Ujenzi wa Gaza chini ya Uangalizi wa Wauaji na Wanaounga Mkono Taifa Haramu
Mkakati Mpya kwa Sura ya Zamani
Habari:
Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza, siku ya Alhamisi, mpango mpya wa kuboresha hali ya maisha katika Ukanda wa Gaza, akionyesha kuwa Marekani inafanya kazi "kuunda mahali ambapo watu wanaweza kuishi katika hali bora". Wakati wa matamshi yake katika Ikulu ya White House, Trump alielezea hali katika Gaza kama "mbaya," akisisitiza kuwa kipaumbele cha sasa ni kurejesha mateka, kisha kuhamia katika hatua ya ujenzi mpya. Trump alifichua mawasiliano na idadi ya nchi tajiri ambazo zimeonyesha utayari wa kufadhili miradi ya ujenzi mpya wa Gaza, akisema: "Kuna nchi tajiri sana ambazo zitashiriki katika ujenzi wa Gaza, na gharama yake sio kubwa kwao kwa sababu wana pesa nyingi." (Tovuti ya Gazeti la Al-Jumhuriya, 2025/10/4)
Maoni:
Trump anazungumza kana kwamba yeye ni upande wa amani, au kana kwamba hana uhusiano wowote na kile kilichotokea na kinachoendelea huko Gaza! Adui wa Mungu na Mtume wake anazungumza kana kwamba hakutenda uhalifu wala dhambi, na haupati katika maneno yake majuto, na hii haishangazi; kwani yeye ni mfuasi mkuu wa taifa la Kiyahudi, anamlisha kwa silaha, anamkinga, anamuunga mkono na kumsaidia. Anazungumza yote haya na hapatiwi hesabu na mtu yeyote, wala hahusishwi na lawama au kulaaniwa, kana kwamba roho za Waislamu zilizopotea huko Gaza hazina uzito wala thamani kwa hawa, na hazistahili kuhesabiwa.
Na vipi itakuwa hivyo, wakati dola ya Kiislamu haipo, na Waislamu wako kama povu la mafuriko? Hakuna uweza wala nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu.
Haitaji, ewe Trump, kwani humpati mtu wa kukuhisabu wala wa kukuadabisha, kana kwamba damu ya Waislamu ni kitu cha bei nafuu zaidi kwenu. Hii ndiyo sura halisi yako na ya Magharibi, ambayo haijafichika tena kwa mtu yeyote. Mambo yamefichuka na utata umeondoka. Ingawa Magharibi yote, na Amerika na Uingereza haswa, wamemwaga damu ya Waislamu kama mito, lakini walikuwa wakishikilia itikadi tupu na misemo ya kupendeza, kama vile uhuru, haki za binadamu, haki za mtoto, haki za mwanamke, haki za raia, na mengineyo ambayo wanakuza usiku na mchana.
Lakini vita vya hivi karibuni vya Gaza vimeondoa vinyago, na kufichua ukweli wazi kama jua la adhuhuri. Uongo huu wote umeanguka, na Trump anashughulika na kiburi na majivuno haya, na anatoa matamshi kwa uhuru kamili katika kivuli cha kutokuwepo kwa mhasibu, mrekebishaji na mwenye kulipiza kisasi. Trump, ambaye anajionyesha leo kama kiongozi wa amani, ni mchinjaji anayemwaga damu, kwani alikuwa mfuasi mkuu na wa kudumu wa taifa la Kiyahudi katika vita vyake dhidi ya watu wa Gaza. Na Trump, ambaye anashtushwa na hali katika Gaza na anaona kuwa ni mbaya, ndiye yeye mwenyewe alikuwa akitengeneza hali hii chini ya macho yake, na kwa msaada na uangalizi wake!
Kisha anasema kwamba watu katika mitaa ya nchi za Kiislamu wanacheza kwa furaha! Fahamu, ewe adui wa Mungu, adui wa Mtume wake, na adui wa waumini, kwamba watu wanafurahi sio kwa sababu ya uamuzi wako, lakini kwa ajili ya kusitisha mauaji na ukatili dhidi ya ndugu zao dhaifu, mbele ya macho na masikio ya watawala wa Ruvibedha, walinzi wa Magharibi, na walinzi wa Wayahudi.
Enyi umma wa Kiislamu: Huyu hapa Trump anaua na anaendelea kuwaua Waislamu na kusimamisha mauaji kwa maamuzi yake na makubaliano yake bila mhasibu, je, huu ndio maadili ya Waislamu ambao Mola wao alisema kuwahusu: ﴿NA WALE AMBAO WANAPOWAPATA DHULUMA, WANALIPISA﴾? Na tuko wapi kutokana na kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: ﴿NA MKIADHIBU, ADHIBUNI KWA MFANO WA VILE MLIVYOADHIBIWA﴾?
Enyi askari wa umma na watu wa nguvu zake: Hakika ulinzi wa ardhi yenu, na udhihirisho wa dini yenu, hautakuwa ila kwa kusimamisha dola ya Khilafa Rashidah ya pili kwa njia ya Utume. Basi wekeni mikono yenu katika mikono ya Hizb ut-Tahrir, na rudieni kwenye njia ya Mola wenu, na kwenye sunna ya Nabii wenu ﷺ, mpate radhi za Mola wenu, na Mwenyezi Mungu atukuzie Uislamu na watu wake kupitia nyinyi, na adhalilishe ukafiri na watu wake kupitia nyinyi.
Enyi majeshi ya umma: Tunawaweka mbele ya wajibu wa kisheria ambao Mwenyezi Mungu amewalazimu na ambao mtaulizwa kuuhusu mbele ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama, na watu wa Misri na Ardhi Iliyobarikiwa watang’ang’ania shingo zenu, bali na umma kwa ujumla, ikiwa mtakaa chini na msiwasaidie na msiwaunge mkono wale wanaofanya kazi ya kusimamisha dola yake na kurejesha mamlaka yake, basi himeni kwani fursa iko mikononi mwenu na kheri inawaita, na unganisheni kamba zenu na wale wanaoaminika wanaofanya kazi ya kutekeleza Uislamu na kurejesha mamlaka yake upya, huenda Mwenyezi Mungu akawasamehe yaliyopita na kuandika kheri kupitia mikono yenu, na isimamishwe dola ambayo umma unaingojea na ambayo Mwenyezi Mungu Ameahidi na kumletea bishara Nabii wake ﷺ; Khilafa Rashidah kwa njia ya Utume.
﴿ENYI MLIOAMINI! MTEKELEZENI MWENYEZI MUNGU NA MTUME ANAPOKUITENI KWENYE YALE YANAYOKUHUISHA﴾
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir
Bilal Abdullah - Wilaya ya Misri