July 08, 2025

Jarida la Al-Raya: Katika kumbukumbu ya Hijra ya Mtume, nini maana ya kukosekana kwa dola ya Khilafa?!

Al Raya sahafa

2025-07-09

Jarida la Al-Raya:

Katika kumbukumbu ya Hijra ya Mtume

Nini maana ya kukosekana kwa dola ya Khilafa?!

Hakika Uislamu bila shaka ni kanuni sahihi pekee yenye uwezo wa kushughulikia matatizo ya maisha ya binadamu katika nyanja zake mbalimbali, kwa sababu itikadi yake ndiyo wazo pekee kamili la uponyaji ambalo limeeleza ukweli wa uwepo huu na kabla yake na baada yake, na limetatua maswali ya fundo kuu kwa jibu linalosadikisha akili, linalokubaliana na maumbile na linaloujaza moyo utulivu.

Na itikadi haiwi ya msingi isipokuwa ikiwa inaeleza mtazamo wake juu ya ukweli wa uwepo huu, na mfumo unaotokana nayo unaeleza kwa watu kazi yao ndani yake. Hili ni kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine, kanuni, kanuni yoyote ile, haiwezi kutekeleza jukumu lake katika uhalisia wa maisha ya kivitendo isipokuwa kuwe na chombo tendaji kinachotumia mifumo yake kwa matumizi ya kivitendo katika uhalisia wa maisha, vinginevyo kanuni hii itakuwa falsafa tu ya kinadharia ya kufikirika ambayo haina athari katika uhalisia wa maisha ya kivitendo, kwa sababu wazo la kanuni lazima liwe na njia ya kulidhihirisha na kulitekeleza katika uhalisia wa maisha, ili kuwepo kwake kuwe kuwepo kwa kivitendo na si wazo tu la kinadharia la kifalsafa, na kwa hivyo kuwepo kwa dola ya Kiislamu kulikuwa ni lazima ili kuifanya itikadi ya Kiislamu kuwa wazo la kivitendo linalotawala jamii, na ilikuwa lazima Khilafa iwe ndiyo umbo ambalo Waislamu wanapaswa kulihifadhi na kulitimiza mfululizo, kila Khalifa anapoondoka, wamteue Khalifa mwingine anayewawakilisha katika kusimamisha hukumu kwa yale ambayo Mungu ameyateremsha, kama njia ya kujitenga na dhima katika kubeba amana ya Uislamu ambayo Mungu aliyewaumba na kuwafanya makhalifa katika ardhi amewakabidhi. Na Hadithi za Mtume ﷺ katika upande huu ni nyingi; ambapo Mtume ﷺ aliamrisha umuhimu wa kuhifadhi kuwepo kwa dola ya Kiislamu, akasema ﷺ: «TIMIZENI BAIA YA WA KWANZA, WA KWANZA», na katika Hadithi nyingine alisema ﷺ: «AKIAPISHWA MAKHALIFA WAWILI, BASI MUUWENI YULE MWINGINE KATIKA WAO», basi Khilafa ndiyo njia ya kisheria ya kutumia mifumo ya Uislamu kwa matumizi ya kivitendo katika uhalisia wa maisha, na kubeba ujumbe wa Uislamu kwa ulimwengu kwa njia ya da'wa na jihad, kuvunja nguvu za batili zinazozuia kufika kwa kheri ambayo Mtume ﷺ alitumwa nayo kama rehema kwa walimwengu, na kuwepo kwake kunamaanisha kuwepo kwa Uislamu, na kutokuwepo kwake kunamaanisha kuuondoa Uislamu kutoka katika maisha, na kuingiza mfumo mwingine unaoendesha watu kwa batili na kutunza mambo yao kwa yale ambayo mataaghuti wanayapenda.

Na inasikitisha kwamba Waislamu walipuuza dola ya Khilafa, ambapo ukoloni wa kigeni uliweza kuibomoa mwaka 1342 Hijria, sawa na mwaka 1924 Miladia, na kinachotia huzuni zaidi ni tunapoona maadui zetu wametambua maana ya kuwepo kwa Khilafa, huku tunawaona watu wetu wenyewe wameghafilika na jambo hili, na utaona kuwa maadui wa Uislamu wamezingatia katika mipango yao kuwaepusha Waislamu na kufikiria kuirejesha Khilafa tena, na wametumia kila wanachomiliki cha mbinu za ujanja na udanganyifu, na wamewaajiri kwa ajili hiyo vibaraka na walioathirika, huku tunawaona Waislamu leo wakikumbatiana katika udanganyifu wa suluhu za kutoka katika mzunguko huu ambao unawakumba kwa majanga na maumivu bila ya kutambua kwamba kutokuwepo kwa Khilafa ndiyo tatizo kubwa ambalo wanapaswa kulishughulikia kwa kulichukulia kama kichwa cha mambo ya muhimu kama suala la hatima linalowataka wao kulisimamisha, pamoja na kwamba Mtume ﷺ alielekeza umuhimu wa kufanya kazi ya kusimamisha suluhu hii ya kimsingi ambayo itasimama juu ya magofu ya mifumo hii ya kidhalimu, ambapo alisema ﷺ: «KUTAKUWEPO KHILAFA JUU YA NYUZO ZA UTUME».

Na katika hali halisi hii chungu ambayo mifumo ya kikafiri ya kidhalimu imeanza kutawala jamii, ilikuwa ni lazima kuwepo kwa kundi la msingi la kisiasa lililoaminifu linalobeba mradi wa Uislamu ukiwa safi na linalofanya kazi ya kusimamisha Khilafa Rashidah iliyoahidiwa, tukichochewa na njia ya Mtume ﷺ katika kusimamisha dola ya kwanza ya Uislamu, kupitia:

1- Kuelimisha na kuunganisha

2- Kuingiliana kwa mzozo wa kiitikadi na mapambano ya kisiasa na kutafuta nusra kutoka kwa watu wenye nguvu na kinga

3- Kupokea hukumu na uamuzi

Na haisemekani kwamba hili haliwezekani, kwani hasemi hivi isipokuwa wajinga wa itikadi yetu yenye uwezo wa kushawishi akili na kuathiri nafsi kwa sababu ya kukubaliana kwake na maumbile ya kibinadamu. Na viongozi wa Ansar, radhi za Mungu ziwe juu yao, walikuwa mfano kwa watu wa nguvu na kinga ambao walifanya heshima na mamlaka yao katika kuunusuru Uislamu na wale wanaofanya kazi ya kuusimamisha katika baia ya uongofu, ambapo walikabidhi uamuzi wa hukumu kwa kiongozi mfano Muhammad ﷺ katika baia ya pili ya Aqaba, ambayo ni baia ya kukabidhi hatamu za hukumu na si kuthibitisha utume ambao umethibitishwa na muujiza wa Qur'ani Tukufu.

Na nchi yoyote ya Kiislamu ambayo da'wa ya kundi hili lililoaminifu ilizaa matunda ndani yake, na watu wake wakakomaa kiakili na wakatambua umuhimu wa Khilafa Rashidah kama ahadi na faradhi kubwa, na ikaelezewa kwao ni chama gani kinachoongoza kinachostahili kuungwa mkono, na ufahamu wa Khilafa ukawa ndio unaotawala katika eneo hilo la nchi za Waislamu, basi ni jambo la kawaida kwa joto la da'wa ya kweli kufika kwa watu wa nguvu na kinga, kwa sababu wao kwa hakika ni sehemu ya wana wa umma na jamii hii ambayo ufahamu wake umekomaa juu ya wazo la suluhu ya kimsingi la kimsingi ya kushughulikia matatizo ya Waislamu na watu wote kwa ujumla. Na tuna hakika kamili kwamba wana wa umma wa Kiislamu katika nchi zote za Kiislamu wamekuwa na ufahamu zaidi kuliko hapo awali, hasa nchi za Sham ambazo Mtume ﷺ alisema juu yake: «KITOVU CHA NYUMBA YA UISLAMU NI SHAM» na ni ardhi iliyobarikiwa ambayo itakuwa mahali pa kushuka Khilafa Rashidah iliyoahidiwa kwa idhini ya Mungu.

Hii ndiyo suluhu ya msingi ambayo Hizb ut-Tahrir inawalingania tangu ilipoanzishwa katika Baitul Muqaddas mwaka 1372 Hijria - 1953 Miladia, na ni ahadi isiyo ya uongo, na bishara ya Mtume ﷺ na imekuwa karibu sana kwa idhini ya Mungu.

Imeandikwa na: Mwalimu Ramzi Rajih - Wilaya ya Yemen

Chanzo: Jarida la Al-Raya

More from null

Jarida la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Al Raya sahafa

2025-11-12

Jarida la Ar-Raya:Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Enyi watu wa Sudan: Vita nchini Sudan na kwingineko vitaendelea kuwa kichocheo cha tamaa za kimataifa na mizozo yao kwa mipango yao mibaya, uingiliaji wao, na kuwapa pande zinazozozana silaha ili kuimiliki kikamilifu hadi lini?! Wanawake na watoto wenu wanateseka kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na mzozo huu wa umwagaji damu ambao hautimizi chochote ila maslahi ya nchi za Magharibi na vibaraka wao katika kudhibiti hatima ya Sudan, ambayo daima imekuwa ni kitu cha kutamaniwa kwao kwa sababu ya eneo lake na utajiri wake, hivyo ni kwa maslahi yao kuipasua na kuitawanya. Na kutekwa kwa Al-Fashir na vikosi vya Rapid Support Forces ni sehemu nyingine tu ya mipango hii, ambapo Marekani inataka kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan na kukomesha ushawishi wa Uingereza humo.

===

Lengo la ziara ya Ortagus

Nchini Lebanon!

Katika mazingira ya mashambulizi ya Marekani dhidi ya Lebanon na eneo hilo kwa mradi wa kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha, na jitihada za utawala wa Marekani chini ya uongozi wa Trump na timu yake za kuunganisha idadi kubwa ya watawala wa nchi za Waislamu kwenye makubaliano ya Abraham, ziara ya mjumbe wa Marekani, Morgan Ortagus, nchini Lebanon na nchi haramu ya Kiyahudi inakuja ikiwa na shinikizo, vitisho, na masharti ya kisiasa, kiusalama na kiuchumi kwa Lebanon, ikijua kwamba ziara hii imefanyika sambamba na ziara ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na Mkurugenzi wa Ujasusi wa Misri, ambayo inaonekana kuelekea mwelekeo uleule.

Kuhusiana na ziara hizi, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Lebanon ilisisitiza mambo yafuatayo:

Kwanza: Uingiliaji wa Marekani na wafuasi wake katika nchi za Waislamu ni kuhudumia maslahi ya Marekani na nchi haramu ya Kiyahudi, sio kuhudumia maslahi yetu, haswa kwani Marekani ndiye msaidizi mkuu wa nchi haramu ya Kiyahudi katika siasa, uchumi, fedha, silaha, na vyombo vya habari, waziwazi.

Pili: Ziara ya mjumbe sio ziara ya upande wowote kama wengine wanavyoweza kufikiria! Badala yake, inakuja katika muktadha wa sera ya wazi ya Marekani katika eneo hilo ambayo inasaidia nchi haramu ya Kiyahudi na inachangia kuiwezesha kijeshi na kisiasa, na kile ambacho mjumbe wa Marekani anatoa ni kulazimisha utawala, kuimarisha utegemezi, na kupunguza uhuru, na ni aina ya kujisalimisha na kujinyenyekeza kwa Wayahudi, na hili ndilo Mungu anawakataza watu wa Uislamu.

Tatu: Kukubali maagizo haya na kusaini makubaliano yoyote ambayo yanaimarisha udhibiti wa kigeni ni usaliti kwa Mungu, Mtume Wake, na Umma, na kwa kila mtu ambaye alipigana au kujitolea ili kuiondoa nchi hii haramu kutoka Lebanon na Palestina.

Nne: Kushughulika na nchi haramu ya Kiyahudi kwa idadi kubwa ya watu wa Lebanon, Waislamu na wasio Waislamu, ni uhalifu katika dhana ya kisheria, na hata katika sheria chanya ambayo mamlaka ya Lebanon inahukumu kwayo, au sheria ya kibinadamu kwa ujumla, haswa baada ya nchi hiyo haramu kufanya mauaji ya kimbari huko Gaza, ambayo haitasita kufanya kama hayo huko Lebanon na nchi zingine za Waislamu.

Tano: Kampeni na mashambulizi ya Marekani dhidi ya eneo hilo hayatapita, na Marekani haitafanikiwa katika jitihada zake za kuunda eneo hilo kama inavyotaka, na ikiwa ina mradi wake kwa eneo hilo, ambao unategemea ukoloni, unyanyasaji wa watu, kuwapotosha Waislamu, na hata kuwatoa kwenye dini yao kwa kuita (Dini ya Abraham), basi Waislamu, kwa upande mwingine, wana mradi wao ulioahidiwa kuonyeshwa na Mungu Mwenyezi; mradi wa Khilafah ya pili kwa mfumo wa Utume, ambao umekaribia sana, kwa idhini ya Mungu Mwenyezi, na mradi huu ndio utachora upya eneo hilo, na hata ulimwengu mzima, kwa mara nyingine tena, kama inavyothibitishwa na maneno ya Mtume ﷺ: «Hakika Mwenyezi Mungu aliniandalia ardhi, nikaona mashariki yake na magharibi yake, na hakika ufalme wa umma wangu utafikia kile nilichoandaliwa kutoka kwake» Imesimuliwa na Muslim, na nchi haramu ya Kiyahudi itaangamizwa kama Mtume ﷺ alivyobashiri katika hadithi yake: «Saa haitasimama mpaka Waislamu wapigane na Wayahudi, na Waislamu watawaua...» Imekubaliwa.

Hatimaye, Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Lebanon inaendelea kuunga mkono kukabiliana na kampeni ya Marekani na mashambulizi yake ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha kwa Lebanon na eneo hilo, na hakuna chochote kitakachoizuia kufanya hivyo, na tunaionya mamlaka ya Lebanon dhidi ya kufuata njia ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha! Na tunawasihi kujilinda kwa watu wao ili kukabiliana na hilo, na wasicheze na jambo hilo kwa kisingizio cha mipaka au ujenzi mpya na ushawishi wa mfumo wa kimataifa, ﴿Na Mwenyezi Mungu ni Mshindi juu ya jambo lake, lakini watu wengi hawajui﴾.

===

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan

Unakutana na idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, siku ya Jumatatu, Novemba 3, 2025, ulizuru idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini. Ujumbe huo ulikuwa chini ya uongozi wa Mwalimu Al-Nadhir Muhammad Hussein Abu Minhaj, mjumbe wa Baraza la Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Mwalimu Muhammad Saeed Boukeh, wajumbe wa Hizb ut-Tahrir.

Ambapo ujumbe huo ulikutana na kila mmoja wa:

Mwalimu Khalid Hussein - Mkuu wa Chama cha Muungano wa Kidemokrasia, tawi la Jalaa Al-Azhari.

Dkt. Abdullah Youssef Abu Seil - Mwanasheria na mhadhiri wa sheria katika vyuo vikuu.

Sheikh Abdul Rahim Jouda - kutoka kundi la Ansar al-Sunna.

Bw. Ahmed Muhammad - Mwandishi wa Shirika la Habari la Suna.

Mikutano hiyo ilizungumzia mada ya sasa; kuanguka kwa Al-Fashir na uhalifu uliokuwa umeambatana nayo uliofanywa na wanamgambo dhidi ya watu wa jiji hilo, na kuachwa na viongozi wa jeshi, ambao hawakutimiza wajibu wao kwa watu wa Al-Fashir na kuondoa kuzingirwa kwao, na wana uwezo wa kufanya hivyo katika kipindi chote cha kuzingirwa, na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi yao zaidi ya mashambulizi 266.

Kisha ujumbe huo uliwakabidhi nakala ya broshua ya Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan yenye kichwa: "Kuanguka kwa Al-Fashir kunafungua njia kwa mpango wa Marekani wa kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan, hadi lini tutakuwa kichocheo cha mzozo wa kimataifa?!". Majibu yao yalikuwa ya kipekee na waliomba mikutano hii iendelee.

===

Mazoezi ya "Phoenix Express 2025"

Sura kutoka sura za Tunisia kujisalimisha kwa utawala wa Marekani

Maandalizi ya Tunisia ya kuandaa toleo jipya la zoezi la majini la pande nyingi la "Phoenix Express 2025" yanakuja wakati wa mwezi wa Novemba, ambalo ni zoezi ambalo Kamandi ya Marekani ya Afrika imeanza kuandaa kila mwaka baada ya utawala wa Tunisia kuhusisha nchi kwa kusaini na Marekani, tarehe 2020/09/30, makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi, ambayo Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Mark Esper, alielezea kama ramani ya barabara itakayoendelea kwa miaka kumi.

Katika suala hili, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Tunisia ilikumbusha kwamba chama hicho kilibainisha wakati wa kusainiwa kwa makubaliano haya hatari kwamba jambo hilo linazidi makubaliano ya jadi, kwani Marekani inachora mradi mkubwa ambao unahitaji kukamilika kwa miaka 10 kamili, na kwamba ramani ya barabara, kulingana na madai ya Marekani, inahusiana na ufuatiliaji wa mipaka, ulinzi wa bandari, kupambana na mawazo ya itikadi kali, na kukabiliana na Urusi na China, na hii inamaanisha kwa dharau zote, kupunguza uhuru wa Tunisia, badala yake ni uangalizi wa moja kwa moja juu ya nchi yetu.

Taarifa hiyo ilisisitiza kwamba Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Tunisia, licha ya unyanyasaji, kukamatwa, na kesi za kijeshi ambazo vijana wetu wanakumbana nazo kwa sababu ya kusema ukweli, inathibitisha tena wito wake wa kuvunja makubaliano haya ya kikoloni yaliyolaaniwa ambayo yanalenga kuivuta nchi na nchi zote za Maghrib ya Kiislamu na kuzinyenyekeza kwa sera mbaya za Marekani, na pia ilirudia wito wake kwa watu wa nguvu na ulinzi huko Tunisia na nchi zingine za Waislamu kuwa waangalifu juu ya kile ambacho maadui wa Umma wanawafanyia njama na kuwavuta kwacho, na kwamba wajibu wa kisheria unahitaji wao kuunga mkono dini yao na kukabiliana na adui ambaye anavizia nchi yao na Umma wao, na kuinua neno la Mungu kwa kuunga mkono wale wanaofanya kazi ya kutekeleza sheria zake na kuanzisha dola yake, Dola ya Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume ulioahidiwa hivi karibuni kwa idhini ya Mungu.

===

Dharau ya Marekani kwa raia wake

Inawaacha wanawake na watoto wakiwa na njaa

Mpango wa Msaada wa Lishe ya Ziada (SNAP) ni mpango wa shirikisho ambao husaidia watu binafsi na familia zenye kipato cha chini na wenye ulemavu kupata faida za kielektroniki zinazotumiwa kununua chakula na vinywaji, isipokuwa pombe, na mimea ya kulima chakula chao wenyewe. Ripoti zinaonyesha kuwa Wamarekani milioni 42 wanategemea faida za (SNAP) kulisha wao wenyewe na familia zao. 54% ya watu wazima wanaopokea faida za chakula ni wanawake, na wengi wao ni mama wasio na waume, na 39% yao ni watoto, ambayo inamaanisha kuwa karibu mtoto mmoja kati ya watano anategemea faida hizi kuhakikisha kuwa hawapati njaa. Kufungwa kwa shirikisho pia kumesababisha baadhi ya majimbo kutafuta njia zingine za kufadhili mipango ya chakula ya bure na iliyopunguzwa katika maeneo yao ya elimu, ili watoto wanaotegemea chakula wakati wa siku ya shule wasilazimike kuishi bila chakula. Kama matokeo, maduka mengi ya chakula yaliyoenea kote nchini yanachapisha picha za rafu tupu, na kuwaomba watu kutoa chakula na kadi za zawadi za maduka ya mboga ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya chakula.

Kuhusu hilo, Idara ya Wanawake katika Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Tunapaswa kuuliza ni jinsi gani nchi tajiri zaidi ulimwenguni inaweza kupuuza ukweli kwamba mamilioni ya raia wake walio hatarini zaidi hawapati chakula cha kutosha? Unaweza kujiuliza Amerika inatumia pesa zake wapi, hata wakati wa kufungwa? Vema, badala ya kuhakikisha kuwa Wamarekani wanapata chakula cha kutosha, wanatuma mabilioni ya dola kwa nchi haramu ya Kiyahudi kuwaua Wapalestina. Ni mtawala ambaye anaona kuwa kujenga ukumbi wa sherehe za kifahari ni muhimu kuliko kitu kingine chochote, wakati manaibu wengine wanaona uwekezaji wao wa kibinafsi unachukuliwa kuwa muhimu kuliko ustawi wa watu ambao wanapaswa kuwawakilisha! Kama unavyoona, Amerika ya kibepari haijawahi kujali kutunza masuala ya raia wake, badala yake ilikuwa inajali tu kutoa msaada wa kijeshi na kifedha kwa wale wanaowanyima watoto kote ulimwenguni haki yao ya usalama, chakula, makazi, na elimu, ambazo ni mahitaji ya msingi. Kwa hivyo, inawaacha watoto huko Amerika pia wakiteseka na njaa na ukosefu wa usalama, na wanakosa elimu sahihi na huduma ya afya.

===

«Muislamu yeyote yule ni haramu kwa Muislamu mwenzake; damu yake, mali yake, na heshima yake»

Kwa kila Muislamu, kwa kila afisa na askari, kwa kila mtu anayemiliki silaha: Hakika Mwenyezi Mungu ametupa akili ili tufikiri kwayo, na ametulazimisha kuitumia matumizi sahihi, kwa hivyo mtu asitende au kufanya kazi yoyote au kutamka neno lolote kabla ya kujua hukumu yake ya kisheria, na kujua hukumu ya kisheria kunahitaji kuelewa hali halisi ambayo hukumu ya kisheria inataka kuletwa, kwa hivyo lazima Muislamu awe na ufahamu wa kisiasa, ili aweze kufahamu mambo kama yalivyo, na asifuate mipango ya makafiri wakoloni ambao hawatutakii mema sisi wala Uislamu, na wanafanya bidii kwa kila wawezalo kwa nguvu, hila na akili kutupasua vipande vipande na kuudhibiti nchi yetu na kunyakua rasilimali zetu na utajiri wetu, kwa hivyo Muislamu anawezaje kukubali kuwa chombo mikononi mwa makafiri hao wakoloni, au mtendaji wa maagizo ya vibaraka wao?! Je, anatamani kitu kidogo cha starehe za dunia hii zinazopita na anapoteza Akhera yake na anakuwa miongoni mwa watu wa Motoni milele humo, amelaaniwa na kufukuzwa kutoka kwa rehema za Mungu? Je, Muislamu anakubali kumridhisha mtu yeyote yule miongoni mwa wanadamu viumbe dhaifu huku anamkasirisha Mungu Mwenyezi ambaye mikononi mwake iko dunia na Akhera?!

Hakika Hizb ut-Tahrir inawasihi kuinua kiwango cha ufahamu wa kisiasa, kuzingatia hukumu za Mungu Mwenyezi, na kufanya kazi nayo ili kuhukumu kwa yale ambayo Mungu ameyateremsha, ili kuwaondoa mikono ya makafiri wakoloni na vibaraka wao, na kushindwa mipango yao katika nchi yetu.

===

Ninyi ndio mnaowaweka Waislamu katika njaa

Ewe Masoud Pezeshkian!

Chini ya kichwa hiki, Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Iran imetangaza kufilisika kwa benki kubwa zaidi ya kibinafsi nchini humo, ambayo ni benki ya (Ayandeh), na benki hii ina matawi 270 nchini Iran, baada ya madeni kuongezeka hadi dola bilioni tano, na cha kushangaza ni kukosoa kwa rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, kushindwa kwa utawala, akisema: "Tuna mafuta na gesi, lakini tuna njaa"!

Taarifa hiyo ilisisitiza: Mwenye dhamana ya kushindwa huko kwa utawala ambako rais wa Iran anazungumzia ni rais mwenyewe, kwa nini watu wa Iran wana njaa - Ewe Masoud Pezeshkian - na mna mafuta, gesi, na utajiri mwingine na madini? Je, siyo matokeo ya sera zenu za kijinga? Je, siyo kwa sababu ya umbali wenu kutoka kwa kuhukumu kwa Uislamu? Na vivyo hivyo, inasemwa kwa nchi zingine za Waislamu, watawala wajinga ndani yake wanapoteza utajiri mwingi wa Umma, na wanawezesha makafiri wakoloni kupata utajiri huo, na wananyima Umma utajiri huo, kisha mmoja wao anakuja kuhalalisha sababu ya njaa kwa kusema kwamba ni kushindwa kwa utawala!

Hatimaye, taarifa hiyo kwa vyombo vya habari iliwahutubia Waislamu: Ujinga wa watawala hawa ambao wanachukua masuala yenu umeonekana kwa kila mwenye macho na ufahamu, na hawafai kuchukua masuala hayo, umefika wakati wa kuwazuia, kwani hii ndiyo hukumu ya mjinga; kumzuia kutumia pesa na kumdhibiti, na mumpatie Bay'ah Khalifa mmoja anayewahukumu kwa sheria ya Mungu Mwenyezi, na afute mfumo wa riba katika nchi yenu ili Mola wenu akuridhieni na Mtume Wake ﷺ, na arejeshe utajiri wenu ulionyaganywa, na arejeshe heshima yenu na fahari yenu, na hapa kuna Hizb ut-Tahrir, mwanzilishi ambaye watu wake hawasemi uongo, anawasihi kufanya kazi nayo ili kuanzisha Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume.

 </