2025-07-23
Jarida la Ar-Raya: Itikadi ya Kiislamu ndio msingi wa wokovu na dira ya maisha
Itikadi kwa lugha ni kile kinacho fungamana moyoni, na katika sheria ni kuamini Mwenyezi Mungu na Malaika wake na Vitabu vyake na Mitume wake na siku ya mwisho na Qadar kheri yake na shari yake, kama ilivyokuja katika Sahih mbili kutoka kwa Omar bin Al-Khattab kwamba mtu alikuja kwa Nabii ﷺ akimuuliza na kumsadikisha mpaka akasema: NIJULISHE KUHUSU IMANI? Akasema: «UAMINI KWA MWENYEZI MUNGU NA MALAIKA WAKE NA VITABU VYAKE NA MITUME WAKE NA SIKU YA MWISHO NA UAMINI QADAR KHERI YAKE NA SHARI YAKE».
Nayo ni kusadiki kwa yakini kunakoendana na uhalisia kutokana na dalili, na itikadi ya Kiislamu ni itikadi ya kiakili, kwani inampasa mwanadamu kuifanya akili yake kuwa dalili ya kuamini ulazima wa kuwepo Muumbaji mtukufu, na kwamba ameumba ulimwengu kutoka hakuna, na kwamba hafanani na chochote katika viumbe vyake, na kwamba Qur'an ni maneno ya Mwenyezi Mungu, na kwamba Muhammad ﷺ ni mjumbe kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kisha achukue kile kilicholetwa na dalili ya nakili kutoka katika nguzo za imani na jukumu la akili linasimama katika kusadiki kwa yakini kile kilicholetwa na dalili zenye kukata zenye akili haziwezi kuwa dalili juu yake.
Na itikadi ya Kiislamu ni itikadi ya kisiasa, yaani, sio itikadi ya kikuhani, muumini anatosheka kuamini kwamba ulimwengu una Muumbaji tu, na anaitenganisha na masuala yote ya maisha yake au baadhi yake, bali ni itikadi ya kisiasa kwa maana kwamba inatokana na mfumo unaoendesha maisha ya mwanadamu na maslahi yake, na unaongoza masuala yake na kuyatunza, kutoka kwake hutokana na hukumu za sheria ya Kiislamu ambayo inaandaa mahusiano yote ya mwanadamu, iwe uhusiano wake na Muumbaji wake au uhusiano wake na nafsi yake au na viumbe wengine, na kutoka katika mahusiano haya kuna uhusiano wa utawala kati ya mtawala na anaye tawaliwa, nayo ni kwamba Mwenye kumiliki ulimwengu, ambaye ni Mwenyezi Mungu pekee, ana haki ya kumiliki na kutumia na kupanga katika alicho umba.
Tunaona kwamba miongoni mwa mambo ya lazima ya itikadi, ni kwamba inaandaa suala la utawala, hivyo Muislamu anaamini kwamba utawala ni wa Mwenyezi Mungu, na kutoka hapa umekuja msamiati wa itikadi ya utawala.
Na itikadi ni msingi wa mabadiliko ya kimsingi ya akili na nafsi ya mwanadamu, ambapo humfanya kuwa mtu mwenye tabia ya Kiislamu. Na itikadi ya utawala ndio haki ya kwanza ya neno la tauhidi, yaani haki ya kwanza ya shahada laa ilaaha illallah Muhammad Rasulullah. Bila ya itikadi ya utawala, neno la tauhidi linakuwa halina maana halisi, bali athari yake inakuwa ya kawaida au ya kupita. Itikadi ya utawala ndio matakwa ya kivitendo ya maisha ya Kiislamu, au kwa maana nyingine ndio msingi wa mapambano kati ya Uislamu na ukafiri.
Itikadi ya utawala kinadharia kwa wafasiri wa itikadi inapatikana katika mambo mawili: Jambo la kwanza ni utawala wa kimaumbile, yaani kwamba Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kutawala ulimwengu kwa kuumba na kwa kadari na kwa kukadiria, na hili halikanushwi isipokuwa na makafiri. Lakini mada yetu ni jambo la pili, nalo ni utawala wa kisheria ambao kwa upande wa umuhimu wake uko katika jambo la tatu.
Ni kweli kwamba makafiri hawataki Uislamu kwa ujumla, lakini kuna mambo matatu ikiwa watafanikiwa katika moja yao watakuwa wamewadhibiti Waislamu.
- Jambo la kwanza ni kuondoa utakatifu kutoka katika maandiko ya Qur'ani, na mashariki walitunga kitabu kwa ajili ya hili kinachoitwa "Historia ya Qur'ani" na ilichukua uandishi wake karibu miaka 80, na mwandishi wake alikuwa shetani wa mashariki Lundke. Wao wanaona kwamba Qur'ani ni maneno ya mwanadamu yanayoweza kukosolewa na kuchambuliwa na kujadiliwa na kutafitiwa na kufikiriwa, hivyo kwao wao haikubaliki na haitakatifu. Lakini hawakufanikiwa kwa hili kwa sababu Waislamu wanatukuza dini yao haijalishi hali inakuwaje.
- Jambo la pili ni kupiga ukweli wa Sunna na kuchafua vitabu vya Bukhari na Muslim na vinginevyo, na vile vile hawakufanikiwa kwa hili kwa umma wa Waislamu, na ikiwa waliweza kupata watu wanaojiita wenye nuru, lakini kwa hakika hawakuweza kuingiza sumu yao katika umma wa Kiislamu, kwa hivyo hawakufanikiwa hata kwa kupiga ukweli wa Sunna.
- Ama jambo la tatu ni vita dhidi ya itikadi ya utawala, na kwa hili wamefanikiwa na wameweza kuwadhibiti Waislamu. Na tutaeleza kwa undani jinsi walivyofanikiwa katika baadhi ya mambo ili kukaribisha akili.
Qur'ani inaamrisha kushikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, lakini wamefanikiwa kuigawa umma. Na Qur'ani inaamrisha kutowafanya makafiri kuwa marafiki, na Waislamu leo wanakwenda kwenye Baraza la Usalama na Mahakama ya Kimataifa ambayo ni taasisi za kikoloni ambazo hazihudumii isipokuwa maslahi ya makafiri, na uhalisia ni shahidi na ushahidi mkubwa.
Na Qur'ani inaamrisha kufanya Jihadi ili kuinua neno la Mwenyezi Mungu, na leo Waislamu wanapigana kwa ajili ya taifa kati yao, na wanasahau itikadi ya ﴿Hakika Waumini ni ndugu﴾, na Qur'ani haikubali mfumo mwingine isipokuwa mfumo wa Uislamu, na makafiri wameweza kufanya mifumo ya utawala katika nchi za Waislamu kuwa jamhuri na kifalme... na mifumo mingineyo inayokhalifu itikadi ya Uislamu, ambayo inaimarisha utengano wa umma.
Na Qur'ani inatuamrisha kuwanusuru ndugu zetu Waislamu wanao dhulumiwa katika nchi yoyote, na leo Gaza inakufa na majeshi yanalinda mipaka iliyo chorwa na ukoloni katika makubaliano kama vile Sykes-Picot. Na kuna zaidi ya aya sitini kutoka katika Kitabu kitukufu zinazozungumzia kuhusu utawala wa Mwenyezi Mungu.
Kwa hivyo, bila itikadi ya utawala, shahada mbili hazina maana kamili, bali haiwezekani kufikia imani na kuikamilisha isipokuwa kwa hiyo, ﴿La hasha! Naapa kwa Mola wako Mlezi! Hawataamini mpaka wakufanye wewe hakimu katika yale wanayo khitalifiana, kisha wasione dhiki nyoyoni mwao kwa hukumu yako, na wajisalimishe kabisa﴾, bila ya itikadi ya utawala Uislamu unakuwa ni ibada tu zinazofanywa katika misikiti, bali ibada zitaachwa bila ya kuziunganisha nayo.
Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ anasema: «Zitafunguliwa fundo za Uislamu fundo moja baada ya nyingine, kila fundo itakapofunguliwa watu watashikamana na inayofuata, na ya kwanza kufunguliwa ni hukumu na ya mwisho ni sala». Kwa hivyo Uislamu umefanya ulazima wa hukumu kuwa katika nafasi ya taji la ulazima ambalo likisusiwa hukumu zilizobaki zinatoweka mpaka ya mwisho iwe sala.
Kwa hivyo tunapoangalia uhalisia wa watu tunawaona wanaishi kwa viwango tofauti katika maisha, kila mtu ana kiwango chake. Unamuona mtu kiwango chake ni maslahi ya kibinafsi, hajali jamii yake wala nchi yake wala hata dini yake, na hana chochote cha dini anacho shikamana nacho isipokuwa kile kinachomhusu kama vile sala na saumu, na unamuona akitamka dai (muache kiumbe kwa Muumbaji), mtu huyu na wengineo ambao wako mfano wake unaona kuwepo kwao na kutokuwepo kwao ni sawa, wanaishi kwa maslahi yao binafsi tu. Na Mwenyezi Mungu anasema juu ya yule ambaye hali yake iko hivi: ﴿Je! Umemuona yule aliye fanya matamanio yake kuwa ndiyo mungu wake?﴾ Mwenye maslahi ya kibinafsi kwa hakika anafuata matamanio; Kwa sababu anapingana na dini ya Mwenyezi Mungu kwa kuchukua dini ya Mwenyezi Mungu kwa uchaguzi, anachukua kile kinachokubaliana na maslahi yake na kile kinachopingana na maslahi yake kana kwamba hakukisikia!
Ama kiwango cha pili ni kana kwamba ni mfuasi wa bwana wake au sheikh wake au mfuasi wa rais wake kwa jumla; Yeyote ambaye hali yake iko hivi, amemfanya rais wake ambaye ni mwanadamu kama yeye kuwa mola badala ya Mwenyezi Mungu. Kutoka kwa Adiy bin Hatim amesema: Nilimjia Nabii ﷺ na shingoni mwangu nina msalaba wa dhahabu, akasema: Nilimsikia akisema: ﴿Wamewafanya makuhani wao na watawa wao kuwa miungu badala ya Mwenyezi Mungu﴾. Akasema: Nikasema: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, hakika wao hawakuwa wakiwaabudu. Akasema: «Ndio, lakini wanawahalalishia kile ambacho Mwenyezi Mungu amekiharamisha, basi wao wanahalalisha, na wanawaharamishia kile ambacho Mwenyezi Mungu amekihalalisha, basi wao wanaharamisha, basi hiyo ndiyo ibada yao kwao».
Ama mwenye kiwango cha tatu yeye ni mtu mwenye itikadi ambaye anaenda katika maisha kwa hukumu ya Mwenyezi Mungu, anazunguka na dalili popote ilipo zunguka, na hageuki kwa maslahi yake ikiwa anadhani kwamba inapingana na dalili, mtu huyu hakimu wake katika maisha ni Mwenyezi Mungu, anatembea ndani yake na hana hakimu ghairi ya Mwenyezi Mungu.
Imeandikwa na: Ustadh Mayas Al-Mukaradi - Wilaya ya Yemen
Chanzo: Jarida la Ar-Raya