Mateka Wasio na Mwenye Kuwaokoa!!
Habari:
Klabu ya Mateka ya Palestina imethibitisha kwamba uvamizi unaendelea kuwakamata wanawake 49 wa Kipalestina, wakiwemo wasichana wadogo wawili na mfungwa kutoka Gaza, ambao wanakabiliwa na uhalifu uliopangwa na wa kimfumo wa kukandamiza ndani ya magereza ya uvamizi na vituo vya uchunguzi. Klabu hiyo ilieleza, katika taarifa yake iliyotolewa kwenye kile kinachoitwa (Siku ya Kitaifa ya Wanawake wa Palestina), kwamba kasi ya uhalifu huu imeongezeka kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa tangu kuzuka kwa vita vya mauaji ya kimbari ambayo yameunda hatua mbaya zaidi katika historia ya watu wa Palestina, na bado athari zake zinaacha alama zao kali kwenye hali halisi ya wanawake wafungwa.
Maoni:
Tangu tarehe saba Oktoba 2023 hadi leo, zaidi ya visa 595 vya kukamatwa kwa wanawake vimerekodiwa katika Ukingo wa Magharibi, Jerusalem, na maeneo yanayokaliwa mwaka 1948, huku takwimu sahihi za idadi ya wanawake waliokamatwa kutoka Gaza hazipatikani. Sera ya kuwakamata wanawake kama mateka imeshuhudia ongezeko kubwa wakati wa vita, kwani uvamizi ulitumia mbinu hii kuwashinikiza watu kutoka familia za wafungwa kujisalimisha. Sera hii ilijumuisha wake za wafungwa na mashahidi na mama wazee zaidi ya miaka sabini, na iliambatana na vitendo vya unyanyasaji na uharibifu wa nyumba, kunyang'anywa mali, kuwatisha watoto, pamoja na kuwatishia wafungwa kwa kuwaua waume zao au watoto wao wanaoshikiliwa.
Hatua iliyofuata vita vya mauaji ya kimbari ilileta mabadiliko makubwa katika hali ya kuwekwa kizuizini kwa wanawake wafungwa kwa upande wa ukatili na kiwango, na iliambatana na msururu wa uhalifu wa ukandamizaji, muhimu zaidi ambao - kulingana na ushuhuda wa wafungwa - ni kuwekwa kwao katika seli chafu ambazo hazina mahitaji ya msingi ya maisha. Uvamizi wa mara kwa mara katika seli hizo na kufichuliwa kwao kwa upekuzi wa uchi, kuzuiliwa, kupigwa, unyanyasaji, na vitisho vya ubakaji, kupelekwa kwa udhalilishaji katika uwanja wa gereza, kulazimishwa kuchukua nafasi za kudhalilisha, kupewa chakula kilichoharibika na magodoro yaliyochakaa ambayo hayafai kutumika, na kugeuza mahitaji rahisi zaidi ya wafungwa kuwa chombo cha adhabu ya pamoja, ikiwa ni pamoja na taulo za usafi na nguo. Pia wamenyimwa njia za uingizaji hewa katika majira ya joto na njia za kupasha joto wakati wa baridi, pamoja na kuzuia ziara za familia na mawakili, na kutengwa kwa pamoja endelevu kama ilivyoripotiwa na wafungwa waliokombolewa na wengine ndani ya magereza katika ushuhuda uliothibitishwa.
Ni muhimu kukumbuka kuwa sababu muhimu zaidi za kukamatwa katika hatua hii, kwa misingi ya uhuru wa maoni na kujieleza, au kile ambacho uvamizi unadai kuwa uchochezi kwenye njia za mawasiliano ya kielektroniki, ambapo wafungwa wengi wanashikiliwa leo kwa misingi ya uchochezi, na 12 kati yao wako chini ya kizuizi cha kiutawala. Wakati wengine wanashikiliwa kiutawala kwa kisingizio cha faili ya siri.
Huu ndio uvamizi dhalimu ambao hufanya kila aina ya vurugu na mateso dhidi ya wanawake, watoto na wanaume bila mahitaji ya chini kabisa ya ubinadamu, na ama wanasiasa na viongozi wanatazama tu na wameishughulisha dunia na mateka wachache wa Kiyahudi ambao hawafanyiwi ukatili wowote. Hii inatokea na Mamlaka vibaraka badala ya kufanya kazi ya kuwaachilia huru wafungwa hawa, wanajishughulisha na mipango ya kuharibu wanawake na jamii, na kuficha ufisadi wao na ufisadi wa watu wao, na kuwafuata watu waaminifu na wale wanaosema ukweli na kuwafunga magerezani ili kunyamazisha sauti zao, wakifuata sera ya ukandamizaji ambayo haitofautiani sana na sera ya Wayahudi kwani wote wana lengo moja, nalo ni kumaliza suala la Palestina.
Lakini kama Bwana Mwenye Ukuu alivyosema katika kitabu chake kitukufu: ﴿Na kumbuka walipokufanyia vitimbi wale walio kufuru ili wakufunge au wakuue au wakutoe, nao wanafanya vitimbi na Mwenyezi Mungu anafanya vitimbi, na Mwenyezi Mungu ni mbora wa wenye kufanya vitimbi﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Muslima Al-Shami (Um Suhaib)