2025-07-02
Jarida la Ar-Raya: Matukio Mbalimbali ya Ar-Raya – Toleo la 554
Hakika Hizb ut Tahrir inaunyoosha mkono wake kwa Ummah na majeshi yake yote kufanya kazi nayo ili kusimamisha Khilafah Rashidah ya pili kwa njia ya Utume, kwani imeandaa maandalizi yake, basi fanyeni kazi nasi ili huenda tukaanza mwaka huu badala ya kuadhimisha kumbukumbu ya kubomolewa kwake, tuanze kusherehekea kila mwaka kumbukumbu ya kusimamishwa kwake, InshaAllah.
===
Kwa nini wanathubutu
Mayahudi na Wahindu
dhidi ya Waislamu?!
Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Bangladesh, ilifanya, Ijumaa 20/06/2025, baada ya Sala ya Ijumaa, misimamo na maandamano makubwa katika idadi ya misikiti katika mji mkuu Dhaka na mji wa Chittagong, kulaani mauaji yanayoendelea huko Gaza, ya kuzingirwa, njaa na mauaji ya kimbari, pamoja na uchokozi wa hivi karibuni wa Kiyahudi dhidi ya Iran. Miongoni mwa yaliyokuja katika hafla hizo, kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na ofisi ya habari ya Hizb ut Tahrir/ Wilaya ya Bangladesh:
Licha ya hasira na mivutano ya dunia, lakini kwa msaada wa moja kwa moja kutoka Amerika, Kiyahudi kilicholaaniwa kinaendelea kufanya mauaji ya kimbari ya kikatili zaidi katika historia dhidi ya Waislamu huko Gaza kwa miezi ishirini, ambapo nyumba na hospitali zimebomolewa, waandishi wa habari, madaktari na wafanyikazi wa misaada wameuawa, na Gaza imezingirwa, watu wake wanapewa njaa na kufyatuliwa risasi wenye njaa kwa kisingizio cha kusambaza misaada!
Pia alisema: Usaliti wa watawala vibaraka wa Kiislamu umeongeza ujasiri wa Amerika, na sasa inapanua vita vyake dhidi ya Waislamu. Mmeona kwa macho yenu ndege za Kiyahudi zinazovuka anga la nchi za Kiislamu, zikishambulia Iran, na kurudi salama bila kupigwa risasi moja kutoka Syria, Iraq, Misri, Uturuki au kwingineko! Bali hali imefikia watawala wasaliti wa Jordan kuangusha makombora ya Iran katika anga la nchi yao, kuutetea Kiyahudi! Walishambulia na kurudi ... na watawala wanatazama kwa ukimya wa waoga! Watawala hawa walipuuza au walikusudia kupuuza matokeo mabaya ya unyenyekevu huu.
Kuhusu jukumu la kichwa cha uovu, Amerika, taarifa kwa vyombo vya habari ilisema: Amerika imekabidhi jukumu chafu kwa kila mmoja wa Kiyahudi katika nchi za Kiarabu, na Wahindu wenye msimamo mkali nchini India, ili wawe mikono yake dhidi ya Waislamu, kwa sababu inajua kwamba Mayahudi na washirikina ni maadui wakubwa wa Waislamu, kama Mwenyezi Mungu alivyosema: ﴿Hakika utawakuta watu walio na uadui mkubwa zaidi kwa wale walio amini ni Mayahudi na wale walio shiriki﴾, na wakati majeshi ya Waislamu yalipoanza kuwatisha makafiri walioshindwa, na kukaribia ushindi, watawala vibaraka waliingilia kati kwa maagizo ya Amerika kusimamisha wimbi la ushindi, kukandamiza ummah, na kusaliti damu ya mashahidi. Na hakuna kinachoonyesha kiwango cha utegemezi wa watawala hawa kuliko matamshi ya Trump mwenyewe kwenye jukwaa lake la ukweli wa kijamii aliposema: "Iran na (Israeli) zitafikia makubaliano, na amani itapatikana, kama vile nilivyoilazimisha India na Pakistani kufikia makubaliano ... Mawasiliano na mazungumzo yanaendelea sasa".
Kuhusu kufichuliwa kwa watawala wa Kiislamu na aibu yao mbele ya Ummah, taarifa ilisema: Vinyago vimeanguka kutoka kwa nyuso za vibaraka ambao wanatekeleza mipango ya Magharibi ya kikoloni. Na Ummah wa Kiislamu leo unawaita wanawe waaminifu kutoka kwa maafisa na askari kulikomboa Palestina iliyobarikiwa, Kashmir, Arakan, na kila ardhi iliyonyakuliwa, nao wanaitikia wito wa Ummah kwa idhini ya Mungu. Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ alisema: «Hakika Imamu ni ngao, anapiganwa nyuma yake na anahofiwa naye» Sahihi Muslim, kwa hivyo Khalifa pekee ndiye kiongozi wa kweli wa Ummah, na chini ya bendera yake mikono ya Amerika itakatwa, na Kiyahudi na Uhindu wa India watashindwa, kwa idhini ya Mungu. Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Hawatakudhuru isipokuwa kwa maudhi tu, na wakikupigeni vita watakugeuzieni migongo, kisha hawatasaidiwa﴾.
Taarifa kwa vyombo vya habari ilihitimisha hotuba yake kwa Waislamu: Sisi katika Hizb ut Tahrir tunatoa wito kwa Ummah kuungana kwa lengo la kusimamisha Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume, dola tukufu ambayo itakusanya umoja wake, na kuwataka wanawe katika majeshi kutoa nusra kwa Hizb ut Tahrir ili kusimamisha Khilafah. Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Amri ni ya Mwenyezi Mungu kabla na baadae, na siku hiyo Waumini watafurahi * kwa nusra ya Mwenyezi Mungu, humpa ushindi amtakaye, naye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu﴾.
===
Hizb ut Tahrir kiongozi ambaye hasemi uongo kwa watu wake
anakualika kumnusuru na kufanya kazi naye ili kurejesha Khilafah Rashidah
Hakika hawa Ruwaibidhah - watawala wa Waislamu - watatoweka na dola ya Kiislamu, Khilafah Rashidah, itarudi kuwa dola ya kwanza ulimwenguni ikisambaza mema ndani yake kwa idhini ya Mungu, na mapigano dhidi ya Mayahudi na kuondoa uvamizi wao yatakuwepo kwa idhini ya Mungu, kwani Mkweli Mwaminifu ﷺ alisema katika Musnad Ahmad kutoka kwa Hudhaifa: «... Kisha itakuwepo Khilafah kwa njia ya Utume» vile vile Bukhari amepokea kutoka kwa Abd Allah bin Umar, Mwenyezi Mungu awaridhie wote wawili, alisema: Nilimsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu ﷺ akisema: «Mayahudi watakupigeni vita na mtawashinda..» na pia Muslim amepokea kwa tamko kutoka kwa Ibn Umar kutoka kwa Mtume ﷺ alisema: «Hakika mtawapiga vita Mayahudi na hakika mtawaua..» Na kisha ardhi huangaza kwa nusra ya Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu, Mwenye enzi, Mwenye hikima. ﴿Hakika katika hilo kuna ukumbusho kwa mwenye moyo au akatii akisikiliza naye ni shahidi﴾.
Na hakika Hizb ut Tahrir, kiongozi ambaye hasemi uongo kwa watu wake, anakualika kumnusuru na kufanya kazi naye ili kurejesha Khilafah Rashidah tena, Uislamu na watu wake wapate nguvu, na ukafiri na watu wake wanyenyekee, na hiyo ndiyo ushindi mkuu ﴿Na siku hiyo Waumini watafurahi * kwa nusra ya Mwenyezi Mungu, humpa ushindi amtakaye, naye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu﴾.
Amir wa Hizb ut Tahrir, mwanachuoni mtukufu, Ata bin Khalil Abu Rashta
===
Dola ya Kihindu inaendelea na uchokozi na uzushi wake
dhidi ya Hizb ut Tahrir na vijana wake
Mnamo Juni 14, 2025, Wakala wa Kitaifa wa Upelelezi ulifanya uvamizi ulioratibiwa katika maeneo matatu katika jiji la Bhopal, jimbo la Madhya Pradesh, na maeneo mengine mawili huko Jalaur, jimbo la Rajasthan, kama sehemu ya kile kinachoitwa "kesi ya Hizb ut Tahrir". Wakala huo ulidai kuwa operesheni hii ililenga kukusanya ushahidi zaidi dhidi ya chama, na ulidai kuwa ulikamata "vifaa vya kidijitali na nyenzo zinazolaani chama", ambazo mara nyingi ni vitabu na vifaa vya uandishi. Kabla ya uvamizi huu, kitengo cha kupambana na ugaidi cha jimbo la Jharkhand kilikuwa kimewakamata watu wawili kuhusiana na kesi hiyo hiyo. Serikali ya India ilikuwa imetoa uamuzi usio wa haki wa kuipiga marufuku Hizb ut Tahrir mnamo Oktoba 10, 2024, kwa madai kwamba inafanya kazi ya kuanzisha Khilafah ya kimataifa kupitia kile wanachoelezea kwa uwongo kama (ugaidi na itikadi kali).
Ar-Raya: Wakala wa Kitaifa wa Upelelezi umeshindwa kuthibitisha tuhuma zozote za ugaidi dhidi ya Hizb ut Tahrir au vijana wake. Ukweli ni kwamba serikali za India zilizopita, pamoja na serikali ya sasa, zimelenga kimfumo Waislamu, makabila, na tabaka zilizotengwa (Dalit) kupitia sera za ubaguzi wa rangi na sheria kandamizi. Sheria kama vile sheria ya uchochezi, sheria ya kuzuia shughuli haramu, sheria ya usalama wa taifa, na sheria ya vikosi vya jeshi, zimetumika kunyamazisha wapinzani na kuwatisha Waislamu, na hivyo kuimarisha hali ya woga na kuwafanya Waislamu kuwa raia wa daraja la pili. Serikali tawala ya sasa imeongeza mara dufu mbinu hii, imeweka vikwazo kwa haki za kikatiba, na imewataka Waislamu kuthibitisha uaminifu wao kwa njia ya kupita kiasi na ya kudhalilisha. Hata hivyo, Waislamu wa India bado wamesimama imara, wakichota nguvu zao kutoka kwa imani yao na urithi wao wa kihistoria, wakikataa kujisalimisha kwa simulizi za kitaifa zinazogawanya.
===
Enyi Waislamu:
Adui yenu anajua ukubwa wenu zaidi yenu
Enyi Waislamu, hakika adui yenu anaogopa kwamba baadhi yenu watamiliki silaha inayomtishia, adui yenu anajua ukubwa wenu wa kweli, na anajua siri ya nguvu yenu, kwamba ipo katika itikadi yenu na kanuni yenu, itikadi yenu ambayo imewafanya kuwa Ummah bora uliotolewa kwa watu, itikadi yenu ambayo imewafanya mashahidi kwa watu kwa kubeba ujumbe wa Uislamu kwao, itikadi yenu ambayo imeamrisha umoja wenu, na kufanya vita yenu moja, na amani yenu moja, itikadi yenu ambayo imeunganisha uwepo wenu na Mwenyezi Mungu, mnamtegemea, na mnamuomba msaada, na kwake mnamshinda adui yenu.
Enyi Waislamu: Msemaji wenu atasema: Hakika watawala wenu wanawazuia kupigana na Jihadi, na kwamba majeshi katika nchi yenu yanahusiana na amri za watawala hao, na hii inamaanisha kuwa mmejua sababu ya hali ambayo mko nayo, na mmejua sababu ya kushindwa kwenu mbele ya kundi dogo la Mayahudi waovu, na mmejua sababu ya utawala wa nchi za Magharibi makafiri wakoloni juu ya nchi yenu, basi mishale yenu ielekezwe kwa watawala hao Ruwaibidhah, na juhudi zenu ziungane katika kuwaondoa, na kumsimika Khalifa mmoja atakayetawala kwa kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah za Mtume wake ﷺ, na hii ndiyo Hizb ut Tahrir, kiongozi ambaye hasemi uongo kwa watu wake, mbebaji wa mradi wa Khilafah, anakuombeni msaada kutimiza umoja wenu, kumridhisha Mola wenu, na kurejesha heshima yenu na utukufu wenu, basi mnusuruni.
===
Mkataba wa Younis - Tariq huko London
lengo lake ni kuhifadhi utawala wa Amerika
Mnamo Juni 13, 2025, Waziri Mkuu wa muda, Dk. Younis, anayeishi London, alikatisha tamaa matumaini ya watu wa Bangladesh kwa kufanya makubaliano ya kisiasa na Tariq Rahman, Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Kitaifa cha Bangladesh. Watu wa Bangladesh hawajasahau historia nyeusi ya watawala na ufisadi uliofanywa na tabaka tawala katika Chama cha Kitaifa cha Bangladesh.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na ofisi ya habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Bangladesh imeionya serikali ya mpito na mrengo wa kisiasa kwamba watu wa Bangladesh hawatawahi kuvumilia njama yoyote ya kuimarisha utawala wa nchi za kikafiri na washirikina juu ya ardhi hii ya Kiislamu. Na wanapaswa kujifunza somo kutokana na kuanguka kwa mtawala anayechukiwa Hasina, Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Wale wanao wachukua makafiri kuwa marafiki badala ya Waumini, je, wanatafuta utukufu kwao? Hakika utukufu wote ni wa Mwenyezi Mungu﴾ Kwa hivyo, serikali ya mpito lazima iandae mazingira sahihi ya kisiasa ili kufikia makubaliano ya kisiasa kulingana na Uislamu, maslahi ya watu na kulinda uhuru wa nchi, ili kuonyesha na kutimiza matumaini na matarajio ya watu. Mwenyezi Mungu anasema: ﴿Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu wawili, na mcheni Mwenyezi Mungu ili mpate kurehemewa﴾ Kwa hivyo, lazima tuunganishe safu zetu kwa kusahau tofauti zetu, na kuwakataa makafiri na washirikina.
Enyi watu: Msiumwe tena kutoka shimo lile lile la mfumo wa kilimwengu kibepari, kupitia makubaliano ya kisiasa na kugawana madaraka kati ya tabaka tawala zinazounga mkono Magharibi, haswa Amerika ... Ni lazima kuwe na umoja wa kisiasa ili kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume, ihifadhi maslahi ya Ummah wa Kiislamu.
===
Chanzo: Jarida la Ar-Raya