Kati, alimjulisha Shavkat Mirziyoyev kwamba sasa amefunguliwa njia ya moja kwa moja ya kufika Ikulu ya White House.
Kwa kuzingatia maelezo haya na mengine, si vigumu kuelewa kwamba lengo kuu la ziara ya Mirziyoyev na wasomi wa kisiasa wanaomfuata ilikuwa kuhamia katika zizi la Marekani na kuimarisha mamlaka yake. Kwa kusudi hili, utajiri wa madini ambao ni mali ya watu wetu Waislamu nchini Uzbekistan ulitawanywa chini ya miguu ya Trump kafiri na milango ilifunguliwa kwa upana kwa makampuni ya Marekani kupenya uchumi, nishati na sekta nyinginezo katika nchi yetu. Idadi ya wachambuzi wa kisiasa na vyombo vya habari katika nchi yetu waliona mafanikio ya Mirziyoyev katika kuvutia umakini na msaada wa Amerika, nchi yenye nguvu zaidi ulimwenguni, kama ustadi na ujanja wa kisiasa kutoka kwake!
Lakini walisahau au walikusudia kuficha ukweli mchungu; Mnamo Oktoba 7, 2025, haswa miaka miwili ilipita, ambayo ni siku 730, tangu operesheni ya Mvua ya Mawe ya Al-Aqsa dhidi ya chombo cha Kiyahudi kinachovamia. Ambayo ndugu zetu Waislamu huko Gaza na Ukingo wa Magharibi wanapitia na wameteseka wakati wa siku hizi 730 za kutisha ambazo haziwezi kuelezewa kwa maneno.
Ingawa operesheni ya Mvua ya Mawe ya Al-Aqsa ilianzishwa na ndugu zetu mashujaa waliopo katika ardhi takatifu ya Palestina, maana yake kwa hakika ni pana zaidi na ni wito kwa taifa zima! Wito huu unaweza kuonyeshwa kama ifuatavyo: Enyi Umma wa Kiislamu! Tumeanza kupinga uvamizi tukimtegemea Mungu na tuko tayari kujitolea roho zetu kwa ajili ya ukombozi wa Al-Aqsa na ardhi takatifu ya Palestina, msikiti aliotembelea Mtume ﷺ! Je, kuna watu wa kweli miongoni mwenu ambao watafanya kazi hii tukufu na kukomesha kabisa chombo cha Kiyahudi na kukifuta kutoka usoni mwa dunia?! Ndiyo, nyuma ya operesheni hii kuna wito kama huu, wito unaoelekezwa kwa Umma wa Kiislamu, hasa majeshi yake! Mtu yeyote mwenye akili timamu, hata kama anafikiria kidogo, hakika atalielewa hilo.
Je, itikio la mifumo inayotutawala kwa wito huu lilikuwaje? Kama tulivyoona, walijibu kwa maneno matupu, kulaani kwa uongo, kukata tamaa, mikutano na makongamano mengi yasiyo na maana. Wakati huohuo, walikuwa wanashughulika kuwazuia Waislamu kusaidia ndugu zao huko Gaza, kunyamazisha sauti na kutetea chombo cha Kiyahudi. Jambo la kuumiza zaidi ni kwamba walitaka kumridhisha Amerika, ambayo iliunga mkono kwa kila njia mtoto wake mpendwa, chombo cha Kiyahudi, na kupata upendeleo wa rais wake, Trump. Hasa Rais wa Uzbekistan Mirziyoyev, ambaye alionyesha uaminifu wake kwa Amerika, ambayo ndiye mlinzi mkuu wa chombo cha Kiyahudi, wakati wa ziara hii.
Wakati Waislamu wanakufa chini ya mvua ya mabomu na wanakabiliwa na njaa na ugonjwa, watawala ambao wanajiona kuwa Waislamu wanawaza tu jinsi ya kulinda viti vyao vya enzi. Basi hakuna jema linaloweza kutoka kwao, na hawakuhisi mateso ya Waislamu wanaoteseka si siku moja au mbili, bali siku 730!
Leo, ni wazi zaidi kuliko wakati mwingine wowote kwamba Khilafah ndiyo kimbilio pekee kwetu sisi Waislamu ambayo itatutunza na itakuwa paradiso yetu! Kwa hiyo, kuanzisha dola yetu iliyobarikiwa ni suala la hatima kwa Umma wa Kiislamu na taji la faradhi! Mtume ﷺ alisema: «Hakika Imamu ni ngao, anapiganwa nyuma yake na anaogopwa kwa ajili yake».
Imeandikwa kwa Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Islam Abu Khalil - Uzbekistan