2025-08-06
Jarida la Ar-Raya: Mkutano wa 25 wa Umoja wa Ulaya na China
Je, ulimaliza tofauti zao?
Mkutano wa Umoja wa Ulaya na China ulifanyika Beijing tarehe 2025/7/24 kuadhimisha kumbukumbu ya miaka hamsini ya uhusiano wao. Rais wa China Xi aliufungua kwa msimamo mkali dhidi ya Wazungu, akisema "China sio chanzo cha changamoto za sasa zinazoikabili Ulaya. Hakuna mgongano wa maslahi kati ya China na Umoja wa Ulaya, na hakuna tofauti za kimsingi za kijiografia". Jambo linaloonyesha kina cha tofauti kati ya pande hizo mbili. Na kwa hivyo aliwataka kuelewana, akisema: "Kadiri hali ya kimataifa inavyozidi kuwa hatari na ngumu, ndivyo inavyowalazimu viongozi wa China na Ulaya kuongeza mawasiliano, kuimarisha uaminifu wa pande zote, na kuimarisha ushirikiano ... na kuonyesha busara na kujitolea na kufanya chaguo sahihi la kimkakati ambalo linakidhi matarajio ya watu na kustahimili uchaguzi wa historia."
Viongozi wa Ulaya waliohudhuria walionyesha tofauti zao na China, ambapo Rais wa Tume ya Ulaya, Von der Leyen, alisema, "Ni muhimu kwamba China na Ulaya zitambue wasiwasi wa kila upande na kutoa suluhu madhubuti ... kadiri ushirikiano wetu unavyozidi kuongezeka, ndivyo ukiukwaji unavyoongezeka ... ni muhimu kurejesha usawa katika uhusiano wetu wa nchi mbili". Rais wa Baraza la Ulaya, Kosta, alisema: "Umoja wa Ulaya ungependa kuona maendeleo madhubuti katika masuala yanayohusiana na biashara na uchumi".
Kwa hivyo, kuna tofauti kubwa kati ya pande hizo mbili, na mkutano huu haukuweza kuzitatua. Na kinachothibitisha hilo ni tangazo la ghafla la China kwamba utaishia kwa siku moja baada ya kupangwa kuwa wa siku mbili. Vile vile, Xi alikataa hapo awali mwaliko wa Ulaya wa kumtembelea na kufanya mkutano huko Brussels, hivyo alinyenyekea na kukubali kuufanya huko Beijing, jambo linaloonyesha uhitaji wake mkubwa wa kuboresha uhusiano na China, huku Mei iliyopita alitembelea Urusi kushiriki katika sherehe ya ushindi wake katika Vita vya Pili vya Dunia, ili kutuma ujumbe kwamba China inaiunga mkono Urusi katika vita vyake na Magharibi huko Ukraine. Ikumbukwe kwamba Waziri wake wa Mambo ya Nje, Wang Yi, alilitaja hilo waziwazi kwa mwenzake, Kaya Callas, mwakilishi wa sera za kigeni za Ulaya, walipokutana Brussels tarehe 2025/7/3 kujiandaa kwa mkutano huu kwamba "China haitaki kuipoteza Urusi kwenye vita nchini Ukraine."
Ushindi wa Urusi katika vita unaimarisha msimamo wa China dhidi ya Magharibi na kuishawishi kufanya uvamizi wa Taiwan. Lakini inachukuliwa kuwa ya hatari kwa Ulaya, kwa sababu Urusi inaitishia kwa uvamizi wa mashariki mwa Ukraine, na ikiwa itashinda, itatamani kuvamia nchi za Baltic zinazozunguka Kaliningrad ya Urusi, na kisha Poland, kwani iko ndani ya mkakati wake. Rais wake, Putin, alikiri kwamba kukubali kwa Urusi kuanguka kwa Ukuta wa Berlin na kujiondoa kwake kutoka Ulaya Mashariki ilikuwa hila ya Amerika na kosa la kihistoria. Na kama alivyotaja Kiongozi wa Kisovieti, Stalin, "Poland ni mstari wa kwanza wa ulinzi mbele ya Magharibi."
Vita vya Ukraine vilianzishwa na Amerika wakati ilimfanya mteja wake, Zelensky, amkasirishe Urusi kufanya uvamizi wa Ukraine mwaka 2022, na kusababisha mpasuko kati ya Urusi na Ulaya ili kumaliza nguvu zao, na kudhoofisha ukaribu kati yao, na kuimarishana dhidi yake, na pia kudhoofisha uhusiano kati yake na China.
Balozi wa China katika Umoja wa Ulaya, Tsai Run, alieleza kuwa "mshirika wa ushirikiano, mshindani wa kiuchumi, na hasimu wa kimfumo. Hii ni sawa na taa za trafiki zinazowaka kijani, machungwa na nyekundu, lakini haziweki tu harakati, bali pia husababisha matatizo na kizuizi". China inatambua kwamba Ulaya, licha ya ushirikiano kati yao, kuna ushindani na uadui, hivyo inabaki kuwa na wasiwasi nayo.
Ulaya inahitaji kuimarisha uhusiano wake wa kibiashara na China kutokana na mivutano ya uhusiano wa kiuchumi na Amerika kutokana na kupandisha ushuru wa forodha kwa bidhaa za Ulaya na kuvuruga minyororo ya usambazaji ambayo inachukuliwa kuwa muhimu sana kwa uthabiti wa uchumi wa Ulaya.
China inachukuliwa kuwa chanzo kikubwa zaidi cha uagizaji wa bidhaa katika Umoja wa Ulaya, soko la tatu kwa ukubwa la bidhaa zake na makampuni yake, na chanzo muhimu cha madini adimu na betri kwa asilimia 43.8, paneli za jua kwa asilimia 97, na vipengele amilifu vya dawa na bidhaa nyinginezo. Inaathiri misingi ya sekta ya Ulaya.
Gazeti la Le Monde la Ufaransa lilisema tarehe 2025/7/26: "Katika kivuli cha sera kali za Marekani kuhusu ushuru wa forodha, Ulaya inahangaika kutafuta suluhisho. Marekani inatarajia Ulaya kusimama dhidi ya China, lakini misimamo ya baadhi ya nchi za Umoja wa Ulaya, kama vile Ujerumani, ambayo inathamini biashara yake na China, haipendezi Marekani na haitaki kuingia katika uadui na China." Marekani inatafuta kuunda mpasuko kati ya Ulaya na China ili kudhoofisha kama nguvu pinzani kwake.
Gazeti hilo lilisema, "Mkutano huo ulifichua nguvu za China na ukubwa wa tofauti kubwa katika nyanja za kibiashara na kidiplomasia ambazo zimeanza kutenganisha bara la kale na China. Labda Von der Leyen mwenyewe aligundua wakati wa ziara yake kwamba "kuna ulimwengu mpya umeibuka nchini China: magari mapya, mengi yao yakiwa ya umeme au mseto, bidhaa mpya, utaalamu wa viwanda ambao hauwezi kulinganishwa". Von der Leyen alikiri kwamba "mahusiano yamefikia hatua muhimu, lakini hakuna kinachoonyesha kuwa Umoja wa Ulaya una mwanzo wa suluhu kwa matatizo haya".
Gazeti hilo liliongeza, "Mkutano huo ulibadilika na kuwa mazungumzo ya viziwi, hakukuwa na makubaliano hata katika suala la hali ya hewa ambalo linapaswa kukubaliwa, jambo ambalo lilihitaji juhudi kubwa kuandaa taarifa ya pamoja, tofauti zilionekana wazi. Na katika upande wa kibiashara, nakisi ya biashara ya Ulaya na China inaongezeka mara mbili katika miaka kumi na kuzidi euro bilioni 300 kwa mwaka, kutokana na msaada wa serikali na hatua za ulinzi, jambo linalofanya ushindani usio wa haki, na unatishia ajira na sekta ya Ulaya".
Hivyo, Ulaya inajaribu bure kukubaliana na China ili kurekebisha uchumi wake ulioporomoka, na kuweza kukabiliana na vita vya biashara vya Amerika dhidi yake, ambavyo inaviona kama mshindani, ambapo Rais wake Trump alisema tarehe 2025/2/27: "Umoja wa Ulaya ulianzishwa ili kuidhulumu Amerika ... na wamefanya kazi nzuri. Na jambo hili litakoma mara moja chini ya uongozi wangu." Na alituma ujumbe kwa Von der Leyen tarehe 2025/7/11 akilalamika "kuhusu sera za forodha na zisizo za forodha na vikwazo vya kibiashara vya Umoja wa Ulaya."
Ulaya imekuwa katika msukosuko mgumu, na kutoka kwake ni ngumu zaidi, dada yake na mshirika wake, Amerika, inazindua vita kali vya kiuchumi dhidi yake, pamoja na vita vya kisiasa vya kuvunja umoja wake, pamoja na kumaliza nguvu zake katika vita vya Ukraine. Haiwezi kupata katika China mshirika wala nguvu isiyo na upande ambayo inaweza kushughulika nayo kwa urahisi.
Hili lilielezwa na Ingin Eroglu, Mkuu wa ujumbe wa Bunge la Ulaya kwa China, akisema "Uaminifu dhaifu kati ya China na Umoja wa Ulaya umerekodi viwango vipya vya kushuka katika mazingira haya ya kutokuaminiana kimkakati, kuna mvutano ingawa sio hali ya kukwama."
Na China inatambua udhaifu wa Ulaya, hivyo inakuwa kali nayo, ili kubaki katika msimamo madhubuti dhidi yake, na ili isisalimu amri katika suala la nakisi yake ya kibiashara nayo. Na imeipoteza Urusi, ambapo ilikuwa ikinufaika nayo sana. Hali yake inazidi kuwa mbaya na haipati suluhu. Na inajaribu kutumia nguvu zake za ndani, hivyo Ufaransa, Ujerumani na Uingereza, ambazo ni nguvu kuu za Ulaya, zinatafuta kufanya kazi za pamoja, na ni vigumu kutatua matatizo haya yote katika muda mfupi.
Hivyo, nguvu za uovu zinagombana Mashariki na Magharibi ili kuongeza taabu ya wanadamu ambao wanatafuta mwokozi wao. Na zinapanga njama za kuzuia kuibuka kwa mwokozi huyu, naye si mwingine bali Uislamu uliomo katika dola ya Khilafa Rashida kwa njia ya Utume.
Imeandikwa na: Profesa Asaad Mansour
Chanzo: Jarida la Ar-Raya