Je, Washington Inafanya Mapatano na Baraza la Urais la Yemen?
Habari:
Rais na wanachama wa Baraza la Urais la Yemen pamoja na kamati ya kijeshi wanajiandaa kuelekea Washington. (Kituo cha Televisheni cha Belqees, Septemba 11, 2025).
Maoni:
Marekani imeliita Baraza la Urais la Yemen pamoja na kamati ya kijeshi kwenda Washington wakati ambapo vitisho vya Wahouthi vimerudi katika Bahari Nyekundu na dhidi ya taasisi ya Kiyahudi, na mashambulizi ya anga ya Kiyahudi dhidi ya Sanaa inayodhibitiwa na Wahouthi hayajafanikiwa, kwani hayazidi kuwa mashambulizi dhidi ya miundombinu ya kiraia na dhidi ya watu wasio na ushawishi katika muundo wa kisiasa na kijeshi wa Wahouthi.
Marekani leo inafanya kazi ya kuiuza taasisi ya Kiyahudi kama nguvu ya kwanza katika eneo hilo na kwamba inamiliki mkono unaoweza kufika Sanaa, Doha na hata Tehran wakati wowote inapenda, na kwamba serikali katika eneo hilo hazina budi ila kuweka rehani nafsi zao kwa Marekani kwa ajili ya ulinzi na kuendelea kuendesha viwanda vya silaha za Marekani, haswa mifumo ya ulinzi wa anga, na kwa hili Trump anapata karata ya kiuchumi dhidi ya wapinzani wake wa Kidemokrasia, na sio hili tu bali Trump atazilazimisha serikali zilizopo katika nchi za Kiislamu kuelekea katika kuanzisha uhusiano wa wazi na taasisi ya Kiyahudi, wakati ambapo baadhi ya nchi za dunia zinalazimika kuondoa mabalozi wao kutoka kwake kutokana na mauaji inayoyafanya huko Palestina na katika eneo kwa ujumla.
Basi hivi ndivyo Marekani inavyopanga kwa ajili ya mwanawe mpendwa, taasisi ya Kiyahudi; kuwa boogeyman mbadala wa Iran katika eneo hilo, na kupanuka kuelekea kusini mwa Lebanon, Syria na pengine zaidi ya hayo, na kuwa sehemu ya mfumo tawala katika eneo hilo chini ya ushawishi wa bunduki ya Marekani.
Na kwa kuwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya Wahouthi hayakufanikiwa katika kusimamisha tishio lao dhidi ya taasisi ya Kiyahudi, na mashambulizi ya taasisi yenyewe hayakufanikiwa dhidi yao, na kuendelea kwa uungaji mkono wa Iran kwao, Marekani imealika Baraza la Urais la Yemen kwake pamoja na kamati ya kijeshi pengine kwa ajili ya kufanya mapatano nalo ili kuliunga mkono kijeshi kuwalazimisha Wahouthi kuingia katika mazungumzo ya amani na kuunda serikali ya Yemen iliyounganishwa na Wahouthi, itakayolinda maslahi ya Marekani nchini Yemen, pamoja na uwepo wa Saudia ndani ya Yemen, na kwa hili Baraza la Urais linaloungwa mkono na Ulaya litakuwa limezungukwa na uwepo wa Wahouthi na uwepo wa kisiasa wa Saudia ili kulinda maslahi ya Marekani bila ya kurejea katika operesheni kubwa ya kijeshi ambayo Marekani inaweza isijue jinsi ya kuimaliza, kwa hivyo uwepo wa Imarati ambao unahudumia maslahi ya Uingereza haupuuzwi huko Aden na katika miji ya pwani na katika visiwa vya Yemen, na vile vile Baraza la Mpito la Kusini ambalo lilianzishwa na Imarati linamiliki uwepo mpana wa hadhara kwani linatumia karata ya suala la kusini na linatishia kutenganisha kusini mwa Yemen na kaskazini mwake, pamoja na kuwa Baraza la Urais linawakilisha kundi la vyama vya Yemen ambavyo vinaunga mkono Uingereza huko Aden pamoja na uwepo wa mabaki ya mfumo wa marehemu Ali Saleh anayewakilishwa na Tariq Saleh na jeshi lake katika pwani ya magharibi, na hivi majuzi Uingereza ilitangaza kuwapa silaha walinzi wa pwani wa Yemen kwa kisingizio cha kulinda usafiri wa kimataifa.
Kwa hivyo, mwaliko wa Baraza la Urais na kamati yake ya kijeshi kwenda Washington unaweza kuzaa mapatano ya kijeshi ya kulinda Bahari Nyekundu dhidi ya Wahouthi na pengine kuwazuia kurusha ndege zisizo na rubani na makombora dhidi ya taasisi ya Kiyahudi.
Hivi ndivyo Marekani inapanga kusimamia Mashariki ya Kati Mpya kwa kutumia watawala watiifu ambao hawawezi hata kuinua vichwa vyao mbele yake, hata wakati inakiuka mamlaka yao na kupora mali zao bila pingamizi! Na kwa kutumia wanamgambo wa kijeshi ambao wanapaza sauti mbiu ya mauti kwa Marekani wakati ambapo hakuna aijuaye mauti kutoka kwake ila wananchi wa Yemen!
Lakini huenda Marekani isisaidiwe na wakati, na umma unachemka kila mahali dhidi yake na dhidi ya taasisi ya Kiyahudi na Magharibi yote, na hakuna kilichosalia ila kidogo tu mpaka umma wa Kiislamu uinue bendera za Khilafah ambayo itamfukuza kafiri wa Magharibi kutoka katika nchi zote na kuukomboa ulimwengu kutoka katika ushawishi wa Kizayuni-Kimarekani, ﴿NA ALLAH NI MWENYE KUSHINDA JUU YA MAMBO YAKE, LAKINI WATU WENGI HAWATAMBUI﴾.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut Tahrir
Abdul Aziz Al-Hamid - Wilaya ya Yemen