Hotuba ya Erdogan katika Umoja wa Mataifa: Maneno Matupu!
Hotuba ya Erdogan katika Umoja wa Mataifa: Maneno Matupu!

Habari:

0:00 0:00
Speed:
October 02, 2025

Hotuba ya Erdogan katika Umoja wa Mataifa: Maneno Matupu!

Hotuba ya Erdogan katika Umoja wa Mataifa: Maneno Matupu!

(Imetafsiriwa)

Habari:

Katika hotuba yake kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Erdogan alielezea kile kinachotokea Gaza kama mauaji ya kimbari, akisisitiza kwamba taasisi ya Kiyahudi inaua watoto kila siku, na akatoa wito kwa mfumo wa kimataifa kuchukua hatua. Alichapisha picha kutoka Gaza, na kusema: "Hakuna vita huko Gaza; ni sera ya uvamizi, uhamishaji na mauaji ya halaiki."

Alirudia msemo wake maarufu "Ulimwengu ni mkuu kuliko tano," akikosoa muundo wa Umoja wa Mataifa, na akatangaza kwamba uhusiano na Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) na Amerika unaimarika, na kwamba Uturuki itakuwa mwenyeji wa mkutano wa kilele wa shirika hilo mwaka 2026. Miongoni mwa mambo muhimu mengine katika hotuba yake ni umakini wake kuhusu mazingira, akili bandia, kupunguza taka na familia.

Maoni:

Erdogan alielekeza umakini kwa masuala mengi ya kimataifa, hasa suala la Palestina. Hata hivyo, maneno yake, kwa mtazamo wa Kiislamu, yanaonekana kuwa matupu, yamejitenga na uhalisia, hayako huru na vizuizi vya mfumo wa kikoloni wa kimataifa.

Huenda maneno ya Erdogan yamegusa hisia, hasa kuhusu Palestina. Lakini kwa mtazamo wa Kiislamu, kasoro kubwa katika hotuba hii ni kwamba maneno hayo yenye nguvu hayatafsiriwi kuwa matendo. Wakati watoto wa Gaza wanakufa kwa njaa, na eneo hilo linageuka kuwa kambi ya kifo na uharibifu chini ya mzingiro kamili, sauti ya wanaodhulumiwa ni maneno tu.

Ukosoaji wake kwa Umoja wa Mataifa pia ulikuwa wa juu juu. Umoja wa Mataifa ambao unaitwa "kurekebishwa" ni mfumo uleule ulioanzishwa na wadhalimu. Wajibu wa umma si kuuhuisha, bali kuanzisha mfumo mpya wa kimataifa kwa misingi ya Uislamu. Inaonekana kwamba msemo wa Erdogan unaorudiwa "Ulimwengu ni mkuu kuliko tano" ni ukosoaji wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lenye wanachama watano. Ingawa msemo huu umepokea mwangwi mzuri miongoni mwa watu wanaodharau mfumo wa kimataifa, ukweli ni kwamba Amerika yenyewe haifurahishwi na mfumo wa baada ya Vita vya Pili vya Dunia iliyounda na inataka kuubadilisha. Kwa hivyo, wito wa Erdogan wa mageuzi unaambatana na maslahi ya Amerika yenyewe.

Zaidi ya hayo, sifa ya Erdogan ya kuimarisha uhusiano na NATO ni udhalilishaji kwa Waislamu, si heshima kwao. Ushirikiano na shirika ambalo limeua mamilioni ya Waislamu kutoka Afghanistan hadi Iraq, na kutoka Syria hadi Libya, si jambo la kujivunia, bali ni jambo la aibu.

Pia, dhana ya "suluhisho la mataifa mawili" ni zao la mawazo ya kikoloni. Katika muktadha wa Palestina na Cyprus, msemo huu unamaanisha tu kutambua uwepo wa Wayahudi kwenye ardhi ya Palestina na uwepo wa Wagiriki katika kisiwa cha Cyprus. Hata hivyo, wote wawili wamevamiwa. Suluhisho si kuhalalisha uvamizi huu na kuutambua, bali kuukomesha.

Ingawa hotuba ya Erdogan ilijumuisha maneno na maoni ya kushangaza, haina uzito wowote ikilinganishwa na msimamo halisi wa kisiasa wa Uturuki katika miaka miwili iliyopita katikati ya mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza.

Maelezo ya mkutano wa Erdogan na Trump baada ya hotuba yake katika Umoja wa Mataifa yanaonyesha jinsi Uturuki, licha ya eneo lake kubwa la kimkakati na mienendo ya nguvu kubwa, imeanguka katika hali ya udhaifu. Makubaliano makubwa yalifikiwa na Amerika ambayo wigo wake kamili bado haujafichuliwa. Miongoni mwa vipengele vyake ni ujenzi wa mitambo ya nyuklia ya kiraia nchini Uturuki, ununuzi wa Shirika la Ndege la Uturuki wa mamia ya ndege za abiria kutoka Amerika, ndege za kivita za aina ya F-35 na F-16, vifaa vya kijeshi, usafirishaji wa gesi asilia iliyoyeyushwa kupitia meli za Amerika, na hata ugawaji wa baadhi ya madini adimu ya ardhini kutoka Uturuki kwenda Amerika.

Kukaribishwa kwa Trump kwa Erdogan alipoingia, matumizi yake ya itifaki ya ngazi ya juu, kuvuta kiti chake, kuketi karibu naye, kufanya mkutano wa faragha wa zaidi ya saa mbili, na kumsifu mara kwa mara, haikuwa bila sababu.

Maneno ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio yanaeleza ambapo alisema: "Mataifa mengine yote, ikiwa ni pamoja na Uturuki, kimsingi yanatuomba tuingilie kati katika masuala haya... Hatimaye, kuna viongozi ambao wanaomba kushiriki katika hili. Wanapiga simu na kusema: Je, tunaweza kusalimiana na Rais kwa dakika tano?".

Wakati viongozi wengi wa ulimwengu wanaomba kusalimiana na Trump kwa dakika tano, mkutano wa Erdogan wa saa mbili unaonyesha makubaliano makubwa yaliyotolewa na Uturuki na majukumu mapya ambayo imepangwa kuchukua katika utekelezaji wa mipango ya kikanda ya Amerika!

Imeandikwa kwa Idhaa ya Afisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Ramzi Uzair

More from null

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Usitishaji Mapigano huko Gaza ni Pazia la Kuandaa Ukweli Mpya kwa Damu na Vifusi

Habari:

Uchunguzi wa Al Jazeera, unaotegemea uchambuzi wa picha za satelaiti, umefichua mifumo ya uharibifu wa kimfumo iliyofanywa na uvamizi huko Gaza kati ya Oktoba 10 na 30 iliyopita.

Shirika la "Sanad" la uhakiki wa habari la mtandao wa Al Jazeera limegundua operesheni za ulipuaji, ubomoaji wa kihandisi na mashambulizi makubwa ya anga yaliyofanywa na uvamizi ndani ya Ukanda huo tangu kuanza kutekelezwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano. (Al Jazeera Net)

Maoni:

Baada ya kutangazwa kwa usitishaji wa vita vilivyojaa mabomu dhidi ya Ukanda wa Gaza chini ya usimamizi wa Trump na kwa makubaliano na baadhi ya nchi za Kiarabu, ilikuwa wazi kuwa ilifikiwa kwa faida ya taasisi ya Kiyahudi. Hili limebainika kulingana na uchambuzi wa picha za satelaiti na ripoti za hivi karibuni za habari, kwamba jeshi la Kiyahudi lililipua maelfu ya majengo huko Gaza, haswa huko Shuja'iyya na Khan Yunis katika maeneo yaliyo chini ya udhibiti wao, na vile vile Rafah, na maeneo yaliyo mashariki mwake ambayo yalishuhudia operesheni kubwa za uharibifu.

Uharibifu mkubwa huko Gaza sio wa bahati mbaya, lakini una malengo ya kimkakati ya muda mrefu, kama vile kuharibu mazingira yanayounga mkono upinzani. Kuondoa Gaza ya miundombinu yake, shule zake na makazi yake, inafanya kuwa ngumu kwa upinzani kujipanga upya au kujenga upya uwezo wake. Hii ni kizuizi cha muda mrefu kwa kuharibu uwezekano na kulazimisha ukweli mpya ambao unaifanya Gaza kuwa dhaifu na kuiacha ikiwa imepooza kiuchumi na haifai kwa makazi, ambayo huandaa njia ya kukubali suluhisho zozote za kisiasa au kiusalama, au hata kukubali wazo la uhamishaji, kwa sababu kuacha Gaza kama kifusi, inafanya kuwa ngumu kwa ujenzi kuwa mikononi mwa watu wake pekee. Badala yake, nchi na mashirika yataingilia kati kwa masharti ya kisiasa, na uvamizi unatambua kuwa yeyote anayejenga upya ndiye anayemiliki uamuzi. Hivyo basi uharibifu wa leo ni sawa na udhibiti wa kisiasa kesho!

Kwa kweli, kuelezea makubaliano ya kusitisha vita dhidi ya Gaza kama "yenye mabomu" haikuwa bure, kwa sababu ilikuwa ya sehemu, na malengo ya madai ya kijeshi hayakujumuishwa, ambayo inaruhusu Wayahudi kuendelea na uvamizi na uharibifu kwa kisingizio cha kiusalama. Vivyo hivyo, ilifikiwa na nchi kubwa zaidi inayounga mkono taasisi bila dhamana thabiti za kimataifa, ambayo inafanya kuwa dhaifu na inakabiliwa na ukiukwaji, haswa kwa kukosekana kwa uwajibikaji wa kimataifa, ambayo inafanya taasisi ya Kiyahudi kuwa juu ya uwajibikaji.

Tutaendelea kuwa taifa lenye unyenyekevu na linalokubali, tukitazama watu waliodhoofika, waliochoka, waliopotea na wenye njaa mpaka lini?! Na juu ya yote hayo, wanaruhusiwa wakati wowote?! Hebu sote tuwe Saladin al-Ayyubi, kwa sababu Gaza leo inakumbusha taifa kwamba Saladin hakuwa tu mtu shujaa, lakini alikuwa kiongozi katika dola iliyokuwa na mradi na jeshi na taifa moja nyuma yake. Kwa hivyo, wito wa kuwa Saladin haimaanishi ushujaa wa mtu binafsi, lakini kufanya kazi ya kuanzisha dola ambayo inafanya watoto wote wa taifa kuwa askari katika safu moja chini ya bendera moja.

Mwenyezi Mungu amesema: ﴿Mna nini hamkupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili ya wanyonge miongoni mwa wanaume na wanawake na watoto﴾.

Imeandikwa kwa Radio ya Ofisi ya Habari Kuu ya Hizb ut-Tahrir

Manal Um Ubaidah

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Abdul Malik al-Houthi hachangii kutoka kwa mali yake au mali ya baba yake!

Habari:

Kituo cha Yemen Sana'a kilirusha hewani Jumatano jioni, 2025/11/12, kipindi cha kibinadamu "Nchi Yangu", na katika sehemu ya "Tuko nanyi", kipindi kilionyesha kesi ya mwanamke ambaye alikuwa ameambukizwa ugonjwa adimu na alihitaji kusafiri kwenda India kwa gharama ya dola elfu 80, ambapo kiasi cha dola elfu 70 kilikusanywa kutoka kwa mashirika na wahisani, lakini mtangazaji wa kipindi alizungumzia sana sifa za mchangiaji wa mwisho wa dola elfu kumi, na ikawa wazi kuwa alikuwa Abdul Malik al-Houthi, na alisifu jukumu lake la mara kwa mara katika kusaidia kesi za kibinadamu ambazo zinaonekana kwenye kipindi.

Maoni:

Hakika, mtawala katika Uislamu ana jukumu kubwa, ambalo ni kutunza maslahi ya watu kwa kutumia kile kinachowanufaisha na kutoa kila kitu kinachowafariji. Kimsingi yeye ni mtumishi wao, na hawezi kufurahia maisha hadi atakapohakikisha hali zao. Jukumu hili sio ihsani au upendeleo, bali ni wajibu wa kisheria ambao Uislamu umemlazimisha, na anahesabiwa kuwa amepungukiwa ikiwa atalipuuza. Uislamu umewajibisha umma kumuwajibisha anapopungukiwa. Amani na baraka zimshukie: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, ni upuuzi kufurahia usikivu wa watawala au serikali kwa mahitaji fulani na kuita hiyo kazi ya kibinadamu, wakati kimsingi ni kazi ya kichungaji ya lazima.

Moja ya dhana hatari zaidi ambayo imekita mizizi na ubepari na utawala wake duniani ni kukataa kwa serikali kutunza watu na kuacha utunzaji wa watu kwa mashirika na vyama vya hisani vinavyoendeshwa na watu binafsi au vikundi, na watu huenda kwao mara nyingi kuwasaidia na kutimiza mahitaji yao. Wazo la vyama lilionekana kwanza huko Uropa wakati wa Vita vya Ulimwengu, ambapo familia nyingi zilipoteza wazazi wao na zikawa zinahitaji mlinzi, na serikali, kulingana na mfumo wa kidemokrasia wa kibepari, haitunzi masuala, bali ni mlinzi wa uhuru tu. Matajiri waliogopa mapinduzi ya maskini dhidi yao, kwa hivyo walianzisha vyama hivi.

Uislamu umefanya kuwepo kwa sultani kuwa wajibu wa kutunza masuala ya umma ili kuhifadhi haki zao za kisheria na kukidhi mahitaji yao sita ya msingi ambayo lazima yakidhiwe kwa watu binafsi na vikundi; chakula, mavazi na makazi lazima yatolewe na serikali kwa kila mtu mmoja mmoja, Waislamu na wasio Waislamu, na usalama, matibabu na elimu hutolewa na serikali bure kwa wote. Mtu mmoja alikuja kwa Khalifa wa Waislamu, Omar bin al-Khattab, Mungu amuwiye radhi, akiwa na mke wake na binti zake sita, akasema: (Ewe Omar, hawa ni binti zangu sita na mama yao, walishe, wavishe na uwe ngao kwao kutoka kwa wakati) Omar akasema: (Na vipi ikiwa sitafanya hivyo?!) Bedui akasema: (Nitakwenda) Omar akasema: (Na vipi ikiwa utakwenda?) Akasema: (Utaulizwa kuhusu hali yao Siku ya Kiyama, ukisimama mbele ya Mungu ama kuelekea Motoni au Paradiso), Omar akasema: (Umma huu hautapotea maadamu kuna watu kama hawa).

Enyi Waislamu: Hii sio ndoto, bali ni Uislamu ambao umefanya utunzaji kuwa wajibu kwa Khalifa wa Waislamu kwa kila mtu mmoja mmoja, Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehma na amani zimshukie, alisema: «Imam ni mchungaji na anaulizwa kuhusu kundi lake». Kwa hivyo, lazima turudishe hukumu hizi na kuzifanya ziwe za utekelezaji, Mwenyezi Mungu Mtukufu alisema: ﴿Hakika Mwenyezi Mungu habadilishi yaliyomo kwa watu mpaka wabadili yaliyomo katika nafsi zao﴾. Hivyo, kitakachobadilisha hali yetu kuwa haki na ustawi ni Uislamu.

Imeandikwa kwa ajili ya Redio ya Ofisi Kuu ya Habari ya Hizb ut-Tahrir

Sadiq al-Sarari