Jarida la Ar-Raya: Umoja wa Kweli wa Umma wa Kiislamu Hautakuwa kwa Maneno na Hotuba
September 23, 2025

Jarida la Ar-Raya: Umoja wa Kweli wa Umma wa Kiislamu Hautakuwa kwa Maneno na Hotuba

Al Raya sahafa

2025-09-24

Jarida la Ar-Raya: Umoja wa Kweli wa Umma wa Kiislamu

Hautakuwa kwa Maneno na Hotuba

Shughuli za Kongamano la 39 la Kimataifa la Umoja wa Kiislamu zilianza asubuhi ya Jumatatu, Septemba 8, 2025, katika ukumbi wa mikutano wa Mkutano wa Kiislamu katika mji mkuu wa Iran, Tehran, chini ya uongozi wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kuleta Karibu Madhehebu za Kiislamu.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kuleta Karibu Madhehebu za Kiislamu Dkt. Shahriyari alieleza: "Katika hatua hii nyeti ambayo ulimwengu unateseka kutokana na mzozo wa wazi, nadharia ya umoja wa Kiislamu inayotegemea kuzingatia mamlaka ya kimungu na udugu wa kiimani imekuwa muhimu zaidi kuliko wakati wowote ule, na leo umoja wa Kiislamu umekuwa jambo la lazima lisiloepukika katika uwanja wa utendaji."

Rais wa Iran Massoud Pezeshkian alikosoa udhaifu wa mshikamano kati ya nchi za Kiislamu, akiongeza: "Ikiwa sisi ni wafuasi wa Nabii Muhammad, kwa nini tumekuwa tumetengana? Tatizo si Israeli au Amerika, bali ni migawanyiko yetu na migogoro ya ndani." Alisisitiza kwamba dola ya Kiyahudi na Amerika "isingethubutu kuwashambulia Waislamu kama ulimwengu wa Kiislamu ungekuwa umeungana," akionyesha kwamba tofauti za ndani zimefungua mlango wa kuchochea fitina na kuzitumia kuuza silaha kwa nchi za Kiislamu chini ya kivuli cha hofu.

Mazungumzo kuhusu umoja wa Kiislamu si mazungumzo yasiyo wazi au ya jumla, na umoja si usiojulikana kwa hukumu na jinsi, bali ni faradhi na suala la hatima na linajulikana katika kitabu cha Mola wetu Mtukufu na Sunna za Nabii wetu ﷺ, na ni madai ya kisheria kwa kila Muislamu aliye mwanachama wa umma wake, na ibada miongoni mwa ibada kubwa zaidi, na kufanya kazi kwa ajili yake ni miongoni mwa matendo na ukaribu mkubwa zaidi kwa Mungu. Na ina maoni ya umma miongoni mwa Waislamu, bila kusahau kuwa ilikuwa tukio na ukweli kwa zaidi ya miaka elfu moja na kafiri aliimaliza kwa kuondoa dola ya Kiislamu ya Khilafa ya Uthmaniyya.

Jambo la ajabu ni kusikia wito wa umoja kutoka kwa mifumo ya utengano, tatizo la umoja si umma wa Kiislamu; kwa sababu unapenda umoja na unau subiri kwa hamu. Tatizo ni wingi wa nchi na watawala ambao kafiri mkoloni aliwateua kwa niaba yake katika kupambana na Uislamu na kuzuia umoja, la sivyo ni nini kinakuzuieni na umoja ikiwa mna umiliki uamuzi wenu wa kisiasa?!

Je, si nchi za kikafiri ziliwasimamisha na kugawanya nchi za Kiislamu baada ya kuondoa dola ya Khilafa, na kumfanya kila mmoja wenu kuwa na mipaka ya bandia na nguvu ambayo uwepo wake unategemea Magharibi na kuunyima umma mamlaka yake? Basi mnaliliaje umoja na uwepo wenu ni utengano wenyewe?! Au ni hotuba ya kupotosha kama kawaida yenu? Udanganyifu huu na upotoshaji haujafichika tena kwa umma, nyinyi ni vibaraka wa Magharibi na zana zake za kuzuia Uislamu kufikia utawala na kutimiza umoja.

Vita vya Wayahudi huko Gaza na Ukingo wa Magharibi vimelifichua umma ukweli wa uwepo wenu kwa namna isiyo na utata na vimelieleza kuwa uwepo wenu ni udhalili, aibu, fedheha na usaliti, Mtume wa Mungu ﷺ alisema: «Karibu mataifa yatakukaribishieni kama vile watu wenye njaa wanavyo karibisha chakula kwenye sahani yao», Mtu mmoja akasema: Je, tutakuwa wachache siku hiyo? Akasema: «Bali nyinyi siku hiyo mtakuwa wengi lakini mtakuwa kama povu la mafuriko, na Mungu ataondoa hofu yenu kutoka katika vifua vya adui yenu, na Mungu ataweka unyonge katika mioyo yenu». Mtu mmoja akasema: Ewe Mtume wa Mungu, ni nini unyonge? Akasema: «Kupenda dunia na kuchukia mauti».

Hakuna dola wala Khalifa wa kupigana nyuma yake na kujikinga naye, wala umoja wa kuunganisha utengano wake katika dola moja chini ya bendera moja, vipi isiwe hivi na Mola wa utukufu anasema: ﴿HII NI DINI YENU, DINI MOJA, NA MIMI NDIYE MOLA WENU, BASI NIABUDUNI﴾? Na anasema Subhana: ﴿ENYI MITUME! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi najua mnayo yatenda. * Na hakika hii dini yenu ni dini moja, na Mimi ndiye Mola wenu, basi mcheni.﴾.

Dini yenu imefaradhisha umoja wa umma na kuendelea kwake kwenye moyo wa mtu mmoja, faradhi ambayo anayeikhalifu ataadhibiwa vikali zaidi, naye ni mauti kwa yule anayekhalifu na kutoka nje ya jamaa, kutoka kwa Mtume wa Mungu ﷺ alisema: «Mtu akikuijieni hali yakuwa jambo lenu liko sawa juu ya mtu mmoja anataka kuipasua fimbo yenu au kuwafarakanisha kundi lenu basi muuweni» Na alisema ﷺ: «Yeyote anayetaka kuifarakisha amri ya umma huu na hali wao wamekusanyika, basi mpigeni kwa upanga awe ni nani yeye» Katika Sahih Muslim: «Akiapishwa Khalifa wawili basi muuweni yule wa mwisho miongoni mwao» Na alisema ﷺ: «Na yeyote anayempa imamu mkono wake na matunda ya moyo wake basi amtii ikiwa anaweza, akija mwingine kumgombania basi pigeni shingo ya yule mwingine».

Magharibi kafiri inatambua hatari ya kuanzishwa dola ya Kiislamu na inatambua hatari ya umoja wa umma, Curzon, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, alisema katika taarifa baada ya kufanikiwa kubomoa Khilafa ya Uthmaniyya: "Tumeiangamiza Uturuki ambayo haitasimama tena leo, kwa sababu tumeondoa nguvu zake zinazo wakilishwa na mambo mawili: Uislamu na Khilafa".

Na Henry Kissinger anasema katika hotuba yake nchini India mwaka 2004: "Vitisho havitoki kwa ugaidi, kama vile tulivyo shuhudia Septemba 11, lakini tishio linatoka kwa Uislamu wenye msimamo mkali ambao unafanya kazi ya kudhoofisha Uislamu wa wastani ambao unapingana na kile wanachokiona wafuasi wa msimamo mkali katika suala la Khilafa ya Kiislamu".

Na kamanda wa majeshi ya muungano Richard Myers anasema: Hatari ya kweli na kubwa zaidi kwa usalama wa Marekani ni itikadi kali ambayo inataka kuanzisha dola ya Khilafa.

Na umoja si usiojulikana kwa jinsi, sio mkusanyiko katika chuo kikuu au ushirikiano wa Kiislamu au Kiarabu ulioanzishwa na ukafiri na kuhifadhi mipaka ya kila nchi kama ilivyo, bali wanajaribu kuigawanya pia, na sio mkutano wa watawala walioteuliwa na kafiri mkoloni kukemea, kulaani na kuzungumzia umoja na kulilia kile ambacho mambo yamefikia.

Suala la umoja wa umma si kwa maneno na hotuba, bali ni suala la hatima ambalo halipaswi kupuuzwa, na kuanzishwa kwa hadhi kwa Waislamu kunahitaji kabla ya kila jambo kuwa wawe umoja mmoja kwa msingi wa Uislamu, na wajibu wa umoja uko juu ya umma mzima, watu binafsi na majeshi, kwa kuwa majeshi ndiyo yenye nguvu ambayo inawezesha kuchukua hatamu ya jambo na kubadilisha hali kwa faida ya dini ya Mungu na sheria yake, lakini umma pia unawajibika kufanya kazi kwa bidii endelevu ili kurejesha mshikamano kwa umma huu mtukufu na kushinikiza majeshi kutimiza jambo hili ili hadhi na hadhi ya umma virejee, ili Muumba wa ardhi na mbingu awe radhi nao, na hilo si gumu kwa Mungu.

Imeandikwa na: Mwalimu Abdul Hakim Abdullah – Jimbo la Jordan

Chanzo: Jarida la Ar-Raya

More from null

Jarida la Ar-Raya: Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Al Raya sahafa

2025-11-12

Jarida la Ar-Raya:Mada Mbalimbali za Ar-Raya – Toleo la 573

Enyi watu wa Sudan: Vita nchini Sudan na kwingineko vitaendelea kuwa kichocheo cha tamaa za kimataifa na mizozo yao kwa mipango yao mibaya, uingiliaji wao, na kuwapa pande zinazozozana silaha ili kuimiliki kikamilifu hadi lini?! Wanawake na watoto wenu wanateseka kwa zaidi ya miaka miwili kutokana na mzozo huu wa umwagaji damu ambao hautimizi chochote ila maslahi ya nchi za Magharibi na vibaraka wao katika kudhibiti hatima ya Sudan, ambayo daima imekuwa ni kitu cha kutamaniwa kwao kwa sababu ya eneo lake na utajiri wake, hivyo ni kwa maslahi yao kuipasua na kuitawanya. Na kutekwa kwa Al-Fashir na vikosi vya Rapid Support Forces ni sehemu nyingine tu ya mipango hii, ambapo Marekani inataka kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan na kukomesha ushawishi wa Uingereza humo.

===

Lengo la ziara ya Ortagus

Nchini Lebanon!

Katika mazingira ya mashambulizi ya Marekani dhidi ya Lebanon na eneo hilo kwa mradi wa kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha, na jitihada za utawala wa Marekani chini ya uongozi wa Trump na timu yake za kuunganisha idadi kubwa ya watawala wa nchi za Waislamu kwenye makubaliano ya Abraham, ziara ya mjumbe wa Marekani, Morgan Ortagus, nchini Lebanon na nchi haramu ya Kiyahudi inakuja ikiwa na shinikizo, vitisho, na masharti ya kisiasa, kiusalama na kiuchumi kwa Lebanon, ikijua kwamba ziara hii imefanyika sambamba na ziara ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na Mkurugenzi wa Ujasusi wa Misri, ambayo inaonekana kuelekea mwelekeo uleule.

Kuhusiana na ziara hizi, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Ofisi ya Habari ya Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Lebanon ilisisitiza mambo yafuatayo:

Kwanza: Uingiliaji wa Marekani na wafuasi wake katika nchi za Waislamu ni kuhudumia maslahi ya Marekani na nchi haramu ya Kiyahudi, sio kuhudumia maslahi yetu, haswa kwani Marekani ndiye msaidizi mkuu wa nchi haramu ya Kiyahudi katika siasa, uchumi, fedha, silaha, na vyombo vya habari, waziwazi.

Pili: Ziara ya mjumbe sio ziara ya upande wowote kama wengine wanavyoweza kufikiria! Badala yake, inakuja katika muktadha wa sera ya wazi ya Marekani katika eneo hilo ambayo inasaidia nchi haramu ya Kiyahudi na inachangia kuiwezesha kijeshi na kisiasa, na kile ambacho mjumbe wa Marekani anatoa ni kulazimisha utawala, kuimarisha utegemezi, na kupunguza uhuru, na ni aina ya kujisalimisha na kujinyenyekeza kwa Wayahudi, na hili ndilo Mungu anawakataza watu wa Uislamu.

Tatu: Kukubali maagizo haya na kusaini makubaliano yoyote ambayo yanaimarisha udhibiti wa kigeni ni usaliti kwa Mungu, Mtume Wake, na Umma, na kwa kila mtu ambaye alipigana au kujitolea ili kuiondoa nchi hii haramu kutoka Lebanon na Palestina.

Nne: Kushughulika na nchi haramu ya Kiyahudi kwa idadi kubwa ya watu wa Lebanon, Waislamu na wasio Waislamu, ni uhalifu katika dhana ya kisheria, na hata katika sheria chanya ambayo mamlaka ya Lebanon inahukumu kwayo, au sheria ya kibinadamu kwa ujumla, haswa baada ya nchi hiyo haramu kufanya mauaji ya kimbari huko Gaza, ambayo haitasita kufanya kama hayo huko Lebanon na nchi zingine za Waislamu.

Tano: Kampeni na mashambulizi ya Marekani dhidi ya eneo hilo hayatapita, na Marekani haitafanikiwa katika jitihada zake za kuunda eneo hilo kama inavyotaka, na ikiwa ina mradi wake kwa eneo hilo, ambao unategemea ukoloni, unyanyasaji wa watu, kuwapotosha Waislamu, na hata kuwatoa kwenye dini yao kwa kuita (Dini ya Abraham), basi Waislamu, kwa upande mwingine, wana mradi wao ulioahidiwa kuonyeshwa na Mungu Mwenyezi; mradi wa Khilafah ya pili kwa mfumo wa Utume, ambao umekaribia sana, kwa idhini ya Mungu Mwenyezi, na mradi huu ndio utachora upya eneo hilo, na hata ulimwengu mzima, kwa mara nyingine tena, kama inavyothibitishwa na maneno ya Mtume ﷺ: «Hakika Mwenyezi Mungu aliniandalia ardhi, nikaona mashariki yake na magharibi yake, na hakika ufalme wa umma wangu utafikia kile nilichoandaliwa kutoka kwake» Imesimuliwa na Muslim, na nchi haramu ya Kiyahudi itaangamizwa kama Mtume ﷺ alivyobashiri katika hadithi yake: «Saa haitasimama mpaka Waislamu wapigane na Wayahudi, na Waislamu watawaua...» Imekubaliwa.

Hatimaye, Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Lebanon inaendelea kuunga mkono kukabiliana na kampeni ya Marekani na mashambulizi yake ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha kwa Lebanon na eneo hilo, na hakuna chochote kitakachoizuia kufanya hivyo, na tunaionya mamlaka ya Lebanon dhidi ya kufuata njia ya kurejesha uhusiano wa kawaida na kujisalimisha! Na tunawasihi kujilinda kwa watu wao ili kukabiliana na hilo, na wasicheze na jambo hilo kwa kisingizio cha mipaka au ujenzi mpya na ushawishi wa mfumo wa kimataifa, ﴿Na Mwenyezi Mungu ni Mshindi juu ya jambo lake, lakini watu wengi hawajui﴾.

===

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan

Unakutana na idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad

Ujumbe kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan, siku ya Jumatatu, Novemba 3, 2025, ulizuru idadi ya viongozi wa mji wa Al-Abyad, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini. Ujumbe huo ulikuwa chini ya uongozi wa Mwalimu Al-Nadhir Muhammad Hussein Abu Minhaj, mjumbe wa Baraza la Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Mwalimu Muhammad Saeed Boukeh, wajumbe wa Hizb ut-Tahrir.

Ambapo ujumbe huo ulikutana na kila mmoja wa:

Mwalimu Khalid Hussein - Mkuu wa Chama cha Muungano wa Kidemokrasia, tawi la Jalaa Al-Azhari.

Dkt. Abdullah Youssef Abu Seil - Mwanasheria na mhadhiri wa sheria katika vyuo vikuu.

Sheikh Abdul Rahim Jouda - kutoka kundi la Ansar al-Sunna.

Bw. Ahmed Muhammad - Mwandishi wa Shirika la Habari la Suna.

Mikutano hiyo ilizungumzia mada ya sasa; kuanguka kwa Al-Fashir na uhalifu uliokuwa umeambatana nayo uliofanywa na wanamgambo dhidi ya watu wa jiji hilo, na kuachwa na viongozi wa jeshi, ambao hawakutimiza wajibu wao kwa watu wa Al-Fashir na kuondoa kuzingirwa kwao, na wana uwezo wa kufanya hivyo katika kipindi chote cha kuzingirwa, na mashambulizi ya mara kwa mara dhidi yao zaidi ya mashambulizi 266.

Kisha ujumbe huo uliwakabidhi nakala ya broshua ya Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Sudan yenye kichwa: "Kuanguka kwa Al-Fashir kunafungua njia kwa mpango wa Marekani wa kutenganisha mkoa wa Darfur na kuimarisha ushawishi wake nchini Sudan, hadi lini tutakuwa kichocheo cha mzozo wa kimataifa?!". Majibu yao yalikuwa ya kipekee na waliomba mikutano hii iendelee.

===

Mazoezi ya "Phoenix Express 2025"

Sura kutoka sura za Tunisia kujisalimisha kwa utawala wa Marekani

Maandalizi ya Tunisia ya kuandaa toleo jipya la zoezi la majini la pande nyingi la "Phoenix Express 2025" yanakuja wakati wa mwezi wa Novemba, ambalo ni zoezi ambalo Kamandi ya Marekani ya Afrika imeanza kuandaa kila mwaka baada ya utawala wa Tunisia kuhusisha nchi kwa kusaini na Marekani, tarehe 2020/09/30, makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi, ambayo Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Mark Esper, alielezea kama ramani ya barabara itakayoendelea kwa miaka kumi.

Katika suala hili, taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Hizb ut-Tahrir/ Wilaya ya Tunisia ilikumbusha kwamba chama hicho kilibainisha wakati wa kusainiwa kwa makubaliano haya hatari kwamba jambo hilo linazidi makubaliano ya jadi, kwani Marekani inachora mradi mkubwa ambao unahitaji kukamilika kwa miaka 10 kamili, na kwamba ramani ya barabara, kulingana na madai ya Marekani, inahusiana na ufuatiliaji wa mipaka, ulinzi wa bandari, kupambana na mawazo ya itikadi kali, na kukabiliana na Urusi na China, na hii inamaanisha kwa dharau zote, kupunguza uhuru wa Tunisia, badala yake ni uangalizi wa moja kwa moja juu ya nchi yetu.

Taarifa hiyo ilisisitiza kwamba Hizb ut-Tahrir katika Wilaya ya Tunisia, licha ya unyanyasaji, kukamatwa, na kesi za kijeshi ambazo vijana wetu wanakumbana nazo kwa sababu ya kusema ukweli, inathibitisha tena wito wake wa kuvunja makubaliano haya ya kikoloni yaliyolaaniwa ambayo yanalenga kuivuta nchi na nchi zote za Maghrib ya Kiislamu na kuzinyenyekeza kwa sera mbaya za Marekani, na pia ilirudia wito wake kwa watu wa nguvu na ulinzi huko Tunisia na nchi zingine za Waislamu kuwa waangalifu juu ya kile ambacho maadui wa Umma wanawafanyia njama na kuwavuta kwacho, na kwamba wajibu wa kisheria unahitaji wao kuunga mkono dini yao na kukabiliana na adui ambaye anavizia nchi yao na Umma wao, na kuinua neno la Mungu kwa kuunga mkono wale wanaofanya kazi ya kutekeleza sheria zake na kuanzisha dola yake, Dola ya Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume ulioahidiwa hivi karibuni kwa idhini ya Mungu.

===

Dharau ya Marekani kwa raia wake

Inawaacha wanawake na watoto wakiwa na njaa

Mpango wa Msaada wa Lishe ya Ziada (SNAP) ni mpango wa shirikisho ambao husaidia watu binafsi na familia zenye kipato cha chini na wenye ulemavu kupata faida za kielektroniki zinazotumiwa kununua chakula na vinywaji, isipokuwa pombe, na mimea ya kulima chakula chao wenyewe. Ripoti zinaonyesha kuwa Wamarekani milioni 42 wanategemea faida za (SNAP) kulisha wao wenyewe na familia zao. 54% ya watu wazima wanaopokea faida za chakula ni wanawake, na wengi wao ni mama wasio na waume, na 39% yao ni watoto, ambayo inamaanisha kuwa karibu mtoto mmoja kati ya watano anategemea faida hizi kuhakikisha kuwa hawapati njaa. Kufungwa kwa shirikisho pia kumesababisha baadhi ya majimbo kutafuta njia zingine za kufadhili mipango ya chakula ya bure na iliyopunguzwa katika maeneo yao ya elimu, ili watoto wanaotegemea chakula wakati wa siku ya shule wasilazimike kuishi bila chakula. Kama matokeo, maduka mengi ya chakula yaliyoenea kote nchini yanachapisha picha za rafu tupu, na kuwaomba watu kutoa chakula na kadi za zawadi za maduka ya mboga ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka ya chakula.

Kuhusu hilo, Idara ya Wanawake katika Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Tunapaswa kuuliza ni jinsi gani nchi tajiri zaidi ulimwenguni inaweza kupuuza ukweli kwamba mamilioni ya raia wake walio hatarini zaidi hawapati chakula cha kutosha? Unaweza kujiuliza Amerika inatumia pesa zake wapi, hata wakati wa kufungwa? Vema, badala ya kuhakikisha kuwa Wamarekani wanapata chakula cha kutosha, wanatuma mabilioni ya dola kwa nchi haramu ya Kiyahudi kuwaua Wapalestina. Ni mtawala ambaye anaona kuwa kujenga ukumbi wa sherehe za kifahari ni muhimu kuliko kitu kingine chochote, wakati manaibu wengine wanaona uwekezaji wao wa kibinafsi unachukuliwa kuwa muhimu kuliko ustawi wa watu ambao wanapaswa kuwawakilisha! Kama unavyoona, Amerika ya kibepari haijawahi kujali kutunza masuala ya raia wake, badala yake ilikuwa inajali tu kutoa msaada wa kijeshi na kifedha kwa wale wanaowanyima watoto kote ulimwenguni haki yao ya usalama, chakula, makazi, na elimu, ambazo ni mahitaji ya msingi. Kwa hivyo, inawaacha watoto huko Amerika pia wakiteseka na njaa na ukosefu wa usalama, na wanakosa elimu sahihi na huduma ya afya.

===

«Muislamu yeyote yule ni haramu kwa Muislamu mwenzake; damu yake, mali yake, na heshima yake»

Kwa kila Muislamu, kwa kila afisa na askari, kwa kila mtu anayemiliki silaha: Hakika Mwenyezi Mungu ametupa akili ili tufikiri kwayo, na ametulazimisha kuitumia matumizi sahihi, kwa hivyo mtu asitende au kufanya kazi yoyote au kutamka neno lolote kabla ya kujua hukumu yake ya kisheria, na kujua hukumu ya kisheria kunahitaji kuelewa hali halisi ambayo hukumu ya kisheria inataka kuletwa, kwa hivyo lazima Muislamu awe na ufahamu wa kisiasa, ili aweze kufahamu mambo kama yalivyo, na asifuate mipango ya makafiri wakoloni ambao hawatutakii mema sisi wala Uislamu, na wanafanya bidii kwa kila wawezalo kwa nguvu, hila na akili kutupasua vipande vipande na kuudhibiti nchi yetu na kunyakua rasilimali zetu na utajiri wetu, kwa hivyo Muislamu anawezaje kukubali kuwa chombo mikononi mwa makafiri hao wakoloni, au mtendaji wa maagizo ya vibaraka wao?! Je, anatamani kitu kidogo cha starehe za dunia hii zinazopita na anapoteza Akhera yake na anakuwa miongoni mwa watu wa Motoni milele humo, amelaaniwa na kufukuzwa kutoka kwa rehema za Mungu? Je, Muislamu anakubali kumridhisha mtu yeyote yule miongoni mwa wanadamu viumbe dhaifu huku anamkasirisha Mungu Mwenyezi ambaye mikononi mwake iko dunia na Akhera?!

Hakika Hizb ut-Tahrir inawasihi kuinua kiwango cha ufahamu wa kisiasa, kuzingatia hukumu za Mungu Mwenyezi, na kufanya kazi nayo ili kuhukumu kwa yale ambayo Mungu ameyateremsha, ili kuwaondoa mikono ya makafiri wakoloni na vibaraka wao, na kushindwa mipango yao katika nchi yetu.

===

Ninyi ndio mnaowaweka Waislamu katika njaa

Ewe Masoud Pezeshkian!

Chini ya kichwa hiki, Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir ilisema katika taarifa kwa vyombo vya habari: Iran imetangaza kufilisika kwa benki kubwa zaidi ya kibinafsi nchini humo, ambayo ni benki ya (Ayandeh), na benki hii ina matawi 270 nchini Iran, baada ya madeni kuongezeka hadi dola bilioni tano, na cha kushangaza ni kukosoa kwa rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, kushindwa kwa utawala, akisema: "Tuna mafuta na gesi, lakini tuna njaa"!

Taarifa hiyo ilisisitiza: Mwenye dhamana ya kushindwa huko kwa utawala ambako rais wa Iran anazungumzia ni rais mwenyewe, kwa nini watu wa Iran wana njaa - Ewe Masoud Pezeshkian - na mna mafuta, gesi, na utajiri mwingine na madini? Je, siyo matokeo ya sera zenu za kijinga? Je, siyo kwa sababu ya umbali wenu kutoka kwa kuhukumu kwa Uislamu? Na vivyo hivyo, inasemwa kwa nchi zingine za Waislamu, watawala wajinga ndani yake wanapoteza utajiri mwingi wa Umma, na wanawezesha makafiri wakoloni kupata utajiri huo, na wananyima Umma utajiri huo, kisha mmoja wao anakuja kuhalalisha sababu ya njaa kwa kusema kwamba ni kushindwa kwa utawala!

Hatimaye, taarifa hiyo kwa vyombo vya habari iliwahutubia Waislamu: Ujinga wa watawala hawa ambao wanachukua masuala yenu umeonekana kwa kila mwenye macho na ufahamu, na hawafai kuchukua masuala hayo, umefika wakati wa kuwazuia, kwani hii ndiyo hukumu ya mjinga; kumzuia kutumia pesa na kumdhibiti, na mumpatie Bay'ah Khalifa mmoja anayewahukumu kwa sheria ya Mungu Mwenyezi, na afute mfumo wa riba katika nchi yenu ili Mola wenu akuridhieni na Mtume Wake ﷺ, na arejeshe utajiri wenu ulionyaganywa, na arejeshe heshima yenu na fahari yenu, na hapa kuna Hizb ut-Tahrir, mwanzilishi ambaye watu wake hawasemi uongo, anawasihi kufanya kazi nayo ili kuanzisha Khilafah Rashidah ya Pili kwa mfumo wa Utume.

 </