Jarida la Ar-Raya: Jibu la Swali: Uchokozi wa Taasisi ya Kiyahudi dhidi ya Iran na Matokeo yake
July 01, 2025

Jarida la Ar-Raya: Jibu la Swali: Uchokozi wa Taasisi ya Kiyahudi dhidi ya Iran na Matokeo yake

Al Raya sahafa

2025-07-02

Jarida la Ar-Raya:

Jibu la Swali

Uchokozi wa Taasisi ya Kiyahudi dhidi ya Iran na Matokeo yake

Swali:

Al-Arabiya ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo 2025/6/27: (Vyanzo 4 vya kuaminika vilisema kuwa utawala wa Rais Donald Trump ulijadili uwezekano wa kuisaidia Iran kupata hadi dola bilioni 30 ili kujenga mpango wa nyuklia wa kuzalisha nishati kwa madhumuni ya kiraia. Vyanzo viliongeza kuwa mazungumzo haya yaliendelea wiki hii baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano kufikiwa. Maafisa wa utawala wa Trump walithibitisha kuwasilisha mapendekezo kadhaa, ambayo ni mapendekezo ya awali na yaliyokuzwa na kipengele kimoja kisichobadilika ambacho hakiwezi kujadiliwa ambacho ni "kusimamisha kabisa urutubishaji wa uranium wa Iran"). Trump alikuwa ametangaza kuanza kutumika kwa usitishaji mapigano aliyopendekeza kati ya Iran na taasisi ya Kiyahudi, (Netanyahu alisema kuwa alikubali pendekezo la Trump. Shirika la habari la Reuters pia lilimnukuu afisa mkuu wa Iran akisema kwamba Tehran ilikubali kusitisha mapigano kupitia usuluhishi wa Qatar na pendekezo la Amerika. Al-Jazeera, 2025/6/24). Haya yote yalitokea baada ya vikosi vya Trump mnamo 2025/6/22 kushambulia vituo vya nyuklia vya Iran, na baada ya taasisi ya Kiyahudi kuzindua uchokozi mpana wa ghafla dhidi ya Iran tangu 2025/6/13. Swali hapa ni kwa nini taasisi ya Kiyahudi ilifanya uchokozi huu wa ghafla, ambao haifanyi isipokuwa kwa amri ya Amerika? Je, Iran haitembei katika mzunguko wa Amerika, kwa hivyo Amerika ilishiriki vipi katika kushambulia vituo vya nyuklia vya Iran? Asante.

Jibu:

Ili jibu liwe wazi, tutaangalia mambo yafuatayo:

1- Ndiyo, mpango wa nyuklia wa Iran unachukuliwa kuwa hatari kubwa kwa taasisi ya Kiyahudi, kwa hivyo inataka kuiondoa kwa njia zote, na kwa sababu hiyo ilishangilia uamuzi wa Rais Trump mwaka 2018 kujiondoa kwenye makubaliano ya 2015, na msimamo wa taasisi ya Kiyahudi ulikuwa wazi kuwa inakubali tu mfumo wa Libya na Iran kuvunja mpango wake wa nyuklia, yaani, Iran kuachana na mpango wake wa nyuklia kabisa. Iliimarisha majasusi wake ndani ya Iran kwa ajili hiyo. Shambulio la taasisi ya Kiyahudi katika siku yake ya kwanza lilifichua jeshi la vibaraka ndani ya Iran ambao walikuwa wakifuatilia na kushirikiana na shirika la ujasusi la taasisi ya Kiyahudi "Mossad" kwa ajili ya kupata dirhamu chache, wanaagiza vipuri vya ndege zisizo na rubani na kuzikusanya katika warsha ndogo ndani ya Iran na kuzirusha kwenye malengo ambayo yanajumuisha nyumba za viongozi wa serikali ya Iran katika hali ambayo inafanana na kile kilichotokea kwa chama cha Iran nchini Lebanon wakati taasisi ya Kiyahudi ilipowaua viongozi wake!

2- Msimamo wa Amerika ulikuwa msaada mkuu kwa taasisi ya Kiyahudi, bali ni kichocheo chao dhidi ya mradi wa nyuklia wa Iran, lakini Trump aliweka mezani kufanikisha hilo: Suluhisho la mazungumzo na suluhisho la kijeshi. Hivyo ndivyo Amerika na Iran zilielekea Muscat-Oman mnamo Aprili 2025 kwa mazungumzo, na utawala wa Trump ulikuwa ukisifu kwa kina cha makubaliano ambayo yalikuwa yakifanyika katika mazungumzo ya nyuklia kana kwamba makubaliano mapya ya nyuklia yalikuwa karibu sana. Trump alikuwa ameweka muda wa miezi miwili kukamilisha makubaliano haya, na maafisa wa taasisi ya Kiyahudi walikuwa wakikutana na mjumbe wa Marekani katika eneo hilo na mpatanishi mkuu wa Iran, Witkov, karibu mara moja kabla ya kila mkutano na ujumbe wa Iran kumjulisha mpatanishi wa Marekani kile kilichokuwa kinaendelea katika mazungumzo...

3- Utawala wa Trump uliunga mkono maoni magumu ya baadhi ya watu wake muhimu, maoni ambayo yanaendana na taasisi ya Kiyahudi. Hiyo iliambatana na kuibuka kwa maoni magumu huko Ulaya pia, kwani nchi za Ulaya zilikasirishwa na ukweli kwamba Amerika ilikuwa ikizungumza na Iran peke yake, ambayo inamaanisha kwamba Amerika ingepata sehemu kubwa ya makubaliano yoyote na Iran, haswa kwani Iran ilikuwa ikitamanisha utawala wa Trump kwa kuzungumza juu ya mamia ya mabilioni ya dola ambazo kampuni za Amerika zinaweza kuwekeza na kufaidika nazo ndani ya Iran kama vile mikataba ya mafuta na gesi, kampuni za ndege na mengine mengi, na maoni hayo magumu yalikamilika kwa kuonekana kwa ripoti ngumu kutoka Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki: (Kwa mara ya kwanza katika karibu miaka 20, Bodi ya Magavana ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki ilitangaza Alhamisi hii "Juni 12/2025" kwamba Iran imekiuka majukumu yake katika uwanja wa kuzuia kuenea kwa silaha za nyuklia... Deutsche Welle ya Ujerumani, 2025/6/12), na Kiongozi Mkuu wa Iran alikuwa amekataa hapo awali kusimamisha urutubishaji: (Khamenei alisema: "Kwa kuwa mazungumzo yanaendelea, nataka kutoa onyo kwa upande mwingine. Upande wa Amerika, ambao unashiriki katika mazungumzo haya yasiyo ya moja kwa moja na unafanya majadiliano, haupaswi kusema maneno ya kipuuzi. Kusema kwao "Hatutaruhusu Iran kurutubisha uranium" ni kosa kubwa; Iran haisubiri idhini ya mtu huyu au yule"... Na Witkov, mjumbe wa Trump katika Mashariki ya Kati, alisema Jumapili kwamba Washington haitakubali kiwango chochote cha urutubishaji wa uranium katika makubaliano yanayoweza kufanyika na Tehran. Witkov aliongeza katika mahojiano na mtandao wa "ABC News": "Hatuwezi kuruhusu hata asilimia moja ya uwezo wa urutubishaji. Kila kitu kinaanzia kwa mtazamo wetu na makubaliano ambayo hayajumuishi urutubishaji." Gazeti la Iran International, 2025/5/20).

4- Kwa kukataa kwa Iran kusimamisha urutubishaji na kusisitiza kwa Amerika kusimamisha, mazungumzo ya Amerika na Iran yalifikia mwisho, hata kama mwisho wa mazungumzo haukutangazwa, lakini na kutolewa kwa ripoti ya Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki mnamo 2025/6/12, taasisi ya Kiyahudi ilikimbilia katika mpango iliyoandaliwa usiku na Amerika na ilifanya shambulio la ghafla mnamo 2025/6/13 ambapo ilishambulia kituo cha nyuklia cha Iran katika eneo la Natanz, ambalo ni kiwanda kikubwa zaidi cha Iran cha kurutubisha uranium na kina vifaa 14,000 vya centrifuges, na ilifanya mfululizo wa mauaji ya viongozi wa Jeshi na Walinzi wa Mapinduzi ya Iran, pamoja na wanasayansi wa nyuklia, na ilishambulia majukwaa ya kurusha makombora, na bila kujali uhalali wa taasisi ya Kiyahudi kwa sababu za shambulio lake kwamba Iran ilikuwa imeanza tena utafiti na maendeleo ya silaha za nyuklia, kulingana na maneno ya Netanyahu (RT, 2025/6/14), lakini haya yote yanapingwa na taarifa nyingi za Iran kwamba Iran haipangi kuzalisha silaha yoyote ya nyuklia, na kwamba inakubali kiwango chochote cha udhibiti wa kimataifa ili kuhakikisha amani ya mpango wake wa nyuklia. Lakini pia ni jambo la hakika kwamba taasisi ya Kiyahudi ilikuwa ikingojea mwanga wa kijani wa Amerika ili kutekeleza, na wakati taasisi ilipoona kwamba dirisha hili limefunguliwa na mwanga wa kijani, ilianza shambulio.

5- Hivyo, haiwezekani kwa mtu mwenye akili timamu kufikiria taasisi ya Kiyahudi kufanya shambulio kama hilo bila mwanga wa kijani kutoka kwa Amerika, kwani hii haiwezekani kabisa, (Balozi wa Marekani nchini Israel, Mike Huckabee, alisema Alhamisi hii kwamba hatarajii Israel kuishambulia Iran bila kupata "mwanga wa kijani" kutoka Marekani. Arab 48, 2025/6/12). Na baada ya mazungumzo ya simu ya dakika 40 kati ya Trump na Netanyahu (afisa wa Israel alifichua kwa gazeti la "Times of Israel" Ijumaa hii kwamba Tel Aviv Washington walifanya "kampeni kubwa ya kupotosha vyombo vya habari na kiusalama", kwa ushiriki mzuri kutoka kwa Donald Trump, kwa lengo la kumshawishi Iran kwamba shambulio dhidi ya vituo vyake vya nyuklia halikuwa karibu,... Alieleza kwamba vyombo vya habari vya Israel vilipokea wakati huo uvujaji unaodai kwamba Trump alikuwa ameonya Netanyahu dhidi ya kuishambulia Iran, akielezea uvujaji huo kama "sehemu ya operesheni ya udanganyifu". Al-Jazeera Net, 2025/6/13). Inaweza kuongezwa kwa hayo yote Amerika kuipatia taasisi ya Kiyahudi silaha maalum kabla ya shambulio na zilitumika katika shambulio: (Ripoti za vyombo vya habari zilifichua kwamba Marekani kimyakimya ilisafirisha takriban makombora 300 ya aina ya AGM-114 Hellfire hadi Israel Jumanne iliyopita, kulingana na maafisa wa Marekani. Kulingana na gazeti la Jerusalem Post, maafisa hao walithibitisha kwamba Washington ilikuwa na ufahamu wa awali wa mipango ya Israel ya kushambulia malengo ya nyuklia na kijeshi ya Iran alfajiri ya Ijumaa. Pia waliripoti kwamba mifumo ya ulinzi wa anga ya Marekani baadaye ilisaidia kukatiza zaidi ya makombora 150 ya balistiki ya Iran yaliyorushwa kujibu shambulio hilo. Afisa mkuu wa ulinzi wa Marekani alinukuliwa akisema kwamba makombora ya Hellfire "yalikuwa muhimu kwa Israel," akieleza kwamba Jeshi la Anga la Israel lilitumia zaidi ya ndege 100 kuwashambulia maafisa wakuu wa Walinzi wa Mapinduzi na wanasayansi wa nyuklia na vituo vya udhibiti kuzunguka Isfahan na Tehran. RT, 2025/6/14).

6- Hivyo, utawala wa Trump ulipotosha Iran ambayo inazungumza nayo ili kufanya shambulio kutoka kwa taasisi ya Kiyahudi kuwa na ufanisi na kuathiriwa na mshtuko na hofu, na taarifa za Marekani zinaonyesha hili, yaani, Marekani ilitaka shambulio kutoka kwa taasisi ya Kiyahudi liwe kichocheo kwa Iran kutoa makubaliano katika mazungumzo ya nyuklia, ambayo inamaanisha kwamba shambulio hilo lilikuwa chombo kutoka kwa vyombo vya mazungumzo ya Marekani, na hii inaambatana na utetezi wa wazi wa Marekani kwa shambulio la taasisi ya Kiyahudi kwamba ni kujilinda, kuiunga mkono taasisi na silaha na kuendesha ndege za Marekani na mifumo ya ulinzi wa anga ya Marekani ili kuzuia majibu ya Iran, yote hayo yanafikia kuwa shambulio la Marekani lisilo la moja kwa moja, na kutoka kwa taarifa hizo za Marekani ni kauli ya Trump, wakati wa taarifa zake kwa waandishi wa habari, Jumapili, alipokuwa akielekea kwenye mkutano wa G7 nchini Kanada, kwamba ("Vita zingine haziepukiki kabla ya kufikia makubaliano".. Katika mahojiano na mtandao wa "ABC" Trump alionyesha uwezekano wa Marekani kuingilia kati kuisaidia Israel kuondoa mpango wa nyuklia wa Iran.. Arab 48, 2025/6/16).

7- Marekani inatumia vita kama chombo cha kuinyenyekeza Iran kama ilivyo katika taarifa ya awali ya Trump kwamba (baadhi ya vita haziepukiki kabla ya kufikia makubaliano), na kinachothibitisha hilo ni maelezo ya Trump kwa shambulio hili kwa kusema "Shambulio la Israel dhidi ya Iran ni bora," na alisema "Alipa Wairani fursa na hawakuitumia na walipokea pigo kali sana, akithibitisha kwamba kuna zaidi katika siku zijazo"... ABC ya Marekani 2025/6/13). Trump alisema ("Wairani" wanataka kufanya mazungumzo, lakini walipaswa kufanya hivyo hapo awali nilikuwa na siku 60, na walikuwa na siku 60, na katika siku ya 61 nilisema hatuna makubaliano"... CNN ya Marekani, 2025/6/16). Taarifa hizi ni wazi kwamba Marekani ndiyo iliyoruhusu taasisi ya Kiyahudi kuzindua uchokozi huu, bali iliielekeza kufanya hivyo. Trump aliandika kwenye jukwaa la "Truth Social": ("Iran ilipaswa kusaini "makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia" ambayo niliwaomba wasaini..." Aliongeza: "Kwa kifupi, Iran haiwezi kumiliki silaha za nyuklia. Nilisema hivyo mara kwa mara." RT, 2025/6/16). Afisa kutoka taasisi ya Kiyahudi alieleza kuhusu ushiriki wa Marekani katika kulipua tovuti ya Fordow iliyohifadhiwa chini ya ardhi nchini Iran (kwamba Marekani inaweza kujiunga na operesheni ya kijeshi dhidi ya Iran, akieleza kuwa Trump alionyesha wakati wa mazungumzo na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kwamba atafanya hivyo ikiwa ni lazima. Al-Arabiya, 2025/6/15).

8- Hivi ndivyo ilivyotokea kweli, Trump alitangaza alfajiri ya Jumapili 2025/6/22 (kulenga vituo 3 vya nyuklia vya Iran akithibitisha mafanikio ya shambulio la Marekani, na Trump alieleza kulenga maeneo ya Fordow, Natanz na Isfahan ya nyuklia akihimiza Iran kufanya amani na kumaliza vita, kwa upande wake Waziri wa Ulinzi wa Marekani Bert Hegeeset alithibitisha kwamba shambulio la Marekani limeondoa matarajio ya nyuklia ya Iran. BBC, 2025/6/22) na kisha (mtandao wa CNN ulifichua jioni ya Jumatatu kwamba Iran ilishambulia kambi ya Al-Udeid ya Marekani nchini Qatar na makombora ya balistiki ya masafa mafupi na ya kati, ikionyesha kwamba ndege za kijeshi za Marekani zilizokuwa zimeegeshwa kwenye kambi ya ndege zilihamishwa mwishoni mwa wiki iliyopita.. Shirika la habari la Reuters pia lilisema: "Iran iliarifu Marekani saa kadhaa kabla ya kuzindua mashambulio dhidi ya Qatar na pia iliarifu Doha". Sky News Arabia, 2025/6/23) Trump alisema Jumatatu ("Ningependa kuishukuru Iran kwa kutuarifu mapema, ambayo iliruhusu kutokuwa na majeruhi." Sky News, 2025/6/24).

9- Kisha baada ya mashambulio haya ya Marekani na taasisi ya Kiyahudi na majibu ya Iran ambapo hasara za mali zilikuwa kubwa pamoja na hasara za watu: (Msemaji wa Wizara ya Afya ya Iran alisema kuwa mashambulio ya Israel yalisababisha mashahidi 610 na majeruhi wengine 4,746 tangu mwanzo wa mzozo. Kulingana na Wizara ya Afya ya Israel.. idadi ya vifo tangu Juni 13 imeongezeka hadi watu 28.. BBC News, 2025/6/25), baada ya mashambulio haya, Trump kama alivyoanza kwa kuishinikiza taasisi ya Kiyahudi kufanya uchokozi dhidi ya Iran na yeye alishiriki ndani yake, anarudi sasa kutangaza kusitisha mapigano na Wayahudi na Iran wanakubali, kana kwamba Trump ndiye anayeendesha vita kati ya pande hizo mbili na pia ndiye anaihusisha! (Trump alitangaza kuanza kutumika kwa usitishaji mapigano aliyopendekeza kati ya Iran na taasisi ya Kiyahudi). (Netanyahu alisema kuwa alikubali pendekezo la Trump. Shirika la habari la Reuters pia lilimnukuu afisa mkuu wa Iran akisema kwamba Tehran ilikubali kusitisha mapigano kupitia usuluhishi wa Qatar na pendekezo la Amerika. Al-Jazeera, 2025/6/24). Hii inamaanisha kwamba vita hivi ambavyo Trump alizianzisha na kuzisimamisha zilikuwa za kufanikisha malengo yake ya kuondoa ufanisi wa silaha za nyuklia na makombora kutoka Iran (Katika hotuba yake kwa waandishi wa habari kabla ya kuondoka kwenda kuhudhuria mkutano wa kilele wa Jumuiya ya Atlantiki ya Kaskazini "NATO" huko The Hague, Trump alisema ("Uwezo wa nyuklia wa Iran umekwisha na haitajenga tena mpango wake wa nyuklia kamwe" na akaendelea "Israel haitaishambulia Iran. Usitishaji mapigano unaanza kutumika." Al-Jazeera, 2026/6/24).

10- Kuhusu mzunguko wa Iran katika mzunguko wa Amerika, ndiyo, Iran ni nchi inayozunguka katika mzunguko wa Amerika, inatafuta kufanikisha maslahi yake kupitia kufanikisha maslahi ya Amerika. Kwa hivyo ilisaidia Amerika katika uvamizi wake wa Afghanistan na Iraq na kuimarisha uvamizi wake ndani yake. Pia ilingilia kati Syria kulinda wakala wa Amerika Bashar al-Assad, na mfano kama huo huko Yemen na Lebanon. Kwa hivyo inataka kufanikisha maslahi yake katika nchi hizi na kuwa nchi kubwa ya kikanda katika eneo hilo hata kwa kuzunguka katika mzunguko wa Amerika! Lakini walisahau kwamba Amerika ikiwa itaona kwamba maslahi yake yamekwisha kutoka kwa nchi ya mzunguko na inataka kupunguza jukumu na nguvu yake, basi inafanya shinikizo la kidiplomasia, na ikiwa ni lazima kijeshi, kama inavyotokea na Iran katika mashambulio ya hivi karibuni, ili kurekebisha mdundo kwa nchi inayozunguka kwenye mzunguko. Kwa hivyo, kupitia shambulio hili ambalo lilikuwa kwa amri yake na utekelezaji wa taasisi ya Kiyahudi na kwa msaada wake, inafanya mauaji ya uongozi wa kijeshi, hasa sehemu ya nyuklia na washauri ambao walijaribu katika kipindi cha hivi karibuni kuwa na maoni katika kushughulika na taasisi ya Kiyahudi kinyume na matakwa ya Amerika, na haijali nchi hizi kwa sababu inatambua kwamba nchi hizi mwishowe zitakubali suluhisho ambalo Amerika inatengeneza!

11- Hili ndilo limeanza kuonekana waziwazi katika mpango wa Marekani baada ya kusitisha mapigano ili kukomesha silaha za kijeshi za nyuklia za Iran: (Vyanzo 4 vya kuaminika vilisema kuwa utawala wa Rais Donald Trump ulijadili uwezekano wa kuisaidia Iran kupata hadi dola bilioni 30 ili kujenga mpango wa nyuklia wa kuzalisha nishati kwa madhumuni ya kiraia, na kupunguza vikwazo na kuachilia mabilioni ya dola za fedha za Iran zilizozuiliwa, na yote hayo ni sehemu ya jaribio kubwa la kuirudisha Tehran kwenye meza ya mazungumzo, kulingana na mtandao wa CNN wa Marekani. Vyanzo viliripoti kwamba wahusika wakuu kutoka Marekani na Mashariki ya Kati walifanya mazungumzo na Wairani nyuma ya pazia hata katikati ya wimbi la mashambulio ya kijeshi dhidi ya Iran na Israel katika wiki mbili zilizopita. Vyanzo viliongeza kwamba mazungumzo haya yaliendelea wiki hii baada ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. Maafisa wa utawala wa Trump walithibitisha kuwasilisha mapendekezo kadhaa, ambayo ni mapendekezo ya awali na yaliyokuzwa na kipengele kimoja kisichobadilika ambacho hakiwezi kujadiliwa ambacho ni "kusimamisha kabisa urutubishaji wa uranium wa Iran"... Al-Arabiya, 2025/6/27).

12- Mwishowe, janga la umma huu liko katika watawala wake, kwani Iran inatishiwa kushambuliwa na haichukui hatua ya kushambulia kujitetea, na shambulio ni njia bora ya kujilinda dhidi ya Wayahudi, bali ilibaki kimya hadi vituo vyake viliposhambuliwa na wanasayansi wake waliuawa, kisha ikaanza kujibu, na vivyo hivyo kwa shambulio la Amerika. Kisha Trump anatangaza kusitisha mapigano na Wayahudi na Iran wanakubali. Baada ya hapo, Amerika inaendesha majadiliano na kuweka mapendekezo, na inasema kuhusu "kusimamisha kabisa urutubishaji wa uranium wa Iran" kwamba ni jambo lisilobadilika ambalo haliwezi kujadiliwa! Tunaonya kwamba vita hivi vinaweza kusababisha amani yoyote na taasisi ya Kiyahudi, au kuondolewa kwa silaha za Iran. Kuhusu watawala wengine katika nchi za Waislamu, hasa wale walio karibu na taasisi ya Kiyahudi, ndege za adui zinapita juu ya vichwa vyao na kushambulia nchi za Waislamu na kurudi salama bila kurushiwa risasi! Wao ni laini kwa Amerika. Wanatafsiri kujizuia na kutukuza mipaka, na wamesahau au wamejifanya kusahau kwamba nchi za Waislamu ni moja, iwe iko mbali zaidi au karibu zaidi! Na usalama wa waumini ni mmoja, na vita yao ni moja, haifai kuwatenganisha madhehebu yao mradi tu ni Waislamu. Watawala hawa ni wameharibiwa kwa kile walichomo wanafanya wanafikiri kwamba kwa kunyenyekea Amerika wataokoka, na hawajui kwamba Amerika itawatawala na kuwaondoa silaha zao ambazo zinaweza kuwa tishio kwa taasisi ya Kiyahudi, kama ilivyofanya huko Syria wakati iliporuhusu taasisi ya Kiyahudi kuharibu vituo vyake vya kijeshi, na hivyo ndivyo inavyofanya huko Iran, na kisha itawarithisha watawala hawa wadogo juu ya wadogo duniani na akhera ﴿UTAWAPATA WALE WALIOFANYA MAKOSA DHIKI MBELE YA ALLAH NA ADHABU KALI KWA SABABU YA HILA ZAO﴾ Je, wanaelewa? Au wao ni ﴿VIZIWI, BUBVU, VIPOFU, HAWAELEWI﴾, Je?

Enyi Waislamu: Mnaona na mnasikia kile ambacho watawala wenu wamewafanyia cha unyonge, udhalili na utegemezi kwa makafiri wakoloni, hata Wayahudi ambao wamepigwa na udhalili na unyonge wanazikalia ardhi iliyobarikiwa!.. Na bila shaka mnajua kwamba hakuna heshima kwenu ila kwa Uislamu na dola ya Uislamu, Khilafa Rashidah, mnangozwa ndani yake na Khalifa Rashid ambaye anapigana kutoka nyuma yake na anakingwa naye, na bila shaka itakuja kwa idhini ya Mwenyezi Mungu mikononi mwa waumini wakweli na inatimiza kauli yake ﷺ: «MTAWAPIGA VITA WAYAHUDI NA MTAWAUA..» Na kisha ardhi huangaza kwa ushindi wa Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, Mwenye uweza, Mwenye hikima...

Na mwishowe, Hizb ut-Tahrir, kiongozi ambaye watu wake hawadanganyi, inakualika kuinusuru na kufanya kazi nayo kurejesha Khilafa Rashidah tena ili Uislamu na watu wake uwe na nguvu na ukafiri na watu wake udhalilike na huo ndio ushindi mkuu; ﴿NA SIKU HIYO WATAWA FURAHIA WA

More from null

Jarida la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Al Raya sahafa

2025-11-12

Jarida la Ar-Raya:Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Enyi watu wa Sudan: Vita nchini Sudan na kwingineko vitaendelea kuwa kichocheo cha tamaa za kimataifa na mizozo yao kwa mipango yao mibaya, uingiliaji wao, na kuwapa pande zinazozozana silaha ili kuimiliki kikamilifu hadi lini?! Wanawake na watoto wenu wanateseka kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na mzozo huu wa umwagaji damu ambao hautimizi chochote ila maslahi ya nchi za Magharibi na vibaraka wao katika kudhibiti hatima ya Sudan, ambayo daima imekuwa ni kitu cha kutamaniwa kwao kwa sababu ya eneo lake na utajiri wake, hivyo ni kwa maslahi yao kuipasua na kuitawanya. Na kutekwa kwa Al-Fashir na vikosi vya Rapid Support Forces ni sehemu nyingine tu ya mipango hii, ambapo Marekani inataka kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan na kukomesha ushawishi wa Uingereza humo.

===

Lengo la ziara ya Ortagus

Nchini Lebanon!

Katika mazingira ya mashambulizi ya Marekani dhidi ya Lebanon na eneo hilo kwa mradi wa kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha, na jitihada za utawala wa Marekani chini ya uongozi wa Trump na timu yake za kuunganisha idadi kubwa ya watawala wa nchi za Waislamu kwenye makubaliano ya Abraham, ziara ya mjumbe wa Marekani, Morgan Ortagus, nchini Lebanon na nchi haramu ya Kiyahudi inakuja ikiwa na shinikizo, vitisho, na masharti ya kisiasa, kiusalama na kiuchumi kwa Lebanon, ikijua kwamba ziara hii imefanyika sambamba na ziara ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na Mkurugenzi wa Ujasusi wa Misri, ambayo inaonekana kuelekea mwelekeo uleule.

Kuhusiana na ziara hizi, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Lebanon ilisisitiza mambo yafuatayo:

Kwanza: Uingiliaji wa Marekani na wafuasi wake katika nchi za Waislamu ni kuhudumia maslahi ya Marekani na nchi haramu ya Kiyahudi, sio kuhudumia maslahi yetu, haswa kwani Marekani ndiye msaidizi mkuu wa nchi haramu ya Kiyahudi katika siasa, uchumi, fedha, silaha, na vyombo vya habari, waziwazi.

Pili: Ziara ya mjumbe sio ziara ya upande wowote kama wengine wanavyoweza kufikiria! Badala yake, inakuja katika muktadha wa sera ya wazi ya Marekani katika eneo hilo ambayo inasaidia nchi haramu ya Kiyahudi na inachangia kuiwezesha kijeshi na kisiasa, na kile ambacho mjumbe wa Marekani anatoa ni kulazimisha utawala, kuimarisha utegemezi, na kupunguza uhuru, na ni aina ya kujisalimisha na kujinyenyekeza kwa Wayahudi, na hili ndilo Mungu anawakataza watu wa Uislamu.

Tatu: Kukubali maagizo haya na kusaini makubaliano yoyote ambayo yanaimarisha udhibiti wa kigeni ni usaliti kwa Mungu, Mtume Wake, na Umma, na kwa kila mtu ambaye alipigana au kujitolea ili kuiondoa nchi hii haramu kutoka Lebanon na Palestina.

Nne: Kushughulika na nchi haramu ya Kiyahudi kwa idadi kubwa ya watu wa Lebanon, Waislamu na wasio Waislamu, ni uhalifu katika dhana ya kisheria, na hata katika sheria chanya ambayo mamlaka ya Lebanon inahukumu kwayo, au sheria ya kibinadamu kwa ujumla, haswa baada ya nchi hiyo haramu kufanya mauaji ya kimbari huko Gaza, ambayo haitasita kufanya kama hayo huko Lebanon na nchi zingine za Waislamu.

Tano: Kampeni na mashambulizi ya Marekani dhidi ya eneo hilo hayatapita, na Marekani haitafanikiwa katika jitihada zake za kuunda eneo hilo kama inavyotaka, na ikiwa ina mradi wake kwa eneo hilo, ambao unategemea ukoloni, unyanyasaji wa watu, kuwapotosha Waislamu, na hata kuwatoa kwenye dini yao kwa kuita (Dini ya Abraham), basi Waislamu, kwa upande mwingine, wana mradi wao ulioahidiwa kuonyeshwa na Mungu Mwenyezi; mradi wa Khilafah ya pili kwa mfumo wa Utume, ambao umekaribia sana, kwa idhini ya Mungu Mwenyezi, na mradi huu ndio utachora upya eneo hilo, na hata ulimwengu mzima, kwa mara nyingine tena, kama inavyothibitishwa na maneno ya Mtume ﷺ: «Hakika Mwenyezi Mungu aliniandalia ardhi, nikaona mashariki yake na magharibi yake, na hakika ufalme wa umma wangu utafikia kile nilichoandaliwa kutoka kwake» Imesimuliwa na Muslim, na nchi haramu ya Kiyahudi itaangamizwa kama Mtume ﷺ alivyobashiri katika hadithi yake: «Saa haitasimama mpaka Waislamu wapigane na Wayahudi, na Waislamu watawaua...» Imekubaliwa.

Hatimaye, Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Lebanon inaendelea kuunga mkono kukabiliana na kampeni ya Marekani na mashambulizi yake ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha kwa Lebanon na eneo hilo, na hakuna chochote kitakachoizuia kufanya hivyo, na tunaionya mamlaka ya Lebanon dhidi ya kufuata njia ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha! Na tunawasihi kujilinda kwa watu wao ili kukabiliana na hilo, na wasicheze na jambo hilo kwa kisingizio cha mipaka au ujenzi mpya na ushawishi wa mfumo wa kimataifa, ﴿Na Mwenyezi Mungu ni Mshindi juu ya jambo lake, lakini watu wengi hawajui﴾.

===

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan

Unakutana na idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, siku ya Jumatatu, Novemba 3, 2025, ulizuru idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini. Ujumbe huo ulikuwa chini ya uongozi wa Mwalimu Al-Nadhir Muhammad Hussein Abu Minhaj, mjumbe wa Baraza la Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Mwalimu Muhammad Saeed Boukeh, wajumbe wa Hizb ut-Tahrir.

Ambapo ujumbe huo ulikutana na kila mmoja wa:

Mwalimu Khalid Hussein - Mkuu wa Chama cha Muungano wa Kidemokrasia, tawi la Jalaa Al-Azhari.

Dkt. Abdullah Youssef Abu Seil - Mwanasheria na mhadhiri wa sheria katika vyuo vikuu.

Sheikh Abdul Rahim Jouda - kutoka kundi la Ansar al-Sunna.

Bw. Ahmed Muhammad - Mwandishi wa Shirika la Habari la Suna.

Mikutano hiyo ilizungumzia mada ya sasa; kuanguka kwa Al-Fashir na uhalifu uliokuwa umeambatana nayo uliofanywa na wanamgambo dhidi ya watu wa jiji hilo, na kuachwa na viongozi wa jeshi, ambao hawakutimiza wajibu wao kwa watu wa Al-Fashir na kuondoa kuzingirwa kwao, na wana uwezo wa kufanya hivyo katika kipindi chote cha kuzingirwa, na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi yao zaidi ya mashambulizi 266.

Kisha ujumbe huo uliwakabidhi nakala ya broshua ya Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan yenye kichwa: "Kuanguka kwa Al-Fashir kunafungua njia kwa mpango wa Marekani wa kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan, hadi lini tutakuwa kichocheo cha mzozo wa kimataifa?!". Majibu yao yalikuwa ya kipekee na waliomba mikutano hii iendelee.

===

Mazoezi ya "Phoenix Express 2025"

Sura kutoka sura za Tunisia kujisalimisha kwa utawala wa Marekani

Maandalizi ya Tunisia ya kuandaa toleo jipya la zoezi la majini la pande nyingi la "Phoenix Express 2025" yanakuja wakati wa mwezi wa Novemba, ambalo ni zoezi ambalo Kamandi ya Marekani ya Afrika imeanza kuandaa kila mwaka baada ya utawala wa Tunisia kuhusisha nchi kwa kusaini na Marekani, tarehe 2020/09/30, makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi, ambayo Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Mark Esper, alielezea kama ramani ya barabara itakayoendelea kwa miaka kumi.

Katika suala hili, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Tunisia ilikumbusha kwamba chama hicho kilibainisha wakati wa kusainiwa kwa makubaliano haya hatari kwamba jambo hilo linazidi makubaliano ya jadi, kwani Marekani inachora mradi mkubwa ambao unahitaji kukamilika kwa miaka 10 kamili, na kwamba ramani ya barabara, kulingana na madai ya Marekani, inahusiana na ufuatiliaji wa mipaka, ulinzi wa bandari, kupambana na mawazo ya itikadi kali, na kukabiliana na Urusi na China, na hii inamaanisha kwa dharau zote, kupunguza uhuru wa Tunisia, badala yake ni uangalizi wa moja kwa moja juu ya nchi yetu.

Taarifa hiyo ilisisitiza kwamba Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Tunisia, licha ya unyanyasaji, kukamatwa, na kesi za kijeshi ambazo vijana wetu wanakumbana nazo kwa sababu ya kusema ukweli, inathibitisha tena wito wake wa kuvunja makubaliano haya ya kikoloni yaliyolaaniwa ambayo yanalenga kuivuta nchi na nchi zote za Maghrib ya Kiislamu na kuzinyenyekeza kwa sera mbaya za Marekani, na pia ilirudia wito wake kwa watu wa nguvu na ulinzi huko Tunisia na nchi zingine za Waislamu kuwa waangalifu juu ya kile ambacho maadui wa Umma wanawafanyia njama na kuwavuta kwacho, na kwamba wajibu wa kisheria unahitaji wao kuunga mkono dini yao na kukabiliana na adui ambaye anavizia nchi yao na Umma wao, na kuinua neno la Mungu kwa kuunga mkono wale wanaofanya kazi ya kutekeleza sheria zake na kuanzisha dola yake, Dola ya Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume ulioahidiwa hivi karibuni kwa idhini ya Mungu.

===

Dharau ya Marekani kwa raia wake

Inawaacha wanawake na watoto wakiwa na njaa

Mpango wa Msaada wa Lishe ya Ziada (SNAP) ni mpango wa shirikisho ambao husaidia watu binafsi na familia zenye kipato cha chini na wenye ulemavu kupata faida za kielektroniki zinazotumiwa kununua chakula na vinywaji, isipokuwa pombe, na mimea ya kulima chakula chao wenyewe. Ripoti zinaonyesha kuwa Wamarekani milioni 42 wanategemea faida za (SNAP) kulisha wao wenyewe na familia zao. 54% ya watu wazima wanaopokea faida za chakula ni wanawake, na wengi wao ni mama wasio na waume, na 39% yao ni watoto, ambayo inamaanisha kuwa karibu mtoto mmoja kati ya watano anategemea faida hizi kuhakikisha kuwa hawapati njaa. Kufungwa kwa shirikisho pia kumesababisha baadhi ya majimbo kutafuta njia zingine za kufadhili mipango ya chakula ya bure na iliyopunguzwa katika maeneo yao ya elimu, ili watoto wanaotegemea chakula wakati wa siku ya shule wasilazimike kuishi bila chakula. Kama matokeo, maduka mengi ya chakula yaliyoenea kote nchini yanachapisha picha za rafu tupu, na kuwaomba watu kutoa chakula na kadi za zawadi za maduka ya mboga ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya chakula.

Kuhusu hilo, Idara ya Wanawake katika Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Tunapaswa kuuliza ni jinsi gani nchi tajiri zaidi ulimwenguni inaweza kupuuza ukweli kwamba mamilioni ya raia wake walio hatarini zaidi hawapati chakula cha kutosha? Unaweza kujiuliza Amerika inatumia pesa zake wapi, hata wakati wa kufungwa? Vema, badala ya kuhakikisha kuwa Wamarekani wanapata chakula cha kutosha, wanatuma mabilioni ya dola kwa nchi haramu ya Kiyahudi kuwaua Wapalestina. Ni mtawala ambaye anaona kuwa kujenga ukumbi wa sherehe za kifahari ni muhimu kuliko kitu kingine chochote, wakati manaibu wengine wanaona uwekezaji wao wa kibinafsi unachukuliwa kuwa muhimu kuliko ustawi wa watu ambao wanapaswa kuwawakilisha! Kama unavyoona, Amerika ya kibepari haijawahi kujali kutunza masuala ya raia wake, badala yake ilikuwa inajali tu kutoa msaada wa kijeshi na kifedha kwa wale wanaowanyima watoto kote ulimwenguni haki yao ya usalama, chakula, makazi, na elimu, ambazo ni mahitaji ya msingi. Kwa hivyo, inawaacha watoto huko Amerika pia wakiteseka na njaa na ukosefu wa usalama, na wanakosa elimu sahihi na huduma ya afya.

===

«Muislamu yeyote yule ni haramu kwa Muislamu mwenzake; damu yake, mali yake, na heshima yake»

Kwa kila Muislamu, kwa kila afisa na askari, kwa kila mtu anayemiliki silaha: Hakika Mwenyezi Mungu ametupa akili ili tufikiri kwayo, na ametulazimisha kuitumia matumizi sahihi, kwa hivyo mtu asitende au kufanya kazi yoyote au kutamka neno lolote kabla ya kujua hukumu yake ya kisheria, na kujua hukumu ya kisheria kunahitaji kuelewa hali halisi ambayo hukumu ya kisheria inataka kuletwa, kwa hivyo lazima Muislamu awe na ufahamu wa kisiasa, ili aweze kufahamu mambo kama yalivyo, na asifuate mipango ya makafiri wakoloni ambao hawatutakii mema sisi wala Uislamu, na wanafanya bidii kwa kila wawezalo kwa nguvu, hila na akili kutupasua vipande vipande na kuudhibiti nchi yetu na kunyakua rasilimali zetu na utajiri wetu, kwa hivyo Muislamu anawezaje kukubali kuwa chombo mikononi mwa makafiri hao wakoloni, au mtendaji wa maagizo ya vibaraka wao?! Je, anatamani kitu kidogo cha starehe za dunia hii zinazopita na anapoteza Akhera yake na anakuwa miongoni mwa watu wa Motoni milele humo, amelaaniwa na kufukuzwa kutoka kwa rehema za Mungu? Je, Muislamu anakubali kumridhisha mtu yeyote yule miongoni mwa wanadamu viumbe dhaifu huku anamkasirisha Mungu Mwenyezi ambaye mikononi mwake iko dunia na Akhera?!

Hakika Hizb ut-Tahrir inawasihi kuinua kiwango cha ufahamu wa kisiasa, kuzingatia hukumu za Mungu Mwenyezi, na kufanya kazi nayo ili kuhukumu kwa yale ambayo Mungu ameyateremsha, ili kuwaondoa mikono ya makafiri wakoloni na vibaraka wao, na kushindwa mipango yao katika nchi yetu.

===

Ninyi ndio mnaowaweka Waislamu katika njaa

Ewe Masoud Pezeshkian!

Chini ya kichwa hiki, Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Iran imetangaza kufilisika kwa benki kubwa zaidi ya kibinafsi nchini humo, ambayo ni benki ya (Ayandeh), na benki hii ina matawi 270 nchini Iran, baada ya madeni kuongezeka hadi dola bilioni tano, na cha kushangaza ni kukosoa kwa rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, kushindwa kwa utawala, akisema: "Tuna mafuta na gesi, lakini tuna njaa"!

Taarifa hiyo ilisisitiza: Mwenye dhamana ya kushindwa huko kwa utawala ambako rais wa Iran anazungumzia ni rais mwenyewe, kwa nini watu wa Iran wana njaa - Ewe Masoud Pezeshkian - na mna mafuta, gesi, na utajiri mwingine na madini? Je, siyo matokeo ya sera zenu za kijinga? Je, siyo kwa sababu ya umbali wenu kutoka kwa kuhukumu kwa Uislamu? Na vivyo hivyo, inasemwa kwa nchi zingine za Waislamu, watawala wajinga ndani yake wanapoteza utajiri mwingi wa Umma, na wanawezesha makafiri wakoloni kupata utajiri huo, na wananyima Umma utajiri huo, kisha mmoja wao anakuja kuhalalisha sababu ya njaa kwa kusema kwamba ni kushindwa kwa utawala!

Hatimaye, taarifa hiyo kwa vyombo vya habari iliwahutubia Waislamu: Ujinga wa watawala hawa ambao wanachukua masuala yenu umeonekana kwa kila mwenye macho na ufahamu, na hawafai kuchukua masuala hayo, umefika wakati wa kuwazuia, kwani hii ndiyo hukumu ya mjinga; kumzuia kutumia pesa na kumdhibiti, na mumpatie Bay'ah Khalifa mmoja anayewahukumu kwa sheria ya Mungu Mwenyezi, na afute mfumo wa riba katika nchi yenu ili Mola wenu akuridhieni na Mtume Wake ﷺ, na arejeshe utajiri wenu ulionyaganywa, na arejeshe heshima yenu na fahari yenu, na hapa kuna Hizb ut-Tahrir, mwanzilishi ambaye watu wake hawasemi uongo, anawasihi kufanya kazi nayo ili kuanzisha Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume.

 </