Je, Trump amechoshwa na Urusi?
Habari:
Zelensky alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano kati ya Ukraine na Shirika la Nchi za Magharibi (NATO) na kuongeza matumizi ya ulinzi ya nchi wanachama. Hapo awali, tovuti ya Axios ilifichua kuwa Marekani inapanga kuuza silaha zenye thamani ya karibu dola bilioni 10 kwa washirika wake katika shirika hilo katika awamu ya kwanza, na kisha silaha hizi zitapelekwa Ukraine.
Habari hii inafuatia kauli ya Trump, wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika Ikulu ya White House alipomkaribisha Katibu Mkuu wa NATO Mark Rutte, ambapo alitangaza kuwa ataweka ushuru wa asilimia 100 kwa Urusi, ikiwa hakuna makubaliano yatakayofikiwa na Ukraine ndani ya siku 50. (Rai Al-Youm)
Maoni:
Mazungumzo yanarejea tena kuhusu kufufua usambazaji wa silaha kwa Ukraine na kuiunga mkono kwa makombora ya masafa marefu, afisa wa Ukraine alinukuu kutoka kwa utawala wa Marekani kwamba umehimiza Ukraine kulenga ndani ya Urusi kama njia ya kuilazimisha Urusi kukaa kwenye meza ya mazungumzo na kupunguza kiwango cha madai yake, ambayo iliongeza sana baada ya matamko ya utawala wa Trump tangu alipoingia madarakani kwamba hataunga mkono Ukraine kwa silaha na kwamba anataka amani na kukomesha faili la vita vya Urusi na Ukraine, kwa hivyo Urusi ilitumia matamko haya kukandamiza kijeshi na kisiasa, na hivyo kuongeza kiwango cha madai yake hadi kufikia hatua ya kutaka kuilazimisha Ukraine kuvunja silaha zake na kubaki kama eneo la usalama kati yake na NATO, yote hayo Urusi inafanya kwa hila ikitumia fursa ya kuchanganyikiwa kwa utawala wa Trump na kuzama kwake katika faili kubwa na za kimataifa ambazo hadi leo haijaweza kutatua yoyote kati yake; Vita vya chombo cha Kiyahudi dhidi ya watu wa Palestina vimevuta matokeo makubwa ambayo yamehusisha Marekani na kuifunga kwa sababu ya uungaji mkono kamili kwa chombo hicho, na kufuatiwa na vita na Iran, na vile vile upya wa joto la faili la Syria, bila kusahau faili la China, hakuna yoyote kati ya haya ambayo imetatuliwa, na hii ndiyo iliyohimiza Urusi kudai ikiwa katika msimamo wa nguvu.
Mwingiliano huu wote umeufanya utawala wa Trump kurudi kutishia kwa shinikizo la kijeshi ili kuilazimisha Urusi iwe na akili timamu zaidi na ikubali kukomesha vita.
Pia imebainika kuwa Marekani itaiunga mkono Ukraine kwa silaha lakini kutoka hazina ya Ulaya na NATO, na huu ni mabadiliko muhimu kwa utawala wa Trump na hatua ambayo Marekani inataka.
Ama Uingereza imekaribisha hatua hii kupitia mdomo wa waziri wake wa ulinzi, ambaye alisema tutasimama na Ukraine kufikia ushindi kamili dhidi ya Urusi, ambayo ni kwamba Uingereza haitaki vita iishe bali inafanya kazi kuirefusha na kuleta makabiliano ya moja kwa moja kati ya Marekani na Urusi, labda itapata kitu kutoka kwa historia yake ya zamani, kama ilivyo desturi yake ya ujanja, udanganyifu na kuangusha nchi zinazoshindana nayo.
Hitimisho ni kwamba Trump hataki vita kamili na kali kati ya Urusi na Ukraine, bali anaitaka ili kuishinikiza Urusi kufanya mazungumzo na kukomesha vita, labda hili litakuwa mafanikio yake ya kwanza katika mwaka wa kwanza wa muhula wake wa urais. Na swali ni je, Urusi italainika? Au itaendelea kushinikiza kufikia maslahi yake mengi iwezekanavyo?
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Dkt. Muhammad Al-Tumaizi