Ujenzi wa Gaza chini ya Uangalizi wa Wauaji na Wanaounga Mkono Taifa Haramu: Mkakati Mpya kwa Sura ya Zamani
Ujenzi wa Gaza chini ya Uangalizi wa Wauaji na Wanaounga Mkono Taifa Haramu: Mkakati Mpya kwa Sura ya Zamani

Habari:

0:00 0:00
Speed:
October 12, 2025

Ujenzi wa Gaza chini ya Uangalizi wa Wauaji na Wanaounga Mkono Taifa Haramu: Mkakati Mpya kwa Sura ya Zamani

Ujenzi wa Gaza chini ya Uangalizi wa Wauaji na Wanaounga Mkono Taifa Haramu

Mkakati Mpya kwa Sura ya Zamani

Habari:

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza, siku ya Alhamisi, mpango mpya wa kuboresha hali ya maisha katika Ukanda wa Gaza, akionyesha kuwa Marekani inafanya kazi "kuunda mahali ambapo watu wanaweza kuishi katika hali bora". Wakati wa matamshi yake katika Ikulu ya White House, Trump alielezea hali katika Gaza kama "mbaya," akisisitiza kuwa kipaumbele cha sasa ni kurejesha mateka, kisha kuhamia katika hatua ya ujenzi mpya. Trump alifichua mawasiliano na idadi ya nchi tajiri ambazo zimeonyesha utayari wa kufadhili miradi ya ujenzi mpya wa Gaza, akisema: "Kuna nchi tajiri sana ambazo zitashiriki katika ujenzi wa Gaza, na gharama yake sio kubwa kwao kwa sababu wana pesa nyingi." (Tovuti ya Gazeti la Al-Jumhuriya, 2025/10/4)

Maoni:

Trump anazungumza kana kwamba yeye ni upande wa amani, au kana kwamba hana uhusiano wowote na kile kilichotokea na kinachoendelea huko Gaza! Adui wa Mungu na Mtume wake anazungumza kana kwamba hakutenda uhalifu wala dhambi, na haupati katika maneno yake majuto, na hii haishangazi; kwani yeye ni mfuasi mkuu wa taifa la Kiyahudi, anamlisha kwa silaha, anamkinga, anamuunga mkono na kumsaidia. Anazungumza yote haya na hapatiwi hesabu na mtu yeyote, wala hahusishwi na lawama au kulaaniwa, kana kwamba roho za Waislamu zilizopotea huko Gaza hazina uzito wala thamani kwa hawa, na hazistahili kuhesabiwa.

Na vipi itakuwa hivyo, wakati dola ya Kiislamu haipo, na Waislamu wako kama povu la mafuriko? Hakuna uweza wala nguvu ila kwa Mwenyezi Mungu.

Haitaji, ewe Trump, kwani humpati mtu wa kukuhisabu wala wa kukuadabisha, kana kwamba damu ya Waislamu ni kitu cha bei nafuu zaidi kwenu. Hii ndiyo sura halisi yako na ya Magharibi, ambayo haijafichika tena kwa mtu yeyote. Mambo yamefichuka na utata umeondoka. Ingawa Magharibi yote, na Amerika na Uingereza haswa, wamemwaga damu ya Waislamu kama mito, lakini walikuwa wakishikilia itikadi tupu na misemo ya kupendeza, kama vile uhuru, haki za binadamu, haki za mtoto, haki za mwanamke, haki za raia, na mengineyo ambayo wanakuza usiku na mchana.

Lakini vita vya hivi karibuni vya Gaza vimeondoa vinyago, na kufichua ukweli wazi kama jua la adhuhuri. Uongo huu wote umeanguka, na Trump anashughulika na kiburi na majivuno haya, na anatoa matamshi kwa uhuru kamili katika kivuli cha kutokuwepo kwa mhasibu, mrekebishaji na mwenye kulipiza kisasi. Trump, ambaye anajionyesha leo kama kiongozi wa amani, ni mchinjaji anayemwaga damu, kwani alikuwa mfuasi mkuu na wa kudumu wa taifa la Kiyahudi katika vita vyake dhidi ya watu wa Gaza. Na Trump, ambaye anashtushwa na hali katika Gaza na anaona kuwa ni mbaya, ndiye yeye mwenyewe alikuwa akitengeneza hali hii chini ya macho yake, na kwa msaada na uangalizi wake!

Kisha anasema kwamba watu katika mitaa ya nchi za Kiislamu wanacheza kwa furaha! Fahamu, ewe adui wa Mungu, adui wa Mtume wake, na adui wa waumini, kwamba watu wanafurahi sio kwa sababu ya uamuzi wako, lakini kwa ajili ya kusitisha mauaji na ukatili dhidi ya ndugu zao dhaifu, mbele ya macho na masikio ya watawala wa Ruvibedha, walinzi wa Magharibi, na walinzi wa Wayahudi.

Enyi umma wa Kiislamu: Huyu hapa Trump anaua na anaendelea kuwaua Waislamu na kusimamisha mauaji kwa maamuzi yake na makubaliano yake bila mhasibu, je, huu ndio maadili ya Waislamu ambao Mola wao alisema kuwahusu: ﴿NA WALE AMBAO WANAPOWAPATA DHULUMA, WANALIPISA﴾? Na tuko wapi kutokana na kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: ﴿NA MKIADHIBU, ADHIBUNI KWA MFANO WA VILE MLIVYOADHIBIWA﴾?

Enyi askari wa umma na watu wa nguvu zake: Hakika ulinzi wa ardhi yenu, na udhihirisho wa dini yenu, hautakuwa ila kwa kusimamisha dola ya Khilafa Rashidah ya pili kwa njia ya Utume. Basi wekeni mikono yenu katika mikono ya Hizb ut-Tahrir, na rudieni kwenye njia ya Mola wenu, na kwenye sunna ya Nabii wenu ﷺ, mpate radhi za Mola wenu, na Mwenyezi Mungu atukuzie Uislamu na watu wake kupitia nyinyi, na adhalilishe ukafiri na watu wake kupitia nyinyi.

Enyi majeshi ya umma: Tunawaweka mbele ya wajibu wa kisheria ambao Mwenyezi Mungu amewalazimu na ambao mtaulizwa kuuhusu mbele ya Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama, na watu wa Misri na Ardhi Iliyobarikiwa watang’ang’ania shingo zenu, bali na umma kwa ujumla, ikiwa mtakaa chini na msiwasaidie na msiwaunge mkono wale wanaofanya kazi ya kusimamisha dola yake na kurejesha mamlaka yake, basi himeni kwani fursa iko mikononi mwenu na kheri inawaita, na unganisheni kamba zenu na wale wanaoaminika wanaofanya kazi ya kutekeleza Uislamu na kurejesha mamlaka yake upya, huenda Mwenyezi Mungu akawasamehe yaliyopita na kuandika kheri kupitia mikono yenu, na isimamishwe dola ambayo umma unaingojea na ambayo Mwenyezi Mungu Ameahidi na kumletea bishara Nabii wake ﷺ; Khilafa Rashidah kwa njia ya Utume.

﴿ENYI MLIOAMINI! MTEKELEZENI MWENYEZI MUNGU NA MTUME ANAPOKUITENI KWENYE YALE YANAYOKUHUISHA

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Bilal Abdullah - Wilaya ya Misri

More from null

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Habari:

Uchunguzi wa Al Jazeera, unaotegemea uchambuzi wa picha za satelaiti, umefichua mifumo ya uharibifu wa kimfumo iliyofanywa na uvamizi huko Gaza kati ya Oktoba 10 na 30 iliyopita.

Shirika la "Sanad" la uhakiki wa habari la mtandao wa Al Jazeera limegundua operesheni za ulipuaji, ubomoaji wa kihandisi na mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na uvamizi ndani ya Ukanda huo tangu kuanza kutekelezwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. (Al Jazeera Net)

Maoni:

Baada ya kutangazwa kwa usitishaji wa vita vilivyojaa mabomu dhidi ya Ukanda wa Gaza chini ya usimamizi wa Trump na kwa makubaliano na baadhi ya nchi za Kiarabu, ilikuwa wazi kuwa ilifikiwa kwa faida ya taasisi ya Kiyahudi. Hili limebainika kulingana na uchambuzi wa picha za satelaiti na ripoti za hivi karibuni za habari, kwamba jeshi la Kiyahudi lililipua maelfu ya majengo huko Gaza, haswa huko Shuja'iyya na Khan Yunis katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao, na vile vile Rafah, na maeneo yaliyo mashariki mwake ambayo yalishuhudia operesheni kubwa za uharibifu.

Uharibifu mkubwa huko Gaza sio wa bahati mbaya, lakini una malengo ya kimkakati ya muda mrefu, kama vile kuharibu mazingira yanayounga mkono upinzani. Kuondoa Gaza ya miundombinu yake, shule zake na makazi yake, inafanya kuwa ngumu kwa upinzani kujipanga upya au kujenga upya uwezo wake. Hii ni kizuizi cha muda mrefu kwa kuharibu uwezekano na kulazimisha ukweli mpya ambao unaifanya Gaza kuwa dhaifu na kuiacha ikiwa imepooza kiuchumi na haifai kwa makazi, ambayo huandaa njia ya kukubali suluhisho zozote za kisiasa au kiusalama, au hata kukubali wazo la uhamishaji, kwa sababu kuacha Gaza kama kifusi, inafanya kuwa ngumu kwa ujenzi kuwa mikononi mwa watu wake pekee. Badala yake, nchi na mashirika yataingilia kati kwa masharti ya kisiasa, na uvamizi unatambua kuwa yeyote anayejenga upya ndiye anayemiliki uamuzi. Hivyo basi uharibifu wa leo ni sawa na udhibiti wa kisiasa kesho!

Kwa kweli, kuelezea makubaliano ya kusitisha vita dhidi ya Gaza kama "yenye mabomu" haikuwa bure, kwa sababu ilikuwa ya sehemu, na malengo ya madai ya kijeshi hayakujumuishwa, ambayo inaruhusu Wayahudi kuendelea na uvamizi na uharibifu kwa kisingizio cha kiusalama. Vivyo hivyo, ilifikiwa na nchi kubwa zaidi inayounga mkono taasisi bila dhamana thabiti za kimataifa, ambayo inafanya kuwa dhaifu na inakabiliwa na ukiukwaji, haswa kwa kukosekana kwa uwajibikaji wa kimataifa, ambayo inafanya taasisi ya Kiyahudi kuwa juu ya uwajibikaji.

Tutaendelea kuwa taifa lenye unyenyekevu na linalokubali, tukitazama watu waliodhoofika, waliochoka, waliopotea na wenye njaa mpaka lini?! Na juu ya yote hayo, wanaruhusiwa wakati wowote?! Hebu sote tuwe Saladin al-Ayyubi, kwa sababu Gaza leo inakumbusha taifa kwamba Saladin hakuwa tu mtu shujaa, lakini alikuwa kiongozi katika dola iliyokuwa na mradi na jeshi na taifa moja nyuma yake. Kwa hivyo, wito wa kuwa Saladin haimaanishi ushujaa wa mtu binafsi, lakini kufanya kazi ya kuanzisha dola ambayo inafanya watoto wote wa taifa kuwa askari katika safu moja chini ya bendera moja.

Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Mna nini hamkupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya wanyonge miongoni mwa wanaume na wanawake na watoto﴾.

Imeandikwa kwa Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Manal Um Ubaidah

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Habari:

Kituo cha Yemen Sana'a kilirusha hewani Jumatano jioni, 2025/11/12, kipindi cha kibinadamu "Nchi Yangu", na katika sehemu ya "Tuko nanyi", kipindi kilionyesha kesi ya mwanamke ambaye alikuwa ameambukizwa ugonjwa adimu na alihitaji kusafiri kwenda India kwa gharama ya dola elfu 80, ambapo kiasi cha dola elfu 70 kilikusanywa kutoka kwa mashirika na wahisani, lakini mtangazaji wa kipindi alizungumzia sana sifa za mchangiaji wa mwisho wa dola elfu kumi, na ikawa wazi kuwa alikuwa Abdul Malik al-Houthi, na alisifu jukumu lake la mara kwa mara katika kusaidia kesi za kibinadamu ambazo zinaonekana kwenye kipindi.

Maoni:

Hakika, mtawala katika Uislamu ana jukumu kubwa, ambalo ni kutunza maslahi ya watu kwa kutumia kile kinachowanufaisha na kutoa kila kitu kinachowafariji. Kimsingi yeye ni mtumishi wao, na hawezi kufurahia maisha hadi atakapohakikisha hali zao. Jukumu hili sio ihsani au upendeleo, bali ni wajibu wa kisheria ambao Uislamu umemlazimisha, na anahesabiwa kuwa amepungukiwa ikiwa atalipuuza. Uislamu umewajibisha umma kumuwajibisha anapopungukiwa. Amani na baraka zimshukie: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, ni upuuzi kufurahia usikivu wa watawala au serikali kwa mahitaji fulani na kuita hiyo kazi ya kibinadamu, wakati kimsingi ni kazi ya kichungaji ya lazima.

Moja ya dhana hatari zaidi ambayo imekita mizizi na ubepari na utawala wake duniani ni kukataa kwa serikali kutunza watu na kuacha utunzaji wa watu kwa mashirika na vyama vya hisani vinavyoendeshwa na watu binafsi au vikundi, na watu huenda kwao mara nyingi kuwasaidia na kutimiza mahitaji yao. Wazo la vyama lilionekana kwanza huko Uropa wakati wa Vita vya Ulimwengu, ambapo familia nyingi zilipoteza wazazi wao na zikawa zinahitaji mlinzi, na serikali, kulingana na mfumo wa kidemokrasia wa kibepari, haitunzi masuala, bali ni mlinzi wa uhuru tu. Matajiri waliogopa mapinduzi ya maskini dhidi yao, kwa hivyo walianzisha vyama hivi.

Uislamu umefanya kuwepo kwa sultani kuwa wajibu wa kutunza masuala ya umma ili kuhifadhi haki zao za kisheria na kukidhi mahitaji yao sita ya msingi ambayo lazima yakidhiwe kwa watu binafsi na vikundi; chakula, mavazi na makazi lazima yatolewe na serikali kwa kila mtu mmoja mmoja, Waislamu na wasio Waislamu, na usalama, matibabu na elimu hutolewa na serikali bure kwa wote. Mtu mmoja alikuja kwa Khalifa wa Waislamu, Omar bin al-Khattab, Mungu amuwiye radhi, akiwa na mke wake na binti zake sita, akasema: (Ewe Omar, hawa ni binti zangu sita na mama yao, walishe, wavishe na uwe ngao kwao kutoka kwa wakati) Omar akasema: (Na vipi ikiwa sitafanya hivyo?!) Bedui akasema: (Nitakwenda) Omar akasema: (Na vipi ikiwa utakwenda?) Akasema: (Utaulizwa kuhusu hali yao Siku ya Kiyama, ukisimama mbele ya Mungu ama kuelekea Motoni au Paradiso), Omar akasema: (Umma huu hautapotea maadamu kuna watu kama hawa).

Enyi Waislamu: Hii sio ndoto, bali ni Uislamu ambao umefanya utunzaji kuwa wajibu kwa Khalifa wa Waislamu kwa kila mtu mmoja mmoja, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehma na amani zimshukie, alisema: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, lazima turudishe hukumu hizi na kuzifanya ziwe za utekelezaji, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: ﴿Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyomo kwa watu mpaka wabadili yaliyomo katika nafsi zao﴾. Hivyo, kitakachobadilisha hali yetu kuwa haki na ustawi ni Uislamu.

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Sadiq al-Sarari