Siku ya Ijumaa, Waziri wa Awqaf Awaita Uzushi!
Habari:
Waziri wa Awqaf na Mwongozo wa Yemen, Dkt. Muhammad Shabiba, amewataka wahutubu, maimamu wa misikiti, wanazuoni, na wahubiri katika mikoa mbalimbali kutenga hotuba za Ijumaa na masomo kwa ajili ya kufufua maana na malengo ya mapinduzi ya Septemba na Oktoba na kushikamana na maadili ya uhuru na jamhuri. (Aden Al-Ghad, Septemba 21, 2025).
Maoni:
Mtume ﷺ alisema: «Hakika yeyote atakayeishi miongoni mwenu ataona tofauti nyingi, basi shikamaneni na Sunnah zangu, na Sunnah za Makhalifa Waongofu Waongozaji, ziumeni kwa magego, na tahadharini na mambo ya uzushi, kwani kila uzushi ni upotofu» Imesimuliwa na Al-Hakim katika Al-Mustadrak.
Hadithi hii ambayo haikosi katika hotuba ya Ijumaa, waziri wa Awqaf anakuja na kuipuuza kabisa, bali anawaita watu kwenye uzushi na kuuhuisha badala ya kuupiga vita!
Hakika Mtume ﷺ katika mawaidha haya anawaita Waislamu baada yake kushikamana na mfumo wa kisiasa wa Kiislamu ambao ni mfumo wa Khilafa pekee. Amewataka wafuate Sunnah za Makhalifa Waongofu, nayo ni mfumo wa kisiasa ambao walitawala nao kwa dalili ya neno makhalifa si masahaba, na wakati huo huo Mtume ﷺ anaonya dhidi ya uzushi wowote au mabadiliko katika mfumo huu na anasema kuwa ni upotofu ambao ni njia ya kwenda motoni.
Hakika waziri wa Awqaf badala ya kuwakumbusha watu katika kumbukumbu ya mapinduzi haya mawili yaliyoshindwa ambayo yamezalisha mfumo wa jamhuri na kuleta demokrasia ambayo ni kichwa cha uzushi katika wakati huu, na badala ya kuita umma kusahihisha mwelekeo wa mapinduzi haya ambayo yamezalisha kudorora, umaskini, na ukiwa, utegemezi, na kuwa mateka wa Magharibi makafiri na kuondoa Uislamu kutoka kwenye maisha na utawala, anakuja kwa ujasiri wote kuwaita watu kwenye uzushi na kwenye mfumo wa jamhuri wa Magharibi!!
Asili ya wanazuoni, wahutubu, na masheikh wote ni kuwaita Waislamu kurejesha mfumo wa Uislamu unaowakilishwa na Khilafa kwa njia ya Utume, na kuwakumbusha jinsi hali yao ilivyokuwa chini ya utawala wa Uislamu, na jinsi walivyo leo kama mayatima kwenye meza za watu bakhili! Hafla hizi zinatukumbusha kwamba hakuna mafanikio duniani wala Akhera kwa kufuata miradi ya Magharibi na itikadi za uongo za uhuru wakati tunateseka chini ya utawala wa Magharibi katika nyanja zote za maisha, na ya kwanza ni utawala.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Omar Abdullah - Wilaya ya Yemen