2025-09-10
Jarida la Al-Raya: Kupenya kwa Wayahudi ndani ya Taasisi ya Kijeshi ya Misri
Tangu utawala wa Misri uliposaini mkataba wa Camp David mwaka 1979, taasisi ya kijeshi ya Misri iliingia katika mkondo wa utegemezi na kupenya, jambo ambalo liliifanya iwe mbali na itikadi yake ya asili iliyoanzishwa kwa misingi ya kulinda taifa na kutetea mipaka yake dhidi ya maadui zake wa kweli, na miongoni mwao ni Wayahudi waliokwapua Palestina. Taasisi hii imebadilika polepole kuwa chombo kilichofungwa, kinachotii masharti ya adui, na hata kushiriki katika kumlinda na kumwezesha, kupitia makubaliano ya kijeshi, kiusalama, kiuchumi na ushauri, ambayo yameunda mfumo kamili wa ushawishi wa Wayahudi ndani ya jeshi na serikali.
Kituo kikuu kilikuwa katika mkataba wa Camp David ambao ulieleza kugawanywa kwa Sinai katika kanda za kijeshi, ambazo idadi ya askari na aina ya silaha zingebainishwa, chini ya usimamizi wa kimataifa. Hivyo, Sinai iliondolewa uwepo wowote wa kijeshi wa kweli wenye uwezo wa kukabiliana na adui msaliti anayevizia, na vikosi vya kimataifa vikawa jicho lililo wazi kwa manufaa ya taifa haramu na Marekani. Mkataba huu ulibadilisha mipaka ya mashariki ya Misri kuwa mstari salama wa mbele kwa taifa la Kiyahudi, baada ya kuwa chanzo cha tishio la kudumu kwake, na huu ndio msingi wa kupenya.
Jambo hilo halikuishia kwenye mipaka ya mkataba, bali Marekani, mshirika mkuu wa taifa la Kiyahudi, iliimarisha kupenya huku kupitia misaada ya kijeshi yenye masharti. Kila mwaka, jeshi la Misri hupokea takriban dola bilioni 1.3 za vifaa, lakini kwa sharti kwamba halitamiliki silaha yoyote itakayovunja uwiano na Wayahudi, na kwamba litaendelea kuhitaji vipuri, mafunzo na usaidizi wa usafirishaji kutoka Marekani. Mpango huu umeifanya jeshi kuwa mateka wa Marekani, na hivyo kuifichua kwa Wayahudi. Itikadi yake ya kijeshi imerekebishwa kupitia mazoezi ya pamoja kama vile "Bright Star" ili ugaidi, kwa maana yake ya kimagharibi, yaani Uislamu katika uhalisia wake, uwe adui, sio Wayahudi au taifa lao haramu, na huu ndio mabadiliko makubwa ya kimkakati katika dhamiri ya jeshi ambalo hapo awali lilielezewa kama "jeshi la taifa na ngao yake".
Baada ya muda, njia za mawasiliano ya moja kwa moja zilifunguliwa kati ya ujasusi wa Misri na Mossad, kwa kisingizio cha "uratibu wa kiusalama" huko Sinai na Gaza. Vyombo vya habari vya Magharibi, ikiwa ni pamoja na New York Times, vimekiri kwamba ndege za taifa haramu zilitekeleza mamia ya mashambulizi ndani ya Sinai kwa idhini kamili na uratibu wa Misri, kati ya 2015 na 2018. Hiyo ni kusema kwamba jeshi la Misri halitetei tena ardhi yake tu, bali limeanza kuruhusu Wayahudi kutumia anga ya Misri dhidi ya wale wanaowaita "magaidi", ambao kwa kweli ni Waislamu wanaokataa utawala wa Magharibi na uwepo wa taifa haramu.
Jeshi la Misri, kupitia jukumu lake la kiuchumi, limeingia katika ushirikiano wa wazi au usio wa moja kwa moja na kampuni zinazohusiana na taifa la Kiyahudi, hasa katika sekta ya nishati na gesi. Mnamo mwaka 2018, Misri ilitia saini makubaliano na kampuni za taifa la Kiyahudi kusafirisha gesi hadi vituo vya kusindika maji vya Misri na kuisafirisha tena, jambo ambalo vyombo vya habari vya Kiyahudi vilielezea kama "makubaliano ya karne" ambayo yaliipa taifa la Kiyahudi njia ya kimkakati ya kuuza gesi yake. Jeshi halikuwa mbali na hilo, kwani kampuni zake ziliingiliana na shughuli za usindikaji na usafirishaji, ambayo ina maana kwamba taasisi ya kijeshi ambayo inatakiwa kulinda mali ya taifa, imekuwa mshirika katika kuwawezesha Wayahudi wanyang'anyi kupata mali hiyo.
Jambo hatari zaidi katika hatua hii ni kufunguliwa kwa faili la ubinafsishaji wa kampuni za jeshi lenyewe, kama vile Wataniya Petroleum, Safi, Sayilo Foods, na Shell Out. Misri imeajiri ofisi za ushauri za kimataifa kusimamia mchakato wa upangaji upya na utoaji, kama vile PwC na nyinginezo, na kampuni hizi zina ofisi zinazofanya kazi ndani ya taifa la Kiyahudi, zikiipa huduma za kifedha na ushauri, baadhi yake kwa serikali ya taifa hilo lenyewe. Hivyo, adui amefahamishwa kuhusu maelezo ya kifedha na kimuundo ya kampuni za jeshi, katika tukio hatari ambalo halijawahi kutokea hata kileleni mwa uvamizi halisi. Hiyo ni kusema kwamba kupenya hakuko tena katika itikadi na silaha pekee, bali kumefika katika muundo wa ndani wa kiuchumi wa taasisi ya kijeshi.
Tangu enzi ya Sadat, na kufikia Sisi, hotuba ya jeshi na vyombo vya habari rasmi zimebadilishwa na kuwa taifa dogo la Kiyahudi si adui bali ni mshirika katika kudumisha usalama. Sisi mwenyewe alisema mwaka 2016 kwamba "amani na Israel ni imara na endelevu, na kila mtu anapaswa kuimarisha uaminifu nayo." Hivyo, mipaka na Wayahudi imekuwa mstari salama zaidi wa mbele kwao, huku jeshi likielekezwa kupigana na wana wa taifa katika Sinai, Libya na Sudan, chini ya kichwa cha kupambana na ugaidi. Mapinduzi haya katika itikadi hayawezi kuelezewa isipokuwa kwa kuwepo kwa kupenya kamili kwa akili ya kijeshi ya Misri.
Kupenya kwa Wayahudi ndani ya taasisi ya kijeshi ya Misri haikuwa bahati mbaya, wala sio mahusiano ya muda tu, bali ni matunda ya sera iliyopangwa ambayo ilianza na mikataba ya kujisalimisha, na kukamilishwa na utegemezi wa kijeshi kwa Marekani, uratibu wa kiusalama na ujasusi, kupenya kwa kiuchumi, na kuishia na ubinafsishaji wa kampuni za jeshi kupitia washauri ambao wana mizizi katika taifa la Kiyahudi. Na haya yote hayabadilishi tu asili ya jeshi, bali yanabadilisha nafasi ya Misri katika mlinganyo wa taifa.
Enyi watu wa Kinana: Hakika kile ambacho kimefanyika na kinachofanyika cha kukabidhi ardhi kwa adui kupitia mikataba, na kutoa maamuzi ya kijeshi na kiuchumi kwa Marekani, na kufungua milango ya uratibu wa kiusalama na Wayahudi, na kuwawezesha kufahamu utajiri wa Waislamu na siri za taasisi zao kupitia kampuni zao za ushauri, yote hayo ni mambo ambayo sheria imeyaharamisha kufanya na kuyaendesha, bali imeyafanya kuwa usaliti kwa Mwenyezi Mungu, Mtume wake na waumini. Mwenyezi Mungu ametuamrisha tuweke tayari nguvu za kukabiliana na maadui zetu, na tusifanye urafiki nao au kuwapa siri, na tulinde mali ya taifa na amana yake, tusiipe adui mkaazi, wala tusimwezeshe kuwatawala Waislamu. Na kile kinachoendelea leo ni kile ambacho Mwenyezi Mungu amekataza na kuonya dhidi yake. Sera hizi zote zimeharamishwa na Uislamu, bali ni miongoni mwa aina kubwa zaidi za uzembe na usaliti; kwa sababu zinamana na kuachana na wajibu wa jihadi, kumwezesha adui, na kumsaidia kusalia katika ardhi ya Waislamu, wakati kanuni ni kwamba anapaswa kupigwa vita mpaka ardhi itakaswe kutokana na uchafu wake.
Kutoka hapa, ilikuwa ni wajibu wenu, enyi watu wa Misri, wananchi na jeshi, kutambua hatari ya kile kinachokusudiwa kwa jeshi lenu na nchi yenu, na kusimama pamoja katika kukabiliana na kupenya huku. Kinachotakiwa kwenu sio kukaa kimya au kujisalimisha, bali kupaza sauti zenu juu na kufanya kazi ya kuangusha mikataba hii batili ambayo imemfanya adui awe salama na imewaweka chini ya vikwazo, na kurejesha jeshi kwenye itikadi yake ya asili ya Kiislamu, kwamba kupigana na Wayahudi ni faradhi sio hiari, mpaka ukombozi kamili wa Palestina, na ukombozi wa uamuzi wa kisiasa, kijeshi na kiuchumi kutoka kwa utegemezi kwa Marekani na Magharibi, na kufunga milango yote ya ushawishi wa kigeni na kampuni zinazohusiana na adui, na kurejesha rasilimali za taifa kwenye mamlaka yake sahihi.
Enyi watu wa Kinana: Hakika Uislamu unakutaka isimame mbele ya jeshi lako ili kulirejesha kwenye nafasi yake ya kweli: jeshi la taifa ambalo linapigana katika njia ya Mwenyezi Mungu, sio jeshi linaloendeshwa na maamuzi ya adui au maslahi yake. Na jueni kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ amewabashiria mwisho wa mzozo na Wayahudi, akisema: «MTAWAPIGA VITA WAYAHUDI NA MTAWAUA, HATA JIWE LISEME: EWE MUISLAMU, HUYU NI MUYAHUDI NYUMA YANGU, NJOO UMUE» (Imesimuliwa na Muslim).
Hii ndiyo bishara yenu, na hii ndiyo njia yenu, na hii ndiyo faradhi yenu, basi msigeukie meza za unyonge wala ahadi za makafiri. Hakika njia ya heshima ni moja: kuinuka kwa misingi ya Uislamu, ili muanzishe mamlaka yenu huru, na mlirejeshe jeshi lenu liwe upanga mbele ya adui na sio ukuta wa kumlinda.
Imeandikwa na: Ustadhi Said Fadl
Mjumbe wa Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Misri
Chanzo: Jarida la Al-Raya