Makubaliano ya Abrahamu na Asia ya Kati: Lengo Baya la Kijiografia la Trump
Habari:
Kulingana na shirika la habari la Reuters, wawakilishi wa utawala wa Trump - haswa Steve Witkoff na Aryeh Lightstone - wanafanya mazungumzo na Azerbaijan, Kazakhstan, na labda nchi zingine za Asia ya Kati kuhusu makubaliano ya Abrahamu.
Maoni:
Kitendo hiki kinafanyika wakati ambapo chombo haramu cha Kiyahudi kinaendelea kufanya kila aina ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu huko Gaza, na kuwachinja bila huruma makumi ya maelfu ya wanawake na watoto, jambo hili linaifanya kuwa hatua ya kidiplomasia ya aibu na hatari zaidi.
Amerika haijaacha nia yake ya kudumisha ubabe wake wa kijiografia duniani kwa kuidhibiti eneo la Kiislamu ambalo lina utajiri mkuu duniani na ardhi za umuhimu wa kimkakati.
Kwa sababu hiyo, inajitahidi kudhibiti eneo la Ghuba ya Kiarabu na eneo la Bahari ya Caspian, ambako rasilimali kuu na mishipa mikuu ya njia zinazisafirisha katika eneo la Mashariki ya Kati zinapatikana. Na imechagua kufikia malengo haya kupitia chombo haramu cha Kiyahudi. Ili kufanikisha hili, inafanya kazi ya kuhimiza tawala vibaraka zilizopo katika nchi za Kiislamu kuitambua rasmi kupitia mipango ya kidiplomasia inayoitwa makubaliano ya Abrahamu, na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kijeshi nayo, na kuikubali kama mhusika aliyejumuishwa na halali na nguvu inayoongoza katika eneo la Kiislamu, pamoja na kuchukua jukumu la mtoaji anayeilisha.
Amerika inafanya kazi ya kulinda kituo cha ushawishi na ubabe katika eneo la Kiislamu kwa chombo haramu cha Kiyahudi kwa kuwadhalilisha watawala wa Waislamu waoga na kuwageuza kuwa zana za kifedha na vifaa vyake. Trump adui wa Uislamu na Waislamu analenga kufikia malengo yake ya kijiografia kwa msaada wa chombo haramu cha Kiyahudi ambacho ni saratani katika mwili wa Umma, kudhibiti rasilimali na mtiririko wake, kutumia mkakati wa ushindi kwa nguvu, kuunda hali ya ukosefu wa utulivu, mizozo na njama katika nchi za Waislamu, kukuza hatua za kikoloni, na muhimu zaidi, kuzuia juhudi za Umma katika kuanzisha tena maisha ya Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume.
Makubaliano ya Abrahamu, yaliyoanzishwa na Trump mwaka 2020, yamepanuliwa kujumuisha Caucasus na Asia ya Kati baada ya Trump kuomba zaidi ya marabi 50 rasmi kupanua wigo wa makubaliano hayo ili kujumuisha nchi zinazozungumza Kituruki.
Kupitia makubaliano haya, Amerika haipati tu faida ya kijiografia dhidi ya China na Urusi, lakini pia inajaribu kuziba nyufa katika sera ya kigeni ya Trump.
Ingawa mwakilishi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uzbekistan, Ahrar Burhanov, alisisitiza kwamba "Uzbekistan haijapokea mwaliko wowote kutoka Amerika kuhusu suala hili," kuimarisha mfumo wa Mirziyoyev wa mahusiano na chombo haramu cha Kiyahudi kunaonyesha kinyume chake, Je, inawezekana kwamba Mirziyoyev na mfumo wake hawajui maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ﴿Utakuta walio na uadui mkali zaidi kwa walioamini ni Mayahudi na washirikina﴾, au ﴿Enyi mlio amini! Msiwafanye Mayahudi na Wakristo kuwa marafiki. Wao ni marafiki wao kwa wao. Na miongoni mwenu anayewafanya marafiki basi huyo ni miongoni mwao. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhalimu﴾؟!
Mirziyoyev na mfumo wake wanapaswa kujua kwamba kukubali makubaliano ya Abrahamu na kushiriki katika aina yoyote ya mawasiliano au ushirikiano na chombo haramu cha Kiyahudi ni usaliti kwa Mwenyezi Mungu, Mtume wake ﷺ na Umma! Huu ni uharibifu wa ardhi takatifu; safari ya Mtume ﷺ na Masjid al-Aqsa! Hii ni kukanyaga damu na miili ya watoto na wachanga iliyoungua! Hii ni dharau kwa miili ya wanawake na wazee, iliyoraruliwa au kugeuka kuwa mifupa kutokana na njaa! Huu ni ushirikiano katika uhalifu wa kikatili unaofanywa na chombo haramu! Hili ni makubaliano ya usaliti yaliyofanywa juu ya kilio cha mama na watoto!
Mirziyoyev na mfumo wake wanapaswa kutambua kwamba haki za makumi ya maelfu ya mashahidi wa Gaza hazitapotea bure, na kwamba saa ya kulipiza kisasi iko karibu! Na wasisahau kwamba Khilafah Rashidah itasimama hivi karibuni kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, ahadi ya kweli na haki!
﴿Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walio amini miongoni mwenu na wakatenda mema, ya kwamba atawafanya makhalifa katika ardhi kama alivyowafanya makhalifa wale walio kuwa kabla yao, na kwa yakini atawathibitishia Dini yao aliyo wapendelea, na atawabadilishia amani baada ya khofu yao﴾
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Islam Abu Khalil - Uzbekistan