2025-08-06
Jarida la Al-Raya: Malengo ya Ziara ya Masoud Boulos
Nchini Libya
Ziara hiyo ilifanyika kati ya Julai 23 na 27, 2025 na ilikuwa ya kwanza kwa afisa mkuu wa Marekani katika enzi ya Trump. Boulos alikutana katika ziara yake na Abdul Hamid al-Dabaiba, waziri mkuu wa serikali ya magharibi ya Libya inayotambuliwa kimataifa. Alikutana pia na Muhammad al-Manfi, mkuu wa Baraza la Urais, ambapo Masoud alisisitiza "msaada wa Amerika kwa mchakato wa Umoja wa Mataifa nchini Libya."
Na alitoa wito katika hotuba yake kwa kufanyika uchaguzi kulingana na makubaliano ya kikatiba yanayotambuliwa. Alikutana pia katika kituo cha Al-Rajma huko Al-Marj na Khalifa Haftar, akihudhuriwa na mwanawe Saddam, na hakukutana na Baraza la Wawakilishi wala Baraza la Dola.
Kisha mikataba ilisainiwa wakati wa ziara na Shirika la Mafuta kwa ajili ya kuendeleza mashamba ya mafuta na utafutaji wa gesi baharini katika maji ya eneo la Libya. Mkutano na Shirika la Mafuta ulifanyika bila kuhudhuriwa na Abdul Hamid al-Dabaiba. Pia ilichapishwa kwamba alikutana na gavana wa Benki Kuu.
Msomaji anayeizingatia kwa makini mienendo ya ziara hiyo, katika hali nyingi, anaona kwamba ina tabia ya kiuchumi hasa, na masuala ya kisiasa hayakujadiliwa isipokuwa kwa madhumuni ya kufanikisha na kuimarisha miradi ya kiuchumi, Marekani inajali hasa kutawala rasilimali za nchi na kuwaondoa wengine kwenye uwanja wa kiuchumi, hasa Wazungu. Ambapo mikutano iliyoangaziwa ililenga na Shirika la Mafuta wakati wa ziara, na kusaini mikataba ya kuendeleza mashamba ya mafuta na kuchimba mashamba mapya na utafutaji wa gesi na uwekezaji katika sekta ya gesi.
Ikumbukwe hapa kwamba ziara hiyo ni sehemu ya ziara inayojumuisha Tunisia, Algeria na Morocco, ambayo inaashiria msisitizo wa Marekani katika kuwezesha ushawishi wake Afrika Kaskazini, hasa Libya, na vita vinavyoendelea vya udhibiti nchini Tunisia, Algeria na Morocco kati ya Marekani kwa upande mmoja na Ufaransa na Uingereza kwa upande mwingine haufichiki.
Na tukirejea kwenye mienendo ya ziara, mikataba miwili ilisainiwa kati ya Shirika la Mafuta na kampuni mbili za Marekani, mojawapo ikiwa ni kampuni maarufu ya Hill. Mkataba pia ulisainiwa kwa ajili ya uwekezaji katika sekta muhimu kama vile mafuta na miradi mikuu kama sehemu ya mfumo wa muda mrefu wa mahusiano ya Marekani na Libya, kwa madai ya kuimarisha ushirikiano.
Pia alikutana huko Tripoli na Hana Tetteh, mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, ili kuelewana juu ya jukumu ambalo ujumbe wa Umoja wa Mataifa unatekeleza nchini Libya, bila shaka ni chombo kinachofuatilia utekelezaji wa sera ya Marekani kuhusu mgogoro wa Libya na kuzuia suluhu na kuzuia mlipuko ikiwa itatokea. Ni lazima izingatiwe wakati wa kuangalia hali ya Libya katika miaka ya hivi karibuni kwamba Marekani imekuwa makini kuzuia suluhu kwa hali hii mbaya, mara nyingi huweka vizuizi mbele ya suluhu ama kupitia wakala wake Haftar au kupitia utawala wa Misri, au ujumbe wa Umoja wa Mataifa, kila mazungumzo ya Libya na Libya yanapokaribia kufikia suluhu, Marekani inamsukuma wakala wake Haftar kuharibu, au ujumbe wa Umoja wa Mataifa unaanzisha kipengele kipya cha kuharibu na kuendeleza mzunguko wa mazungumzo ambayo hayatowi suluhu yoyote, na vitendo na udanganyifu wa Ghassan Salama au shughuli za mazungumzo ambazo zilikuwa zikifanyika wakati wa Stephanie Williams na waliokuja baada yake zinashuhudia hilo. Marekani ndiyo inayowazuia Walibya kupata suluhu, haitaki kulipua hali hiyo na vita vikali kutokea, na wakati huo huo inawazuia Walibya kufikia suluhu ambayo inaunganisha nchi na kuwaepusha na madhara ya vita ambayo yanaweza kuifikisha nchi katika hali ya utulivu na ujenzi, lakini inafanya kazi ya kuacha nchi kama ilivyo sasa (wala si tegemezi wala si talaka) kama wanasema!
Kwa hivyo, Marekani katika hali hii inajaribu kuimarisha ushawishi wake na kujenga uhusiano wa kiuchumi na kisiasa ambao unasaidia makampuni yake kudhibiti uwezo wa nchi, na kutafuta mawakala wake katika nguvu za kisiasa na kijeshi ambao wanaendesha nchi kama inavyotaka. Inakubali waziwazi Brigade ya 444, uongozi na wafanyakazi, na hata silaha na mafunzo, na Brigade ya 111 pia, ingawa kimsingi si yake, lakini imeonekana hivi karibuni ziara za mara kwa mara za uongozi na wafanyakazi wa brigades hizo kwenda Marekani na kujadili nao hali ilivyo, kisha baada ya ziara hizi, nguvu ya kusaidia utulivu ilifutwa na kiongozi wake Abdul Ghani al-Kikli, ambaye inaonekana alikua zaidi ya inavyoruhusiwa, aliuawa, na kama si uhamasishaji wa wanamgambo wengine huko Tripoli, Al-Zawiya na kwingineko, ambao walihisi hatari, wote walihama wakisahau tofauti zao, kama si hivyo, mapigano yasingesimama na mfululizo wa mauaji ungaliendelea, Marekani baada ya kugundua kuwa njia ya hatua za kijeshi inaweza kusababisha hali ambayo haifai, ilirejea kwenye mtindo wa hatua za kiuchumi na kujaribu kuunganisha nchi kiuchumi kupitia kuingia kwa makampuni yake katika sekta ya mafuta na gesi na kuidhibiti, na kutowaruhusu wapinzani wake na washirika wa Ulaya kupata chochote, ama Warusi, iliwaingiza kupitia wakala wake Haftar ili iwe rahisi kuwatoa inapohitaji.
Ikumbukwe hapa kwamba takriban miezi miwili iliyopita, habari zilitoka kupitia vyombo vya habari kwamba Marekani inataka kuwatuma baadhi ya wahalifu waliopo katika magereza ya Marekani kwenda Libya kwa makubaliano na baadhi ya wanamgambo na nguvu za ndani, lakini habari hiyo ilikanushwa baada ya kuonekana upinzani mkali. Pia ilitangazwa kwamba Marekani inataka kufungua vivuko huko Gaza ili kuwatoa watu wake na kuwashawishi kukaa Libya kwa ajili ya Wayahudi, lakini jambo hilo lilikabiliwa na upinzani mpya wa umma na halikufanyika, "ndiyo sababu baadhi ya duru za kisiasa nchini Libya" zilisubiri ziara ya Masoud Boulos anayoifanya Tripoli na Benghazi kwa tahadhari kubwa, je, Boulos atazungumzia mambo haya katika ziara yake?!! Hakuna hata moja ya mambo haya iliyozungumziwa.
Hitimisho la kile kilichofanyika katika ziara ya Masoud Boulos ni kulenga kujenga ushirikiano wa kiuchumi kama Marekani na vibaraka wake wanavyodai nchini, na miradi yenye thamani ya dola bilioni 70 ilipendekezwa katika nyanja za nishati, miundombinu, afya na teknolojia.
Na ilikuja katika Al-Jazeera Net kwamba "lengo lilikuwa wazi katika faili ya kiuchumi kurejesha jukumu la Marekani huku ikipuuza Baraza la Wawakilishi na Dola katika mikutano..." Hii inaonyesha kwamba ziara hiyo ilikuwa ya kiuchumi kwa ubora. Na miradi ya kisiasa haikujadiliwa, au haikuwa na kipaumbele. Ziara ya Abdul Hamid al-Dabaiba nchini Uturuki na mkutano wa pande tatu (Uturuki, Italia, Libya), na Italia na Uturuki si wapinzani wa Marekani, ingawa kuna mbio za maslahi, inaruhusiwa kati yao.
Lakini nawazungumzia baadhi ya Walibya ambao wanafikiri kwamba katika kuitikia Marekani kuna maslahi kwa Libya, kama anavyofikiria mtu kwamba kuna maji katika mirage ya kumaliza kiu chake! Mwenyezi Mungu amesema: ﴿NA WALE WALIO KUFURU, AMALI ZAO NI KAMA SARABI KATIKA UWANDA, MWENYE KUIHITAJI ANAIDHANIA KUWA NI MAJI, HATA AKIYAENDEA HAKUTAMBUA CHOCHOTE, NA AKAMKUTA ALLAH KWAKE, AKAMTIMIZIA HESABU YAKE, NA ALLAH NI MWEPESI WA HESABU﴾. Kwa hiyo hamna kimbilio kwenu kutoka kwa adui ila kwa Mwenyezi Mungu.
Imeandikwa na: Profesa Ahmed Al-Muhadhab
Chanzo: Jarida la Al-Raya