Demokrasia Imejaribu Kuonyesha Haki za Wanawake na Inaunga Mkono Kila Kitu Kibaya
(Imetafsiriwa)
Habari:
Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) liliripoti kwamba Mbunge wa Uingereza Steve Reed alionyesha hasira kali baada ya kujua kuhusu kutengwa kwa wanawake kutoka mbio za hisani katika Victoria Park, Mashariki mwa London. Mbio hizo, zilizochukua kilomita tano na kuandaliwa na msikiti wa Mashariki mwa London, zilivutia mamia ya washiriki, lakini zilizuia kuingia kwa wanaume, wavulana na wasichana chini ya umri wa miaka 12, licha ya kutangazwa kama "jumuishi".
Mbunge Steve Reed alilaani ubaguzi wa kijinsia na kuueleza kuwa "hauwezi kukubalika kabisa" wakati wa mahojiano na redio ya LBC, akieleza "hofu na mshtuko" wake kutokana na kutengwa huko. Alisema kwamba kamati ya usawa na haki za binadamu itachunguza suala hilo, na uwezekano wa kuwekwa vikwazo baadaye.
Reed alisisitiza: "Hatutaki hali katika nchi hii ambapo wanaume wanaruhusiwa kufanya mambo ambayo wanawake wanazuiwa kuyafanya. Hatuwezi kuvumilia hilo," akilaani hasa matumizi ya maeneo ya umma kwa tukio lililozuiliwa kijinsia. Latfur Rahman, Meya wa Tower Hamlets, alinukuliwa kwenye tovuti ya msikiti akiwapongeza washiriki, "hasa vijana, wazee na jamii kwa ujumla kwa ushiriki wao leo," bila kutaja vizuizi vilivyowekwa kwa jinsia. Msikiti huo, ambao unaeleza tukio la kila mwaka la kuchangisha fedha kama tukio kuu katika kalenda ya Kiislamu ya London Mashariki ili kuchangisha fedha kwa ajili ya miradi ya vijana na kuwasaidia wakimbizi, haukujibu moja kwa moja ukosoaji huo, lakini ulisisitiza kujitolea kwake kusaidia wanawake katika shughuli mbalimbali za michezo. Baraza limeomba ufafanuzi wa haraka.
Maoni:
Unafiki katika maneno ya waziri huyo unastaajabisha sana! Hapa tuna wasiwasi mkubwa wa uongo kuhusu kuwashirikisha wanawake Waislamu nchini Uingereza, na hasira kwa kutoweza kwao "kugombea" huko London.
Hata hivyo, waziri huyo huyo anaunga mkono serikali ambayo imetoa silaha na kuruhusu mauaji na njaa ya makumi ya maelfu ya wanawake Waislamu huko Gaza.
Wanawake na watoto hao wanalazimishwa kukimbia dhuluma na mauaji yanayoendelea kwa miongo kadhaa.
Dada hawa wanalazimika kukimbia, wakiwa wamebeba watoto wao na baadhi ya mali zao.
Hakuna chaguo lingine kwa mama hawa ila kukimbia mali zao na utajiri wao ambao wameuacha nyuma ili kunyakuliwa na maadui wa Uislamu.
Bibi wanalazimika kukimbia kutoka kwa starehe zao na kukabiliana na hofu na shida zisizovumilika.
Mabinti wa umma huu wanakimbia elimu yao na vyeti vyao huku vyuo vikuu na shule zikigeuzwa kuwa makaburi ya pamoja.
Mabinti zetu wacha Mungu wanakimbia peke yao, wapweke, wakati walezi wao wote wa kiume wanapokamatwa au kuteswa au kutekwa nyara.
Waandishi wa habari kwenye mitandao ya kijamii waliandika kumbukumbu za wavulana na wasichana wadogo wakiwabeba ndugu zao wachanga kwa maili nyingi wanapotengwa na familia zao. Hawajui wanakokimbilia au wanaweza kumpata nani wa kuwasaidia, na maisha ya wengi wao yataendelea kuwa mafupi kwa sababu ya ugonjwa au ukosefu wa dawa, chakula na maji.
Upuuzi ulioongezwa katika maoni haya ya "uwezeshaji" kutoka kwa wanasiasa wa kilimwengu wanaoabudu ubepari ni kwamba hawaoni malalamiko yoyote kutoka kwa wanawake Waislamu wenyewe kwa sababu wamefurahi sana kudumisha heshima na utu wao.
Hata hivyo, wanawake Waislamu wanapozungumzia haki zao, maslahi ya Magharibi ambayo yanatafuta tu kuthamini haki za binadamu kwa misingi ya hasara na faida ya kikoloni huwapuuza.
Lazima tukumbuke maneno ya Mwenyezi Mungu tunapotahadharishwa dhidi ya adui aliyefichika; ﴿Na ukiwaona, miili yao inakupendeza, na wakisema, unasikiliza maneno yao; kama kwamba ni miti iliyoegemezwa. Wanadhani kila ukelele uko juu yao. Hao ndio adui, basi tahadhari nao. Mwenyezi Mungu awaangamize! Wamegeuzwa wapi?﴾.
Lazima tuwaonye vijana wetu na kuwa waangalifu dhidi ya ajenda kama za nyoka ambazo zinaonekana kufanya kazi vizuri lakini zimeundwa tu kukengeusha na kuumiza.
Imeandikwa kwa Idhaa ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Umrana Muhammad
Mwanachama wa Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir