Hadi Lini Enyi Umma wa Kiislamu; Watu Wake na Majeshi Yake?!
Habari:
Ukatili wa utawala wa Jordan dhidi ya kijana Hamza Bani Issa na kumtesa kinyama kulisababisha kung'olewa jicho lake kwa tuhuma za (ugaidi), na sababu ni kuamrisha mema na kukataza maovu na kuonyesha huruma kwa Gaza na watu wake.
Maoni:
"Simba kwangu na katika vita ni mbuni" ni mfano unaotolewa kwa wale wanaoonyesha ujasiri na nguvu mradi tu wako salama kutoka kwa adui zao, kisha wanapohisi hatari ya maadui huogopa na kuwa waoga, na huu ndio msimamo wa watawala wa zama hizi waoga, ambapo wanawashambulia watu wao, huku wakiinamisha vichwa vyao wakati wanapodhalilishwa na adui zao.
Mwanzoni tunampongeza ndugu Hamza kwamba jicho lake limemtangulia kwenda peponi, Mungu akipenda, na hii ndiyo hali ya kila mtu ambaye amepata kutoka kwa watu wa Gaza waliojeruhiwa aina za mateso, njaa, kiu na mauaji ya kimfumo, mpaka hali imefikia kufanya wale wanaokusanyika ili kupata unga na baadhi ya mahitaji yao, kama panya wanavyowawinda kwa risasi na mabomu ... kana kwamba Kiyama kimesimama huko Gaza na hakuna paa linaloonekana la kusimamisha mauaji hayo.
Tunasema: Miongoni mwa sunna za Mwenyezi Mungu katika umma wake ni mitihani: ﴿NA TUTAKUJARIBUNI KWA KITU KIDOGO KATIKA UOGA NA NJAA NA UPUNGUFU WA MALI NA NAFSI NA MATUNDA. NA WABASHIRIE WENYE KUSUBIRI. AMBAO WANAPOSIBIWA NA MSIBA, HUSEMA: HAKIKA SISI NI WA MWENYEZI MUNGU, NA KWAKE YEYE TUTAREJEA. HAO WATAPATA BARAKA KUTOKA KWA MOLA WAO NA REHEMA, NA HAO NDIO WALIOONGOKA﴾, na anasema Mwenyezi: ﴿NA TUTAKUJARIBUNI MPAKA TUWAJUE WENYE KUFANYA JIHADI MIONGONI MWENU NA WENYE KUSUBIRI, NA TUZIJARIBU HABARI ZENU﴾.
Na Mwenyezi Mungu anapotaka kumsaidia mnyonge, huwashughulisha wenye nguvu kwa wao kwa wao, ili amtoe mnyonge kutoka miongoni mwao, naye aokoke au awashinde, anasema Mwenyezi Mungu: ﴿NA LAU SI MWENYEZI MUNGU KUONDOA WATU BAADHI YAO KWA BAADHI, BILA SHAKA DUNIA INGELIFISIDIKA, LAKINI MWENYEZI MUNGU NI MWENYE FADHILA JUU YA WALIMWENGU﴾. Amesema Ibn Abbas: Na lau si Mwenyezi Mungu kuondoa adui kwa majeshi ya Waislamu, washirikina wangewashinda na kuwaua waumini na kuharibu nchi na misikiti.
Na kwa sababu tunafuata sunna za Bwana wetu Muhammad ﷺ, tutachukua mfano kutoka vita vya Ahzab, ambapo Mwenyezi Mungu aliwatosheleza waumini na vita pale alipoona ukweli wa mwelekeo wao na kutokubali kwao matakwa ya kidunia ya makafiri, basi subira na kusubiriana na kulinda mipaka na kumcha Mwenyezi Mungu ndio anwani ya mafanikio na ufanisi na ushindi, ndio, Mwenyezi Mungu anasikia na anaona na hakika Yeye yuko macho kwa hawa madhalimu, basi simameni enyi Waislamu msimamo wa mkweli kwa Mwenyezi Mungu na mtiifu Kwake, msimamo wa utukufu na kumtegemea Mwenyezi Mungu, kwani yeyote anayemtegemea Mwenyezi Mungu, basi hatadhilika wala hachoki wala hapotei wala hababaiki.
Na yeyote anayetembea kuelekea kwenye utukufu na kufanya kazi ili kuupata, Mwenyezi Mungu atakuwa naye na kumvika vazi la utukufu katika dunia na atakuwa na thawabu kubwa Akhera, ama yule anayeridhia unyonge na kunyenyekea kwa adui kafiri na vibaraka wake, inampasa Mwenyezi Mungu kumvika vazi la unyonge katika dunia na Akhera, na hii ndiyo hali ya watawala wetu na juu yao ni wale waliofungua nchi zao na kumpokea Rais wa Marekani na kummwagia pesa ambazo si haki yao bali ni haki ya umma wa Kiislamu uliodhoofika na kuonewa, basi Mwenyezi Mungu asiwabariki hawa watu wajinga na yeyote anayetembea katika njia yao na kufuata nyayo zao.
Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir
Radhia Abdullah