Gazeti la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 566
September 23, 2025

Gazeti la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 566

Al Raya sahafa

2025-09-24

Gazeti la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 566

Enyi Waislamu: Umefika wakati wa kukaza mambo yenu na kufanya uamuzi wenu wenyewe mbali na hao watawala mafidhuli, ambao wamewekwa na kafiri mkoloni juu ya shingo zenu, hawawaheshimu ila na ahadi, wala hawajali masuala yenu, wala kuhifadhi maslahi yenu, na imewalazimu kuwavua, na kumweka bay'ah khalifa atakayewahukumu kwa kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna za Mtume wake, na aendeshe majeshi kuwanusuru Waislamu, na kuwarejeshea heshima yenu na hadhi yenu, na hamna mbele yenu ila Hizb ut-Tahrir, mwenye mradi wa uamsho wenu kwa msingi wa Uislamu, basi msaidieni Mwenyezi Mungu ili akusaidieni na athibitishe nyayo zenu.

===

Taasisi ya Kiyahudi na Wanaoiunga mkono

Ndio Tatizo la Ulimwengu

Vyombo vya habari viliripoti kauli ya Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu Gaza, ambayo anasema: "Gaza ni tatizo kubwa kwa (Israel) na Mashariki ya Kati". Na hatukumsikia yeyote kati ya watawala mafidhuli katika nchi za Waislamu akijibu maneno yake, na kumwambia: Kwamba taasisi ya Kiyahudi inayokalia ardhi kwa mabavu ndio tatizo kubwa katika nchi za Waislamu, na nyinyi ndio mnaoipa vifaa vya kivita na msaada wa kisiasa na kiuchumi; kwa hivyo nyinyi ndio tatizo kubwa katika ulimwengu mzima, kwa sababu itikadi yenu ya kibepari ndio sababu ya dhiki ya ulimwengu, na nyinyi ndio sababu ya kuzigawa nchi za Waislamu katika nchi dhaifu na taasisi bandia zinazowategemea.

Haya yalikuja katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na ofisi ya habari kuu ya Hizb ut-Tahrir, na taarifa hiyo iliongeza: Rais huyu jeuri hangeweza kutoa kauli kama hiyo lau angempata mtu mmoja tu katika watawala wa Waislamu akijibu kauli yake, na aendeshe majeshi kuiondoa taasisi ya Kiyahudi iliyoharibika, na kumrudisha huyu anayefumbia macho ukweli katika akili yake na usawa wake, na kwamba taasisi ya Kiyahudi ndio iliyokalia ardhi iliyobarikiwa, na ndio inayowatesa watu wake vibaya, bali imefikia hatua ya kiburi kwa nchi jirani na za mbali pia.

Na ikaendelea: Tatizo la nchi za Kiislamu lilianza tangu kubomolewa kwa dola la Khilafah mwaka 1924 BK, na kugawanywa kwake katika nchi ndogo na dhaifu, zinazodhibitiwa na makafiri wakoloni, kisha kukafuata kukaliwa kwa mabavu kwa Palestina na kuanzishwa kwa taasisi ya Kiyahudi iliyoharibika humo, kwa msaada wa Uingereza, kisha uangalizi wa Amerika, na usaliti wa watawala wa Waislamu, ambao waliimarisha taasisi ya Kiyahudi, kisha wakaikinga na kuwazuia Waislamu wasiikomboe Palestina, ndio hali ya watawala mafidhuli katika nchi zetu; baadhi yao wanaikinga taasisi ya Kiyahudi, na baadhi yao wamefanya nayo makubaliano na kubadilishana uhusiano wa kidiplomasia hadharani, na baadhi yao wameanzisha nayo uhusiano kwa siri, na baadhi yao wanailalamikia kwa Baraza la Usalama inapoishambulia ardhi yake na uhuru wake kwa ndege zake, na baadhi yao wanakemea mapambano ya Waislamu dhidi yake huko Palestina, na baadhi yao wanashiriki kuwazunguka watu wa Gaza, na baadhi yao wameingia katika makubaliano ya Ibrahimu, na wote wanazifunga majeshi katika kambi zao na wanayazuia kuikomboa Palestina, na wanawazuia watu wao hata wasieleze kukataa kwao mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza, hakika ni uovu ulioje wanaoufanya!

Na taarifa kwa vyombo vya habari ilihitimisha kwa kusema: Na sisi katika ofisi kuu ya habari ya Hizb ut-Tahrir tunampongeza Trump na viongozi wa taasisi ya Kiyahudi iliyoharibika, kwamba hali hii haitaendelea, na mmeyaona mabadiliko katika maoni ya umma wa kimataifa kuhusu uhalifu wa taasisi ya Kiyahudi huko Gaza, na umma wa Kiislamu umeelewa suala lake, na unaenda kwa hatua za haraka kuelekea kuanzisha dola yake, dola ya Khilafah ambayo inajaza mioyo yenu hofu na uoga, na wakati huo hamtasikia jibu kutoka kwa khalifa wa Waislamu; bali mtaona majeshi makubwa ambayo mwanzo wake uko kwenu na mwisho wake uko kwake, na Hizb ut-Tahrir unaongoza umma kwa hatua za haraka kufikia lengo hili, basi furahieni kwa yale ambayo yanawaudhi, na hakika kesho inamngojea anayeingojea.

===

Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan

Watekeleza Msimamo Mashariki ya Nile

Vijana wa Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan mashariki ya Nile siku ya Jumatano 25 Rabi'ul Awwal 1447 Hijria sawa na 17 Septemba 2025 BK baada ya swala ya adhuhuri, katika msikiti mkubwa katika soko la sita Al-Wahda, walifanya msimamo ambao ndani yake kulikuwa na mabango yanayowataka Waislamu kusimama kwa nguvu, kuzuia mpango wa kuigawa Sudan kwa kuitenga Darfur.

Na katika msimamo ilisomwa hotuba iliyowataka Waislamu kutekeleza wajibu wao, wa kuzuia mpango huo, na msimamo ulikumbana na maingiliano kutoka kwa hadhira iliyokuwepo, ambapo idadi yao walisimama kusikiliza hotuba.

===

Wasaidieni Watu wa Gaza

Kabla Mayahudi Hawajawafutilia Mbali Kabisa

Taasisi ya Kiyahudi inaendeleza vita vya mauaji ya halaiki dhidi ya Ukanda wa Gaza ikilenga kwa mashambulizi ya anga na makombora makali sehemu mbalimbali za Ukanda huo, ambayo husababisha vifo vya makumi ya mashahidi na majeruhi kila siku. Na kwa wiki chache, inazidisha mashambulizi yake dhidi ya mji wa Gaza ulijaa watu wake na wakimbizi kutoka kaskazini mwa Ukanda huo, ikiwa inajiandaa kuukalia tena, ambapo inalenga shule na vituo vya makazi, na inafanya operesheni kubwa za kulipua nyumba za makazi nzima, na kuharibu majengo ya makazi ikifuatiisha kwa kuwapa watu maonyo ya ulazima wa kuondoka kuelekea kusini mwa Ukanda huo.

Enyi Waislamu: Mayahudi wamezidi katika uovu wao na wanaendelea katika kutekeleza mipango yao ya kuwaua idadi kubwa ya watu wa Gaza na kuwahamisha wale waliosalia kati yao, ili waendelee katika kufanikisha ndoto zao za kitorati za kuanzisha dola yao kutoka Nile hadi Frati kama viongozi wao wanavyotangaza kwa ujasiri wote, nao wanaitegemea Amerika na rais wake mhalifu jeuri Trump, bali ukatili wao na uhalifu wao umevuka ardhi iliyobarikiwa hadi kufikia Syria, Lebanon, Yemen, Iran na Qatar, na kamba inaendelea kubururwa, nao katika uhalifu wao huu wanategemea usaliti na njama za watawala wenu haswa watawala wa nchi zinazowazunguka ambao wanawaikinga na wanawabana watu wa Gaza na wanazuia harakati yoyote ya kuwanusuru, basi hadi lini kukaa kimya huku dhidi ya watawala hawa wasaliti wahalifu?! Je, haujafika wakati wa kuhamasisha wivu, hamasa na ujasiri katika mioyo na akili za watiifu katika majeshi ya Waislamu?! Je, hamuwahisi ndugu zenu kabla hawajafutiliwa mbali kabisa?! Je, hamuwaokoi na kujiokoa kabla haijawashukia hasira ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake kutokana na ukimya huu na udhalilishaji?! Mwenyezi Mungu anasema: ﴿NA MKIGEUKA YEYE ATALETA WATU WENGINE WASIO KUWA NYINYI, KISHA HAWATAKUWA MFANO WENU﴾.

===

Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan

Yakutana na Sheikh Farouk Al-Hajj Abdullah Sheikh Dafa Allah

Jumanne 2025/9/16 ujumbe wa kamati ya mawasiliano kuu ya Hizb ut-Tahrir katika wilaya ya Sudan, kwa kushiriki kwa Ustadh Abdullah Hussein mratibu wa kamati, na Sheikh Abdul Qadir Abdul Rahman mwanachama wa Hizb, walikutana na Sheikh Farouk Al-Hajj Abdullah Sheikh Dafa Allah, katibu wa uaminifu wa Da'wah na Utamaduni wa kabila la Al-Kalaklat.

Mkutano huo ulizungumzia mpango wa nchi za Magharibi kwa ujumla, na haswa Amerika, katika juhudi za kugawanya lililogawanyika katika Sykes-Picot mpya na mipaka ya damu, na huu ndio mpango wake nchini Sudan baada ya kuitenga kusini kwake, inataka kuitenga Darfur, na kinachotakiwa kutoka kwa watu wote wa nchi ni kufanya kazi ya kushindwa mpango huu, haswa wanazuoni ambao wana ulazima wa kusema ukweli, na kuwafahamisha watu kuhusu mpango huu na ulazima wa kufanya kazi kwa ajili ya umoja wa nchi, bali na kufanya kazi ya kuziunganisha nchi za Waislamu kwa ujumla kwa kumpa bay'ah khalifa wa Waislamu.

Sheikh Farouk Al-Hajj Abdullah alilishukuru ujumbe huo kwa ziara hii akisema, Mwenyezi Mungu abariki juhudi na jitihada za Hizb ut-Tahrir, na alimrehemu Sheikh Ali Saeed msemaji mkuu wa zamani wa Hizb, na alisisitiza mawasiliano na ushirikiano katika yale yanayoboresha hali ya umma, na alitupatia maono ya uaminifu wa Da'wah na Utamaduni kwa ajili ya kuyasoma na kuyajibu.

===

Watoto wa Gaza wenye Ulemavu

Ndio Waathirika Zaidi wa Vita Wanateseka

Vita vya maafa vinavyoendelea huko Gaza tangu tarehe saba ya Oktoba 2023 vimeathiri nyanja zote za maisha humo, za watu, miti, mawe na rasilimali, na kifo na uharibifu vimeenea kila mahali.

Na kwa mujibu wa kile ambacho kamati teule ya Umoja wa Mataifa iliripoti hivi karibuni kwamba iliarifiwa kuwa watu 157,114 kati ya tarehe saba ya Oktoba 2023 na tarehe 21 Agosti mwaka huu wamepata majeraha, 25% kati yao wanakabiliwa na hatari ya kupata ulemavu ambao utaendelea maisha yao yote. Na ilitangaza kuwa takriban watoto 40,500 walipata majeraha yanayohusiana na vita katika kipindi cha miaka miwili ambayo imepita tangu kuzuka kwa vita, na kwamba zaidi ya nusu yao wanasumbuliwa na ulemavu. Hivyo basi zaidi ya watoto 21,000 huko Gaza wamekuwa wenye ulemavu!!

Idara ya wanawake katika ofisi kuu ya habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Yote haya na zaidi yanatendeka mbele ya masikio na macho ya ulimwengu mzima na taasisi na mashirika yake ambayo yanadai ubinadamu na haki, na haizidi kile wanachokifanya maandamano ya kimaumbo hapa, au kuwasilisha ripoti kule, au kujaribu kuingiza misaada ambayo haitoshelezi na haiondoi njaa! Na watawala wa Waislamu wamejishughulisha na kuhifadhi viti vyao na viti vya enzi vyao juu ya vipande vya miili na damu za Waislamu na mateso yao haswa huko Gaza, wamesahau wameghafilika na kauli yake ﷺ: «HAJALINDA MTU MUSLIMU KATIKA MAHALI AMBAO UTAKIIUKWA UTUKUFU WAKE NA KUPUNGUNZWA HESHIMA YAKE ILA MWENYEZI MUNGU ATAMTOSA KATIKA MAHALI ANAPOPENDA USHINDI WAKE NA HAJAMSIDIA MTU MUSLIMU KATIKA MAHALI AMBAO UTAPUNGUNZWA UTUKUFU WAKE NA KUTOSWA HESHIMA YAKE ILA MWENYEZI MUNGU ATAMSIDIA KATIKA MAHALI ANAPOPENDA USHINDI WAKE», na hakika siku ya kulipiza kisasi kutoka kwao inakaribia kwa idhini yake Mwenyezi Mungu.

===

Amerika Inasisitiza Kuondoa Mapinduzi Kutoka Yaliyomo Yake

Na Kuiimarisha Mfumo wa Kisekula nchini Syria

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Syria Geir Pedersen, siku ya Jumamosi 9/6 katika Damascus, alikutana na Waziri wa Mambo ya Nje katika Serikali ya Mpito nchini Syria Asaad Al-Shaibani, na alijadili naye mchakato wa mpito wa kisiasa nchini humo na mwelekeo wake wa kikanda na kimataifa.

Pia mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa alisisitiza kwamba Umoja wa Mataifa utaendelea kuunga mkono serikali na watu wa Syria ili kufikia amani na utulivu wa kudumu, kupitia mchakato wa mpito wa kisiasa jumuishi, wa uwazi na wa kuaminika, kwa mujibu wa azimio la Baraza la Usalama nambari 2254 la mwaka 2015. (Shirika la Habari la Hawar)

 Ar-Raya: Hakika huyu muovu Pedersen alijitahidi sana katika miaka ya hivi karibuni ya mapinduzi kuokoa serikali katili na kuihuisha na kutekeleza suluhisho la kisiasa la Amerika, lakini kwa fadhila za Mwenyezi Mungu kisha kwa bidii ya wakweli kutoka kwa wana wa mapinduzi alikatishwa tamaa na alishindwa katika makusudio yake, na watu wa mapinduzi waliweza kumuondoa Bashar licha ya Amerika na washirika wake.

Na leo Pedersen anarudi tena kugonga milango iliyofungwa na anatumia vibaya udhaifu wa utawala mpya, na kujisalimisha kwake kwa Amerika na kutekeleza mipango yake kwa kuiacha mfumo wa kisekula ukiendelea kutumika nchini Syria, na kuijenga upya jeshi na usalama ili kulinda maslahi ya Amerika, na ili Syria iendelee kuwa koloni la kisiasa la Amerika, na chini ya mfumo wa kimataifa.

Kwa hivyo ni lazima kwa watu wetu waasi katika Sham kuwa waangalifu na hila zinazowazunguka, na watambue kwamba hakuna ukombozi kwao ila kwa kutumia sheria ya Mwenyezi Mungu na kukamilisha mapinduzi kwa utawala wa Uislamu katika dola ya Khilafah Rashidah ya pili kwa njia ya Utume, na katika hilo kuna utukufu wa dunia na neema ya akhera kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.

===

Uislamu Bila Mengineyo

Unaweza Kuwachanganya Watu Katika Umma Mmoja

Hakika Uislamu mkuu ndio pekee katika historia ya mwanadamu ambao ulichanganya watu, rangi na makabila tofauti katika umma mmoja, haukuwa umefungwa katika Madina bali ulienea katika kisiwa chote na yalifanyika mapinduzi ya Kiislamu kwa ajili ya kueneza Uislamu, hivyo Waislamu waliifungua Iraq, na ilikuwa inakaliwa na Wakristo, Wamazdakia na Wazoroasta kutoka kwa Waarabu na Waajemi, na waliifungua Uajemi na ilikuwa inakaliwa na Wajemi, Mayahudi na Warumi, na waliifungua Sham na ilikuwa mkoa wa Kirumi unaokaliwa na Wasiria, Waarmenia, Warumi na Waarabu, na waliifungua Afrika Kaskazini ambapo kuna Waberber, na waliifungua Sindh, Khwarazm, Samarkand na Andalusia, na wakawachanganya watu hao wote katika umma mmoja, hakuna ubaguzi kati yao, hivyo nuru ya Uislamu ilienea katika pembe za dunia katika kipindi kifupi; hiyo ni kwa sababu amri za Uislamu zinahitaji kuangalia raia kwa mtazamo wa kibinadamu, sio mtazamo wa kibaguzi, au wa kimadhehebu, au wa kimashirika, kwani hukumu za Uislamu zilitumika kwa wote, hivyo watu wote wakawa raia wa dola ya Kiislamu hakuna tofauti kati ya Muislamu na asiye Muislamu wala hakuna anayemdhulumu mwingine na ikitokea basi Uislamu unamkemea na kumzuia, Mwenyezi Mungu anasema: ﴿WALA KUCHUKIANA NA WATU KUSIWAFANYE MUWE SI WAADILIFU. FANYENI UADILIFU. HUKO NDIO KUKARIBIA ZAIDI UCHAMUNGU﴾, na watu wote wako sawa katika hukumu mbele ya mahakama, na mfumo wa utawala unahukumu kwa umoja kati ya sehemu za dola, kama unavyohukumu kwa kuhakikisha mahitaji ya kila wilaya bila kujali mapato yake kwa hazina, ambayo inafanya mchanganyiko kuwa wa lazima kati ya wana wa wilaya zote za dola.

Kwa hivyo ilikuwa wajibu kwa kila Muislamu na Muislamu kufanya kazi ya kusimamisha faradhi hii kuu iliyo ghaibu, jumba la Khilafah Rashidah kwa njia ya Utume. ﴿HII DINI YENU NI DINI MOJA, NA MIMI NDIYE MOLA WENU, BASI NIABUDUNI﴾.

===

Njia Pekee ya Ukombozi wa Umma Kutoka Kwa Adhabu Zake

Hakika njia pekee ya ukombozi wa umma kutoka kwa adhabu zake ni kurejesha utukufu wake na heshima yake, ili utoke kutoka katika makucha ya utumwa kwa Magharibi, na urudi kwenye sheria ya Mola wake.

More from null

Jarida la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Al Raya sahafa

2025-11-12

Jarida la Ar-Raya:Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Enyi watu wa Sudan: Vita nchini Sudan na kwingineko vitaendelea kuwa kichocheo cha tamaa za kimataifa na mizozo yao kwa mipango yao mibaya, uingiliaji wao, na kuwapa pande zinazozozana silaha ili kuimiliki kikamilifu hadi lini?! Wanawake na watoto wenu wanateseka kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na mzozo huu wa umwagaji damu ambao hautimizi chochote ila maslahi ya nchi za Magharibi na vibaraka wao katika kudhibiti hatima ya Sudan, ambayo daima imekuwa ni kitu cha kutamaniwa kwao kwa sababu ya eneo lake na utajiri wake, hivyo ni kwa maslahi yao kuipasua na kuitawanya. Na kutekwa kwa Al-Fashir na vikosi vya Rapid Support Forces ni sehemu nyingine tu ya mipango hii, ambapo Marekani inataka kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan na kukomesha ushawishi wa Uingereza humo.

===

Lengo la ziara ya Ortagus

Nchini Lebanon!

Katika mazingira ya mashambulizi ya Marekani dhidi ya Lebanon na eneo hilo kwa mradi wa kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha, na jitihada za utawala wa Marekani chini ya uongozi wa Trump na timu yake za kuunganisha idadi kubwa ya watawala wa nchi za Waislamu kwenye makubaliano ya Abraham, ziara ya mjumbe wa Marekani, Morgan Ortagus, nchini Lebanon na nchi haramu ya Kiyahudi inakuja ikiwa na shinikizo, vitisho, na masharti ya kisiasa, kiusalama na kiuchumi kwa Lebanon, ikijua kwamba ziara hii imefanyika sambamba na ziara ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na Mkurugenzi wa Ujasusi wa Misri, ambayo inaonekana kuelekea mwelekeo uleule.

Kuhusiana na ziara hizi, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Lebanon ilisisitiza mambo yafuatayo:

Kwanza: Uingiliaji wa Marekani na wafuasi wake katika nchi za Waislamu ni kuhudumia maslahi ya Marekani na nchi haramu ya Kiyahudi, sio kuhudumia maslahi yetu, haswa kwani Marekani ndiye msaidizi mkuu wa nchi haramu ya Kiyahudi katika siasa, uchumi, fedha, silaha, na vyombo vya habari, waziwazi.

Pili: Ziara ya mjumbe sio ziara ya upande wowote kama wengine wanavyoweza kufikiria! Badala yake, inakuja katika muktadha wa sera ya wazi ya Marekani katika eneo hilo ambayo inasaidia nchi haramu ya Kiyahudi na inachangia kuiwezesha kijeshi na kisiasa, na kile ambacho mjumbe wa Marekani anatoa ni kulazimisha utawala, kuimarisha utegemezi, na kupunguza uhuru, na ni aina ya kujisalimisha na kujinyenyekeza kwa Wayahudi, na hili ndilo Mungu anawakataza watu wa Uislamu.

Tatu: Kukubali maagizo haya na kusaini makubaliano yoyote ambayo yanaimarisha udhibiti wa kigeni ni usaliti kwa Mungu, Mtume Wake, na Umma, na kwa kila mtu ambaye alipigana au kujitolea ili kuiondoa nchi hii haramu kutoka Lebanon na Palestina.

Nne: Kushughulika na nchi haramu ya Kiyahudi kwa idadi kubwa ya watu wa Lebanon, Waislamu na wasio Waislamu, ni uhalifu katika dhana ya kisheria, na hata katika sheria chanya ambayo mamlaka ya Lebanon inahukumu kwayo, au sheria ya kibinadamu kwa ujumla, haswa baada ya nchi hiyo haramu kufanya mauaji ya kimbari huko Gaza, ambayo haitasita kufanya kama hayo huko Lebanon na nchi zingine za Waislamu.

Tano: Kampeni na mashambulizi ya Marekani dhidi ya eneo hilo hayatapita, na Marekani haitafanikiwa katika jitihada zake za kuunda eneo hilo kama inavyotaka, na ikiwa ina mradi wake kwa eneo hilo, ambao unategemea ukoloni, unyanyasaji wa watu, kuwapotosha Waislamu, na hata kuwatoa kwenye dini yao kwa kuita (Dini ya Abraham), basi Waislamu, kwa upande mwingine, wana mradi wao ulioahidiwa kuonyeshwa na Mungu Mwenyezi; mradi wa Khilafah ya pili kwa mfumo wa Utume, ambao umekaribia sana, kwa idhini ya Mungu Mwenyezi, na mradi huu ndio utachora upya eneo hilo, na hata ulimwengu mzima, kwa mara nyingine tena, kama inavyothibitishwa na maneno ya Mtume ﷺ: «Hakika Mwenyezi Mungu aliniandalia ardhi, nikaona mashariki yake na magharibi yake, na hakika ufalme wa umma wangu utafikia kile nilichoandaliwa kutoka kwake» Imesimuliwa na Muslim, na nchi haramu ya Kiyahudi itaangamizwa kama Mtume ﷺ alivyobashiri katika hadithi yake: «Saa haitasimama mpaka Waislamu wapigane na Wayahudi, na Waislamu watawaua...» Imekubaliwa.

Hatimaye, Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Lebanon inaendelea kuunga mkono kukabiliana na kampeni ya Marekani na mashambulizi yake ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha kwa Lebanon na eneo hilo, na hakuna chochote kitakachoizuia kufanya hivyo, na tunaionya mamlaka ya Lebanon dhidi ya kufuata njia ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha! Na tunawasihi kujilinda kwa watu wao ili kukabiliana na hilo, na wasicheze na jambo hilo kwa kisingizio cha mipaka au ujenzi mpya na ushawishi wa mfumo wa kimataifa, ﴿Na Mwenyezi Mungu ni Mshindi juu ya jambo lake, lakini watu wengi hawajui﴾.

===

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan

Unakutana na idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, siku ya Jumatatu, Novemba 3, 2025, ulizuru idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini. Ujumbe huo ulikuwa chini ya uongozi wa Mwalimu Al-Nadhir Muhammad Hussein Abu Minhaj, mjumbe wa Baraza la Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Mwalimu Muhammad Saeed Boukeh, wajumbe wa Hizb ut-Tahrir.

Ambapo ujumbe huo ulikutana na kila mmoja wa:

Mwalimu Khalid Hussein - Mkuu wa Chama cha Muungano wa Kidemokrasia, tawi la Jalaa Al-Azhari.

Dkt. Abdullah Youssef Abu Seil - Mwanasheria na mhadhiri wa sheria katika vyuo vikuu.

Sheikh Abdul Rahim Jouda - kutoka kundi la Ansar al-Sunna.

Bw. Ahmed Muhammad - Mwandishi wa Shirika la Habari la Suna.

Mikutano hiyo ilizungumzia mada ya sasa; kuanguka kwa Al-Fashir na uhalifu uliokuwa umeambatana nayo uliofanywa na wanamgambo dhidi ya watu wa jiji hilo, na kuachwa na viongozi wa jeshi, ambao hawakutimiza wajibu wao kwa watu wa Al-Fashir na kuondoa kuzingirwa kwao, na wana uwezo wa kufanya hivyo katika kipindi chote cha kuzingirwa, na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi yao zaidi ya mashambulizi 266.

Kisha ujumbe huo uliwakabidhi nakala ya broshua ya Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan yenye kichwa: "Kuanguka kwa Al-Fashir kunafungua njia kwa mpango wa Marekani wa kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan, hadi lini tutakuwa kichocheo cha mzozo wa kimataifa?!". Majibu yao yalikuwa ya kipekee na waliomba mikutano hii iendelee.

===

Mazoezi ya "Phoenix Express 2025"

Sura kutoka sura za Tunisia kujisalimisha kwa utawala wa Marekani

Maandalizi ya Tunisia ya kuandaa toleo jipya la zoezi la majini la pande nyingi la "Phoenix Express 2025" yanakuja wakati wa mwezi wa Novemba, ambalo ni zoezi ambalo Kamandi ya Marekani ya Afrika imeanza kuandaa kila mwaka baada ya utawala wa Tunisia kuhusisha nchi kwa kusaini na Marekani, tarehe 2020/09/30, makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi, ambayo Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Mark Esper, alielezea kama ramani ya barabara itakayoendelea kwa miaka kumi.

Katika suala hili, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Tunisia ilikumbusha kwamba chama hicho kilibainisha wakati wa kusainiwa kwa makubaliano haya hatari kwamba jambo hilo linazidi makubaliano ya jadi, kwani Marekani inachora mradi mkubwa ambao unahitaji kukamilika kwa miaka 10 kamili, na kwamba ramani ya barabara, kulingana na madai ya Marekani, inahusiana na ufuatiliaji wa mipaka, ulinzi wa bandari, kupambana na mawazo ya itikadi kali, na kukabiliana na Urusi na China, na hii inamaanisha kwa dharau zote, kupunguza uhuru wa Tunisia, badala yake ni uangalizi wa moja kwa moja juu ya nchi yetu.

Taarifa hiyo ilisisitiza kwamba Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Tunisia, licha ya unyanyasaji, kukamatwa, na kesi za kijeshi ambazo vijana wetu wanakumbana nazo kwa sababu ya kusema ukweli, inathibitisha tena wito wake wa kuvunja makubaliano haya ya kikoloni yaliyolaaniwa ambayo yanalenga kuivuta nchi na nchi zote za Maghrib ya Kiislamu na kuzinyenyekeza kwa sera mbaya za Marekani, na pia ilirudia wito wake kwa watu wa nguvu na ulinzi huko Tunisia na nchi zingine za Waislamu kuwa waangalifu juu ya kile ambacho maadui wa Umma wanawafanyia njama na kuwavuta kwacho, na kwamba wajibu wa kisheria unahitaji wao kuunga mkono dini yao na kukabiliana na adui ambaye anavizia nchi yao na Umma wao, na kuinua neno la Mungu kwa kuunga mkono wale wanaofanya kazi ya kutekeleza sheria zake na kuanzisha dola yake, Dola ya Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume ulioahidiwa hivi karibuni kwa idhini ya Mungu.

===

Dharau ya Marekani kwa raia wake

Inawaacha wanawake na watoto wakiwa na njaa

Mpango wa Msaada wa Lishe ya Ziada (SNAP) ni mpango wa shirikisho ambao husaidia watu binafsi na familia zenye kipato cha chini na wenye ulemavu kupata faida za kielektroniki zinazotumiwa kununua chakula na vinywaji, isipokuwa pombe, na mimea ya kulima chakula chao wenyewe. Ripoti zinaonyesha kuwa Wamarekani milioni 42 wanategemea faida za (SNAP) kulisha wao wenyewe na familia zao. 54% ya watu wazima wanaopokea faida za chakula ni wanawake, na wengi wao ni mama wasio na waume, na 39% yao ni watoto, ambayo inamaanisha kuwa karibu mtoto mmoja kati ya watano anategemea faida hizi kuhakikisha kuwa hawapati njaa. Kufungwa kwa shirikisho pia kumesababisha baadhi ya majimbo kutafuta njia zingine za kufadhili mipango ya chakula ya bure na iliyopunguzwa katika maeneo yao ya elimu, ili watoto wanaotegemea chakula wakati wa siku ya shule wasilazimike kuishi bila chakula. Kama matokeo, maduka mengi ya chakula yaliyoenea kote nchini yanachapisha picha za rafu tupu, na kuwaomba watu kutoa chakula na kadi za zawadi za maduka ya mboga ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya chakula.

Kuhusu hilo, Idara ya Wanawake katika Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Tunapaswa kuuliza ni jinsi gani nchi tajiri zaidi ulimwenguni inaweza kupuuza ukweli kwamba mamilioni ya raia wake walio hatarini zaidi hawapati chakula cha kutosha? Unaweza kujiuliza Amerika inatumia pesa zake wapi, hata wakati wa kufungwa? Vema, badala ya kuhakikisha kuwa Wamarekani wanapata chakula cha kutosha, wanatuma mabilioni ya dola kwa nchi haramu ya Kiyahudi kuwaua Wapalestina. Ni mtawala ambaye anaona kuwa kujenga ukumbi wa sherehe za kifahari ni muhimu kuliko kitu kingine chochote, wakati manaibu wengine wanaona uwekezaji wao wa kibinafsi unachukuliwa kuwa muhimu kuliko ustawi wa watu ambao wanapaswa kuwawakilisha! Kama unavyoona, Amerika ya kibepari haijawahi kujali kutunza masuala ya raia wake, badala yake ilikuwa inajali tu kutoa msaada wa kijeshi na kifedha kwa wale wanaowanyima watoto kote ulimwenguni haki yao ya usalama, chakula, makazi, na elimu, ambazo ni mahitaji ya msingi. Kwa hivyo, inawaacha watoto huko Amerika pia wakiteseka na njaa na ukosefu wa usalama, na wanakosa elimu sahihi na huduma ya afya.

===

«Muislamu yeyote yule ni haramu kwa Muislamu mwenzake; damu yake, mali yake, na heshima yake»

Kwa kila Muislamu, kwa kila afisa na askari, kwa kila mtu anayemiliki silaha: Hakika Mwenyezi Mungu ametupa akili ili tufikiri kwayo, na ametulazimisha kuitumia matumizi sahihi, kwa hivyo mtu asitende au kufanya kazi yoyote au kutamka neno lolote kabla ya kujua hukumu yake ya kisheria, na kujua hukumu ya kisheria kunahitaji kuelewa hali halisi ambayo hukumu ya kisheria inataka kuletwa, kwa hivyo lazima Muislamu awe na ufahamu wa kisiasa, ili aweze kufahamu mambo kama yalivyo, na asifuate mipango ya makafiri wakoloni ambao hawatutakii mema sisi wala Uislamu, na wanafanya bidii kwa kila wawezalo kwa nguvu, hila na akili kutupasua vipande vipande na kuudhibiti nchi yetu na kunyakua rasilimali zetu na utajiri wetu, kwa hivyo Muislamu anawezaje kukubali kuwa chombo mikononi mwa makafiri hao wakoloni, au mtendaji wa maagizo ya vibaraka wao?! Je, anatamani kitu kidogo cha starehe za dunia hii zinazopita na anapoteza Akhera yake na anakuwa miongoni mwa watu wa Motoni milele humo, amelaaniwa na kufukuzwa kutoka kwa rehema za Mungu? Je, Muislamu anakubali kumridhisha mtu yeyote yule miongoni mwa wanadamu viumbe dhaifu huku anamkasirisha Mungu Mwenyezi ambaye mikononi mwake iko dunia na Akhera?!

Hakika Hizb ut-Tahrir inawasihi kuinua kiwango cha ufahamu wa kisiasa, kuzingatia hukumu za Mungu Mwenyezi, na kufanya kazi nayo ili kuhukumu kwa yale ambayo Mungu ameyateremsha, ili kuwaondoa mikono ya makafiri wakoloni na vibaraka wao, na kushindwa mipango yao katika nchi yetu.

===

Ninyi ndio mnaowaweka Waislamu katika njaa

Ewe Masoud Pezeshkian!

Chini ya kichwa hiki, Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Iran imetangaza kufilisika kwa benki kubwa zaidi ya kibinafsi nchini humo, ambayo ni benki ya (Ayandeh), na benki hii ina matawi 270 nchini Iran, baada ya madeni kuongezeka hadi dola bilioni tano, na cha kushangaza ni kukosoa kwa rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, kushindwa kwa utawala, akisema: "Tuna mafuta na gesi, lakini tuna njaa"!

Taarifa hiyo ilisisitiza: Mwenye dhamana ya kushindwa huko kwa utawala ambako rais wa Iran anazungumzia ni rais mwenyewe, kwa nini watu wa Iran wana njaa - Ewe Masoud Pezeshkian - na mna mafuta, gesi, na utajiri mwingine na madini? Je, siyo matokeo ya sera zenu za kijinga? Je, siyo kwa sababu ya umbali wenu kutoka kwa kuhukumu kwa Uislamu? Na vivyo hivyo, inasemwa kwa nchi zingine za Waislamu, watawala wajinga ndani yake wanapoteza utajiri mwingi wa Umma, na wanawezesha makafiri wakoloni kupata utajiri huo, na wananyima Umma utajiri huo, kisha mmoja wao anakuja kuhalalisha sababu ya njaa kwa kusema kwamba ni kushindwa kwa utawala!

Hatimaye, taarifa hiyo kwa vyombo vya habari iliwahutubia Waislamu: Ujinga wa watawala hawa ambao wanachukua masuala yenu umeonekana kwa kila mwenye macho na ufahamu, na hawafai kuchukua masuala hayo, umefika wakati wa kuwazuia, kwani hii ndiyo hukumu ya mjinga; kumzuia kutumia pesa na kumdhibiti, na mumpatie Bay'ah Khalifa mmoja anayewahukumu kwa sheria ya Mungu Mwenyezi, na afute mfumo wa riba katika nchi yenu ili Mola wenu akuridhieni na Mtume Wake ﷺ, na arejeshe utajiri wenu ulionyaganywa, na arejeshe heshima yenu na fahari yenu, na hapa kuna Hizb ut-Tahrir, mwanzilishi ambaye watu wake hawasemi uongo, anawasihi kufanya kazi nayo ili kuanzisha Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume.

 </