Harakati za Uhuru Zilikuwa Ulaghai Tu kwa Umma
(Imetafsiriwa)
Habari:
Tarehe 14 Oktoba inachukuliwa kuwa siku ya mapumziko ya umma nchini Tanzania, ambayo huadhimisha kila mwaka kumbukumbu ya kifo cha Julius Nyerere, "Baba wa Taifa" ambaye alifariki London mnamo 1999.
Maoni:
Siku hii ni muhimu nchini Tanzania, kwani inaadhimisha kumbukumbu ya maisha na urithi wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye anachukuliwa kuwa kiongozi mkuu ambaye alichukua jukumu muhimu kama mwanaharakati wa kupinga ukoloni, na mwananadharia wa kisiasa ambaye alichangia katika kuunda sura ya mustakabali wa nchi.
Licha ya utawala wa kimabavu wa Nyerere ambao uliendelea kwa miaka 24, tangu uhuru mwishoni mwa 1961 hadi alipoondoka madarakani mwishoni mwa 1985, lakini yeye, kama wengine wanaoitwa wapigania uhuru, alikuwa mtu wa kuheshimiwa sana, na kupewa nafasi ambayo karibu inamfanya kuwa kinyume na uhalisia.
Picha ya mwisho ya wanaoitwa wanaharakati wa kupinga ukoloni, kama vile Nyerere, ambaye alikuwa mstari wa mbele katika mapambano ya uhuru wa bendera, itakuwa wazi mara tu itakapounganishwa na muktadha wa kimataifa wakati huo.
Baada ya Vita vya Pili vya Dunia, misimamo ya wakoloni wa zamani, haswa Uingereza na Ufaransa, ilidhoofika katika ngazi ya kimataifa. Badala yake, Amerika iliongezeka kukabiliana na ushawishi wao duniani. Licha ya kufanana kwa mfumo wao wa kibepari, mataifa haya yanatofautiana katika maslahi yao ya kitaifa.
Uingereza ilikuja na mikakati kadhaa ya kudumisha na kulinda utawala wake na ushawishi wake unaopungua katika makoloni yake, kama vile kuimarisha Jumuiya ya Madola ya Uingereza, kupanua mitandao yake ya elimu katika shule na vyuo vikuu na kutumia taasisi hizo kuwafunza mawakala waaminifu ambao watapewa aina fulani ya uhuru wa bendera ili kuendana na wimbi la kimataifa linaloongozwa na Marekani ili kudumisha ushawishi wake.
Wafuasi wa Uingereza katika uwanja wa elimu ndani ya makoloni ya Uingereza, kama vile Lord Cromer huko Misri na Lord Macaulay huko India, walieleza kuwa lengo la mfumo wa elimu wa Uingereza ni kuwahifadhi wakaazi wa makoloni yao kama raia asilia kwa sura tu, lakini kuwageuza kuwa ladha, sera, na mitazamo ya Kiingereza.
Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, Afrika Mashariki, kilikuwa mojawapo ya mifano mingi ambayo ilitekeleza mkakati huu wa Uingereza kwa kiasi fulani. Ni wazi kwamba Nyerere alikuwa miongoni mwa wale waliopata uangalizi kama huo huko Makerere, kisha akapata elimu ya ziada na kuboresha ujuzi wake huko Edinburgh nchini Uingereza.
Alikuwa mfuasi mwaminifu wa Uingereza, kiasi kwamba jaribio la mapinduzi lilipotokea mwanzoni mwa miaka ya sitini, Uingereza iliharakisha kuokoa mtu wake mdogo.
Kwa kuongezea, Uingereza ilimkabidhi Nyerere jukumu la kuelekea haraka Zanzibar ili kuwezesha muungano wa kile kinachoitwa jamii za Kiafrika na Shirazi, ambayo ilisababisha kuzaliwa kwa chama cha Afro Shirazi, ambacho kilikuwa kikifanya kazi kwa niaba ya Uingereza kutoka nyuma ya pazia.
Chini ya uongozi wa Nyerere, chama cha Afro Shirazi kilifanikiwa kuipindua serikali ya Zanzibar, na kisha kilifanikiwa kufanikisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar kulingana na maagizo ya Uingereza.
Bila kusahau jinsi chama hiki kinachofanana kilitumiwa kupanda na kuchochea fitina za kikabila na kushiriki katika vitendo vya ukatili kati ya Waislamu wa Zanzibar na umma kwa ujumla.
Katika kesi ya Tanganyika, tunakumbuka jinsi Nyerere aliwatenga Waislamu, akasababisha usumbufu katika umoja wao, akavunja taasisi zao, na akawapuuza licha ya mapokezi makubwa, heshima kubwa kwake, na huduma yao kwake na msaada katika mapambano ya uhuru.
Nyerere aliiacha nchi chini ya udhibiti wa Uingereza, iliyojificha kama uhuru, na akaipa Uingereza fursa zote za kutumia rasilimali za nchi wakati watu wake, Waislamu na wasio Waislamu sawa, walikuwa wakipambana na magumu na ukosefu wa uhakika.
Hivi ndivyo wito wa uhuru na ukombozi ulivyotumiwa kuwadanganya watu na maoni ya umma, ukiwasilisha mashujaa bandia, ambao kwa kweli ni mawakala wa wakoloni. Ukombozi wa kweli hautapatikana na hakutakuwa na mashujaa wa kweli isipokuwa kwa kuimarisha fikra za Kiislamu na dola ya Khilafa.
Imeandikwa kwa ajili ya Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Saeed Bitumwa
Mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir Tanzania